Hii imekaaje, AK Waafrika Hawataki Kiafrikaans lkn wanataka English!

Lakini hapo ndipo Ujinga wetu Waafrika ulipo, kwa maana hapa ukiangalia Kiafrikaans ni lugha ya Wazungu Makaburu unaweza hata kukiita Kiholanzi na Wazungu hawa hawataki kuiacha lugha yao na kuchukuwa English ingawaje wewe unasema ni lugha ya Dunia lkn Mwafrika mweusi anapigania na yuko tayari kuharibu Miundo mbinu ya Chuo Kikuu iliyojengwa kwa fedha nyingi ili Kiingereza kifundishwe!

Sasa ni kwa nini Mzungu anapigania Kiafrikaans chake tena ndani ya Afrika lkn Mwafrika mweusi yuko tayari kufa kupigania Kiingereza na siyo Kizulu chake?
Kumbuka Wazungu (ukiondoa machotara/coloreds) wanaoongea Kiafrikaans kama lugha yao asili hawazidi milioni 2 wkt Kizulu kinaongewa na Watu milioni 11 au asilimia 22 (22%) ya wananchi wa AK, sasa kwa nini nguvu zao Waafrika weusi wasizielekeze hapa kwenye Kizulu badala ya Kiingereza?

Afrikaner si lugha ya Kiafrika. Ni lugha ya makaburu. Makaburu kwa jina jingine huitwa Afrikaners
 
Sawa nakuelewa lkn tupa kule ulete nini? Hicho ndiyo kitu ambacho nashindwa kukielewa!
Hata mimi napenda kukitupa Kiafrikaans kwa maana ni lugha ya kigeni lkn unapopigania kutupa Kiafrikaans lugha ya Kizungu na kutaka kuleta Kiingereza sasa ndiyo umefanya nini?

Mimi ningependa wapiganie kutupa Kiafrikaans na kuleta Kizulu, hapo ndipo Mwafrika ataheshimika kwani Dunia nzima binadamu wote hupigania lugha zao na Afrika kwetu tu tena siyo Afrika yote bali sisi weusi kwa maana hata Somalia na Ethiopia wanapigania Lugha zao ni sisi Wabantu ndiyo tunapigania kuwa na lugha ya kigeni yaani tuko tayari kufa, kuumizwa na Askari kwa ajili ya kupigania Kiingereza!
Mkuu wale wameathirika na ukabila bora lugha ya malkia tu
 
Mkuu...tanzania tulishapata ukombozi...ama kweli Benja hakukosea alivyowaita malofa na wapumbavu
Ukombozi upi kijana??????siye watanganyika tulichokifanya hiyo miaka ya 60 ni kubadili white exploiters(colonialist) master to black exploiters tu and not otherwise......
 
Apartheid si neno tu bali ni mfumo wa kibaguzi uliopewa jina hilo. Mfumo huo haukuanzishwa na waingereza na ndiyo maana kuna wakati maalum wa kuanza na kumalizika, kuwa ni kuanzia mwaka 1948 hadi mwaka 1994. Unajua ni kwa nini wanasema ulianza mwaka 1948?



Ndiyo maana nimekwambia jaribu kwanza kujisomea Historia ili uelewe haya mambo na uache kulishwa!
Apartheid AK haijaanza 1948 ila jina Apartheid ndiyo limeanza kutumika mwaka 1948, lkn mfumo wa Ubaguzi wa rangi AK umeanza zamani sana tangu miaka ya 1800 huko kulikuwa na kitu kinaitwa pass law na pass law iliasisiwa na Waingereza chini ya akina Cecil Rhodes na wenzake sasa sijui unachobisha ni nini hapa? Na pass law ndiyo mzao wa Apartheid tofauti ni jina tu!

Na Waingereza ndiyo waliyoipromote Apartheid system siku zote mpaka siku za mwisho Mandela anaachiwa alikuwa kwenye terrorist list ya Uingereza na Marekani, kwa lugha rahisi mandela alikuwa ni gaidi au terrorist kwa Waingereza na Marekani kama vile alivyokuwa Osama Bin laden mpaka siku anaachiwa huru Apartheid imeisha tu baada ya Thatcher (aliyekuwa Kiongozi wa Uingereza) kuondoka vita baridi kuisha na Waingereza na rafiki zake kama Marekani kukubali kuishinikiza AK ya Makaburu kuruhusu demokrasia ya wote!
 
Haswa, Waingereza ndiyo Marchitect wa Ubaguzi wa rangi AK, neno Apartheid maana yake ndiyo hiyo ubaguzi wa watu kulingana na asili yao, na Waanzilishi ni Waingereza na siyo waanzilishi tu bali hata walioipa support Apartheid mpaka dakika ya mwisho ni Waingereza chini ya Churchil na Margaret Thatcher!

Walichofanya makaburu ni kuendeleza tu mfumo lkn uliasisiwa na Waingereza na hata walioufanya udumu mpaka miaka 90' ni Waingereza hao hao, wao ndiyo waliokuwa wanwakingia kifua makaburu miaka yoote!
Nikweli kabisa, ni sawa na vile sultan alitawala Zanzibar kwa niaba ya uingereza
 
Acha blah blah zako wewe, "Apartheid" imeanza mwaka 1948 hadi 1994 wakait Cecil Rhodes alikufa mwaka 1902. Kama kila ubaguzi unauita "Apartheid" basi hata Ubaguzi unaoendelea huko Marekani kwa Wazungu kuwabagua waafrika wewe na mfanano wako na yule "Kibajaji" wenu basi uite ubaguzi huo 'Apartheid" kama watu wenye kujua watakuelewa!
Issue sio Rhodes alikufa mwaka gani, atuzungumzii mtu,tunazungumzia mfumo, ambapo Uingereza ndio sponsor
 
Binafsi sielewi na bado sijawahi kuielewa reasoning yetu Waafrika hata siku moja. Huko nchini AK kumezuka fujo kubwa iliyopelekea wanafunzi kuchoma na kuharibu Miundo mbinu ya Chuo Kikuu wanachosomea, sasa kisa ni nini?

Ni kwamba Wanafunzi Waafrika (weusi) hawataki kufundishwa kwa lugha ya Kiafrikaans ambayo ni lugha rasmi ya Makaburu wanasema kwamba ni lugha ya Kikoloni na ya ukandamizaji na wanataka Vyuo vyao vifundishwe kwa kutumia Kiingereza, hapo ndipo nilipochoka ningeelewa kama wangegoma kufundishwa Kiafrikans na kutaka wafundishwe Kizulu, Xhosa , Kitwsana au hata Kiswahili kama shida ni lugha ya Kikoloni lkn wanataka Kiingereza sasa Kiingereza ni lugha ya nani?

Unakataaje Kiafrikaans kwa kigezo kwamba ya Kikoloni halafu unataka Kiingereza?
Inanikumbusha Raisi Kagame wa Rwanda alipoondoa Kifaransa kama Lugha ya Taifa na kuweka Kiingereza kwa nini asingeweka Kirundi/Kinyarwanda? Au Raisi Mugabe wa Zimbambwe anatukana Wazungu na kuwakebehi lkn kwa Kiingereza na nchi yake anatumia Kiingereza kwa nini siyo Kishona?

Kwa mambo kama haya Waafrika hatuwezi kuheshika Duniani kamwe kwani watu wa nje wanatuona hatuna akili, Dunia nzima binadamu hufanya Mapinduzi na kuweka lugha zao sasa tuko tayari kuharibu Miundo mbinu yetu kupigania Kiingereza, sasa Kiingereza kina tofauti gani na Kiafrikaans? Zote si ni lugha za Kikoloni pia!

Hata hapa nyumbani watu wengi wanaona na kuamini kwamba Kiswahili chetu ndiyo adui wa Maendeleo yetu nina uhakika ukifanya kura ya maoni ya kama Kiswahili kifutwe TanZania na kuwekwa Kiingereza au Kifaransa au hata Kireno zaidi ya asilimia 60 wataataka Kiswahili chetu kifutwe, na kama siyo kuwa Sera ya CCM Kiswahili kingekuwa kimeshafutwa kwani kwenye manifesto ya chadema walikwishakiondoa na kubakia somo tu!
Hii ni Afrika kwetu tu hakuna sehemu nyingine Duniani kuna binadamu wa aina kama yetu!

Hata Afrika Kaskazini hawako hivyo Gadafi mpaka anakufa anaongea Lugha yake!



Chini ni Uharibifu uliofanywa na Wanafunzi kwa kuchoma majengo ya Chuo chao kupinga Kiafrikaans na kutaka Kiingereza!

318EF4C700000578-3464350-image-a-10_1456426587394.jpg

318EF4C200000578-3464350-image-a-11_1456426590849.jpg


318EF4BE00000578-3464350-image-a-13_1456426601152.jpg



318CAEF700000578-3464350-image-a-1_1456425531757.jpg


318CAF3300000578-3464350-image-m-6_1456425554501.jpg




SABC News - UP student’s Afrikaans protest grows:Friday 19 February 2016
Kiingereza ni lugha ya dunia.
 
Ndiyo maana nimekwambia jaribu kwanza kujisomea Historia ili uelewe haya mambo na uache kulishwa!
Ni wewe siyo mimi anayepaswa kusoma Historia. Ubaguzi upo wa aina nyingi. Kwa mfano kilichotokea Afrika Kusini Mwaka juzi na kinachotokea huko Ujerumani hivi sasa ni ubaguzi lakini hauitwi "Apartheid" bali "Xenophobia" na kihistoria makaburu hawazaliwi na Waingereza bali wanazaliwa na wadachi!!

Kusema kwamba Apartheid imeanzishwa na Waingereza ni utungaji usio na maana. Apartheid ulifanyika kuwa Mfumo pale sheria ya kuwaweka watu wa Afrika Kusini katika madaraja kwa kuzingatia Rangi zao na kuweka maeneo rasmi kwa ajili ya watu kwa kulingana na rangi zao.
 
Daaahhh....nakumbuka mwalim wangu wa history alinifundish ki2 kama hiki ila kiliitwa "UTOPIAN REVOLUTION" a Mayo ilitokea Uingereza
 
Kiingereza ni lugha ya dunia.
3/4 ya watu wa SA..wanaongea lugha ya kiingereza..sasa linapokuja suala la kuwaforce wajifunze ki Afrikaans..inamaana unawakumpusha machungu ya nyuma..kwanza hiyo lugha ukiiangalia kwa umakini inakuwa sawa tu na lugha za kizulu,khosa na vikabila vingine vidogo..kwa nini ipaishwe hivyo na sio kizulu au khosa??kwanini wasitumie kiingereza ambayo ni international language..yenye faida luluki kuliko hiyo ya afrikaans ambayo ni local language!
 
Ni wewe siyo mimi anayepaswa kusoma Historia. Ubaguzi upo wa aina nyingi. Kwa mfano kilichotokea Afrika Kusini Mwaka juzi na kinachotokea huko Ujerumani hivi sasa ni ubaguzi lakini hauitwi "Apartheid" bali "Xenophobia" na kihistoria makaburu hawazaliwi na Waingereza bali wanazaliwa na wadachi!!

Kusema kwamba Apartheid imeanzishwa na Waingereza ni utungaji usio na maana. Apartheid ulifanyika kuwa Mfumo pale sheria ya kuwaweka watu wa Afrika Kusini katika madaraja kwa kuzingatia Rangi zao na kuweka maeneo rasmi kwa ajili ya watu kwa kulingana na rangi zao.


Nimekwisha kwambia kwamba kabla ya Ubaguzi huko AK kuitwa rasmi apartheid ambalo ni neo la Kiholanzi/afrikaans ambalo maana yake ni kama ,,kutenganisha" kulikuwa na neno lingine au mfumo ulioitwa pass law, na halikuwa na tofauti yoyote ile na Apartheid isipokuwa walibadilisha jina tu ktk pass law kwenda apartheid na pass law ilianzishwa na Waingereza kwa lengo hilo hilo la kubagua watu kwa mujibu wa rangi na asilia yao, yaani Waafrika walikuwa wanabaguliwa na walihitaji pass kama ilivyokuwa baada ya 1948 Apartheid kwenda mahali popote pale kila kitu kilikuwa kimetenganishwa, na Watu weusi wote walikuwa hawaruhusiwi kufanya chochote wala kujichanganya na Wazungu na ndiyo maana ikaitwa pass law yaani walihitaji pass au kibali kufanya chochote kile kama vile ilivyokuwa apartheid!
 
Sawa nakuelewa lkn tupa kule ulete nini? Hicho ndiyo kitu ambacho nashindwa kukielewa!
Hata mimi napenda kukitupa Kiafrikaans kwa maana ni lugha ya kigeni lkn unapopigania kutupa Kiafrikaans lugha ya Kizungu na kutaka kuleta Kiingereza sasa ndiyo umefanya nini?

Mimi ningependa wapiganie kutupa Kiafrikaans na kuleta Kizulu, hapo ndipo Mwafrika ataheshimika kwani Dunia nzima binadamu wote hupigania lugha zao na Afrika kwetu tu tena siyo Afrika yote bali sisi weusi kwa maana hata Somalia na Ethiopia wanapigania Lugha zao ni sisi Wabantu ndiyo tunapigania kuwa na lugha ya kigeni yaani tuko tayari kufa, kuumizwa na Askari kwa ajili ya kupigania Kiingereza!
Unawashauri wengine wakati kwenu lugha ya Universities ni hiyo hiyo English!
 
Ni lazima kuelewa kwamba hawa waafrikaans ndiyo waliokuwa wanapewa upendeleo kipindi kile cha ubaguzi..ndiyo waliokuwa wanaruhusiwa kupata elimu bora, walipewa makazi bora na ndiyo walikuwa wanaruhusiwa kwenda beach...there was no beach for black...kwa hyo kuendeleza matumizi ya KIAFRIKAANS bado inaclick kwenye vichwa vya black kwamba wanaendelea kutawaliwa....
 
Humu jf kuna watu wanajikuta wanajua kila kitu utadhani wengine hatujasoma kabisaaaa simple history ya O level mtu inampa shida wote tunajua makaburu ndio walikuwa wazungu wa mwanzo kabisa kufika AK wakaja waingereza ambao nao waliitawala sana AK lakini hatukusikia apartheid wala hakuna sehemu yoyote kwenye historia ikionyesha muingereza akitumia apartheid kama modal ya administration yake baada ya muingereza kuondoka huyu panya ndio akashika hatamu na cha kwanza kabisa ali formulate constitution iliyozaa apartheid system na moja ya mission yake ni kufanya lugha yao kuwa lugha mama huko AK
 
Sasa huyo profesa maji marefu anakuja na magazeti makuubwaa kutumalizia bundle zetu bure kabisa English is an international lingua hakuna nchi yoyote yenye hati miliki na nchi flani kutumia English kama lugha yao haimaanishi nchi hiyo inaifagilia nchi nyingine au imepotoka na wala sio suala la kuzua mjadala mkuu
 
pass law,partheid!
Ndugu yangu "Pass Law" na "Apartheid" ni vitu viwili tofauti kabisa!! Pass law hata hapa kwetu Tanzania zilikuwepo na madaraja pia yalikuwepo, watu walikuwa wanajua Bar za wazungu ziko wapi na za kwao waswahili ziko wapi, na hata Mwalimu Nyerere aliwahi kukataliwa kuuziwa bia kwenye baa iliyokuwa maalum kwa wazungu. Pia kulikuwa na maeneo ya wazungu wahindi na Waafrika, na ndiyo maana maneno kama "Uswahilini" "Uzunguni" na "Uhindini" yaliibuka. Lakini huwezi kuuita huo mfumo kwamba ni Apartheid ingawa ni Ubaguzi.

Inawezekana Pass Law ikawa ni kiashiria cha ubaguzi, lakini kunawezekana kusiwe na Pass Law na bado Apartheid ikawepo. Boston kwenye ule mgomo mkubwa wa wakazi wa mji ule uliotokana na kupinga madaraja kwenye Magari ya usafiri ambayo yalimbagua Mwafrika, lakini kulikuwa hakuna Apartheid!!
 
Ndugu yangu "Pass Law" na "Apartheid" ni vitu viwili tofauti kabisa!! Pass law hata hapa kwetu Tanzania zilikuwepo na madaraja pia yalikuwepo, watu walikuwa wanajua Bar za wazungu na hata Mwalimu Nyerere aliwahi kukataliwa kuuziwa bia kwenye baa iliyokuwa maalum kwa wazungu. Pia kulikuwa na maeneo ya wazungu wahindi na Waafrika, na ndiyo maana maneno kama "Uswahilini" "Uzunguni" na "Uhindini" yaliibuka. Lakini huwezi kuuita huo mfumo kwamba ni Apartheid ingawa ni Ubaguzi.

Inawezekana Pass Law ikawa ni kiashiria cha ubaguzi, lakini kunawezekana kusiwe na Pass Law na bado Apartheid ikawepo. Boston kwenye ule mgomo mkubwa wa wakazi wa mji ule uliotokana na kupinga madaraja kwenye Magari ya usafiri ambayo yalimbagua Mwafrika, lakini kulikuwa hakuna Apartheid!!


Embu ngoja twende pole pole kwa maana naona kama labda spidi imekuwa kubwa na kupotezana, ngoja tuanze Apartheid kwako unaielewaje? Yaani maana yake nini wanaposema Apartheid AK
 
Back
Top Bottom