Hii imekaaje, AK Waafrika Hawataki Kiafrikaans lkn wanataka English!

Barbarosa

JF-Expert Member
Apr 16, 2015
22,584
27,790
Binafsi sielewi na bado sijawahi kuielewa reasoning yetu Waafrika hata siku moja. Huko nchini AK kumezuka fujo kubwa iliyopelekea wanafunzi kuchoma na kuharibu Miundo mbinu ya Chuo Kikuu wanachosomea, sasa kisa ni nini?

Ni kwamba Wanafunzi Waafrika (weusi) hawataki kufundishwa kwa lugha ya Kiafrikaans ambayo ni lugha rasmi ya Makaburu wanasema kwamba ni lugha ya Kikoloni na ya ukandamizaji na wanataka Vyuo vyao vifundishwe kwa kutumia Kiingereza, hapo ndipo nilipochoka ningeelewa kama wangegoma kufundishwa Kiafrikans na kutaka wafundishwe Kizulu, Xhosa , Kitwsana au hata Kiswahili kama shida ni lugha ya Kikoloni lkn wanataka Kiingereza sasa Kiingereza ni lugha ya nani?

Unakataaje Kiafrikaans kwa kigezo kwamba ya Kikoloni halafu unataka Kiingereza?
Inanikumbusha Raisi Kagame wa Rwanda alipoondoa Kifaransa kama Lugha ya Taifa na kuweka Kiingereza kwa nini asingeweka Kirundi/Kinyarwanda? Au Raisi Mugabe wa Zimbambwe anatukana Wazungu na kuwakebehi lkn kwa Kiingereza na nchi yake anatumia Kiingereza kwa nini siyo Kishona?

Kwa mambo kama haya Waafrika hatuwezi kuheshika Duniani kamwe kwani watu wa nje wanatuona hatuna akili, Dunia nzima binadamu hufanya Mapinduzi na kuweka lugha zao sasa tuko tayari kuharibu Miundo mbinu yetu kupigania Kiingereza, sasa Kiingereza kina tofauti gani na Kiafrikaans? Zote si ni lugha za Kikoloni pia!

Hata hapa nyumbani watu wengi wanaona na kuamini kwamba Kiswahili chetu ndiyo adui wa Maendeleo yetu nina uhakika ukifanya kura ya maoni ya kama Kiswahili kifutwe TanZania na kuwekwa Kiingereza au Kifaransa au hata Kireno zaidi ya asilimia 60 wataataka Kiswahili chetu kifutwe, na kama siyo kuwa Sera ya CCM Kiswahili kingekuwa kimeshafutwa kwani kwenye manifesto ya chadema walikwishakiondoa na kubakia somo tu!
Hii ni Afrika kwetu tu hakuna sehemu nyingine Duniani kuna binadamu wa aina kama yetu!

Hata Afrika Kaskazini hawako hivyo Gadafi mpaka anakufa anaongea Lugha yake!



Chini ni Uharibifu uliofanywa na Wanafunzi kwa kuchoma majengo ya Chuo chao kupinga Kiafrikaans na kutaka Kiingereza!

318EF4C700000578-3464350-image-a-10_1456426587394.jpg

318EF4C200000578-3464350-image-a-11_1456426590849.jpg


318EF4BE00000578-3464350-image-a-13_1456426601152.jpg



318CAEF700000578-3464350-image-a-1_1456425531757.jpg


318CAF3300000578-3464350-image-m-6_1456425554501.jpg




SABC News - UP student’s Afrikaans protest grows:Friday 19 February 2016
 
Unafahamu kuhusu mauaji ya Soweto na lugha ya kiafrikana? That was oppressive language na kwa kuwa lugha ya makaburu ifahamu historia.
Kuchoma university ni alert juu ya ubaguzi unaondelea SA. Tofauti ya utabaka ni hali ya juu..blacks are absolute poor and ignorant na ni matokeo ya ubaguzi wa rangi. Labda colored watafurahi ila hao weusi bora English kuliko Afrikana..it is more than apartheid scurs in the mind of oppressed revolutionaries.
 
Mkuu...katika historia ya SA, Serikali ya Africaans (Makaburu) ndo walianzisha mfumo wa Aparthied ambao waafrika walinyanyaswa sana.....kiufupu, ingawa weusi walitawaliwa na waingereza as well as makaburu, ila ni waingereza walikuwa na afadhali sana
 
Unafahamu kuhusu mauaji ya Soweto na lugha ya kiafrikana? That was oppressive language na kwa kuwa lugha ya makaburu ifahamu historia.
Kuchoma university ni alert juu ya ubaguzi unaondelea SA. Tofauti ya utabaka ni hali ya juu..blacks are absolute poor and ignorant na ni matokeo ya ubaguzi wa rangi. Labda colored watafurahi ila hao weusi bora English kuliko Afrikana..it is more than apartheid scurs in the mind of oppressed revolutionaries.


Naielewa Historia ya AK vizuri tu na ndiyo maana haileti maana kwangu kukataa Kiafrikaans na kushinikiza Kiingereza kwani Waingereza ndiyo waanzilishi wa Apartheid AK kupitia watu kama akina Cecil Rhodes ambayo walipeleka Apartheid mpaka Rhodesia (Zimbabwe) na Namibia, na ndiyo maana sielewi mantiki ya kukikataa Kiafrikaans kwa kigezo cha lugha ya ukandamizaji na kutaka Kiingereza wakati Waingereza na Makaburu (Waafrikaans) wote wawili walikandamiza Waafrika weusi!

Kwa nini Wasipiganie Kizulu kutumiwa badala ya Kiingereza?
 
Lugha ya Kiafrikaans inawakumbusha machungu mengi waliofanyiwa kipindi cha ubaguzi wa rangi wa kiwango cha juu kabisa nchini mwao. Hii sio issue ya logic iko zaidi psychologically.

English haionwi hivyo. Ni lugha ya dunia tayari. Hata wazungu wenyewe hawaoni tena kama ya kwao.

Nadhani hata wewe ungekuwa SA ungewaza kama hawa college students.
 
Lugha ya Kiafrikaans inawakumbusha machungu mengi waliofanyiwa kipindi cha ubaguzi wa rangi wa kiwango cha juu kabisa nchini mwao. Hii sio issue ya logic iko zaidi psychologically.

English haionwi hivyo. Ni lugha ya dunia tayari. Hata wazungu wenyewe hawaoni tena kama ya kwao.

Nadhani hata wewe ungekuwa SA ungewaza kama hawa college students.


Lakini hapo ndipo Ujinga wetu Waafrika ulipo, kwa maana hapa ukiangalia Kiafrikaans ni lugha ya Wazungu Makaburu unaweza hata kukiita Kiholanzi na Wazungu hawa hawataki kuiacha lugha yao na kuchukuwa English ingawaje wewe unasema ni lugha ya Dunia lkn Mwafrika mweusi anapigania na yuko tayari kuharibu Miundo mbinu ya Chuo Kikuu iliyojengwa kwa fedha nyingi ili Kiingereza kifundishwe!

Sasa ni kwa nini Mzungu anapigania Kiafrikaans chake tena ndani ya Afrika lkn Mwafrika mweusi yuko tayari kufa kupigania Kiingereza na siyo Kizulu chake?
Kumbuka Wazungu (ukiondoa machotara/coloreds) wanaoongea Kiafrikaans kama lugha yao asili hawazidi milioni 2 wkt Kizulu kinaongewa na Watu milioni 11 au asilimia 22 (22%) ya wananchi wa AK, sasa kwa nini nguvu zao Waafrika weusi wasizielekeze hapa kwenye Kizulu badala ya Kiingereza?
 
Mkuu...katika historia ya SA, Serikali ya Africaans (Makaburu) ndo walianzisha mfumo wa Aparthied ambao waafrika walinyanyaswa sana.....kiufupu, ingawa weusi walitawaliwa na waingereza as well as makaburu, ila ni waingereza walikuwa na afadhali sana
Kama sisi tu japo ni kweli tulitawaliwa na waingereza na ccm ila bora waingereza tu
 
Waingereza ndiyo waanzilishi wa Apartheid AK kupitia watu kama akina Cecil Rhodes ambayo walipeleka Apartheid mpaka Rhodesia (Zimbabwe) na Namibia,
Yaani Wewe ndiye wamekupa #5 kwenye "Group of 46" wakati huna ulijualo!! Rudia tena... Umesema mfumo wa "Apartheid" ulianzishwa na Waingereza??
 
Mkuu...katika historia ya SA, Serikali ya Africaans (Makaburu) ndo walianzisha mfumo wa Aparthied ambao waafrika walinyanyaswa sana.....kiufupu, ingawa weusi walitawaliwa na waingereza as well as makaburu, ila ni waingereza walikuwa na afadhali sana


Basi labda haujailewa Historia ya AK vizuri, Apartheid haikuanzishwa na makaburu bali Apartheid ingawaje neno Apertheid ni la Kiafrikaans ilianzishwa na Waingereza hata Makaburu wenyewe waliteseka sana chini ya Waingereza mpaka ikapelekea vita kubwa kuzuka iliyojulikana kama Boer-Anglo war!

Lkn Marchitect wa Apartheid AK ni Waingereza na waliyoyafanya huko ndiyo waliyoyafanya Australia na all white policy wakati watu wasiokuwa Wazungu wa Ulaya Magharibi walikuwa hawaruhusiwi kuhamia Australia na kama walihamia walikuwa hawapewi uraisi daraja la kwanza sawa na Wazungu, sera hiyo hiyo waliitumia Zimbabwe (Rhodesia) kwa kiasi fulani Kenya pia!
 
Yaani Wewe ndiye wamekupa #5 kwenye "Group of 46" wakati huna ulijualo!! Rudia tena... Umesema mfumo wa "Apartheid" ulianzishwa na Waingereza??


Haswa, Waingereza ndiyo Marchitect wa Ubaguzi wa rangi AK, neno Apartheid maana yake ndiyo hiyo ubaguzi wa watu kulingana na asili yao, na Waanzilishi ni Waingereza na siyo waanzilishi tu bali hata walioipa support Apartheid mpaka dakika ya mwisho ni Waingereza chini ya Churchil na Margaret Thatcher!

Walichofanya makaburu ni kuendeleza tu mfumo lkn uliasisiwa na Waingereza na hata walioufanya udumu mpaka miaka 90' ni Waingereza hao hao, wao ndiyo waliokuwa wanwakingia kifua makaburu miaka yoote!
 
Basi labda haujailewa Historia ya AK vizuri, Apartheid haikuanzishwa na makaburu bali Apartheid ingawaje neno Apertheid ni la Kiafrikaans ilianzishwa na Waingereza
Acha blah blah zako wewe, "Apartheid" imeanza mwaka 1948 hadi 1994 wakait Cecil Rhodes alikufa mwaka 1902. Kama kila ubaguzi unauita "Apartheid" basi hata Ubaguzi unaoendelea huko Marekani kwa Wazungu kuwabagua waafrika wewe na mfanano wako na yule "Kibajaji" wenu basi uite ubaguzi huo 'Apartheid" kama watu wenye kujua watakuelewa!
 
Binafsi sielewi na bado sijawahi kuielewa reasoning yetu Waafrika hata siku moja. Huko nchini AK kumezuka fujo kubwa iliyopelekea wanafunzi kuchoma na kuharibu Miundo mbinu ya Chuo Kikuu wanachosomea, sasa kisa ni nini?

Ni kwamba Wanafunzi Waafrika (weusi) hawataki kufundishwa kwa lugha ya Kiafrikaans ambayo ni lugha rasmi ya Makaburu wanasema kwamba ni lugha ya Kikoloni na ya ukandamizaji na wanataka Vyuo vyao vifundishwe kwa kutumia Kiingereza, hapo ndipo nilipochoka ningeelewa kama wangegoma kufundishwa Kiafrikans na kutaka wafundishwe Kizulu, Xhosa , Kitwsana au hata Kiswahili kama shida ni lugha ya Kikoloni lkn wanataka Kiingereza sasa Kiingereza ni lugha ya nani?

Unakataaje Kiafrikaans kwa kigezo kwamba ya Kikoloni halafu unataka Kiingereza?
Inanikumbusha Raisi Kagame wa Rwanda alipoondoa Kifaransa kama Lugha ya Taifa na kuweka Kiingereza kwa nini asingeweka Kirundi/Kinyarwanda? Au Raisi Mugabe wa Zimbambwe anatukana Wazungu na kuwakebehi lkn kwa Kiingereza na nchi yake anatumia Kiingereza kwa nini siyo Kishona?

Kwa mambo kama haya Waafrika hatuwezi kuheshika Duniani kamwe kwani watu wa nje wanatuona hatuna akili, Dunia nzima binadamu hufanya Mapinduzi na kuweka lugha zao sasa tuko tayari kuharibu Miundo mbinu yetu kupigania Kiingereza, sasa Kiingereza kina tofauti gani na Kiafrikaans? Zote si ni lugha za Kikoloni pia!

Hata hapa nyumbani watu wengi wanaona na kuamini kwamba Kiswahili chetu ndiyo adui wa Maendeleo yetu nina uhakika ukifanya kura ya maoni ya kama Kiswahili kifutwe TanZania na kuwekwa Kiingereza au Kifaransa au hata Kireno zaidi ya asilimia 60 wataataka Kiswahili chetu kifutwe, na kama siyo kuwa Sera ya CCM Kiswahili kingekuwa kimeshafutwa kwani kwenye manifesto ya chadema walikwishakiondoa na kubakia somo tu!
Hii ni Afrika kwetu tu hakuna sehemu nyingine Duniani kuna binadamu wa aina kama yetu!

Hata Afrika Kaskazini hawako hivyo Gadafi mpaka anakufa anaongea Lugha yake!



Chini ni Uharibifu uliofanywa na Wanafunzi kwa kuchoma majengo ya Chuo chao kupinga Kiafrikaans na kutaka Kiingereza!

318EF4C700000578-3464350-image-a-10_1456426587394.jpg

318EF4C200000578-3464350-image-a-11_1456426590849.jpg


318EF4BE00000578-3464350-image-a-13_1456426601152.jpg



318CAEF700000578-3464350-image-a-1_1456425531757.jpg


318CAF3300000578-3464350-image-m-6_1456425554501.jpg




SABC News - UP student’s Afrikaans protest grows:Friday 19 February 2016
Mkuu ki afrikaan kinawakumbusha machungu ya ubaguzi
kufundisha kiafrikaan ni sawa na kuendeleza ubaguzi
Kiafrikaan kinazungumzwa afrika kusini tu,na baadhi ya makaburu kwa kuendeleza sera ya kikaburu wameanzisha shule zao kuenzi kiafrikaan.
Tupa kule hiyo lugha
 
Acha blah blah zako wewe, Apartheid imeanza mwaka 1948 hadi 1994 wakait Cecil Rhodes alikufa mwaka 1902. Kama kila ubaguzi unauita Apartheid basi hata Ubaguzi unaoendelea huko Marekani kwa Wazungu kuwabagua waafrika wewe na mfanano wako na yule "Kibajaji" wenu basi uite ubaguzi huo Apartheid kama watu wenye kujua watakuelewa!


Ndugu, Apartheid haijaanzia 1948, soma historia tena Apartheid imeanzia AK tangu ujio wa Waingereza huko AK miaka ya 1800, jaribu tena kusoma Historia kwani siwezi kukufanyia hilo, na kama una swali ndiyo uulize na siyo kubisha kumbe hauna uelewa mzuri!
 
Walichokikosa ndugu zetu wa AK ni kutokuwa na common language kama sisi, kwa hyo wanaona bora icho kingereza kuliko huo mlugha wa mkaburu, kila kabila AK wanalugha yao
 
Ndugu, Apartheid haijaanzia 1948, soma historia tena Apartheid imeanzia AK tangu ujio wa Waingereza huko AK miaka ya 1800, jaribu tena kusoma Historia kwani siwezi kukufanyia hilo, na kama una swali ndiyo uulize na siyo kubisha kumbe hauna uelewa mzuri!
Unamaanisha kuwa kila ubaguzi ni Apartheid?
 
Mkuu ki afrikaan kinawakumbusha machungu ya ubaguzi
kufundisha kiafrikaan ni sawa na kuendeleza ubaguzi
Kiafrikaan kinazungumzwa afrika kusini tu,na baadhi ya makaburu kwa kuendeleza sera ya kikaburu wameanzisha shule zao kuenzi kiafrikaan.
Tupa kule hiyo lugha


Sawa nakuelewa lkn tupa kule ulete nini? Hicho ndiyo kitu ambacho nashindwa kukielewa!
Hata mimi napenda kukitupa Kiafrikaans kwa maana ni lugha ya kigeni lkn unapopigania kutupa Kiafrikaans lugha ya Kizungu na kutaka kuleta Kiingereza sasa ndiyo umefanya nini?

Mimi ningependa wapiganie kutupa Kiafrikaans na kuleta Kizulu, hapo ndipo Mwafrika ataheshimika kwani Dunia nzima binadamu wote hupigania lugha zao na Afrika kwetu tu tena siyo Afrika yote bali sisi weusi kwa maana hata Somalia na Ethiopia wanapigania Lugha zao ni sisi Wabantu ndiyo tunapigania kuwa na lugha ya kigeni yaani tuko tayari kufa, kuumizwa na Askari kwa ajili ya kupigania Kiingereza!
 
Unamaanisha kuwa kila ubaguzi ni Apartheid?


Apartheid tu ni neno lililokuja baadaye kwenye jambo ambalo tayari lilikuwepo, yaani kabla ya mwaka 1948 Apartheid ilikuwepo AK sema ilikuwa haiitwi Apartheid kwa hiyo kilichotokea ni kuipa jina jipya tu lkn mfumo huwo wa Ubaguzi na warangi ulikuwepo kabla ya mwaka 1948 na uliasisiwa na Waingereza na ndiyo walioupeka mpaka Zimbabwe (Rhodesia) Kenya na kwingineko!
 
Apartheid tu ni neno lililokuja baadaye...
Apartheid si neno tu bali ni mfumo wa kibaguzi uliopewa jina hilo. Mfumo huo haukuanzishwa na waingereza na ndiyo maana kuna wakati maalum wa kuanza na kumalizika, kuwa ni kuanzia mwaka 1948 hadi mwaka 1994. Unajua ni kwa nini wanasema ulianza mwaka 1948?
 
Back
Top Bottom