HESLB: Serikali imeanza kulipa Malipo ya robo ya nne ya Mwaka wa Masomo 2019/2020 kwa Wanafunzi 132,119 Jumla ya TZS 66.9 Bilioni

Trust None

JF-Expert Member
Feb 12, 2018
1,260
4,415
Kama ilivyo kwenye sheria za bofi ya mikopo, kila mnufaika atapewa kiasi kinachoendana na siku alizokaa chuoni.

Hapo awali kabla ya Corona, boom moja ilikuwa 505,000 hadi 520,000 lakini kwa mfumo huu itakuwa pungufu.

Je, kama boom limepunguzwa, vipi kuhusu ada na direct cost? Vilipunguzwa kulingana na siku za masomo?
1595484530867.png

1595486742838.png
======

Soma ufafanuzi uliotolew na Bodi ya Mikopo:

= >
HESLB: Hatujapunguza mikopo ya Wanafunzi. Tunatoa fedha za kujikimu kulingana na siku za masomo

Baadhi ya Michango ya Wanachama Waliochangia huu Mjadala
HESLB wamesema sababu ya kupunguza boom ni kwamba eti muda wa masomo kwa semista hii ni mdogo sana

Je, kama boom limepunguzwa, vipi kuhusu ada na direct cost? Vilipunguzwa kulingana na siku za masomo?

Kama ndo hivyo serikali inakwama wapi kutoa muongozo kwa vyuo kwamba wanafunzi wapunguziwe ada Mfano wanasema semista hii ni fupi sana hata miezi mitatu haifiki sasa kwanini na ada isipunguzwe?Kwanini watu wapunguziwe maboom lakini pia wasipunguziwe kiasi cha ada kwa muhula huu?

Mimi naona kama wanafunzi wamepunguziwa boom kisa ufupi wa semista basi na ada ipunguzwe maana unakuta chuo ada milioni 3 sasa nusu muula ni milioni 1.5 sasa kwanini mtu alipe 1.5 kama nusu muhula wakati muhula ni mdogo wa miezi 2 na siku chache tu?

Kama wamepunguziwa boom la muhula huu basi na ada ipunguzwe tu maana nina uhakika kuna wanafunzi wengi tu ambao wanatumia boom lao kulipia ada maana sio wote wana asilimia mia moja

Mkuu Kuna sehemu gani kwenye mkataba pameandikwa kuwa pesa ya chakula italipwa kwa semester? Nayo imekuwa Ada?

Mkataba upo wazi kabisa kuwa pesa ya chakula na malazi italipwa kwa Siku ambazo mwanafunzi atakapokuwa masomoni, Sasa Kama mtu anaondoka chuoni August mwishoni unataka apewe pesa ya kujikimu Hadi ya mwezi wa kumi wakati hayupo chuoni kimasomo?

Kuhusu kupewa taarifa ilishatolewa zamani Sana kwenye mkataba Kama mtu alisoma mkataba vizuri na kuuelewa kabla ya kuomba mkopo hawezi shangazwa na mabadiliko haya.

Halfu hajaandikwa kwenye mkataba kuwa pesa ya chakula itatumika kulipa ada Bali hayo Ni matumizi ya mtu binafsi Ila matumizi elekezi ya hiyo pesa Ni chakula na maladhi tu. Ukiitumia kulipia ada, usafiri, kununulia viwalo, kuhonga na n.k hiyo Ni juu yako na Wala siyo wao.
fafanua na ulipaji wa hilo deni... na ile jumla ya pesa wanazoonyesha kwenye account ya muhusika...

je kama kwenye account inaonyesha una jumla ya 3459000 na jumla ya pesa ya kula ikiwemo...
na kwa situation iliyotokea hilo deni linakuwa hivyo hivyo kamili ama kunakuwa na deduction ya hiyo pesa walioipungiza..????

Sent using Jamii Forums mobile app

Naona kitendo cha bodi kimeamsha ari ya wanafunzi vyuoni na vyuo vingine hadi washaanza kupanga maandamano ya amani

Picha ya kwanza ni chuo cha uhasibu Arusha ambapo wanafunzi wanapanga kuandamana

Sio hivyo tu kuna vyuo vingi sana wamepanga maandamano yaanze na hii yote ni kwasababu ya ya mambo ya ajabu yanayofanywa na bodi ya mikopo


Wanafunzi wengine wamepewa laki 1 tu eti ndo boom la kujikimu na sio laki 5 tena halaf siku za kurejesha mkataba unawaforce warejeshe laki 5

Nimeattach na video ya wanafunzi wa udsm pia wakijiandaa kwa maandamano ya amani

Maandamano ya amani ni haki yao ya msingi kama litahitajika kufanyika hivyo
View attachment 1514540View attachment 1514547
View attachment 1514551
 
Kulingana na taarifa iliyotolewa na Mkurungezi wa Bodi ya mikopo ya wanfunzi wa Elimu juu leo katika ukurasa wake wa Twitter inadai kuwa malipo yatafanyika kulingana na siku zilizo bakia kulingana na ratiba za chuo husika. Chini nimeambanisha picha ya tangazo
1595509272480.png
 
mbona yupo sahihi wewe, ndiye umesoma na hujaelewa. Soma vizuri tangazo utaelewa nini amemanisha, coz taarifa inaeleza watalipwa kulingana na siku walizokaa au watakazo kaa vyuo which means boom ni next week hivo kufanya siku 45 tu, ndio bodi watalipa ukipiga mahesabu inakuj 391k.
Tangazo na ulicho kiandika havina uhusiano.
Tumie elimu yako kuchambua mambo kabla hujatuletea mrejesho kamili.
Au stress za mitihan?
 
Maandishi ya blue watu hawajayaelewa...vyuo vingi vilibadilisha ratiba zake hivyo kuna baadhi ya vyuo watamaliza semister kabla ya siku.hivyo watajumlisha siku utakazokuwa chuoni kwa robo ya nne ya mkopo utazidisha kwa 8500.
Hapo kama chuo chako hautakaa siku 60 kwa robo ya nne ya semister jua huna tena laki 5
 
Inaweza kuwa imepunguzwa kweli
Kwani si huwa inatolewa kulingana na idadi ya siku wawapo chuoni.
Kutokana na Covid-19, siku zimepungua.

Robo ya tatu walitoa jumla billioni 63.7,
Robo ya mwisho wametoa 44.5 billioni.
 
Back
Top Bottom