HESLB: Batch One Out Now

HESLB: Batch One Out Now

Nimeona boom inatoka kwa awamu sijui waliojisajili mapema ndiyo wanaowahi kuingiziwa boom.

Sasa sijui kwa waliojisajili awamu ya mwisho wataingiziwa boom lini.
Apana ss wote huku tayari
 
Rufaa sasa kufungwa Ijumaa Novemba 17, 2023

BODI ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetangaza kuongeza muda wa siku nne zaidi hadi Novemba 17, 2023 ili kuwawezesha wanafunzi ambao hawajapangiwa au wanaohitaji kuongezewa viwango vya mikopo kwa mwaka wa masomo 2023/2024 kuwasilisha maombi ya rufaa zao.

Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, Abdul-Razaq Badru amesema uamuzi wa kuongeza muda umetokana na tathtmini iliyofanywa ili kuwawezesha wanafunzi wahitaji watumie muda wa nyongeza kuwasilisha maombi ya rufaa zao kwa usahihi.

“Tulifungua dirisha siku ya Jumatano (Novemba 8, 2023), na baada ya tathmini tumeongeza muda wa siku nne zaidi hadi Ijumaa, Novemba 17 mwaka huu ili kutoa muda wa kutosha kwa waombaji kuwasilisha rufaa zao”, amesema Badru na kusisitiza maombi yote ya rufaa yanawasilishwa kwa njia ya mtandao (OLAMS).

Mkurugenzi Badru amewashauri waombaji wa mikopo wanaokata rufaa kusoma maelekezo kwa umakini na kuyazingatia ikiwemo kuambatisha nyaraka zinazothibitisha uhitaji wao ambazo awali hawakuwa wamezipakia kwenye mfumo na kuongeza kuwa waombaji wanapaswa kutembelea akaunti zao walizotumia kuomba mikopo (SIPA) ili kupata taarifa za mikopo yao.

Serikali kupitia HESLB imepanga kutoa mikopo kwa wanafunzi 220,000 kwa mwaka
Hivi baada ya muda wa appeal inaweza kupita muda gani ndipo wahitaji wa mkopo waweze kujua kama appeals zao zimezaa matunda au la?
 
Bodi wamedai watatoa mkeka wa rufaa jumatano hii.

wamesema hayo leo asubuhi,wakati wakifanya mahojiano na clouds fm
Hapana mkuu hukumsikia vizuri Mkurugenzi Mtendaji ndugu Abdulrazaq alisema ni alhamisi ndiyo mkeka wa rufaa utatoka.

Alisema bado siku mbili tu (jumanne na jumatano) mkeka utoke.
 
Tuzidi kupeana updates za rufaa
IMG-20231123-WA0003.jpg
 
Back
Top Bottom