Sasa kama hamkomoleki mbona ninyi ndio mnaongoza kulialia mitandaoni na vijiweni kuhusu wanawake halafu mnasingizia eti mnawasaidia mnawasaidia nini ikiwa ninyi wenyewe ndio sehemu ya hilo tatizo narudia acheni unafiki, yani ninyi ndio mnaozihitaji hizo bikira halafu ninyi ninyi ndio mnawashawishi mabinti wafanye kabla ya ndoa halafu wakikubali muanze kusema eti ni ujinga wao kana kwamba wao ni malaika na wanaweza kukwepa vishawishi vyote ila ninyi ndio hamuwezi, hao wanawake wangekuwa wanahitaji hizo ndoa kama mnavyosema basi wasingekuwa wanakataa kuolewa na hata wakiolewa wasingekuwa wanaleta usumbufu huko kwenye ndoa na kuwa wa kwanza kudai talaka na kutaka mgawanyo wa mali inaonekana hadi leo hamjajua wanawake wanafuata nini kwenye ndoa mnajifariji tu hapa
Unachofanya ni kuhama hama haujengi hoja ya msingi na kwa hili utachoka wewe mimi ninachofanya ni kukurudisha kwenye msingi.
Swali kwako: wewe ni bikra,kama sio bikra ndoa yako uliyotolewa bikra ipo wapi? Kama haujaolewa bikra ulimpa nani kwa mkataba upi? 😂
Wewe hebu acha kutufanya wote wapumbavu kama wewe kwahiyo hata viongozi wa dini wanapohubiri kuhusu mambo ya kale yaliyoandikwa kwenye vitabu napo wanakosea kwa sababu hawakuwepo, na waalimu nao wanapofundisha historia kuhusu mambo ya ukoloni na vita za dunia napo hawatakiwi kwa sababu hawakuwepo hivi hizi ni akili za wapi, unajua wewe unaongea pumba kiasi unafanya mtu aone anapoteza muda kujadiliana na wewe hivi do you get paid to be this stupid halafu mtu akiacha kukujibu unasingizia anakuogopa kwa hizi pumba na haya mashudu yako au kwa hoja zipi
Tulia wewe mtoto mdogo nikuelekeze. Kuna kuhadithia jambo kama marejeo na kuna kushuhudia jambo kama shuhuda wa macho na masikio. Wewe kuelezea mambo ya miaka ya 1998 kurudi nyuma unayaongelea kama nani na ulikuwapo kuyaona kwa uhakika ukashuhudu? Wakati Papa anakuja Tanzania wewe ulikuwapo pale airport kumpokea ukiwa na wazazi wako?
Michael Jackson alikuja Tanzania,ulikwenda Airport kumpokea , mrema alipokuwa waziri ulishuhudia? So kuna vitu mimi nikikwambia maana nilikuwa naviona kwa macho nikiwa timamu sijahadithiwa wewe unajua na story za kupewa. Acha mbanga hizi wewe.
Waliofanya ni wanawake sababu wanaume wasingeweza kujihusisha moja kwa moja na sehemu za siri za wanawake wasiowahusu ndio maana mangariba walikuwa wanawake, ila haimaanishi kwamba wanawake ndio walioanzisha huo utamaduni wao walikuwa influenced na wanaume tu ila hawakufanya hayo kwa utashi wao kawadanganye wajinga wenzio, hakuna mwanamke atatoka huko ataanzisha utamaduni wa kuwaumiza wao wenyewe nimekuambia unipe faida ya mwanamke kukeketwa naona unarukaruka tu kama bisi kikaangoni
Still unapingana na ukweli kuwa hiyo ilikuwa ni idea na culture iliyotekelezwa na wanawake na sio wanaume. Sasa kama hautaki unataka nikwambiaje maana na wewe unaonekana kama sio ngariba basi ulikuwapo kwenye kamati za ukeketaji.
Nani alikudanganya kwamba wanaume wa zamani walitaka kuwazwa na wake zao wanaume kipaumbele chao kilikuwa heshima na ufahari, na kuenjoy tendo bila kujali wanawake wanajisikiaje kama wangekuwa wanahitaji kuwazwa, basi wasingekuwa wanaoa wanawake wengi in the first place maana hilo tu lilitosha kuwafanya wake zao wasiwawaze sababu ya wivu
Wewe haya uliyaonaje na wakati ukijibu unambie ni mfumo upi ulikuwa unaendesha hizi tabia na kwa faida ipi. Ukiona kitu kinafanyika nyuma yake huwa kuna mfumo.
Ndio maana nikakuambia kila jamii ilikuwa na tamaduni zake ambazo ziliwakandamiza wanawake katika namna tofauti tofauti sijasema kwamba jamii zote zilikuwa na utamaduni huo huo mmoja wa kukeketa ila ni kwamba tu sijaandika yote hapa, halafu mind you hapa siongelei tanzania tu naongelea tamaduni za kiafrica kwa ujumla ndio maana nikakupa huo mfano wa jamii huko somalia ambazo wanawake walioolewa walikuwa wanashonwa sehemu zao za siri pale waume zao wanaposafiri hadi watakaporudi, kuna jamii nyingine huko ethiopia mwanamke kabla hajaolewa analikuwa anatandikwa viboko hamsini vya mgongo kama ishara ya uvumilivu kwenye ndoa akishindwa kuvumilia hivyo viboko haolewi na akiweza ndio anaolewa yani hapo nimekutajia kwa uchache tu sasa wewe sijui ni jamii zipi unazoongelea ambazo wanaume waliwajali wanawake kiasi hicho unachosema
Sawa sasa shida ni kwann utumie minor case evidence kujustfy accusations za population yote. So wewe una tofauti gani na wale watu wanaowalinganisha waislam wote na magaidi kwasababu taleban na Al Qaeda wanajitangaza kwa dini yao, au unatofauti gani na wale wanaowatuhumu Kanisa katoliki na tuhuma za ma'priest wachache wa huko vatican wanaotuhumiwa kuwa molest watoto wa kiume? Jifunze kutengeneza kesi mahakamani utakuwa irrelevant.
Kama feminism ina hasara kwa wanawake mbona wao wenyewe hawatumii nguvu kubwa kuipinga kama mnavyofanya wanaume, nilishakuambia unitajie hasara za moja kwa moja za feminism kwa wanawake bila kuwahusisha wanaume ukaishia kunitajia zinazowahusisha wanaume, ninyi kubalini tu kwamba feminism ina hasara kwenu na si kwa wanawake sababu mnaiona kama threat dhidi ya mfumo dume ambao wanawake wengi wameanza kuukataa hivyo mmeamua kuwamalizia hasira wao halafu ndio mnaterm kama hasara kwao
Ni kama pombe na sigara wanaoipiga vita ni walevi wachache na wavuta sigara wachache wakishirikiana na raia wengine ambao hawajawahi kuvuta sigara wala kunywa pombe. Usitegemee victim wa tatizo ata raise voice kwenye kitu ambacho kina muendesha. Feminism imeandaliwa vema kitaalamu kuwashika akili wanawake wenye trauma na wanaume ambao hawajakamilika kisaikolojia. Mfano wewe hadi sasa haujaolewa na unaona ni sawa tu hizo ni akili za mtoto wa kike aliyesawa sawa?
Yani wamama wawafunze watoto wao wa kiume namna ya kuwanyanyasa wanawake hivi huwa unafikiria kwa kutumia makalio au, vijana walilelewa na mama zao ila haimaanishi wababa hawakuhusika kwenye malezi au unataka kusema huko kwenye majando nako wanaume walikuwa wanafundishwa na wanawake, kama wanawake wangekuwa wanafurahia yote waliyokuwa wanayafanya na kufanyiwa kwanini sasa waliachana nayo baada ya kuanza kupata elimu na uhuru kwanini wasingeyaendeleza kama hayo mambo waliona ni mazuri na yana faida kwao
Ipo hiyo ni phenomenon ya kisaikolojia. Umeshawahi kujiuliza wanaume wenye hasira sana,wanaopiga na kunyanyasa wanawake zao ni zao la malezi yapi?
Nambie mtaala wa JANDO ulikuwa ukifundisha vitu gani?
Nielezee vizuri kuhusu "UHURU" wa wanawake? Walikuwa wafungwa wa nani miaka ipi kwa sheria ipi na kipi kimebadilika sasa?
Yani unasema hakuna mwanaume alishawahi kutaka mwanamke adumu kwenye ndoa yenye manyanyaso halafu hapo hapo unasema unless huyo mwanaume ni sociopath kwamba unakataa hakuna hao wanaume au unasema wanaofanya hayo siyo wanaume sasa ni jinsia gani, kwahiyo wewe unabisha kwamba zamani hakukuwa na wanaume ambao walipiga wake zao halafu uko hapa unabishana na mimi ilihali huna unachokijua kuhusu jamii za zamani hata wakurya wenyewe tu hapo ukiwauliza watakuumbua maana kwa mujibu wa tamaduni zao wanadai mwanaume ni lazima ampige mke wake katika nyakati tofauti tofauti, na mbaya zaidi wakasambaza propaganda kwamba eti wanawake zao wenyewe ndio wanapenda kupigwa na kwamba wasipopigwa wanaona kama hawapendwi kumbe ukifuatilia ni wanaume zao wenyewe ndio waliowaaminisha kuwa mumeo asipokupiga hakupendi hivi kwa akili ya kawaida tu kuna binadamu anayefurahia kupigwa kwa namna yoyote ile hata wanyama wenyewe tu hawafurahii sembuse binadamu mwenye utashi
Sasa mimi sio mkurya na nina uhakika Tanzania na afrika nzima sio wakurya why unatulaumu na maamuzi ya wa kurya? Unatakiwa kuwa "very confused individual" ku frame wanaume wote kwa kipimo cha wachache.
Ila wanawake wa kikurya wenyewe personally husema wanapenda maugomvi. Na ni psychological issue, kama mtu alikua akiona baba na mama wanapigana na kutukanana 99% chances atarudia hiyo life style akiwa kubwa. Wanaita trauma bond. So yeah wanawake wa huko huwa wanataka kupigwa na sio kosa la wanaume ni kosa lao kushindwa kutafuta msaada wa kiakili kusaidiwa kufuta hiyo trauma. The world doesn't owe you sympathy.
Sasa kunyanyasika kwa mwanamke kunahusiana nini na kufa kwa mwanaume kwani ni wanawake ndio waliokuwa wanawaua hao wanaume, wanaume walikufa kwa sababu zao wenyewe ambazo nyingi zilihusiana na majukumu yao ila hilo halibadili ukweli kuwa waliwanyanyasa wanawake zao, na chanzo cha kuwanyanyasa ni kuona kama wanawake walifaidi kwa kufanya majukumu ya nyumbani tu ambayo wao wanaume waliyaona mepesi huku wao wakijiona wanafanya magumu
Unavyoona kwa jicho la ubinafsi na sisi wanaume tunatakiwa kutazama unachokisema kwa ubinafsi kama wewe. Sasa umeshindwaje kujiuliza why men die early at young age kwa magonjwa ambayo si ya kuambukizwa? So kwa mfano: watoto akiwa wanakufa sana before age 3 unataka wazazi especially mama hawatoonekana ni chanzo cha tatizo?
Hivi wewe mbona una bichwa gumu hivyo hebu nioneshe ni wapi niliposema wanawake WOTE walifanya kazi za nyumbani na za shamba nasisitiza nioneshe ni wapi mbweha we, mara ngapi nimekuambia hapa kwamba kila tamaduni nilizoongelea zilikuwepo kwa baadhi ya jamii na si zote na kwamba kila jamii ilikuwa na tamaduni zake tofauti zilizokandamiza wanawake katika namna tofauti, sasa unanibishia nini kwamba hakuna jamii za wanaume ambao ni unproductive wakati mimi nimejionea mwenyewe pamoja na kusimuliwa na wenyeji wa huko
Achana na ugumu wa bichwa langu komaa na mada. Gazeti lako lote linasema hivyo kwamba ni Wanawake wote walifanya hivyo. Halafu me sio mbweha me ni zemanda kudadadeki zako. So kwa mfano wanaume wa kichaga wa rombo ni walevi na wavivu je ni wanaume wa Kichagga wote wapo hivyo na tuwatazame kwa namna hiyo?
Niliwahi kuenda lushoto vijijini kikazi kuna vijiji ndani ndani huko wenyeji wakaniambia wanaume wa kisambaa wanaoishi kule bado wanaishi kijima na ni wavivu kazi yao kufanya na kuzalisha tu wanawake na watoto ndio wanaofanya kazi zote, na ni kweli kila tulikokuwa tunapita tunakutana na malundo ya wanawake na watoto wamebeba mikuni wanapandisha nayo milima na jiografia ya lushoto ilivyo ni milima mitupu kwanza sijui hata kama umewahi kufika kijiji chochote ndani ya hii nchi ukaona mazingira wanayoishi baadhi ya jamii, na hapo unakuta hao wote ni watoto wa familia moja wengi hawamalizi hata la saba ikitokea mmoja akafika la saba mzazi anamuambia we ukiweza kajibu vyovyote ujifelishe tu kwenye hiyo mitihani ya taifa maana hali ya nyumbani ndio kama unavyoiona hata ukifaulu hakuna anayeweza kukupeleka sekondari mwisho wa siku mtoto anafeli anabaki kufanya tu kazi za nyumbani na shambani na wanaobahatika kuja mijini wanaishia kuwa mahousegirl au kufanya kazi nyingine za unskilled labour
Ndio uone sasa tunapambana kila siku hapa wanaume washike usukani wewe unakuja na mawazo yako ya chai ya bange kubishana tunataka kutibu hilo tatizo. Hao wanaume unao waona hapo ni matokeo ya mfumo dhaifu wa malezi ya mtoto wa kiume ambao unamuacha mama kumjenga mtoto wa kiume bila principles za kiume. Mtoto wa kiume mwenye principles hawezi kukubali kuishi jamii ya namna hiyo inayotetea uvivu.
Sasa wewe na ubongo wako wenye shida eneo la "thinking combustion" unakuja na kusema huo ni mfumo dume. Boguz kabisa. Mfumo dume tokea lini ukalea magonjwa ya uvivu na umwinyi? Hayo ni matokeo ya mwanaume aliyekaa na wanawake muda mwingi tokea utotoni,akikua hawezi kujua namna ya kuwa mwanaume hata kidogo ataendelea kudeka tu. Wewe ukiona unasema mfumo dume,hebu toa upuuzi wako hapa kenge mwenye ufyele.
Yani labda itokee bahati tu mtoto afaulu akajiendeleza kielimu ndio anaweza kuja kufanya kazi ya maana ila the rest wanaishia kwenye cycle hiyo hiyo waliyopitia wazazi wao and mind you hapo naambiwa hayo naona kuna makundi ya wanaume wamekaa nje ya nyumba zao na wengine kwenye vilabu vya pombe, wako na misuli tu wanacheza bao na kunywa pombe na unaambiwa hiyo ndio kazi yao kuanzia asubuhi hadi jioni yani wao wamewekeza kwenye kutunza nguvu za kiume tu kwa ajili ya kufanya na kuzalisha watoto, hawana msaada wowote kwa wake zao wala watoto wao na hapa tunaongelea hii ni karne ya 21 vipi huko zamani ambako watoto wa kike walikuwa hawasomi kabisa unadhani jamii za aina hiyo zilikuwaje halafu wewe unabwabwaja hapa eti siwezi kuongelea mambo ya zamani kisa sikuwepo kwani kinachomatter ni mimi kuwepo au kinachomatter ni ukweli kuhusu hizo jamii husika
Ongelea ulichokiona ambacho umeshuhudia ila acha kuelezea kitu ambacho haukuwepo as if ulikwepo. Unatengeneza very strong accusations kwa wanaume as if ulikuwapo miaka hiyo kabla ya uhuru,huu ndio upuuzi ambao mimi na wewe tunagombana kila saa.
Nani kasema wanawake wanalazimishwa kuzaa kwanini unaniwekea maneno we mburura mimi nimesema wanawake wanalazimishwa kuzaa watoto wengi, sasa hao wanawake wanaozaa na waume za watu na hao wanafunzi wanaojikamatisha kwa dunia ya leo wanaishia kuzaa watoto wangapi au umekurupukia tu hoja yangu bila kuelewa, wanawake wengi dunia ya leo wanazaa watoto wachache na wapo ambao hawataki kuzaa kabisa ilihali wana uwezo au hili nalo unabishana we kilaza
Wewe umesema pale juu mimi nikuwekee maneno natoa wapi ujinga na pumba kama hizo kwenye akili yangu? Wewe unadhani haya magazeti unayoandika sisomi kwa umakini? Takataka kabisa 😒😒😒
Wanazaa watoto wachache si kwasababu ya complications za uzazi,muda mfupi wa uzazi sasa mtu anapata mtoto wa kwanza akiwa na miaka 30 unategemea azae wangapi? Kama wewe hapo hadi saa hii haujazaa unategemea kupata watoto 12 watokee wapi?
Umeona uje na takwimu zako za kubumba sasa hebu nipe takwimu za wanawake waliozaa watoto wachache na ambao hawajazaa kabisa wenye hayo magonjwa ya uzazi tulinganishe na ambao hawana hayo magonjwa, unapenda sana kuropoka wewe kwamba unadhani sisi wengine hatuoni yanayoendelea kwenye jamii ni wanawake wa ngapi leo hii wanazaa watoto saba na kuendelea, haya hao wenye watoto wachache au wasio na watoto kabisa ni wangapi wenye hayo magonjwa na ni nani kakuambia kwamba hao wanawake wenye watoto wengi ndio hakuna wanaopata hayo magonjwa hivi wewe unanichukuliaje mimi unahisi mi sifuatilii mambo au nabishana kuhusu nisiyoyajua kama wewe
Nenda kwenye mamlaka ya takwimu wapo pale posta watakupa takwimu. Ungekuwa muelewa ningeshare taarifa but kwasababu upo kubishana then wewe ujajua zaidi so kaproduce majibu yako mwenyewe. Umeshawahi kuona wapi wakili wa ' Plaintiff 'anategemea kupewa ushahidi wa kushinda kesi na wakili wa ' defendant '?🤔 Katafute data mimi nimekupa tu taarifa.
Hakuna aliyesema kuzaa ni jambo baya ila wanawake wanataka kuzaa watoto wachache wanaowamudu kuwalea na kuwahudumia tofauti na wanaume wengi wanaozalisha watoto kwa kutaka sifa tu na kuendeleza jina la ukoo, kwa taarifa yako kuna baadhi ya nchi huko ulaya wanawake wengi wamegoma kuzaa sababu ya wanaume kuwaachia majukumu juzi juzi hapa tulisikia rais ya north korea kim jong un pamoja na udikteta wake akilia mbele za watu kwenye hotuba yake akiwaomba wanawake wazae watoto wengi sababu birth rate nchini kwao inapungua, kwanza kwa dunia ya leo kuzaa watoto wengi ni uharibifu wa mazingira tu huyo aliyewadanganya kwamba dunia inatakiwa ijae yote sijui ni nani yani kwa akili ya kawaida tu mnashindwa kujua kwamba dunia bado inatakiwa iendelee kubaki na mapori ya kutosha kwa faida ya binadamu wenyewe binadamu wanaihitaji zaidi dunia kuliko dunia inavyowahitaji binadamu maana hakuna kiumbe mharibifu wa mazingira kama binadamu
Sio lazima utamke maneno kamili ila unaweza kuimply kwa kauli. Mimi nikisema wewe sio mzuri bila kusema wewe ni mbaya tayari namaanisha wewe ni mbaya.
Niondolee upuuzi wako wa The Clinton Foundation hapa maana ndipo upumbavu mnapotoa huko. Sasa watu wasizaliane dunia jamii itaendaje bila kuwa na replacement ya watu? Aliyekudanganya kuwa dunia inajaa ni nani, nendoa huko Amazon ndipo utajua kuwa dunia haijajaa.
Yani unabisha kwamba hakuna wanawake wasiopenda kuzaa wakati tunakutana na wanawake wengi wenye uwezo wa kuzaa ila hawana watoto na wana umri mkubwa tu hivi unaongelea jamii za wapi mbona unapenda kubishana na uhalisia we mbwiga, sasa umeshasema wanaume hawazai watoto wengi kwa sababu tu ya gharama za maisha ila si kwamba hawapendi yani ukiona mwanaume kakubali kuzaa watoto wachache ujue ni kwa sababu zilizo nje ya uwezo wake vinginevyo wanaume wengi wanapenda watoto wengi, na hata hiyo ya kusema gharama za maisha wala siyo sababu kwa baadhi ya wanaume maana hapa hapa mijini tunaona kuna maeneo huko uswahilini unakuta nyumba moja ina watoto saba na ni kaya masikini wazazi wanajifariji na misemo ya kijinga eti kila mtoto huja na ridhiki yake mwisho wa siku wanaanza kuilaumu serikali kuhusu elimu na ajira utadhani walitumwa kuzaa watoto wengi wasioweza kuwamudu
Ni wachache na sababu zipo wazi wanaogopa kuzaa nje ya ndoa, bila kuwa na baba wa mtoto serious na kukosa social support. Sio rahisi hivyo kama unavyodhani. Wewe kaa bila kuzaa halafu ufike 35 utaelewa kile kichaa cha kukosa mtoto na familia kikishakuvaa. Wewe unaongea tu subiri muda ufike,utanyamaza bila kunyamazishwa.
Kuwa na watoto wengi sio sababu ya umasikini, umasikini ni ukosefu wa mipango endelevu ya kutoka katika hali ngumu ya kiuchumi. Kukosa hela sio umasikini umasikini ni kukosa mbinu na mifumo ya kutengeneza mali na kuondokana na hali ngumu.
Sasa si ndio maana nikakuambia ukiona mwanamke kazaa watoto wengi ujue anaogopa kuachika au kuletewa watoto wa nje, ndio maana unaona ni ngumu wanawake ambao hawajaolewa kuzaa watoto wengi maana wanazaa kwa maamuzi yao tofauti na wanawake walio kwenye ndoa ambao wengi huzaa kwa matakwa ya waume zao kwa kuhofia wakikataa wataachwa au waume zao wataenda kuzaa nje ya ndoa, kuna uzi humu uliwahi kuanzishwa mtu aliuliza kati ya mume na mke nani mwenye maamuzi juu ya idadi ya watoto wanaume wengi wakasema anayetafuta pesa ndiye anayeweka sheria ndani ya nyumba which means ni mume wakasema kama mke atagoma kuzaa idadi ya watoto anayotaka mume basi akazalishe nje ya ndoa
Kupata watoto sio maamuzi ya mtu m'moja ni watu wawili na sababu zao binafsi kila m'moja. So no matter how unajaribu kujizungusha haifuti ukweli kuwa mwanamke anataka kupata watoto wengi na sababu zipo.
Kumtunza na kumjali mwanamke kulikuwa kwa aina gani huko au labda kama maana za hayo maneno zimebadilishwa siku hizi
Yani wewe una akili fupi sana sasa unafananisha hayo majukumu ya mara moja moja na majukumu ya kila siku hapa tunaongelea yale majukumu ambayo ni sehemu ya maisha ya kila siku wewe unaniletea habari za vita kana kwamba hizo vita zilikuwepo kila siku, kuhusu hayo majukumu kugharimu maisha ya wanaume mnasahau kwamba hata uzazi pia huwa unagharimu maisha ya wanawake au napo utabisha kwamba hakuna wanawake wanaokufa kutokana na changamoto za uzazi ila mbona bado wanaendelea kuzaa, tatizo lenu wanaume mnapenda kujitukuza na kuonekana mashujaa kwa majukumu ambayo ni wajibu wenu kuyafanya sababu ya maumbile yenu ila wakati huo huo hamtaki wanawake wajitukuze kwa majukumu yao ya kimaumbile yani mwanamke akisifiwa kwa kuzaa mnasema ni maumbile yake sababu mwanaume hawezi kuzaa, ila mwanaume anaona sawa kusifiwa kwa kufanya kazi ngumu ilihali maumbile yake yanamruhusu na hayo maumbile mwanamke hana kwanini msijisifie kwa yale majukumu yasiyo ya kimaumbile ambayo wanawake wanaweza kuyafanya ila hawataki tu kuyafanya, badala yake mnajisifu kwa majukumu ya kimaumbile hamuoni kama hiyo ni uneven comparison kwa mfano wanawake wanapojisifia kwa kufanya kazi za nyumbani wana haki sababu hayo siyo majukumu ya kumaumbile ni majukumu ambayo hata wanaume wanaweza kuyafanya ila hawataki tu na ninyi mna haki ya kujisifia kwa baadhi ya majukumu ya kutafuta pesa ambayo hata wanawake wanaweza kuyafanya ila hawataki and there you are even
Mwanaume akikupa sehemu ya kulala,chakula,na mavazi na kukutetea kwenye changamoto za kimaisha amesha timiza mambo ya msingi sana mengine ni ziada.
Akili zangu sio fupi ni ndefu,we umeshawahi kuziona wapi huo ufupi ukaupima?😒
Okay so kwenye hii paragraph point yako ilikuwa ni ipi maana umechanganua vitu vingi vya majukumu but sioni relevance. Anyways, moving on to the following paragraph..
Hayo masomo ya ufeminist umenifundisha wewe au hiyo syllabus umetunga wewe, sasa ni general facts gani unazotaka niongelee ikiwa kuna circumstances haziendani na hizo unazoita facts, bado una mengi ya kujifunza kuhusu mijadala na namna ya kujadiliana maana ukibanwa kidogo tu unaanza kulialia na kuja na visingizio vya kitoto
Unaonekana unasoma ufeminist maana sio kwa kuleta ligi na hoja za madaftari.
Hebu acha kunilisha maneno wewe, hata kama ni kweli angekuwa hana mchango kwahiyo ulitaka nisiseme, stop being like a mindless sea urchin
So hana mchango,we mtoto utapata laana.
Sasa mbona unanisema mimi kwa kuchukua sehemu ndogo ya jamii na kuifanya general topic na wakati wewe mwenyewe umefanya kitu hicho hicho, unatolea mfano wa jamii moja ya wanawake kubebesha mimba wanawake wenzao hapa tunaongelea tamaduni original za kiafrika za mwanaume kuoa wake wengi na kuwazalisha watoto, na kuonesha jinsi gani huna research ya kutosha kuhusu unachokibishania hata huo mfano uliotoa siyo sahihi wanaofanya hilo siyo wamakonde bali ni wakurya ila hata kwa akili ya kawaida tu unawezaje kufananisha kile ninachoki point out mimi toka kwenye jamii mbalimbali na hiki ulichoki point out wewe toka kwenye jamii moja
Nimekaa mtwara ndio maana najua wewe umesoma kwenye machapisho ya makaratasi sasa unabishana na macho yangu,ebo wewe umetumwa. Sasa nikikwambia mlima Kilimanjaro upo Dar si utaniplbishia wewe kuwa upo mkoani Kilimanjaro tu na wakati nimeuona kwa macho yangu pale external.
Bora mimi walau siyo mnafiki mimi huwa nayasema maovu yote ya wanaume na wanawake na huwa nasisitiza kila jinsia ibadilike kwa nafasi yake tofauti na ninyi kwanza watu wanafiki kama wewe ni hatari kwa jamii wewe ilitakiwa utandikwe viboko ukiwa uchi kisha ufungwe jiwe kubwa utupwe baharini, ninyi wanaume ndio wa kwanza kuharibu jamii kwa kisingizio eti ninyi hampati madhara yani mnayasemea maovu ya wanawake ila mnatetea maovu yenu halafu mnajidai eti mnarekebisha jamii hivi kwenye suala linalohusisha jinsia mbili unawezaje kusema unarekebisha jamii kwa kukemea jinsia moja na kusifia nyingine, yani mnasingizia eti wanawake ndio wanaopata madhara ya haya matokeo wakati kiuhalisia tunachokiona ni lundo la wanaume kulalamika na kulialia kwa sababu ya kukosa wake wema wenye sifa wanazozitaka ilihali wao ndio wamechangia hao wanawake kukosa hizo sifa what kind of hypocrisy is this
Nionyeshe uzi wako m'moja ambao umewasema wanawake kwa maovu yao? Hakuna kutetea maovu ila kuna kujustfy the misconceptions kwenye jamii juu ya matendo ya kiumeni. Wewe unaweza ona uovu ila ndani hakuna nia ovu.
Hapana bana kwamba unahisi mimi ni mgeni wa kusoma hizi pumba zako na mashudu yako, mara ngapi huwa unaanzisha nyuzi kuhusu sijui hatua wanazopitia mabinti wa kisasa halafu unaandika kana kwamba ni mabinti wote wa kisasa wanapitia hatua hizo, wadanganye wengine ila sisi tunaojua kusoma between the lines tunajua huna lolote ndio wale wale tu misogynists mliojificha kwenye mwamvuli wa kubadilisha jamii na kusaidia wanawake
Nachofurahi kuwa unasoma nondo zangu na zinakujenga ingawa hauta admit wazi wazi you ungrateful little wisked weasel from the zoo. Mimi siwezi kuwa misogynistic halafu at the same time nipambanie watoto wakike kubadilika wawe watu bora.
The joke is on you kujifanya unatetea wanawake but unatetea umalaya/ udangaji ,kuzaa nje ya ndoa,unapinga ndoa, unataka wanawake wawe wabinafsi, hupendi familia, unawatazama wanaume kama washindani wako na maadui, wewe ndio true definition ya mtu anayechukia wanawake na kuwa mwanamke. Ukiendelea hivi utakuja kuwa kichaa fresh mbeleni huko nakwambia tena.
Sasa kama unaona hao wanaume waliozaliwa na single mothers na wanakuwa against na single mothers ni mashujaa kwanini usione na wanawake ambao wamezaliwa na wababa wabinafsi na wanakuwa against wababa wabinafsi nao ni mashujaa, umenikazania hapa kusema eti sitakiwi kuyasema maovu ya wanaume kisa eti baba yangu naye ni mwanaume mara sijui akiona haya atajisikia vibaya ila hapo hapo unaona ni sawa wanaume kuyasema maovu ya wanawake ilihali hata mama zao ni wanawake mbona unakuwa so biased and prejudiced wewe, ndio maana huwa nasema acheni unafiki ninyi ni wanafiki kama wanafiki wengine tu no wonder wanawake hawasikilizi hizi propaganda zenu maana wanauona huu unafiki wenu mnasingizia eti hawana akili za kujua zuri na baya kwao kumbe wanazo sana na wanajua fika wanachokifanya siku wanaume mkiwa tayari kuanza kubadilika ndipo mrudi kwa wanawake muwaambie nao wabadilike vinginevyo kwa sasa tuendelee hivi hivi tutakuja kuelewana hapo baadaye ninyi si mnajifanya vichwa ngumu bana
Kwasababu ni wanawake wa kisasa wanaopambana kumtenganisha baba na mtoto kisa mwanaume hana kipato anachotamani yeye kuwa nacho au kuna life style ambayo mwanaume hajampa ndio ugomvi huanzia hapo. Kwa style hiyo ni sawa hawa watoto wakiume kuwachukia mama zao maana na wao wanakuja kupitia the same fate and therefore wanawaelewa baba zao walipitia nini kwa mama zao.
Huwezi kusema the similar case kwa watoto wa kike kuwachukia baba zao.
Wewe hebu sikiliza, wanawake wa sasa ni chanzo kikubwa sana cha mipasuko na mtawanyiko wa familia na utengano wa baba na watoto wake.
Muulize mwanaume yoyote hata baba yako na kaka yako watakwambia kuwa familia ndio chachu ya maendeleo kwao na kwa mwanaume kuwa na familia ni muhimu kumpa sababu ya kujijenga na kuwa mtu bora.
Wanawake on the flip side wanatumia watoto na wanaume kama chanzo cha mapato kujikimu kwa shida na mahitaji yao. Huwezi kuta mwanamke wa kisasa analinda familia for the same ya familia sababu wanachukia kazi na maagizo ya MUNGU wanaabudu shetani masaa 24.
Wewe hapo tu hadi saa hii hauna familia ni sista wewe? Hufanyi mapenzi? Kwann haujaolewa? Wazazi wako ni masikini,una shida gani? Huwezi nambia kitu wakati shughuli zako ni za mpinga kristo wewe. Mimi huwa sichezewi akili kirahisi hivyo.
Mimi hapa tunagombana ila nina mwanamke wangu and ninaishi nae vizuri tunaelewana. Na nina muona mzuri sana na anajua ninampenda sababu nilimchagua na akakubali hakuniletea ushubwada.
Wewe kwann hadi sasa hauna familia yako,kwann hauolewi kazi ni kumfanyia shetani kazi yake ya kutoa kauli na maneno za ujenzi wa jamii ya masingle mother, wanawake wadangaji wanaojali pesa tu na sio utu, unachukia uzazi , unaopa kuona familia ya baba, mama watoto wengi, Firimasoni mkubwa wewe shindwaaaaaaaaa shetani tokapaaaaaaaaaaah 👺👺👺