Je wewe ulikuwepo enzi hizi?
Ukweli nimepata, niliyoyasikia sikudanganywa oooh.
Kumbe huko Gabon umeshaolewa na mtu mwingine.
Nasema nasikitika kwani ulichokifanya ni cha dhuluma ooh,
Wazimu si wazimu huku nimebaki nalia moyoni.
Sasa ufanye hima uwatumie barua wazazi wako oooh,
Warudishe mahari yangu ili niweze tafuta mchumba mwingine.
.....Nawaarifu ndugu zangu wote,
.....Harusi hii imevunjika jama
.....Niliyetaka kumuoa,
.....Amenikatalia bila kosa mwenzenu
Mkuu,PJ hembu nikumbushe huu wimbo uliimbwa na bendi gani kaka? kwakua umenikuna sana maneno yake!