BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,376
- 8,120
''Msimamo wetu bado ni huo, kutokana na mazingira tuliyopitia mwaka 2019 na mwaka 2020 yalitudhihirishia wazi kwamba hatutashiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka huu (2024) kutokana na yale yaliyotokea yanatupa hofu kwenda kushiriki Uchaguzi tena, lakini kama kuna mambo yatabadilika na Miswada ikiwemo vipengele vya Katiba vinavyokwaza uchaguzi kuwa huru sisi tutakuwa tayari kushiriki uchaguzi" -Heche
John Heche ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA amezungumza hayo wakati akifanya mahojiano maalumu na EATV kupitia Kipindi cha Ahadi Timilifu leo, Jumatatu Januari 15.2024