Hayati Mzee Ali Hassan Mwinyi kuzikwa tarehe 2 badala ya siku ya kesho ndani ya masaa 24 ni kukiuka mazishi ya kiislam. Napendekeza ratiba ibadilishwe

hakuwa kiongozi wa familia
ni kiongozi wa taifa

swala la kuzikwa mapema halipo


ntaungana na weee kwa chikwite huyu masaa matatu mengi sana wakichelewesha
 
Hayati Mzee Ali Hassan Mwinyi kafariki saa 11 na nusu jioni ya leo tarehe 29/2/2024 hivyo kwa taratibu za kiislam inabidi azikwe kesho 01/03/2024 kabla ya saa 11 na nusu jioni, ikipendeza zaidi ilibidi iwe kesho asubuhi au mchana


Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayra رضى الله عنه akisema: Amesema Mtume ﷺ : “Harakisheni mazishi! Kwani kama maiti ni mja mwema basi haifai kumchelewesha, na kama ni mja muovu basi ni shari na balaa mnaweka mabegani mwenu.
Muttafaq Alayhi.

951. Imepokewa kutoka kwa Huswayn bin Wahwah akisema: “Aliumwa Twalha bin al-Baraa’ bin ‘Azib akatembelewa na Mtume nyumbani kwake. Baada ya kumuona, alisema: “Naona mwisho wa maisha ya Abu Twalha unakaribia, hivyo akifariki nijulisheni, na harakisheni kumtayarisha kumzika; kwani haifai kuachwa mzoga wa mwili wa Mwislamu kusalia nyumbani na familia yake” Ameipokea Abu Daud.
Sasa mkuu kama ni hivyo,hata huyo no, moja hakutakiwa kuwa hapa alipo maana dini hailuhusu mwanamuke kua kiongozi mkuu kama hivyo,na hata mwenyewe anajua,na viongozi wa dini kitaifa na dunia wanajua hata bakwata wanajua,mambo mengine ni ya kuacha yaende wewe endelea kusaka ugari wa family yako.
 
Alibdi azikwe Ahsubui mapema Sana .

Wamefanya makosa kwenye UPANDE huu ilibidi hadi muda huu awe ameshazikwa
 
Umepotoka mwili wa Mwinyi uko Hospital sio nyumbani kwa familia yake

Hicho kifungu Kilihusu miaka hiyo ambayo hakukuwa na hospitali wala mortuary maiti zilikuwa zinakuwa nyumbani kwenye familia zao

Kwa Hospital na mortuary muislamu aweza zikwa hata baada ya mwezi hata baada ya mwaka hajakiuka hicho kifungu
Kwa kauli hii jaribu walau kuficha upumbavu wako 👇👇

Kwa Hospital na mortuary muislamu aweza zikwa hata baada ya mwezi hata baada ya mwaka hajakiuka hicho kifungu
 
Huzikwi bila Daktari,kuthibitisha kifo.Na pia toka zamani wapo wanaojua kwa njia za kienyeji,kama mtu ameshafariki au bado.Hata wewe ukifundishwa,unaweza kuelewa.Fikiria wakristo wa zamani,wakati hakuna majokofu,hakuna madaktari wa kisasa,wafu walizikwa vipi.
Huko vijijini mtu anakufa saa 4 saa 10 wameshamzika na hamna doctor je kama amezimia
 
Hayati Mzee Ali Hassan Mwinyi kafariki saa 11 na nusu jioni ya leo tarehe 29/2/2024 hivyo kwa taratibu za kiislam inabidi azikwe kesho 01/03/2024 kabla ya saa 11 na nusu jioni, ikipendeza zaidi ilibidi iwe kesho asubuhi au mchana


Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayra رضى الله عنه akisema: Amesema Mtume ﷺ : “Harakisheni mazishi! Kwani kama maiti ni mja mwema basi haifai kumchelewesha, na kama ni mja muovu basi ni shari na balaa mnaweka mabegani mwenu.
Muttafaq Alayhi.

951. Imepokewa kutoka kwa Huswayn bin Wahwah akisema: “Aliumwa Twalha bin al-Baraa’ bin ‘Azib akatembelewa na Mtume nyumbani kwake. Baada ya kumuona, alisema: “Naona mwisho wa maisha ya Abu Twalha unakaribia, hivyo akifariki nijulisheni, na harakisheni kumtayarisha kumzika; kwani haifai kuachwa mzoga wa mwili wa Mwislamu kusalia nyumbani na familia yake” Ameipokea Abu Daud.
Ili muda wa maziko ya kiisilamu usikiukwe usingeleta mapendekezo ambayo yangesababisha majadiliano ambayo yangeongeza muda wa ukiukwaji wa kanuni bali ungeleta ratiba ya maziko ya ndani ya muda sahihi.
 
Uislam wa siki hizi ,huyo samis alienda makaburini chato kumzika jpm niloshamgaa sana
Uongozi wa nchi zisizofuata sheria za Dini ni ngumu sana
Ukikubali kuwa kiongozi basi na dini haumo tena FACT
Ndio maisha unayochaguliwa na kukataa hiwezi
Huoni mpaka Vatican kaenda halafu huwa hawasemi walienda kufanya nini
 
Unashangaa kwa mwanamke wa kiislam kwenda makaburini?

Vipi hili la mwanamke huyo huyo kuongoza wanaume, halikushangazi?

Uislam halisi waachiwe Taleban, hawa Waislam wa bongo hawapo chini ya sharia.
Nakumbuka zamani wasaudi walikuwa hawataki kuona kiongozi mwanamke na walimkataza kabisa waziri mkuu wa zamani wa Pakistan kuingia kwao
Ila siku hizi utafikiri wamebadili dini
 
Unaweza kuweka angalau aya au kifungu cha sheria hiyo ya kiislam kuipa nguvu hoja yako. Mambo ya imani yanataka vyanzo sio utamaduni.

Kwa ufahamu wangu huo ni utamaduni wa watu wa mashariki ya kati, waarabu na wayahudi. Ndio maana Yesu, Anania na Safira, watu wa mashariki ya kati walizikwa ndani ya 24hrs. Ni utaratibu ninaoupenda maana unasaidia kumpunguzia aliye hai machungu.
Mwanadamu ni mavumbi arudishwe mavumbini alikotoka kwa wepesi.
Na ikumbukwe kipindi hicho hakukuwa na majokofu ya kuhifadhia maiti kwa hiyo waliharakisha miili isije kunuka ndani
 
Nakumbuka zamani wasaudi walikuwa hawataki kuona kiongozi mwanamke na walimkataza kabisa waziri mkuu wa zamani wa Pakistan kuingia kwao
Ila siku hizi utafikiri wamebadili dini
Wanafiki hao , wanabadilika kama vinyonga. Ni wapi kwenye Quran mmeambiwa msichangamane na wanawake? Hija tu wanakuwa pamoja huku wanaume wakiwa vifua wazi.
 
Kwenye nukuu zako Kuna common phrases zimetumika, "haifai kumchelewesha" na harikisheni maziko", SWALI ni muda gani umeainishwa hapo wa kumchelewesha Marehem? Nadhani suala la kumchelewesha na kuwahisha linaendelana na mazingira pia
Halafu hizo ni hadithi, sijui kina Abuhuraia, yaani mpaka sasa tuchukue mawazo ya watu walioishi miaka ya ujima? Loh
 
Sasa mkuu kama ni hivyo,hata huyo no, moja hakutakiwa kuwa hapa alipo maana dini hailuhusu mwanamuke kua kiongozi mkuu kama hivyo,na hata mwenyewe anajua,na viongozi wa dini kitaifa na dunia wanajua hata bakwata wanajua,mambo mengine ni ya kuacha yaende wewe endelea kusaka ugari wa family yako.
Hebu nionyeshe mstari mmoja wa QURAN unaosema mwanamke asiwe kiongozi? Hao hao viongozi wa dini wanampamba kweli kweli mbona hawajawahi kulisema hili?
 
Hayati Mzee Ali Hassan Mwinyi kafariki saa 11 na nusu jioni ya leo tarehe 29/2/2024 hivyo kwa taratibu za kiislam inabidi azikwe kesho 01/03/2024 kabla ya saa 11 na nusu jioni, ikipendeza zaidi ilibidi iwe kesho asubuhi au mchana


Imepokewa kutoka kwa Abu Hurayra رضى الله عنه akisema: Amesema Mtume ﷺ : “Harakisheni mazishi! Kwani kama maiti ni mja mwema basi haifai kumchelewesha, na kama ni mja muovu basi ni shari na balaa mnaweka mabegani mwenu.
Muttafaq Alayhi.

951. Imepokewa kutoka kwa Huswayn bin Wahwah akisema: “Aliumwa Twalha bin al-Baraa’ bin ‘Azib akatembelewa na Mtume nyumbani kwake. Baada ya kumuona, alisema: “Naona mwisho wa maisha ya Abu Twalha unakaribia, hivyo akifariki nijulisheni, na harakisheni kumtayarisha kumzika; kwani haifai kuachwa mzoga wa mwili wa Mwislamu kusalia nyumbani na familia yake” Ameipokea Abu Daud.
Omari ali juma alizikwa baada ya masaa24??
 
Wanafiki hao , wanabadilika kama vinyonga. Ni wapi kwenye Quran mmeambiwa msichangamane na wanawake? Hija tu wanakuwa pamoja huku wanaume wakiwa vifua wazi.
Hapana boss kwa Hijja imeruhusiwa kidini, ila kwa sasa wanajifanya wameendelea na vikwazo vingi wanavikwepa
Yes ni wanafiki maana viongozi wa dini hawana nguvu
 
Back
Top Bottom