Emanueli misalaba
JF-Expert Member
- Dec 12, 2016
- 2,931
- 4,010
Arsebert Ngurumo kundi analolituhumu kwani lina milki dola?Kuna matatizo makubwa sana katika kujadili hoja siku hizi.
Hoja ya msingi yaweza isijadiliwe kukaanza mashambulizi binafsi kutokana na hisia juu ya mtu huyo.
Mie nilidhani watu wangepuuza mengine wakajihoji kuhusu issues zifuatazo hapo;
1. Imekuwaje kampuni ya udalali ya YONO kunyang'anywa leseni kabla haijatekeleza hukumu? Nani yuko nyuma ya hili?
2. Jee kuna ukweli wa fedha nyingi kukutwa a/c ya Dr Bashiru Kakulu na kuwa frozen? Kwa nini ziwe frozen? Kazitoa wapi na alishirikiana na nani kwenye wizi huo kama ni wizi? Una freeze fedha za mwizi halafu unamuacha kwenye utumishi wa umma?
3. Jee hayo mapesa na mali kuna uhusiano gani na yale ya BOT ambayo Rais aliagiza uchunguzi tena kwa kuunda tume lakini hakuna taarifa iliyotoka wazi bali imeacha tetesi zinazo mhusisha pia mtu mwenye nafasi nyeti sasa alipokuwa wizara ya Hazina.
4. Jee kweli hilo kundi alilosema bado lipo kumbe? Usalama wa viongozi wetu ukoje kama wanaweza kufanya lolote?
Ndiyo ya kujiuliza na kujadili kwa upendo sio kuendekeza chuki na visasi na kuwaacha wachache wanafaidi matunda ya nchi huku wakisoma JF na kutucheka tuu
Kama kipindi kile linamiki dola na lilikuwa na mamlaka yote lilishindwaje kumuua Membe lije limuue kipindi hiki ambacho alina nguvu?