NGULI
JF-Expert Member
- Mar 31, 2008
- 4,803
- 637
Niko kijijini kwetu kwa vacation nilikuwa sijafika kwa miaka 2 nimefurahi kukuta maendeleo ambayo ni mazuri kwa mfano barabara ina kiwango cha lami hadi karibu na mpakani.
Ila kilichonishangaza ni hizi nyumba za kifahari kali kuliko hata baadhi ya nyumba za maeneo ya masaki na O'bay ambazo hazina wapangaji wala mtu anayeishi, unakuta nyingi zina babu na bibi ambao wanafanya usafi na kuitunza. Kwa mtazamo wangu tungejenga rum 2/3 kwa ajili ya siku kuu za xsmas na mwaka mpya na hizo hela zikafanya mambo mengine. najua huku kuna mashule na hospital basi tusaidie wengine/wa eneo tofauti. Baadhi ya hizi nyumba zingekuwa zinabebeka zingekuwa dispensary maeneo mengine au hata hospitali za rufaa.
Hapa kijijini kwetu raha kweli ukiwa padre unaheshimika kuliko hata waziri wala mmbunge. Ukisoma seminary ukaacha unaweza pewa radhi na bibi yako...huku padre anaitwa mopiaa....raha kweli.
Kuna makanisa yenye kengele ambazo ingekuwa dar ikipigwa ule mchana kwa mfano st. Peters wangesikia hadi bagamoyo. Ikipigwa hata kama mtu anakunywa/ria pombe ya mbege anaacha na kusali sala ya malaika/anjelusi hata kama amelewa ulevi unakata then unarudi upya baada ya sala.
Kijijini kwetu kweli raha bado mambo ya ndizi na matunda.
Kilichonishangaza zaidi ni kuwa makao makuu ya mkoa kuna gym 1 tena ina masharti magumu sana kuweza kufaidi huduma hio. Zilizokuwepo zote zimefungwa na sijapata sababu ya msingi ila nahisi ni demand kuwa ndogo.
Je kijijini kwako?
Ila kilichonishangaza ni hizi nyumba za kifahari kali kuliko hata baadhi ya nyumba za maeneo ya masaki na O'bay ambazo hazina wapangaji wala mtu anayeishi, unakuta nyingi zina babu na bibi ambao wanafanya usafi na kuitunza. Kwa mtazamo wangu tungejenga rum 2/3 kwa ajili ya siku kuu za xsmas na mwaka mpya na hizo hela zikafanya mambo mengine. najua huku kuna mashule na hospital basi tusaidie wengine/wa eneo tofauti. Baadhi ya hizi nyumba zingekuwa zinabebeka zingekuwa dispensary maeneo mengine au hata hospitali za rufaa.
Hapa kijijini kwetu raha kweli ukiwa padre unaheshimika kuliko hata waziri wala mmbunge. Ukisoma seminary ukaacha unaweza pewa radhi na bibi yako...huku padre anaitwa mopiaa....raha kweli.
Kuna makanisa yenye kengele ambazo ingekuwa dar ikipigwa ule mchana kwa mfano st. Peters wangesikia hadi bagamoyo. Ikipigwa hata kama mtu anakunywa/ria pombe ya mbege anaacha na kusali sala ya malaika/anjelusi hata kama amelewa ulevi unakata then unarudi upya baada ya sala.
Kijijini kwetu kweli raha bado mambo ya ndizi na matunda.
Kilichonishangaza zaidi ni kuwa makao makuu ya mkoa kuna gym 1 tena ina masharti magumu sana kuweza kufaidi huduma hio. Zilizokuwepo zote zimefungwa na sijapata sababu ya msingi ila nahisi ni demand kuwa ndogo.
Je kijijini kwako?