Bata Boy Official
JF-Expert Member
- Sep 19, 2019
- 259
- 308
Wakuu natumai mko poa kabisa
Mimi ni kijana ambaye nimeamua kuwa muwazi kuwa asiyekubali kushindwa si mshindani.
Jiji la Dar es Salaam limenishinda, Nimekubali na sitaki tena maisha ya jiji lolote. Sina degree, diploma wala cheti chochote, pesa yote niliyokuwa najichanga mwisho wa siku inaishia kwenye Kodi, umeme, maji, usafi, ulinzi, taka, chakula, na kulipa madeni. Sasa huu mchezo nimeuchoka. Maana hii ni mark-time, hakuna chenye nna fanya, hata zile raha za jiji wanazozisema sizifaidi maana nikisema nitenge 30k au 50k nikale Bata, ohoo nimeishaa...siioni future kabisa.
Hivyo wakuu nimeamua kwenda kijijini kushika jembe kulima kwa bidii na uaminifu, na kuishi maisha ya chini kabisaa...maisha yangu ikibidi niyamalizie huko huko kabisa. Kusali, kulima, kula, kulala ivyo yaan.
Kwahiyo wanajukwaa naombeni kwa ambaye ni mkulima au anamashamba huko vijijini, au ni mwenyeji wa mikoa ya kilimo sana na ameelewa hali yangu naomba anipokee , hata kama hakuna umeme, au nyumba ya kulala...nipo tayari kulala hata kwenye mahema nje humo humo mashambani endapo hakuna wanyama wakali lakini.
Hata kama sitalipwa pesa yoyote, ilimradi nipate chakula na niwe na amani ya moyo inatosha kabisa. Maana jiji limeninyoosha.
NB: Sijayakatia tamaa maisha, nimelikatia tamaa jiji.
Asanteni sana kwa maoni na michango yenu mnayoenda kuitoa.
Mungu azidi kutupa Amani na Upendo na Mshikamano.
Mimi ni kijana ambaye nimeamua kuwa muwazi kuwa asiyekubali kushindwa si mshindani.
Jiji la Dar es Salaam limenishinda, Nimekubali na sitaki tena maisha ya jiji lolote. Sina degree, diploma wala cheti chochote, pesa yote niliyokuwa najichanga mwisho wa siku inaishia kwenye Kodi, umeme, maji, usafi, ulinzi, taka, chakula, na kulipa madeni. Sasa huu mchezo nimeuchoka. Maana hii ni mark-time, hakuna chenye nna fanya, hata zile raha za jiji wanazozisema sizifaidi maana nikisema nitenge 30k au 50k nikale Bata, ohoo nimeishaa...siioni future kabisa.
Hivyo wakuu nimeamua kwenda kijijini kushika jembe kulima kwa bidii na uaminifu, na kuishi maisha ya chini kabisaa...maisha yangu ikibidi niyamalizie huko huko kabisa. Kusali, kulima, kula, kulala ivyo yaan.
Kwahiyo wanajukwaa naombeni kwa ambaye ni mkulima au anamashamba huko vijijini, au ni mwenyeji wa mikoa ya kilimo sana na ameelewa hali yangu naomba anipokee , hata kama hakuna umeme, au nyumba ya kulala...nipo tayari kulala hata kwenye mahema nje humo humo mashambani endapo hakuna wanyama wakali lakini.
Hata kama sitalipwa pesa yoyote, ilimradi nipate chakula na niwe na amani ya moyo inatosha kabisa. Maana jiji limeninyoosha.
NB: Sijayakatia tamaa maisha, nimelikatia tamaa jiji.
Asanteni sana kwa maoni na michango yenu mnayoenda kuitoa.
Mungu azidi kutupa Amani na Upendo na Mshikamano.