Karibu sana drphone, ukweli utakula kuku mpaka ukumbuke mboga za majani, maana kijijini kwetu mgeni hapewi mboga za majani mpaka aombe
Kijijini kwetu hakuna mabadiriko sana tangu nilipoondoka miaka 4 iliyopita. Lakini kubwa nililoona kuwa kuna ongezeko kubwa la watu. Kwani kutokea makao makuu ya wilaya kwenda kijijini kwetu usafiri bado ni ule wa Mandolin (Landrover 109) na kutokana na wingi wa watu gari hii hubeba watu mpaka sehemu ya mbele ya gari kwa nje (kwenye boneti) na dereva anaachiwa kajinafasi tu ka kuona njia.
Kijijini kwetu umeme bado ni hadithi kubwa, lakini kuna bwana mmoja nimeambiwa ni nduguye "Mathawe, Temba, Mushi na Kimario" jamaa ameweka jenereta yake na kila siku usiku hufanya maonyesho ya sinema kwa kiingilio cha sh.200 kwa kila mtu. Pia huyu bwana amefanya watu wa kijijini kwetu kupata bia na soda za baridi kwa kuwa ana jokofu linalotumia nishati ya mafuta ya taa.
Kijijini kwetu maji ya kunywa, kuoga na kufua ni yale yale ya rangi ya madhiwa (maji ya kisima) na ili kuwza kupata angalau ndoo 2 shurti uamke saa 10 usiku.
Mawasiliano bado ni tatizo nimeambiwa kijijini kwetu ukitaka kuongea na simu au kupigiwa simu kwa muda ulioahidiwa basi unatakiwa kwenda kwenye kichuguu mbele ya nyumba ya mwalimu mkuu, ingawa nimesikia kuwa huyu mwalimu ameamua kufunga mbwa ili kudhibiti udokozi maana juzi juzi aliibiwa gunia la mtama na anahisi ni wale wale wanaojidai wanakwenda kutafuta mawasiliano.
Nilibahatika kukutana na mbunge wa jimbo letu na katika mazungumzo huyu bwana hakuzungumzia kabisa jinsi anaweza kutuletea maendeleo kijijini kwetu zaid ya mikakati aliyonicholea ya kutaka kutetea kiti chake kwa kuwa tu amesikia kuna watu wanataka kugombea nae.
Kimsingi kijijini kwetu hata suala la afya bado kabisa kuna mzee Madaraka ambaye tangu nikiwa mdogo nilikuwa namfahamu kwa kuwatibu watu kwa dawa za mitishamba ndio mpaka leo anaendelea kuwatibu watu.Zahanati iko takribani kilometa 5. Pale kwenye shule mwalimu mmoja ambaye tulisoma nae shule ya msingi ananiambia kuwa shule ina mwaka wa 6 haijatoa hata mwanafuni mmoja kwenda kidato cha kwanza. madai yake ni kuwa serikali imewavunja moyo kiasi kwamba morali ya kazi hakuna. Mwisho wa mwezi mshahara ukitoka walimu wote wanakuwa makao makuu aya wilaya kufata mishahara shule inasimamiwa na mwenyekiti wa kijiji iliupokea wageni wanaoweza kuja shuleni.
@nguli
mkuu umeniacha hoi alafu sikujua kama na ww ni mchaga yani kama ukienda machame uuwiiii yaniutashindwa kuelewa kama upo kijijini utafikiri upo obeyi tatizo kijijini kwetu vijana wamepungua sana na wapo busy sana kuchimba makaburi karibu kila siku watu wanapandishwa kuzikwa kwenye nyumba ya milele
Woo Dr, neewe ni Mmashami da? Mbakwi?
Nimefurahi sana kusikia habari za vijiji vingine vilivyo nilikuwa nacheka sana na sehemu nyingine nimesikitika kwa mfano swala la watu kuzika kila siku ni la kweli na hata hapa kijijini kwetu naona limeshika hatamu.
Wapi Xspin na Sipo sijapata za vijijini kwenu.
picha jamani, acheni stori wekeni imeji tuone! kwetu bado choka tu, vijana niliocheza nao utotoni wameshazeeka vibaya, tena wamechakaa
Mbunge wa uko kwenu anaitwa nani, hapa ni wazi kuwa umeshampigia kampeni ya kutosha dhidi ya wapinzani wakeNiko kijijini kwetu kwa vacation nilikuwa sijafika kwa miaka 2 nimefurahi kukuta maendeleo ambayo ni mazuri kwa mfano barabara ina kiwango cha lami hadi karibu na mpakani.
Niko kijijini kwetu kwa vacation nilikuwa sijafika kwa miaka 2 nimefurahi kukuta maendeleo ambayo ni mazuri kwa mfano barabara ina kiwango cha lami hadi karibu na mpakani.
Ila kilichonishangaza ni hizi nyumba za kifahari kali kuliko hata baadhi ya nyumba za maeneo ya masaki na O'bay ambazo hazina wapangaji wala mtu anayeishi, unakuta nyingi zina babu na bibi ambao wanafanya usafi na kuitunza. Kwa mtazamo wangu tungejenga rum 2/3 kwa ajili ya siku kuu za xsmas na mwaka mpya na hizo hela zikafanya mambo mengine. najua huku kuna mashule na hospital basi tusaidie wengine/wa eneo tofauti. Baadhi ya hizi nyumba zingekuwa zinabebeka zingekuwa dispensary maeneo mengine au hata hospitali za rufaa.
Hapa kijijini kwetu raha kweli ukiwa padre unaheshimika kuliko hata waziri wala mmbunge. Ukisoma seminary ukaacha unaweza pewa radhi na bibi yako...huku padre anaitwa mopiaa....raha kweli.
Kuna makanisa yenye kengele ambazo ingekuwa dar ikipigwa ule mchana kwa mfano st. Peters wangesikia hadi bagamoyo. Ikipigwa hata kama mtu anakunywa/ria pombe ya mbege anaacha na kusali sala ya malaika/anjelusi hata kama amelewa ulevi unakata then unarudi upya baada ya sala.
Kijijini kwetu kweli raha bado mambo ya ndizi na matunda.
Kilichonishangaza zaidi ni kuwa makao makuu ya mkoa kuna gym 1 tena ina masharti magumu sana kuweza kufaidi huduma hio. Zilizokuwepo zote zimefungwa na sijapata sababu ya msingi ila nahisi ni demand kuwa ndogo.
Je kijijini kwako?
@nguli
mkuu umeniacha hoi alafu sikujua kama na ww ni mchaga yani kama ukienda machame uuwiiii yaniutashindwa kuelewa kama upo kijijini utafikiri upo obeyi tatizo kijijini kwetu vijana wamepungua sana na wapo busy sana kuchimba makaburi karibu kila siku watu wanapandishwa kuzikwa kwenye nyumba ya milele