Youth Worker Tanzania
Member
- Nov 2, 2020
- 68
- 90
Wakuu Habari,
Nimeona nikushirikishe wewe kijana mwenzangu ambae bado uko Chuo, Mtaani au tayari kwenye suala la Ajira.
Ni muhimu kuzingatia ni kwa njia gani unaishirikisha jamii ili tu uweze kutoka sehemu moja kwenda nyingine kimaisha.
Mfano mzuri, kama unatafuta kazi kwa njia ya kutuma maombi sehemu tofauti, Kumbuka kujichunguza pia kupitia mitandao yako ya kijamii.
Hapa namaanisha unachopost kila siku kina nafasi na maamuzi ya kwa nini UAJIRIWE au USIAJIRIWE sehemu fulani.
Kuna baadhi ya waajiri hawana haja ya kusumbuka kutafuta wadhamini wako wathibitishe tabia ulionayo, ila wanaenda moja kwa moja kwenda account zako na kuangalia nini unapost au unapenda sana kuishirikisha jamii.
Wengine account zao ndio sehemu ya kujimwaga na viguo vya ajabu, matanuzi na bata za kutosha au ndio sehemu ya kupost vichekesho mwanzo mwisho kama ndio kazi zao.
Simaanishi usipost, ila tumia mitandao yako kuwa sehemu ya kuwafundisha wengine juu ya nini wanaweza fanya kutumia lugha nyepesi isiyo ya kitaalam.
Kile unachokijua jamii inakihitajia, inategemea na kwa vipi unaipa kipaumbele na mfano wa hayo.
Nimeona nikushirikishe wewe kijana mwenzangu ambae bado uko Chuo, Mtaani au tayari kwenye suala la Ajira.
Ni muhimu kuzingatia ni kwa njia gani unaishirikisha jamii ili tu uweze kutoka sehemu moja kwenda nyingine kimaisha.
Mfano mzuri, kama unatafuta kazi kwa njia ya kutuma maombi sehemu tofauti, Kumbuka kujichunguza pia kupitia mitandao yako ya kijamii.
Hapa namaanisha unachopost kila siku kina nafasi na maamuzi ya kwa nini UAJIRIWE au USIAJIRIWE sehemu fulani.
Kuna baadhi ya waajiri hawana haja ya kusumbuka kutafuta wadhamini wako wathibitishe tabia ulionayo, ila wanaenda moja kwa moja kwenda account zako na kuangalia nini unapost au unapenda sana kuishirikisha jamii.
Wengine account zao ndio sehemu ya kujimwaga na viguo vya ajabu, matanuzi na bata za kutosha au ndio sehemu ya kupost vichekesho mwanzo mwisho kama ndio kazi zao.
Simaanishi usipost, ila tumia mitandao yako kuwa sehemu ya kuwafundisha wengine juu ya nini wanaweza fanya kutumia lugha nyepesi isiyo ya kitaalam.
Kile unachokijua jamii inakihitajia, inategemea na kwa vipi unaipa kipaumbele na mfano wa hayo.