kwisha
JF-Expert Member
- Sep 9, 2021
- 1,793
- 5,042
Kuna dada mmoja ambaye nilitokea kumpenda sana, sdada huyo nilimwambia ukweli wangu lakini kwasababu ya umaskini wangu akaniona kama kituko kwake. Maana alikuwa amezoea kutoka na hawa wanaume wa instagram wanaoigizi maisha sana.
Mimi ambaye nilikuwa sina swaga akaniona kama takataka licha ya dada yake kunikubali sana na kutaka nimuoe mdogo wake, lakini mambo ya kawa ndio hivi.
Huyo dada alikuwa jeuri kinoma sana, hata nikimsamia tu akiwa barabarani alikuwa hajibu salamu zangu na kuna mda alikuwa akiniona ana tema mate chini yaani ishara ya kusema kuwa ninatoa harufu mbaya. Nilivumia wala sikujali saana niliendelea na kazi zangu kama kawaida tu
Kwasasa dada huyo ni mgonjwa, anaumwa sana wanasema ana matatizo ya ini. Mimi ambaye alikuwa ana nitukana ndiyo nahangaika na dada yake kwenye mahospitali uko na kwenye waganga wa asili kutafuta dawa za kumsaidia mdogo wake labda Mungu anaweza kusaidia.
Wale akina Instagram kwasasa simuoni yeyote mimi ambaye ninanuka nguo zangu zimekuwa marashi mazuri kwake.
Kwenye maisha usijione bora zaidi ya wengine hata kama una uwezo kivipi mchukulie kila mtu kuwa kama rafiki yako au ndugu yako, hujui ninani atakaye kuja kuwa msaada mkubwa kwako kesho.
Mimi ambaye nilikuwa sina swaga akaniona kama takataka licha ya dada yake kunikubali sana na kutaka nimuoe mdogo wake, lakini mambo ya kawa ndio hivi.
Huyo dada alikuwa jeuri kinoma sana, hata nikimsamia tu akiwa barabarani alikuwa hajibu salamu zangu na kuna mda alikuwa akiniona ana tema mate chini yaani ishara ya kusema kuwa ninatoa harufu mbaya. Nilivumia wala sikujali saana niliendelea na kazi zangu kama kawaida tu
Kwasasa dada huyo ni mgonjwa, anaumwa sana wanasema ana matatizo ya ini. Mimi ambaye alikuwa ana nitukana ndiyo nahangaika na dada yake kwenye mahospitali uko na kwenye waganga wa asili kutafuta dawa za kumsaidia mdogo wake labda Mungu anaweza kusaidia.
Wale akina Instagram kwasasa simuoni yeyote mimi ambaye ninanuka nguo zangu zimekuwa marashi mazuri kwake.
Kwenye maisha usijione bora zaidi ya wengine hata kama una uwezo kivipi mchukulie kila mtu kuwa kama rafiki yako au ndugu yako, hujui ninani atakaye kuja kuwa msaada mkubwa kwako kesho.