Hawa Waha wanaokopesha vyombo ni wachawi kweli kweli

Ivi kwanini mtu anakua na roho ya utapeli,kwanini mtu anachukua kitu Cha mtu unajua kabisa sitomlipa.

Aisee tubadilike.
Kulipa ni ngumu unapojua unatapeliwa kitu cha elf20 dukani yeye anataka akupige 50
 
Nilijaribu kukopa begi la elfu 65 huku nikilipishwa bukumbili kila siku hadi itimie yote, kwa thamani ya lilie begi Kariakoo imezidi sana 35 ndio nikapanga kumlipa 40 kwa huruma yangu.

Sasa hawa jamaa huwezi kuwadhurumu aseee, hata ukisafiri mwaka ukirudi utamkuta anakusubiri.

Kuna jamaa yangu bingwa wa kutapeli lakini amefeli mission zote, yeye alichukua feni sasa kila chocho atakayopita muha huyu hapa, na siku akiwa job muha hatokei ila akiwa home tuh Muha anaoteshwa huko chap amefika na daftari lake, jamaa bila kudaiwa yeye mwenyewe anatoa pesa yake.

Hawa jamaa ni hatari kwa mambo ya mikopo usijaribu kuwakopa kama huna uhakika maana kazi ya kukopeshana na kudaiana ilivyo ngumu lakin kwao wanaimudu kwelikweli.
Acheni dhulma watu wenyewe wamechoka vile anatembeza vyombo kutoka Mbezi mpaka Mbagala bado unataka kumdhulmu?? Kwano amekulazimisha kukopa?
 
Hiyo , Biashara ngumu lakini faida inapatikana Katika kuuza kitu Cha 10k anauza 30 kwa mkopo so probably kila siku akizikusanya bukubuku hizo Kuna Faida atatengeneza mwisho wa mwezi ,
Wengi kupitia Kazi hii wamewekeza kwao kigoma na baadhi wameenda extra miles kwa kumega wake za watu. Na kudhulumia na mwisho kurudi kigoma
 
Yaani mwanaume anatoka nyumbani,,, anaacha mke mjamzito anakuja kutafuta hela dar mpaka mke anajifungua mtoto anafikisha miaka 2 bado anatafuta ili apate chochote cha kurud nacho alafu wewe unakopa chombo chake unamzungusha na matusi juu,,,, yaani kwa uchungu alionao anaweza akakutamkia na laana ikawa juu yako sio mpaka uchawi!!! Heshim jasho la mtu
 
Nilijaribu kukopa begi la elfu 65 huku nikilipishwa bukumbili kila siku hadi itimie yote, kwa thamani ya lilie begi Kariakoo imezidi sana 35 ndio nikapanga kumlipa 40 kwa huruma yangu.

Sasa hawa jamaa huwezi kuwadhurumu aseee, hata ukisafiri mwaka ukirudi utamkuta anakusubiri.

Kuna jamaa yangu bingwa wa kutapeli lakini amefeli mission zote, yeye alichukua feni sasa kila chocho atakayopita muha huyu hapa, na siku akiwa job muha hatokei ila akiwa home tuh Muha anaoteshwa huko chap amefika na daftari lake, jamaa bila kudaiwa yeye mwenyewe anatoa pesa yake.

Hawa jamaa ni hatari kwa mambo ya mikopo usijaribu kuwakopa kama huna uhakika maana kazi ya kukopeshana na kudaiana ilivyo ngumu lakin kwao wanaimudu kwelikweli.
Deni dawa yake rejesho
 
Kuna mama mmoja hpa kitaa deni lilikuwa kubwa akataka akimbie, ile siku ya kuhama Muha amefika ngoma ikaenda hadi kwa mjumbe ikabidi wagawane vyombo
nawaogopaga sijawahi kopa kwao maana vitu vyao maana Bei zao ghalii mnoo mara mbili au tatu ya mjini
 
Nilijaribu kukopa begi la elfu 65 huku nikilipishwa bukumbili kila siku hadi itimie yote, kwa thamani ya lilie begi Kariakoo imezidi sana 35 ndio nikapanga kumlipa 40 kwa huruma yangu.

Sasa hawa jamaa huwezi kuwadhurumu aseee, hata ukisafiri mwaka ukirudi utamkuta anakusubiri.

Kuna jamaa yangu bingwa wa kutapeli lakini amefeli mission zote, yeye alichukua feni sasa kila chocho atakayopita muha huyu hapa, na siku akiwa job muha hatokei ila akiwa home tuh Muha anaoteshwa huko chap amefika na daftari lake, jamaa bila kudaiwa yeye mwenyewe anatoa pesa yake.

Hawa jamaa ni hatari kwa mambo ya mikopo usijaribu kuwakopa kama huna uhakika maana kazi ya kukopeshana na kudaiana ilivyo ngumu lakin kwao wanaimudu kwelikweli.
Umekutana na kiboko ya dhulumati
 
Daah hawa jamaa najiuliza wanapataje hela
Hawa watu wanakiwango kikubwa sana Cha uvumilivu.
Kwa mfano amenunua kitu kwa sh elfu 5. Yeye anakopesha elfu 10. Lkn anakuwa anapewa bukubuku. So unakuta mteja anatoa buku leo. Mara kesho atajifanya Hana,
kesho kutwa tena akimuona muha atajificha ndani watoto wanasema mama hayupo. Kwa hiyo unakuta hiyo elfu kumi inaenda Hadi mwezi kukamilika.
Hawagana hata hasira pia.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom