Elius W Ndabila
JF-Expert Member
- Jul 17, 2019
- 322
- 645
WABUNGE WALIOJIPELEKA BUNGENI NANI ANAWALIPA?
Na Elius Ndabila
0768239284
Jana baada ya Mchango wa Mhe Halima Mdee Bungeni ambao binafsi niliupenda sana kutokana na umahili wake wa kujenga hoja, baadae alisimama Mhe Kunambi na Mhe Jerry Silaa ambao ni Wabunge wa CCM kujaribu kupinga hoja zake.
Mhe Silaa akiwa anaenda kuhitimisha hoja yake alisema kuna Wabunge wapo Bungeni hata vyama vyao vinawakana. Hapa ndipo nitajenga msingi wa hoja yangu.
Turudi kidogo nyuma kwa maana ya misingi ya kisheria inayoongozwa na sheria Mama ambayo ni Katiba ya JMT. Kwa mjibu wa Ibara ya 66(1) imetaja aina ya Wabunge watakao paswa kuwepo Bungeni kuwa ni watano. Lakini mgogoro uliupo sasa ni Wabunge wanaotajwa katika Ibara ya 66(1)(b) Wabunge wanawake.
Mwanzoni baada ya majina yale kuapishwa tuliambiwa yameletwa na CHADEMA. Hata CHADEMA walipokataa kuwa hatujaleta Spika na Tume ya Uchaguzi walisema yametoka CHADEMA.
Ibara ya 67(1) inazungumzia juu ya sifa anazopaswa kuwa nazo mtu anayeitwa Mbunge. Sifa moja wapo kati ya sifa hizo kuu tatu ni sifa inayotajwa katika Ibara ya 67(1)(b) inasema lazima AWE MWANACHAMA wa Chama cha Siasa.
Sambamba na hoja hizo, Ibara ya 78 bado inazungumzia Wabunge wa Viti maalum ambao ndio msingi wa hoja yangu hapo chini. Ibara ya 78(1) inazungumzia namna vyama vya siasa vilivyoshiriki uchaguzi vitakavyo pendekeza majina kwa Tume ya Uchaguzi. Lakini pia Ibara hiyo hiyo ya 78(4) inayotanguliwa na Ibara ndogo ya (3) inasema "Orodha ya majina ya wagombea wanawake iliyowasilishwa kwa Tume ya Uchaguzi na kila Chama kwa ajili ya Uchaguzi mkuu ndiyo itakayotumiwa na Tume ya Uchaguzi baada ya KUSHAURIANA NA CHAMA KINACHOHUSIKA.....
Baada ya kunukuu Ibara ya 66, 67 na 78 ninaomba kuuliza Tume ya Uchaguzi na Ofisi ya Spika Mhe Job Yustin Ndugai. Kwa nini jana wakati Mhe Silaa anawakashifu Wabunge kuwa vyama vyao vinawakaa hukuwatetea? Je ni sheria ipi inayoruhusu mtu kuwa Mbunge bila kuwa na Chama cha Siasa? Je, Silaa ni mwongo, mzushi na mfitini na hali ya kukataliwa siyo kweli? Kama ni kweli wamekataliwa,je kwa mjibu wa Ibara ya 78(4) inayosema Chama cha Siasa kitashauriana na Tume, je Tume ilishauriana na Viongozi wa CHADEMA? Je, kama tume haikushauriana na CHADEMA walitumia sheria ipi kuwafanya watu wasio na Chama kuwa Wabunge?
Wapo wanaojaribu kutumia precedent ya Zitto kama case study ya hawa Wabunge wanaosemekana hawana Chama kilichowadhamini, ukweli ni kuwa kesi ya Mhe Zitto Zuber Kabwe ilikuwa mahakamani na ndio maana kulitokea hiyo injuction. Je hawa wamefungua kesi mahakamani?
Sheria hizi zilitungwa na Bunge, je kama mliotunga sheria mnashindwa kuziheshimu vipi kwa ambao si washiriki wa kutunga hizo sheria. Ninadhani ni muda mwafaka kujitokeza hadharani watu wa Tume ili kuweka uhalali wa hawa watu kuendelea kuitwa Wabunge. Kinyume na hapo Wabunge wako wataendelea kudhalilishana kuitana majina ya hovyo. Lakini hata sisi walipa kodi tunataka kujua kama kodi zetu zinawalipa Wabunge halali au Wabunge wa kutengenezwa.
Ahasante.
Na Elius Ndabila
0768239284
Jana baada ya Mchango wa Mhe Halima Mdee Bungeni ambao binafsi niliupenda sana kutokana na umahili wake wa kujenga hoja, baadae alisimama Mhe Kunambi na Mhe Jerry Silaa ambao ni Wabunge wa CCM kujaribu kupinga hoja zake.
Mhe Silaa akiwa anaenda kuhitimisha hoja yake alisema kuna Wabunge wapo Bungeni hata vyama vyao vinawakana. Hapa ndipo nitajenga msingi wa hoja yangu.
Turudi kidogo nyuma kwa maana ya misingi ya kisheria inayoongozwa na sheria Mama ambayo ni Katiba ya JMT. Kwa mjibu wa Ibara ya 66(1) imetaja aina ya Wabunge watakao paswa kuwepo Bungeni kuwa ni watano. Lakini mgogoro uliupo sasa ni Wabunge wanaotajwa katika Ibara ya 66(1)(b) Wabunge wanawake.
Mwanzoni baada ya majina yale kuapishwa tuliambiwa yameletwa na CHADEMA. Hata CHADEMA walipokataa kuwa hatujaleta Spika na Tume ya Uchaguzi walisema yametoka CHADEMA.
Ibara ya 67(1) inazungumzia juu ya sifa anazopaswa kuwa nazo mtu anayeitwa Mbunge. Sifa moja wapo kati ya sifa hizo kuu tatu ni sifa inayotajwa katika Ibara ya 67(1)(b) inasema lazima AWE MWANACHAMA wa Chama cha Siasa.
Sambamba na hoja hizo, Ibara ya 78 bado inazungumzia Wabunge wa Viti maalum ambao ndio msingi wa hoja yangu hapo chini. Ibara ya 78(1) inazungumzia namna vyama vya siasa vilivyoshiriki uchaguzi vitakavyo pendekeza majina kwa Tume ya Uchaguzi. Lakini pia Ibara hiyo hiyo ya 78(4) inayotanguliwa na Ibara ndogo ya (3) inasema "Orodha ya majina ya wagombea wanawake iliyowasilishwa kwa Tume ya Uchaguzi na kila Chama kwa ajili ya Uchaguzi mkuu ndiyo itakayotumiwa na Tume ya Uchaguzi baada ya KUSHAURIANA NA CHAMA KINACHOHUSIKA.....
Baada ya kunukuu Ibara ya 66, 67 na 78 ninaomba kuuliza Tume ya Uchaguzi na Ofisi ya Spika Mhe Job Yustin Ndugai. Kwa nini jana wakati Mhe Silaa anawakashifu Wabunge kuwa vyama vyao vinawakaa hukuwatetea? Je ni sheria ipi inayoruhusu mtu kuwa Mbunge bila kuwa na Chama cha Siasa? Je, Silaa ni mwongo, mzushi na mfitini na hali ya kukataliwa siyo kweli? Kama ni kweli wamekataliwa,je kwa mjibu wa Ibara ya 78(4) inayosema Chama cha Siasa kitashauriana na Tume, je Tume ilishauriana na Viongozi wa CHADEMA? Je, kama tume haikushauriana na CHADEMA walitumia sheria ipi kuwafanya watu wasio na Chama kuwa Wabunge?
Wapo wanaojaribu kutumia precedent ya Zitto kama case study ya hawa Wabunge wanaosemekana hawana Chama kilichowadhamini, ukweli ni kuwa kesi ya Mhe Zitto Zuber Kabwe ilikuwa mahakamani na ndio maana kulitokea hiyo injuction. Je hawa wamefungua kesi mahakamani?
Sheria hizi zilitungwa na Bunge, je kama mliotunga sheria mnashindwa kuziheshimu vipi kwa ambao si washiriki wa kutunga hizo sheria. Ninadhani ni muda mwafaka kujitokeza hadharani watu wa Tume ili kuweka uhalali wa hawa watu kuendelea kuitwa Wabunge. Kinyume na hapo Wabunge wako wataendelea kudhalilishana kuitana majina ya hovyo. Lakini hata sisi walipa kodi tunataka kujua kama kodi zetu zinawalipa Wabunge halali au Wabunge wa kutengenezwa.
Ahasante.