Hatujui kesho yetu

At the end of the day amebakia kua mtumwa

Pole sana mtumwa
Hiyo ni assumption yako.

Wewe huji hata mtumwa ni nani.

Ukibisha, toa definition ya mtumwa hapa tuichambue kwa kina.
 
Nilichomaanisha ni kwamba unaemzungumzia au unaowazungumzia ni watumwa, nani amekwambia nakurudisha utumwani ikiwa kwamba still bado upo utumwani?

Pole sana mtumwa
Kwanza kabisa,

Mtumwa ni nani.
 
Hiyo ni assumption yako.

Wewe huji hata mtumwa ni nani.

Ukibisha, toa definition ya mtumwa hapa tuichambue kwa kina.
Hivi unataka kusemaje maana hata wewe ni mtumwa pia na utumwa sio neno baya Ila inategemea upo level ipi ya utumwa

Pole sana mtumwa
 
Kwanza kabisa,

Mtumwa ni nani.
Wewe ni mtumwa

slave
/slāv/

noun
>One who is owned as the property of someone else, especially in involuntary servitude.

>One who is subservient to or controlled by another.
"his boss's slave."

>One who is subject to or controlled by a specified influence.
"a slave to alcohol; a slave to an irrational fear."

Jifanyie definition utajigundua kua wewe ni mtumwa

Pole sana kwako mtumwa
 
Yangu ni hii hapa,nilikuwa zanzibar wakati Fulani nafanyakazi hotel(stuff wa kawaida)Sasa Kuna meneja wa manunuzi wa hiyo hotel alikuwa jamaa mmbongo tunaelewana sana,ikawa mara Kwa mara akitaka kwenda sokoni kununua mahitaji ya hotelini hasa Bidhaa za chakula(food stuffs)ananiomba twende wote nimpe kampani,Kule sokoni Kuna wale wapagazi (porters)zanzibar wanaoitwa "WACHUKUZI" Sasa Kuna mwamba mmoja tulikuwa tunamtumia sana kubeba vitu kama mpagazi Hadi to kazoeana nae ikawa kabla hatujaenda tunawasiliana nae acheki Bidhaa Fulani kama zipo hapo sokoni n.k.Baadae niliachakazi pale hotel maslahi madogo nikawa nafanya mishe zingine,siku Moja naona meseji WhatsApp Namba ngeni code ya Canada "Bro mambo niaje?" Hee! Kuuliza nani kumbe yule jamaa mpagazi sikuhizi anaishi Canada! Nilifurahi sana ikabidi nianze kumdodosa katumia njia gani kufikaje Canada(natafuta connection😂)ikabidi aniweke wazi kilichotokea Hadi kufika Canada.Aisee tuishi na watu vizuri Kila mtu anamuda wake wa kutoka katika maisha usimdharau mtu pengine tungeishi vibaya na jamaa asingenitafuta.hii ni true story Hadi Leo jamaa tunawasiliana.
 
Miaka mitano nyuma halafu sasa hivi ana nyota tatu acha uongo ww
 
Kwa nini unaoanisha ''dharau'' na ''mafanikio''? Unasema kwamba tuache kumdharau mtu kwa sababu kesho anaweza kuja kuwa na mafanikio! Huoni unatufundisha jambo baya kabisa? Je, usingemkuta na mafanikio, basi ingekuwa sahihi kumdharau ulipomwona akiwa amechoka? Mimi nadhani ungetuambia tu tuache kudharau binadamu wenzatu kwa sababu ni viumbe kama sisi! Anyways, wewe unawakilisha msimamo wa jamii yetu ulivyo juu ya heshima na mali, au waswahili wanasema utu kwa mali. Halafu kesho kijana akimtongoza demu, akakataliwa kwa sababu hana ukwasi, mnalalamika eti mademu wa siku hizi wanapenda pesa kumbe jamii ndiyo inavyowafundisha.
 
Mazee, katika hali ya kawaida, binadamu tunakiwa tupeane heshima bila kujali kama tunayempa atatufaa kesho au la!
 
Ukute mwanao alikuwa huko uzalendoni kitambo ni vile ulikuwa haujui tu. Usiamini kila unachokiona kuwa ndio ujalisia.
 
Good story mtumwa, uliamua kuacha kazi ya kitumwa na yeye akaamua kwenda kua mtumwa Canada km porter wa masoko ya Canada Ila tu ni mtumwa vile vile na wewe ukatamani ukawe mtumwa Canada sio huku ulipo

Pole sana mtumwa
 
Hivi unataka kusemaje maana hata wewe ni mtumwa pia na utumwa sio neno baya Ila inategemea upo level ipi ya utumwa

Pole sana mtumwa
Utumwa ni nini? Hujajibu swali hili bado.
 
As long as mtu bado ana pumua, yuko hai, anaamka asubuh kwenda kuzurura na kurud jioni (na time nyingine anarud kakosa) , usije ukamdharau. Labda afe na umasikin wake, hapo labda
Maiti pekee yake iliyo futi sita chini ardhini ndiyo ya kuikatia tamaa.

Binadamu anayeishi kamwe usimkatie tamaa kwenye chochote.

Mgonjwa leo,kesho mzimaa.
Kichaa leo, kesho timamuu.
Mlevi leo, kesho sober.
 
Wewe ni mtumwa

slave
/slāv/

noun



"his boss's slave."


"a slave to alcohol; a slave to an irrational fear."

Jifanyie definition utajigundua kua wewe ni mtumwa

Pole sana kwako mtumwa
Wewe kama huwezi kuamua hata tarehe yako ya kuzaliwa, basi pia ni mtumwa.

Unaweza kufikiri kuwa umeamua maisha yako katia dunia hii ya leo, umeamua nini cha kuandika JF.

Kumbe, hata dunia uliyoikuta, hiyo Tanzania uliyoikuta na iliyokuumba, imeumbwa na maamuzi yaliyotiwa saini na JK Nyerete.

Na hata ukiikataa hiyo, hii JF uliyoikuta na kuitumia, ina misingi iliyowekwa na Maxence Melo.

Na yote unayoyajua ni matokeo ya walimu na mambo mengi yaliokufundisha yaliyopita tu.

Hivyo, wewe pia ni mtumwa tu
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…