Baada ya kukosa njia au namna ya kutokea, leo eti ndo anatoa pole kwa waliopoteza maisha yao!
Hiyo si pole ya dhati.
Kaitoa kwa sababu kaona hakuna namna. Ushahidi wa mauaji yake ni mwingi mno.
Wamejaribu kila aina ya spin, imeshindikana.
Walianza na kuwalaumu waandamanaji.
Wakaja na habari za AI, ikagoma.
Wamejaribu kukaa kimya wakiombea Watanzania watasahau, imeshindikana.
Vyombo vya habari vya ndani navyo vimejaribu kumkingia kifua kwa kutokuripoti hayo mauaji, imegonga mwamba.
Vyombo vya habari vya kimataifa kwa kusema ukweli havijaitupa Tanzania.
BBC, DW, First Post, na wengineo, wameendelea kuripoti kuhusu mauaji aliyoyafanya.
Kwenye jumuiya ya kimataifa, wanamcheka kwa dharau.
Watu wote tumeona hakuna watu milioni 32 waliojitokeza kupiga kura.
Sasa eti anakuja na mambo ya pole, sijui tume ya kuchunguza mauaji, sijui maridhiano nini nini….
Mimi nasema hivi…..hatuutaki huo ujinga wako.
Kuua uue wewe halafu wewe huyo huyo ndo uunde tume ya kuchunguza hayo mauaji yako?
Hivi unatuonaje we bibi?
Hayo ndo yaleyale ya tume ya uchaguzi. Unaiunda mwenyewe halafu unakuja kushiriki uchaguzi ambao hiyo tume inauendesha.
Tumeona matokeo yake.
Safari hii imekula kwako. Pole yako baki nayo mwenyewe.
Tume yako baki nayo mwenyewe.
Kwa sasa jiandae tu na kwenda kujibu mashitaka kule ICC.