Abuu Abdurahman
JF-Expert Member
- May 9, 2017
- 1,447
- 1,770
Habari za sasa Mabibi na Mabwana, Matumaini yangu ni kuwa mnaendelea vyema kabisa..
Nawasalimu kwa jina la Jamuhuri ✋
ANGALIZO: Popote utakaposhare post hii au kuihifadhi, tafadhali usibadilishe/usiedit chochote pia toa Credit kwa Muandishi
UTANGULIZI
Kesi yetu stadi tutakayoitumia kwenye maelezo haya ni mtandao huu “ zanturka ”
Huo hapo juu ni mfano wa mtandao nilioutengeneza ndani ya siku 5 zilizopita, nikimaanisha kuwa huo mtandao una umri wa siku 5 kutoka sasa na tayari post zake zote zimekuwa indexed (zinapatikana kwenye Search engine ya google)
Hiyo picha ya juu inaonesha post ya kwanza ikitokea google dakika 6 baada ya kuwa-published
Hiyo picha ya juu inaonesha post mbali mbali zimeanza kutokea baada ya kuwa published
Kujua gharama utakazotumia, Muda na Mahitaji mengine ya tovutu kama hiyo na zinazofanana nazo basi soma mpaka mwisho
2. Upatikanaji wa Internet
3. Kifaa cha kutumia : Simu, Computer (Unaweza ukatumia Simu janja yako kuanzia mwanzo hadi mwisho bila tatizo lolote)
4. Gharama: kati ya 2,900Tsh (elfu mbili na mia tisa) na kuendelea, kulingana na mahitaji yako pamoja na nyakati husika unaofanya malipo.
Ziko kampuni nyingi ambazo zinatumika kusajili jina la Mtandao, zipo za kitanzania pia ziko za kiglobal.
Kampuni Mashuhuri kwa kusajili Domain ni Godaddy na ndio ambayo tutaitumia leo hapa kwaajili ya kusajili mtandao wetu
Ingia kwenye mtandao wao Godaddy kisha search domain name unayotaka kutumia kama nilivoandika na kusearch hapo juu
Then utafuata hatua kukamilisha manunuzi ya domain name hiyo
Ili Tovuti wako uweze kutokea kwenye search engines mfano google, bing nk inabidi uihost kwenye kampuni zinazotoa hosting kama vile :
Hostigator, Hostinger, Interserver, Bluehost nk
Hosting Company mashuhuri tutakayoitumia hapa ni Interserver , kutokana kwamba iko simple, iko-best na wana Offer nyingi.
Ingia kwenye page yao interserver
Weka jina la domain uliyonunua Dodaddy, endelea kwa kuweka mahitaji yako ya hosting na lipia hosting kulingana na Mahitaji yako.
JINSI KUUNGANISHA DOMAIN NA HOST
Utakuta domain yako domain yako kwenye “ Web Hosting ”
Ibonyeze hiyo domain yako.
Utapelekwa ukurasa mwenyinge wenye taarifa ambazo utatakiwa kuzicopy na ukazipaste kwenye mtandao wa Godaddy uliponunulia domain.
Taarifa unazotakiwa kuzicopy utazikuta kwenye kipengele kimeandikwa
“ DEFAULT DNS SERVER ”
Taarifa hizi za juu, taarifa namba 1 na taarifa namba 2, ndio utaziweka Godaddy kwenye sehemu husika namba 1 na namba 2.
Baada ya hapo, tayari umefanikiwa kuunganisha Domain yako na hosting Company
□ Nitaendelea Namna ya kuingiza Worpdress (software ambayo utakuwa unatumia kuendeshea tovuti yako)
□Jinsi ya kutengeneza tovuti kwa kutumia gharama kidogo
□Namna ya kuingiza kipato kutokana na Tovuti
□Na vitu vyengine Muhimu
☆ Kwa usaidizi wa ana kwa ana (premium services) ni pm
Abuu Abdurahman
Karibuni
Nawasalimu kwa jina la Jamuhuri ✋
ANGALIZO: Popote utakaposhare post hii au kuihifadhi, tafadhali usibadilishe/usiedit chochote pia toa Credit kwa Muandishi
UTANGULIZI
- Ikiwa unahitaji kufungua tovuti kwaajili ya mambo yako binafsi/Ofisi hapa ni Mahala pake.
- Ikiwa unahitaji kujiingizia kipato kwa kutumia tovuti hapa pia ni mahala pake
Kesi yetu stadi tutakayoitumia kwenye maelezo haya ni mtandao huu “ zanturka ”
Huo hapo juu ni mfano wa mtandao nilioutengeneza ndani ya siku 5 zilizopita, nikimaanisha kuwa huo mtandao una umri wa siku 5 kutoka sasa na tayari post zake zote zimekuwa indexed (zinapatikana kwenye Search engine ya google)
Hiyo picha ya juu inaonesha post ya kwanza ikitokea google dakika 6 baada ya kuwa-published
Hiyo picha ya juu inaonesha post mbali mbali zimeanza kutokea baada ya kuwa published
Kujua gharama utakazotumia, Muda na Mahitaji mengine ya tovutu kama hiyo na zinazofanana nazo basi soma mpaka mwisho
MAHITAJI
1. Ubunifu : Lazima uwe na idea ya Tovuti unayotaka kutengeza2. Upatikanaji wa Internet
3. Kifaa cha kutumia : Simu, Computer (Unaweza ukatumia Simu janja yako kuanzia mwanzo hadi mwisho bila tatizo lolote)
4. Gharama: kati ya 2,900Tsh (elfu mbili na mia tisa) na kuendelea, kulingana na mahitaji yako pamoja na nyakati husika unaofanya malipo.
HATUA YA KWANZA
Kwanza kabisa utahitaji kusajili jina la mtandao wako utakaotumia (domain name) mfano jamiiforums.com , zanturka.com nk.Ziko kampuni nyingi ambazo zinatumika kusajili jina la Mtandao, zipo za kitanzania pia ziko za kiglobal.
Kampuni Mashuhuri kwa kusajili Domain ni Godaddy na ndio ambayo tutaitumia leo hapa kwaajili ya kusajili mtandao wetu
Ingia kwenye mtandao wao Godaddy kisha search domain name unayotaka kutumia kama nilivoandika na kusearch hapo juu
Then utafuata hatua kukamilisha manunuzi ya domain name hiyo
- Domain name inaweza kukukost kati ya 28,000Tsh kwa kawaida,
- Bei ya chini kabisa 2,900Tsh ( hii huwa inavari/inabalika badilika kulingana na % za Offa)
- Gharama huendelea kuwa juu kulingana na muda husika na aina ya domain ambayo unanunua pia kutegemea na kampuni unayonunua
HATUA YA PILI
Chagua Hosting Company na uunganishe domain yakoIli Tovuti wako uweze kutokea kwenye search engines mfano google, bing nk inabidi uihost kwenye kampuni zinazotoa hosting kama vile :
Hostigator, Hostinger, Interserver, Bluehost nk
Hosting Company mashuhuri tutakayoitumia hapa ni Interserver , kutokana kwamba iko simple, iko-best na wana Offer nyingi.
Ingia kwenye page yao interserver
Weka jina la domain uliyonunua Dodaddy, endelea kwa kuweka mahitaji yako ya hosting na lipia hosting kulingana na Mahitaji yako.
JINSI KUUNGANISHA DOMAIN NA HOST
- Ukishalipia hosting yako utafunguka ukurasa kama huu hapa chini, kwenye hosting acc yako
Utakuta domain yako domain yako kwenye “ Web Hosting ”
Ibonyeze hiyo domain yako.
Utapelekwa ukurasa mwenyinge wenye taarifa ambazo utatakiwa kuzicopy na ukazipaste kwenye mtandao wa Godaddy uliponunulia domain.
Taarifa unazotakiwa kuzicopy utazikuta kwenye kipengele kimeandikwa
“ DEFAULT DNS SERVER ”
Taarifa hizi za juu, taarifa namba 1 na taarifa namba 2, ndio utaziweka Godaddy kwenye sehemu husika namba 1 na namba 2.
- Rudi kwenye ukurasa wa Godaddy, Tafuta na ubonyeze neno “ My products ” => “Manage DNS” => “Change Nameservers”
- Paste zile taarifa ulizozikopi kwenye hosting acc yako, namba 1 paste kwa 1 na namba 2 post kwa 2 then save changes.
Baada ya hapo, tayari umefanikiwa kuunganisha Domain yako na hosting Company
□ Nitaendelea Namna ya kuingiza Worpdress (software ambayo utakuwa unatumia kuendeshea tovuti yako)
□Jinsi ya kutengeneza tovuti kwa kutumia gharama kidogo
□Namna ya kuingiza kipato kutokana na Tovuti
□Na vitu vyengine Muhimu
☆ Kwa usaidizi wa ana kwa ana (premium services) ni pm
Abuu Abdurahman
Karibuni