Khalidoun
JF-Expert Member
- Feb 12, 2013
- 2,842
- 4,474
Hakika sisi tuliokuwepo wakati ,wakati ambao chadema haikuweza kumsimamisha mgombea wa urais tunatambua jasho na damu aliyojitolea Mbowe kuijenga chadema na hata kulijenga taifa.Sikumbuki mwaka lakini nakumbuka kulikuwa na mkutano jangwani,wabunge wote wa kuchaguliwa walikuwepo pale na idadi yao ilikuwa wabunge wa tano tuu na Mbowe akiwepo,walilalamikia uchache wao na jinsi unavyowatesa bungeni.Nikiangalia leo kati ya wabunge hao watano wengine ni marehemu lakini baadhi yao wamekufa wakiwa tayari wamerudi ccm kutetea mkate wao na wengine wamepotea mfano Mheshimiwa.Mtungirehi.Aman Warudi Kabourou aliaga dunia akiwa ccm na hata kuwa mwenyekiti wa ccm mkoa wa Kigoma.Issac Cheyo na na yule mwingine wa Bariad walirudi ccm na hata kupewa ukuu wa wilaya.Mbowe amebaki imara hadi leo.Hakika Mbowe na Chuma cha mjerumani na ni sauti ya zege kama alivyojitambulisha siku ile.Hakika Mbowe ni kiongozi shupavu .
Succession Plan ya Mbowe ipoje? Ameandaaa wa kumrithi? au anahisi bila yake hakuna wa kuindeleza CDM? Kama ni hivyo ina maana basi si kiongozi wa kupigiwa mfano, maana ameshindwa kuindeleza CDM baada yake.