Hatma ya Freeman Mbowe CHADEMA

Hatma ya Freeman Mbowe CHADEMA

Wakati Freeman Aikaeli Mbowe⁩ anachukua nafasi ya uenyekiti wa CHADEMA Taifa kutoka kwa mzee Bob Nyanga Makani, alikuta kuna Wabunge wa 5 na Madiwani wasiozidi 75 nchi nzima. Wabunge wasioweza hata kujaza sebule yenu hapo.

Leo tukielekea kwenye uchaguzi mkuu mwingine wa ndani wa CHADEMA, Mwezi Desemba, 2019 CHADEMA kuna Wabunge zaidi ya 65 madiwani zadi ya 1500 nchi yote, halmashauri za kutosha na wanaunda kambi ya upinzani bungeni (KUB)

Hivyo ni vyema wewe "kijana - baro baro" wa leo mwenye kuendeshwa na "mihemko" kutambua haya mafaniko makubwa kabla ya kusema "Mbowe ameiua CHADEMA", inawezekana hujui hata CHADEMA imefikaje hapa ilipo leo, sio miujiza, ni STRATEGIES!

Kuna Vijana wa leo, labda kwa mihemko na juhudi za kutumika hawajui nguvu iliyotumika, jasho lililomwagika hadi kuifanya leo CHADEMA kuwa chama kikuu cha upinzani. Wanadhani ni kitu rahisi kama kucheza 'BIKO na TATU MZUKA'

Hatusemi kwamba Freeman Mbowe ni malaika, kwamba hakuna dosari na makosa kwenye uongozi wake, hapana, isipokuwa jasho, damu na machozi yake yamemwagika kwa ajili ya CHADEMA, tuhuma zenu zinapaswa kuwa 'Valid' wakati wa kumkosoa, tuhuma za JINAI zithibitishwe!

Freeman Aikaeli Mbowe ni mwenyekiti halali wa CHADEMA, na ataondoka madarakani siku wanachama wa CHADEMA wakisema "imetosha" kupitia mkutano mkuu, sio kwa sababu "Kuna kelele za CCM na mapandikizi" huko nje za "Mbowe ondoka! Mbowe ondoka!"

Mzee Bob Makani alikuwa na kadi namba Tatu ya CHADEMA, kadi namba Mbili ilikuwa ya Mzee Brown Ngilulupi na kadi namba moja ya Mzee Edwin Mtei, hawakukosea kamwe kumuona Freeman Mbowe na kumkabidhi CHADEMA ambayo ameifanya kuwa chama kikuu cha upinzani Tanzania.

Mwisho, kimsingi, CHADEMA imebarikiwa kuwa na mwenyekiti kama Freeman Mbowe, wengine tuliopata fursa ya kufanya nae kazi au kukutana nae, tunajivunia sana, he's a man and a-half!

Stay blessed Chairman!

Mbowe Tano Tena Uchaguzi Mkuu 2019
Nikweli inaweza kama yupo vizuri na kafanya transformation kubwa chadema ila uongozi nikurithishana na kutengeneza watu wenye mtazamo mpya,nilikuwa nampenda sana Hayati Mugabe kwa misimamo yake ila kuendelea kuona yeye ndiye anayefaa kuwa kiongozi pekee nilianza kumchukia,Chadema inaweza kuendelea kuwa na Mbowe ila ikipata mtu mwenye mawazo mapya na mbowe akawa anamsaidia mawazo inaweza kupata kitu tofauti zaidi
 
Rais Magufuli amechukua nchi kutoka kwa Kikwete shirika la ndege ilikiwa limekufa.

Leo hii mandege yananunuliwa tu na shirika linaendelea kufufuliwa,tumenunua rada na miradi kibao inaendelea, hivyo basi rais Magufuli aendelee kutawala tu hata zaidi ya miaka 30.

Mkuu mleta mada, si tunaenda sawa? Si ndicho unachomaanisha?
Wafanyakazi wanalia na kusaga meno.Kwa utilitarianists kama mimi Magufuli is a total failure.
 
Niliwahi kukuahidi miaka mitano iliyopita kuwa sitajibizana na wewe kwa neno lolote maana kwa bahati mbaya tunafahamiana vyema na tunaheshimiana mno.Nikikujibu ninaweza kukuvunjia heshima bure.Naomba iendelee kuwa hivyo
Thanks for much respect, hata mimi bado naikumbuka ile ban yangu ya kwanza na probably ya mwisho, ulionisababishia tena kwa kunisingizia kuwa ni mimi nimekutangaza humu jf Molemo ni nani ndani ya Chadema, wakati aliyekutata wewe sio mimi, ukanishitaki nikala ban na bandiko langu lote likafutwa!, japo nimeisha forgive but not forget, ila nakuheshimu sana, na wapenda demokrasia wote wa kweli hata walioko ndani ya CCM, wanapenda kuona nchi yetu inakuwa na strong na credible opposition, na Chadema was the only hope kwa Tanzania bara, lakini haya maroroso yenu, yanawakatisha sana tamaa walio wengi, msipokubali kubadilika, 2020 you're going to be reduced to nothing!.

Ni kweli Kamanda kafanya mengi makubwa, lakini amefikia optimum performance ya uwezo wake, he can not do anything more than what he can.
P
 
No matter how good one is, ukifikia point ya saturation unakuwa a saturated solution, you can take no more than you can.

One can be very good and very instrumental ukafanya a lot of good things, lakini akifikia optimum ya uwezo wako, you can do no more good than you did.

Waasisi wa Chadema walioweka kipengele cha ukomo wa uongozi ni vipindi viwili vya miaka 5 mitano, ndani ya katiba ya Chadema, walikuwa na maana yao nzuri tuu, lakini jinsi kipengele hicho kilivyo yeyuka into thin air kwa kunyofolewa kinyemela, leaves much to be desired.

Na ukiizungumzia tuu hoja ya ukomo, wanakushukia kama mwewe!.


P
Halafu hao hao wanapigania demokrasia na katiba mpya wakati yakwao wameshindwa kuiishi
 
No matter how good one is, ukifikia point ya saturation unakuwa a saturated solution, you can take no more than you can.

One can be very good and very instrumental ukafanya a lot of good things, lakini akifikia optimum ya uwezo wako, you can do no more good than you did.

Waasisi wa Chadema walioweka kipengele cha ukomo wa uongozi ni vipindi viwili vya miaka 5 mitano, ndani ya katiba ya Chadema, walikuwa na maana yao nzuri tuu, lakini jinsi kipengele hicho kilivyo yeyuka into thin air kwa kunyofolewa kinyemela, leaves much to be desired.

Na ukiizungumzia tuu hoja ya ukomo, wanakushukia kama mwewe!.


P
Mwana Taluma mwenzangu kwanza nianze kwa Kukusalimia habari za siku, sikuweza kuwepo jukwani kutokana Na masomo yanayonikabili,

Kwanza nianze kwa kukukumbusha Freeman Mbowe ataondoka pindi wanachama wakisema aondoke si kwa shinikizo kutoka kwa wanaoitakia chadema mabaya pili mbowe amekitoa chadema sehemu ambayo ccm hawakutegemea kuwa leo chadema kitafika kwahiyo freeman mbowe ndio chaguo la wana chadema na Watanzania kwa ujumla

Wasalam
 
Nikweli inaweza kama yupo vizuri na kafanya transformation kubwa chadema ila uongozi nikurithishana na kutengeneza watu wenye mtazamo mpya,nilikuwa nampenda sana Hayati Mugabe kwa misimamo yake ila kuendelea kuona yeye ndiye anayefaa kuwa kiongozi pekee nilianza kumchukia,Chadema inaweza kuendelea kuwa na Mbowe ila ikipata mtu mwenye mawazo mapya na mbowe akawa anamsaidia mawazo inaweza kupata kitu tofauti zaidi
Chadema haimzuii yeyote kugombea nafasi yoyote.Hiki ni chama cha kidemokrasia ila nikiwa kama mpiga kura mimi binafsi nadhani Mbowe anafaa zaidi kati ya wote watakaojitokeza na kura yangu nitampa
 
Mkuu unaweza kuwa na Hoja nzuri pia ila iko kikatiba zaidi na ndiyo maana kuna mkulima ameenda mahakamani kupinga Ukomo wa Urais.Nadhani tusubiri maamuzi ya mahakama then hoja yako itakuwa Valid
Nyie kama chama mnaamini katika nini?

Je mnaamini ni sahihi kiongozi kukaa sana madarakani kwakuwa tu anafanya mazuri mengi na kwa mawazo yenu hakuna anyeweza kufanya kama yeye?

Au mnaamini katika viongozi wanaoamini katika uongozi wa wengine pia?

Kama chama kikuu cha upinzani nchini, mnaamini ndani ya chama chenu hakuna mtu mwingine mwenye kuweza kuwaongoza kama anavyofanya Mbowe?

Kama jibu ni ndio, je kuna sababu gani nyie kuwa chama kikuu cha upinzani kama hamna viongozi imara na ni Mbowe pekee ndio imara?

Kama Mbowe tangu amekuwa mwenyekiti hadi leo hajaweza kutengeneza kiongozi mwingine imara kama yeye, je, kuna sababu gani ya yeye kuendelea kuwa mwenyekiti kama hata kutengeneza mtu makini kama yeye ameshindwa?
 
Tundu Lissu hafai kuwa Mwenyekti wa Chadema kwa kuwa ana mpango wa kuungana na Wahaini wa Visiwan pamoja na Mbembe mmoja toka Ujiji Kigoma ili kumvunja moto Rais wetu kukomboa Nchi
😎😎😎
 
Wafanyakazi wanalia na kusaga meno.Kwa utilitarianists kama mimi Magufuli is a total failure.
Kama kuna wabunge wanaolalamika michango yao ndani ya chama kuibiwa huoni nao ni sawa na hao 'wafanyakazi' nao pia wanalia na kusaga meno?
 
MNATAKA MBOWE AONDOKE ILI MMUWEKE MTU MWEPESI ASIYEKUWA NA UJASIRI WA KUSIMAMIA MASILAHI YA CHAMA?

OVYO KABISA NYIE.

HATA NYERERE HAKUACHIA WAKATI WA KUPIGANIA UHURU.

HADI KIELEWEKE, NDIPO MBOWE APUMZIKE.
 
Kwa kuwa Rais JPM anafanya vizuri, ataendelea kutuongoza mpaka pale wananchi tutakaposema inatosha. sauti iko sawa huko Ufipa?
Itakuwa sawa km tutapiga Kura ya maoni na kuthibitisha hilo kupitia sanduku LA kura.
 
MNATAKA MBOWE AONDOKE ILI MMUWEKE MTU MWEPESI ASIYEKUWA NA UJASIRI WA KUSIMAMIA MASILAHI YA CHAMA.

HATA NYERERE HAKUACHIA WAKATI WA KUPIGANIA UHURU.

HADI KIELEWEKE, NDIPO MBOWE APUMZIKE.
Una tofauti gani na Musiba au Juma Nkamia.
 
Chadema haimzuii yeyote kugombea nafasi yoyote.Hiki ni chama cha kidemokrasia ila nikiwa kama mpiga kura mimi binafsi nadhani Mbowe anafaa zaidi kati ya wote watakaojitokeza na kura yangu nitampa




Kama katiba inasema hata aliyemaliza vipindi vyake viwili anaweza kuendelea kugombea it's okay,japo si afya sana nani ya chama
 
Mkuu Pascal Mayalla huwa unaheshimika sana hapa jukwaani na muda mwingine huwa unaongea kwa mafumbo lakini hapa Sidhani kama unaongea kwa parables maana upo clear kuwa CHADEMA imefuta kipengele cha uongozi.

Hili swali aliwahi uliza Nape humu jukwaani na akajibiwa na Dr slaa pamoja na JJ Mnyika kwa hoja na nyaraka kwamba kipengele cha ukomo hakikufutwa ila katika kusaka maoni ya kutunga katiba mpya chini ya Prof Baregu suala hilo halikuwekwa na wanachama.

HIVYO BASI unapojenga hoja kuhusu suala hili usiseme kilinyofolewa bali sema katiba mpya haijazungumzia. Maana mtu anaweza dhani ilifanyiwa amendment ikafuta hiko kipengele.

Pascal upo credible so una uwezo wa kutengeneza au kuharibu so kabla hujachangia lolote keep your facts straight!!

Ni hayo tu mkuu wangu
Mkuu Zitto jnr, kwanza asante for much respect.
Utungaji katiba is a process, kila kilichokuwepo kwenye katiba ya mwanzo, kilikuwepo kwa sababu, unapotunga katiba mpya, kila kitakacho ondolewa lazima kijadiliwe with minutes written down.

Katika huo utunzi wa katiba mpya hakuna minutes zozote kuhusu kipengele hicho, as if it's an oversight, kwa taarifa kipengele hicho ni moja ya misingi mikuu kwa Chadema kuitwa Chama cha Demokrasia, how can katiba ya Chadema iwe silent?.
P
 
Rais Magufuli amechukua nchi kutoka kwa Kikwete shirika la ndege ilikiwa limekufa.

Leo hii mandege yananunuliwa tu na shirika linaendelea kufufuliwa,tumenunua rada na miradi kibao inaendelea, hivyo basi rais Magufuli aendelee kutawala tu hata zaidi ya miaka 30.

Mkuu mleta mada, si tunaenda sawa? Si ndicho unachomaanisha?
Km tutapiga kura ya maoni na kulipitisha hilo sioni km kutakuwa na tatizo.
 
Nyie kama chama mnaamini katika nini?

Je mnaamini ni sahihi kiongozi kukaa sana madarakani kwakuwa tu anafanya mazuri mengi na kwa mawazo yenu hakuna anyeweza kufanya kama yeye?

Au mnaamini katika viongozi wanaoamini katika uongozi wa wengine pia?

Kama chama kikuu cha upinzani nchini, mnaamini ndani ya chama chenu hakuna mtu mwingine mwenye kuweza kuwaongoza kama anavyofanya Mbowe?

Kama jibu ni ndio, je kuna sababu gani nyie kuwa chama kikuu cha upinzani kama hamna viongozi imara na ni Mbowe pekee ndio imara?

Kama Mbowe tangu amekuwa mwenyekiti hadi leo hajaweza kutengeneza kiongozi mwingine imara kama yeye, je, kuna sababu gani ya yeye kuendelea kuwa mwenyekiti kama hata kutengeneza mtu makini kama yeye ameshindwa?
Kwa bahati mbaya sana unadhani Chadema ni chama Tawala.Hiyo ni bahati mbaya sana kwako.

Jaribu kujifunza kidogo siasa za Africa na duniani kwa ujumla halafu unipe historia ya vyama vya upinzani na viongozi wake

Jifunze hata historia ya Kenya tu uniambie ni lini Wanamageuzi waliwaweka kando akina Raila Odinga,Uhuru Kenyata,Mwai Kibaki,Kalonzo Musyoka,Kijana Wamalwa,Musalia Mudavadi,William Ruto na wenzao? Mbona hawakuachia uongozi wa vyama vyao?

Kwa Taarifa yako moja ya goal ya kiongozi wa mageuzi ni kushinda uongozi wa dola na baada ya hapo kazi uske inakiwa imekamilika.

Mbowe akimbie uongozi CDM tutamuuliza ni lini amekamilisha kazi tuliyompa ya kukamata dola?
 
MNATAKA MBOWE AONDOKE ILI MMUWEKE MTU MWEPESI ASIYEKUWA NA UJASIRI WA KUSIMAMIA MASILAHI YA CHAMA?

OVYO KABISA NYIE.

HATA NYERERE HAKUACHIA WAKATI WA KUPIGANIA UHURU.

HADI KIELEWEKE, NDIPO MBOWE APUMZIKE.
Hilo ndilo lengo lao kubwa.

Siku tukiona CCM wote wanapiga debe Mbowe achaguliwe kuwa Mwenyekiti ndiyo siku ambayo tutachagua Mwenyekiti mwkngine na kumpumzisha Mbowe
 
Mbowe aendelee hakuna kutoka, jpm asithubutu kutoa ukomo wa urais maana hana maana, hafai anatesa watanzania wengi sana kwa maamuzi yake ya hovyo na ya kikatili, hana busara, hana hekima.
 
Back
Top Bottom