Hatimaye Waraka umemtoa pangoni “mwenyewe”!

Hatimaye Waraka umemtoa pangoni “mwenyewe”!

Kikwete angetafuta jukwaa la kisiasa ayaseme hayo ya kuchanganya dini na siasa. Ingeleta maana zaidi.

Kitendo cha kwenda leo kanisani ambapo baadhi wana jambo lao,... kuwashauri wasichanganye dini na siasa wakati yeye kuchanganya siasa na dini hakuanza leo ni unafiki uliopitiliza.
 
Naam!

Sinema bado inaendelea kwa kasi huku vioja vikiendelea kujitokeza. Leo kuna matukio mawili makubwa yaliyotokea.

Waraka wa Baraza la Maaskofu (Roman Catholic) kupinga mkataba wa ubinafsishaji wa bandari za Tanganyika, ambao umesomwa nchi nzima katika kila kanisa na vigango vyake kote nchini. Jambo hili limewachanganya sana!

Na hivyo kupelekea kuibuka kwa tukio la pili...

Tukio la pili ni lile la kuibuka Rais Mstaafu Awamu ya Nne kutokea huko Rorya-Mara. Yeye anaujibu waraka huo kwa kuigeuza hoja na kuwa "Udini," akiamini yeye kwamba hatuelewi kinachoendelea.

Kiujumla, hawa wakuu wanazidi kujiumbua wao wenyewe, wameona wajaribu kutumia majukwaa ya kidini ili ku-push DP-WORLD.

Kesho tunasubiri tumsikie huyo Kinara wa nchi kwenye Jubilei nyingine ya kanisa lingine kutimiza miaka 60 huko Arusha. Hii ni kwa sababu Mkuu wa Sterling anajua kabisa nguvu ya TEC.

TEC inao uwezo wa kuongea na dunia na ikaeleweka.
View attachment 2723168View attachment 2723169
watatoka wote mkuu
 
Ngoma bado mbichiiii
Waraka wa TEC umekuwa kama bomu la sumu la kulipua serikali nzima. Hakuna chawa, panya wala kiroboto aliyepo mafichoni ataendelea kujificha gizani.
CCM na serikali yake wasipojipanga vyema, hii game wanapigwa knockout mapema sana.
Nyie watu mnajitia ujinga sana. Eti bomb la nyuklia?

Kama ni mgeni kwa siasa za Tanzania basi karibu Tanzania.

Makubaliano ya Bandari yanaendelea na hakuna kitu mtu anaweza fanya. Mark this post
 
Naona mods wanajitahidi kufuta threads zinazohusu maoni ya udini na siasa. But mwisho wa siku ukweli ni kwamba dini na siasa HAVITENGANI!
Wanasiasa ndio hao hao wanadini ama sivyo wakati wa uchaguzi wanasiasa wachaguliwe na wanasiasa wenzao na wanadini wabaki na imani zao!
Nchi ni yetu sote!
Tena waape kwa ilani za chama, nimeandika kodogo ila imeongea mengi......
 
Kikwete alifaidika kwa kiasi fulani na siasa za Udini wakati ule alipozidiwa hoja na Dr. Slaa. Hivyo anaamini akichomeka mambo ya dini yeye na wengine watatupoteza maboya. Suala la bandari halina mahusiano yoyote na dini. Kama anategemea wakitumia kete ya Udini watafanikiwa basi amechemka. TEC wamefanya kweli bila kujali hiyo propaganda mfu ya Udini.
Jk mnafiki sana. Watanzania wameamka
 
S
Naona mods wanajitahidi kufuta threads zinazohusu maoni ya udini na siasa. But mwisho wa siku ukweli ni kwamba dini na siasa HAVITENGANI!
Wanasiasa ndio hao hao wanadini ama sivyo wakati wa uchaguzi wanasiasa wachaguliwe na wanasiasa wenzao na wanadini wabaki na imani zao!
Nchi ni yetu sote!
Sahihi dini na siasa havitengani

Watanzania tunapaswa tudeal na la Dp world Udini ni vita mbaya na tukiendeleza hili litaiharibu nchi kabisa , katika sehemu amani inaweza kutoweka kwa haraka ni maswala ya mgogoro wa kiimani
 
Back
Top Bottom