Write your reply...
uchawi bhana ka hujawahi shuhudia utasema haupo,kuna siku mkoani huko rukwa, tumetoka nyumbani tunaelekea mtoni kuoga mchana mida ya saa 7 hivi,njiani tukakutana na kundi kiasi la watu wakishangaa shangaa,kwenda kuangalia kunani,katikati ya lile kundi tunamkuta kijana kalala uchi wa mnyama huku akilia kwa sauti kubwa sana tusielewe kinachoendelea,watu wakaanza kumsema aache wizi,mara ooohh amezoea kuiba vitu vya watu,wengi wakicheka,wengine wanasikitika,walikuwepo wanaoshangilia,basi wakamnyamazisha...lahaula,kumbe akinyamaza na mlio wa simu unaanza kulia tumboni,aisee ile siku nilishangaa sana,ikabidi niulize huyu bwana kimempata nini?..jamaa ni kibaka na mwizi mzoefu maeneo Yale,sasa siku hiyo aliiba simu kwa mtu asiyemjua kwenye gari ya kwenda mnadani!!ikabidi jamaa wamchujue hadi kituo cha polisi,huku si tukifuata,jamaa akiendelea kulia njia nzima,ile kufika tu polisi wakaanza kushangaa badala ya kutoa huduma,wakamwambia anyamaze ili atoe maelezo,ile ananyamaza tu,na simu nayo inalia tumboni,basi kituo kizima kikaangua kicheko cha haja!!