Hatimaye Kikwete Afanya Kweli

Hatimaye Kikwete Afanya Kweli

Nilipoona Thread hata tarehe si kusoma nikajua mkuu wa kaya keshamtemesha kibarua chenge kumbe thread yenyewe 2 years back shit!. Mkuu wa kaya hana lolote amebakiza miaka miwili wakati anafanya vitu vya kumletea sifa tu baada ya kutumikia waTZ
 
Mbona habari yenyewe ni ya miaka miwili iliyopita...🙁 mimi nilidhani ni ya leo....🙁 Wakuu mkifufua threads za muda mrefu basi itakuwa vizuri mkitoa na warning ili watu wasichuuzike.
 
Bikirembwe, nilikuwa nafufua viporo hivi. Inaweza kuwapa mwanga wale wageni ambao hawakujua kuna mambo haya tuliyajadili miaka miwili iliyopita.

Kipindi hiki wakati JK ameingia madarakani alikuwa anafanya maamuzi ambayo wengi walikuwa wanammwagia sifa kem kem. Bado anaweza kufanya kweli, "tumpe muda"! Na ikiwezekana mwaka 2010 tumwongezee 'tu-miaka tutano tu' aweze kumalizia kazi nzuri aliyopanga kutufanyia watanzania.

Mac

kweli Mac hututakii mema watanzania....ufisadi wote huu bado tumpe muda wa miaka 5 mengine CCM watumalize kabisa mana sasa waTZ tuko hoi
 
Du niliichangamkia hii thread kwa spidi ya ajabu. Nilidhani JK kaamua kumshughulikia Mkapa. Kumbe...
 
Kwa mujibu wa habari, serikali ya JK imesitisha mara moja uuzaji wa nyumba za serikali kwa viongozi na kuanzia sasa nyumba hizo hazitouzwa tena. He got some nerves.... Kuna watu imedaiwa wamekasirishwa na kitendo hicho!!

Soma habari hapa: http://majira.co.tz/kurasa.html?soma=tanzania&habariNamba=737

Mzee Mwanakijiji,

Pole kwa kazi za kutwa nzima, nakuheshimu sana mzee mzima ila hii habari inapunguza kidogo kuamini kuwa uwezo wako wa kufikiri umekuwa wa kiasi cha chini kiasi hiki! "Bygone 2 be bygone" Serikali ikitaka kufanya lake haishindwi! Serikali hiihii iliyopo madarakani Serikali ya CCM wamegoma kumlimpa yule jamaa jina limenitoka mpaka BoT ikamuajiri Mkono kwa ajili ya ile kesi na yule jamaa alishashinda na mahakama ikaamuru alipwe.

Huyo JK aliezuia nyumba zisiuzwe yeye alikuwa katika baraza la mawaziri lililoridhia kuuza nyumba za Serikali na yeye akajitwalia moja iliyopo mtaa wa ursno regent estate!

Huo anaufanya ni muendelezo wa siasa za kisanii za JK.
 
Du niliichangamkia hii thread kwa spidi ya ajabu. Nilidhani JK kaamua kumshughulikia Mkapa. Kumbe...

Alishasema mwacheni Mzee fisadi apumzimke kwa amani....Ooops! Mzee wetu apumzike kwa amani...sasa nadhani anajuta kwanini alitoa kauli hiyo.
 
Field Marshall ES
Daah natamani ningekuwepo enzi hizo humu ndani maana jamaa umechambua mambo balaa ila hatimaye serikali ya kishkaji imeshaondoka.
 
Last edited by a moderator:
Mzee ES, mimi nilikuwa shabiki wa Mkapa just kutokana na habari za magazetini, lakini jinsi JK anavyoanza kufanya haya mambo naanza kujiuliza hivi Mkapa alikuwa ni Rais wa nchi gani? Nafikiri kama kuna mtu ambaye Nyerere anajutia kutupa Watanzania ni Mkapa. Angalau Mwinyi ilikuwa ni majaribio ya utawala bila Mwalimu!! Mimi nafikiri Rais afanya hatua moja zaidi. Kama kuna kiongozi yeyote aliyenunua nyumba za serikali zaidi ya moja, basi warudishe hizo nyingine serikalini!!! Wachague ni ipi wanataka kuendelea kuwa nayo, na hizo nyingine zirudishwe kwenye matumizi ya serikali au ziuzwe kwa wafanyakazi wa kati!!


We mzee mhhhh!!!!!!!!!!!!!!!!!!! vipi zirirudishwa hizo nyumba au ndo ilikuwa siasa za sifa kama huyu Prezdaa mpya,,,,kumbe watu makeke ya uongozi ukiwa rais wanaanza nayo wote
 
Field Marshall ES
Kumbe ndio ilikuwa ndoto ukija bongo uwe mbunge halafu waziri?!, duh! What a loser!!, umeishia kuwa mpambe wa Mosha na kupiga picha na mabebez le supa mtindiz.
Aibu hii.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom