Hatimaye Kikwete Afanya Kweli

Nilidhani hii mada imefungwa, lakini kwa vile bado inaendelea (kuonyesha ni jinsi gani hili linatugusa) nimeonelea nijibu mambo kadhaa.

a. Nchi nyingi tunazozitaja kuwa ni mfano wa nchi zisizoruhusu watu wasio na asili ya kundi la wengi wasiwe marais zina sababu ya hali hiyo. Historia ya nchi hizo ni ya kibaguzi. Marekani, Uingereza, Uarabu n.k zimejengwa kwa misingi ya kibaguzi. Jamani Wamarekani ni wabaguzi tangu mwanzo wa kuundwa Taifa lao!! Waarabu ni wabaguzi tangu enzi na enzi,!! Nchi hizo zimejengwa kwa misingi ya kibaguzi!! Hivyo unapoona nchi hizo haziruhusu au kushabikia kuwapa wazawa wenye nasaba tofauti za uongozi wa juu ni kwa sababu ya historia yao!!! Hata hivyo, Marekani imepiga hatua kubwa, kwa kujaribu kukubali watu weusi kushika nafasi za juu za uongozi!! Hivi sasa Condoleezza Rice ni wa nne katika kushika kiti cha Rais wa marekani in case!

b. Kufikiri kuwa kwa vile nchi zilizoendelea zinaendelea kubagua basi ni sawa na sisi kubagua ni mawazo ya hatari! Hatuwezi kujenga Taifa kwa njia za kibaguzi kwani hatima yake wanaobaguliwa iko siku wataasi!!! Mmeyaona Afrika ya Kusini, Ufaransa, na mmeyaona Rwanda/Burundi etc! Hakuna kitu chochote kinachohalalisha ubaguzi wa rangi/kabila /nasaba kwenye utawala wa nchi ya kidemokrasia! Je watu weusi ni bora zaidi kuliko watu wengine? Je kuwa mweusi ni kibali cha kuwa mtawala mzuri!!!?

c. Njia pekee ya kuhakikisha kuwa hakuna "mtanzania asiye mweusi" au "mzawa" anachukua madaraka ya juu ya nchi ni kuhakikisha watu hao wanaondolewa nchini kwa nguvu au kwa lazima. Tunaweza kufanya hivi kwa kuwafukuza (deportation) au kuwamaliza (extermination)!! Hatuwezi kusema Watanzania wote ni sawa na kuwa sisi hatubagui mtu au watu kwa misingi ya rangi, dini, kabila n.k lakini wakati huo huo tunapigia debe ubaguzi ulio de facto! Kwa sababu hiyo, kina SAS na wote waliotajwa na Olga wanatafutwa na kuondolewa nchini au wanapigwa alama kwenye nyuso zao!!! Aidha sisi ni taifa lisilo na ubaguzi wa aina yoyote ile de facto au de jure ama ni Taifa lenye kuficha hisia za kibaguzi.

d. Kwa vile Watanzania wenzangu hapa wanaonyesha kuanza kusahau tulikotoka ni bora niwakumbushe kidogo. Hili suala la rangi na nasaba siyo geni. Tarehe 9 Disemba 1968, Mwalimu Nyerere alitumia sikukuu ya Jamhuri kuzungumzia mambo ambayo inabidi yabadilishwe. Kati ya aliyozungumzia ni suala la ukabila na ubaguzi wa rangi. Katika sehemu ya Hotuba hiyo Mwalimu alisema hivi:

"...kuna hii minong'ono. Baadhi ya watu wetu wanahisia mbaya dhidi ya wazungu au waasia, siyo kwa sababu ya dhambi hawa watu wametenda, bali tu kwa sababu watu hawa ni Wazungu au Waasia. Ndugu zangu, msisikilize hii minong'ono. Watendeeni watu kwa kadiri ya matendo yao, kama watu binafsi, na siyo kwa kufuata rangi zao!"*

Mwalimu alimalizia hotuba hiyo kwa kusema:

"Kama kweli tumekubali kanuni kuwa 'binadamu wote ni ndugu zangu na Afrika ni moja' basi hatuna budi kuamini -tena kwa wepesi zaidi'- kuwa Watanzania wote ni ndugu zangu, na Tanzania ni moja"! *

Mawazo hayo ya Mwalimu hayakuanza wakati huo. Kabla ya hapo alishalizungumzia hilo la rangi si mara moja tu bali mara nyingi. Mwezi Juni 1961 (JKN akiwa ni Waziri Mkuu) aliandika makala kwenye gazeti la shule ya sekondari ya weupe pekee ya Natal South Afrika. Kati ya baadhi aliyosema ni haya:

"...there is one thing which is quite certain. Africa will belong to Africans. I believe that this word 'Africans' can include all those who have made their home in the continent, black, brown, or white.......people stand as individual citizens, asking only for rights which can be accorded to all other individuals (in that society - M. M. Mwanakijiji)This means forgetting colour, or race, and remembering humanity. On this basis of equality I believe Africa has a good future for all her people!"

Miaka mitatu kabla ya hapo, Mwalimu akihutubia kwenye Baraza la Kutunga Sheria tarehe 15 October 1958 Mwalimu alizungumzia tena hili la rangi.

"What do we want in this country? What we want in this country is that every citizen of Tanganyika (Now Tanzania - M. M. Mwanakijiji) irrespective of his race, as long as he owes allegiance to Tanganyika, is a complete and equal citizen with anyone else"*

Inakuwaje tunasahau mafundisho hayo ndani ya miaka chini ya hamsini?

e. Ndugu zangu, hii ndiyo kanuni ninayoipigania na ninayoijenga hoja. Kama hatujajifunza kitu chochote toka kwa Mwalimu, tujifunze hili, kuwa Tanzania haiwezi kufanikiwa kama viongozi wake au baadhi ya viongozi wake wanasera za kibaguzi au kiupendeleo wa rangi, kabila, au nasaba.!! Kiongozi au mtanzania yoyote anayetaka kutumikia Taifa letu ahukumiwe kwa vigezo vya uwezo, elimu, tabia, n.k isipokuwa vigezo vya rangi, kabila, dini, n.k!

g. Ni kitendo cha kutukejeli kudhania kuwa kwa vile sisi sote ni weusi basi ni lazima tukubaliane na hoja za kutetea weusi wakati hoja hizo ni za kibaguzi. Sihitaji mtu kuniambia kuwa kwa kufanya hivi au vile naonyesha Uafrika wangu au weusi wangu! Kuwa mtu mweusi siyo kibali au leseni ya kuwa kiongozi bora au kustahili kuwa kiongozi!!! Kama kuna mtu Msukuma anayegombea Ubunge lakini hana elimu, uwezo, nia, na kipaji cha kuongoza kwanini apewe nafasi ya kugombea Ubunge dhidi ya Mhindi au Mwarabu ambaye ana elimu, uwezo , nia na kipaji cha kuwatumikia wananchi kisa tu huyo mtu ni Msukuma!? Hili halikubaliki, haliwezi kukubalika, na halitakubalika kamwe!!

h. Kama kuna kiongozi au kikundi cha viongozi ambao wana sera za kibaguzi na kiukandamizaji, viongozi hao hawana nafasi katika Taifa letu na ninatoa wito waachie ngazi kwani wao ni kansa na donda lisilo na tiba!! Hawawezi kutuletea maendeleo zaidi ya kutujaza chuki! Watu hao hawastahili kulipwa mishahara inayotokana na kodi za wananchi wote.

i. Hili la kukubali kuwa na viongozi weusi alimradi tu ni weusi ndo limetupatia viongozi wengi bomu ambao nikianza kutaja majina yao nitapata kichefuchefu!

j. Mwisho nasema hivi, kama kuna kiongozi yeyote wa CCM ambaye alitumia nafasi yake kumtupa nje SAS kwa sababu ya rangi yake na nasaba yake, kiongozi huyo aondolewe au ajiuzulu!!! Hakuna kuna samehewa kwa anayetetea ubaguzi!!! Kama JK na kundi lake walihusika kwa namna moja au nyingine (we have some ideas who did what...) kumbagusa SAS kwa misingi ya damu na rangi yake, JK awe wa kwanza kumtaka radhi SAS na kuhakikisha kuwa anaitumikia nchi yake tena bila ya hofu ya kujiona mgeni!!!! JK afanye hivyo kwa ari mpya, kasi mpya, na nguvu mpya!


* - Uhuru na Maendeleo
* - Uhuru na Umoja
 
Tanzania bara ni nchi ya wabongo regardless ya rangi yao, viongozi wa nchi yetu ni lazima wawe wabongo kisheria,

sasa kisiasa nani awe kiongozi wetu wa boingo ni suala la uamuzi wa wananchi ambao wana macho ya kuona hata kabla ya kuambiwa au kufundishwa siasa na mabingwa wa siasa kama waliomo humu,

Wananchi ndio uamuzi wa mwisho, kama ni dhambi ya kumnyima Salim basi inaanzia na wazanzibari wenzake ambao toka mwaka 1985, walimkataa kwa sababu ya raingi yake, na sisi bara majuzi tukafuata nyayo zao, maana jawabu hapa ni very simple wala huhitaji kuwa genius, kama Zanzibari ambako ndiko kwenu hawakutaki, sisi wa bara tufanye nini?

Kama ni dhambi ya kumkataa basi ni yetu wabongo wote kwani baada ya uchaguzi Dodoma hakuna hata mbongo mmoja aliyemlilia Salim, hata vyama vya upinzani vilinyamaza kimya, lakini kina Seif na Lipumba walipiga kelele sana kuhusu JM kufanyiwa faulo, sasa kama sio ubaguzi mnaodai nyie kina progressive ni nini? Seif huyu Salim sio mwarabu mwenziwe mbona hakulia?

Kuendelea kujifanya hatuuoni ukweli, na kwamba ati ni wanasiasa wa kisasa na we know better than watanzania walionyamaza kimyaaaaa, I am missing the perfect word for it! Salim tumemkataa kwa sababu ya uarabu wake, mahakama tunazo kwa nini asiingie huko kama anaona ameonewa! Halafu ni mwanasiasa gani ambaye ukikataliwa tu unahamaki na kujiondoa katika siasa za nchi? Hivi ni kwa nini nynyi progressive mnatuona sisi wabongo ni wajinga kwamba tunaweza kuupanda mkenge kirahisi hivyo?

Urais sio kitu cha mzchezo guys, ni lazima upitie tanuru kali la siasa ambalo kina JK wamelipitia, kwa kuenguliwa akiwa tayari ameshinda 1995, lakini wakabaki na kujitayarisha upya sio kukimbia siasa na kukasirikia viongozi wengine, yeye binafsi anajua kuwa ubavu wa kupata urais wa bongo hana na najua tatizo la rangi, hakuna kiongozi yoyote anayehitaji kuomba msamaha mtu aliyeshindwa kwa sababu ya kutokuwa makini na kuisoma siasa iliyoko usoni mwake, mzigo wa kushindwa ni wake mwenyewe hatuwezi kuwalaumu viongozi wengine waliokuwa wanatimiza matakwa ya wananchi, na huwezi kusema wananchi wa bongo hawanan sauti kwani juzi tulikataa nyongeza za wabunge na haikupita,

Hapa ni lazima tuheshimu hesabu za mzee Mkira 2 + 2= 4, sio 2+2=22!

Nafikiri ni suala la more common sense zaidi ya intellectualism, na wananchi hawakuhitaji kwenda shule kuelewa kuwa Salim ni mwarabu, we can go on on and on na haki za binadamu, na progressive talk, libertarian talk, tunasema hii bongo ni nchi ya conservatism tuliyoachiwa na waingereza, hatupendi changes lakini for the best of debate na forum we can go on and on jinsi alivyoonewa, jinsi tulivyo wabaguzi wa rangi, hatuheshimu haki za binadamu, blah! blah! blah!

Man just accept the truth kuwa maendeleo ya kutawaliwa na mwarabu sisi wabongo bado hatujayafikia labda huko mbele ya safari lakini sio hii miaka ya 2006s, na Salim a pro-politician alipaswa kuelewa mapema hili, unajua Janet Jackson alifungua ziwa kwenye super bowl, US wananchi walimlaumu sio kwa kutoa ziwa hadharani as they should have, badala yake walisema ametoa mapema muda wake ulikuwa bado angesubiri kidogo kama miaka mitano, sasa na mzee Salim na maapologist wake kubalini kuwa wakati bado kwa wabongo kutawaliwa na mwarabu!
 
Uzuri wa haya maongezi ni kwamba tunabakia kuwa Watanzania na ukweli unabaki pale pale .Naona hapa ndania karibia mtasema na Manji awe Rais wa Tanzania baadaye aje azikwe Canada tukiuliza mseme ni Muislam na kuzikwa mapema bila ya kusafirishwa ama kungoja ni misingi ya Uislam.Nasema na narudia tena kwa sauti nasema si Salim pekee ila Mhindi, Mwarabu , Mzungu no no no way piga ua Tanzania ni ya Watanazania weusi mgeni ukija ukapata uaraia kaa utuangalie tuibie kwa njia zingine tunanyanyase kama aganavyo Manji na wahindi kibao na Waarabu na wasomali lakinji Nchi yetu pale juu tuacheni tufe nayo.Mzee Es nimekubali na nakuabaliana nawe .Mkira asante sana kwa hili .
 
Mzee Es,
Naona sasa umeamua kutuweka ktk kona maanake wengine hapa inapofikia maswala ya Progressive ndani ya TZ, tayari umevuta kura zetu.
Mimi, binafsi nashindwa kuelewa hili swala limepamba moto hasa kwa sababu gani?... Kuna wakati nafikiri Labda Uarabu ndio shida kubwa ya wapinzani na sio asili ya mtu. Yaani kama Salim angekuwa mzungu kutoka Holland ama Sweden angekubalika. Hii pia sio mtazamo wa Conservative ktk swala hili.
Kuna vitu viwili hapa bado mnapiga chenga, na hamtaki kufunga magoli. Kwa sababu hapa kuna swala la 1. Kugombea Urais na 2. Kuchukua kiti cha Urais. Hii ikiwa na maana Salim pamoja wengine wote wa kuja wanaruhusiwa kugombea kiti cha Urais (swala la kwanza) lakini kamwe haitatokea kuchukua urais (swala la pili).
Haya ni mapendekezo ya mtu yeyote na unayo kila haki kuonyesha mtazamo wako kama ikiwa umelenga ktk ASILI YA MZAWA:-, Hii hata Mzee mbeba vyuma Arnold Schwarzenegger pamoja na kuwa mzungu haruhusiwi kugombea urais Marekani. Kwa hiyo hapa swala sio rangi ila Uzawa.
Na ikiwa maelezo yenu yamelenga ktk RANGI na hasa waarabu na wahindi, hapa kuna utata mkubwa na wala sio tena swala la Conservative na Progressive ispokuwa nambari moja kufuatia ya pili nilizotaja hapo juu. Tukitazama chama chetu CCM kinachoongoza, viongozi wake wote sio Conservative kisiasa labda majumbani mwao. Tumeona aliyoyafanya Mkapa na sasa hivi JK yote yanaegemea zaidi upande wa Progressive...na siasa sio mahala pa kuwa kinyonga kuchagua rangi pale panapokuwa na manufaa ya mtu mmoja. Na ajabu kuliko yote wanaoendesha CCM toka tupate uhuru na utawala mzima ni Waarabu na Wahindi wenye nafasi kubwa za kutoa decisions. Je, hawa wageni ama waarabu tuna wachagua kwa unafuu fulani kati yao?..Kwa nini tuwe na rais kibaraka wa waarabu Akina Rajani, Rostam, Manji and the likes hali tunaelewa wao ndio serikali..
Mzee Es, humfahamu vizuri Salim lakini ningekuomba jaribu kuuliza walio karibu naye. Na ikiwa mmesimama kuwa niggers will never be president of USA - well hayo ni mawazo yenu na yanaweza kabisa kuwa na ukweli hilo tena lakini sio swala la Conservatism isipokuwa Racism na sidhani ni vizuri kuli-intertain. Kwa sababu JK mwenyewe anaweza kuwa na damu ya kiarabu.... No one can prove otherwise! na labda wekeni sheria ya DNA kuhakikisha uhalali wa asili ya wagombea rais.
Nikupe siri moja ambayo labda itazidisha chuki yako kwake iwe kwa asili yake ama yeye mwenyewe. Baada ya mapinduzi Zanzibar, Nyerere aliwakusanya vichwa vyote vya Zanzibar (wasomi wa Hizbu) na kuwahamishia Bara kushika nafasi nyeti serikalini. Bahati mbaya ama nzuri hawa jamaa ndio chimbuko la Nyerere kuwa Mjamaa.. Huko Cuba sio Abdul-Rahman Babu aliyempeleka Salim isipokuwa ni Nyerere ktk kuwaandaa vijana wake na siasa ya Ujamaa. Sababu kubwa hasa inayojulikana ni kwamba Salim, Babu na wengine wanne walikuwa wanted huko Unguja na maisha yao bara bado yalikuwa hatarini..Kwa maana hiyo waarabu haohao wa hizbu ndio walitawala kisiasa - Ujamaa kwa miaka ishirini na ushee.
 
Mzee Es,
Well, hayo ni mawazo yako na siwezi kuyapinga zaidi ya kukuombea kheri!
Miaka sio mingi half the population watakuwa na asili za nje tena waarabu ama wahindi -sijui utafuatilia vipi ama donge lako linaishia kwa Salim....Hivi, Nyerere aliwahi kuwa mbunge?
 
Hapo bob,

Unakubaliana na mimi kuwa wakati bdo ukifika hakuna tatizo, Mwalimu alichaguliwa toka enzi za TAA, TANU, na CCM, yeye alikuwa siku zote ni kiongozi wa kuchaguliwa ingawaje sometimes alikuwa akigombea mwenyewe!
 
Mzee ES,

Hilo swali la Mkandara halikuhitaji jibu refu.

JKN hakuwahi kuchaguliwa kuwa mbunge. Mara zote alikuwa akijipitisha mwenyewe, watu walikuwa wanalazimishwa kumchagua kwenye vyeo alivyokuwa anapata.

Kumbuka kujichagua au kutojichagua havikuwa na uhusiano na utendaji wake wa kazi.

FD
 
Fikiraduni,
Eeeeh bwana wee nashukuru kwa support yako!
Nadhani hukuwa umefuatilia hoja ya Mzee Es hapo nyuma. Moja ya sababu ambayo kasema hampitishi Salim kuwa rais ni kwamba hakuwahi kuwa mbunge, nami ndipo niliuliza kama Nyerere aliwahi kuwa mbunge.
Ni imani yangu ubunge na kuchaguliwa mara nyingi hakuwezi kumpa mtu nafasi kubwa ktk kuongoza vizuri. Clinton ameshindwa kuchaguliwa mara kibao kuliko viongozi wengine waliomtangulia lakini tumeyaona aliyoweza kuyafanya. Mzee Edward Kennedy - seneta wa Massachusetts kachaguliwa mara nyingi kuliko maseneta wengine lakini Kennedy mwenyewe hukiri kwamba kiti cha Urais sio mchezo mdogo na hatapenda kujaribu. Tatizo letu Afrika wengi wanapenda kujaribu kwa sababu ya ile sifa kubwa - Title.
Kifupi, hii ndiyo demokrasia ya kweli kwani kila mtu anaweza kumchagua rais kuwa kiongozi wake kutokana na sababu zake mwenyewe, sio lazima sababu hizo ziwe sawa na watu wote. nakumbuka kuna watu hawakumpigia kura Mkapa kwa sababu ya sura yake, iweje rangi ya mtu kutokuwa issue. Huu ni ubaguzi usiokuwa na athari za wazi na kila mmoja wetu anao deep subconsciously, haubadilisha utendaji kazi. Kuna ilani ya ajira inayosema:- Wafanyakazi wa sehmu moja sio lazima wawe marafiki ama kupendana isipokuwa ushirikiano kikazi ni muhimu, kazi ndio iliyowakutanisha sio urafiki ama mapenzi kati ya wafanyakazi.
 
Nimesema Salim hakuwahi kuchaguliwa na wananchi hata mara moja, siku zote alikuwa akichaguliwa na Mwalimu, hakuwahi hata kugombea ubunge labda tungeelewa msimamo wa wananchi,

sasa siku alipojaribu kugombea, tumejionea wenyewe jinsi siku zote za uongozi wake wa kuchaguliwa na Mwalimu ulivyokuwa unawakera wananchi kwani walimkataa kwa sababu ya rangi yake, now look at this maths,

JK= kura 1,000,
Salim= kura 400,

Sasa kweli utasema kuwa JK ana record nzuri ya siasa kuliko Salim? Au wapiga kura wa CCM walikuwa wanamuelewa JK zaidi kuliko Salim?

Sasa nyinyi mabingwa wa siasa hebu tuambieni what happened, kwa sababu hamtaki kukubali kuwa rangi ilikuwa ndio tool ya uamuzi wa CCM?
 
Mzee Es,
Poa kidogo wanguuu!
Mimi sina matatizo kabisa na maamuzi ya Chimwaga... ila nakataa kabisa kwamba maaumuzi hayo yawe mapendekezo yangu pia. Mfano Chimwaga walisema JM hauziki, sijui mzee hana uwezo wa kuongoza na wala hakupita round ya kwanza. binafsi sikubaliani na maamuzi hayo nadhani JM anaweza kuongoza na bado kabisa anauzika hasa kwa kuzingatia nguvu ya CCM.
Vilevile Salim, amekataliwa CCM na sio wananchi kwa sababu zisizo kuwa na maana. Bi mkubwa Meghji na Rostam wote walimkataa Salim, sidhani nao kwa sababu hiyo hiyo. Seif Sharrif na CUF hawampendi Salim kwa sababu Salim kachagua upande wa machogo (CCM) - he pays for that decision both ways, ndio dunia ilinavyokwenda.
Pia kuondolewa kwa kura za marudio huko Dodoma kulichangia sana kushindwa kwa Salim...1000 kwa 400. Hata hivyo yote haya ni dhana hakuna hakika kama Salim angetoka mshindi wala JM angesimama na JK kwa wananchi nani angetoka mshindi.
Mzee Es, hakuna anayekataa matokeo hapa isipokuwa tunachosema sisi ni hiyo propaganda ya mchaguzi kuangalia rangi badala ya uwezo wa mtu kutawala ktk ngazi yetu na sio ya Dodoma. Ikiwa ubunge ni mojawapo ya quality za uongozi nadhani wazee wetu ndio pekee walioshinda sana ubunge ktk majimbo yao pamoja na kwamba hawajaboresha maisha ya wananchi wa sehemu hizo.
Ni right yako kumkataa Salim kwa mtazamo wako kama mimi navyoweza kuwakataa viongozi ama watu fulani kutokana na mapenzi yangu na sio lazima kila mtu ayapende mapenzi yangu..
 
Kama kuna mtanzania ambaye ameitumikia nchi yake na kuliweka jina la Tanzania katika anga za Kimataifa basi ni Dk. Salim A. Salim, Waziri Mkuu wa Zamani, Naibu Waziri Mkuu, Balozi, Waziri wa Mambo ya Nje, Waziri wa Ulinzi, Mwakilishi Maalumu wa Umoja wa Mataifa, Rais wa Baraza la Usalama la UM n.k. Hata hivyo, kama kuna mtu ambaye licha ya kufanya mengi na kushiriki katika uongozi wa taifa letu kwa zaidi ya miaka 40 na baadaye kujikuta akitupwa nje na kuhojiwa Utanzania wake ni Dk. Salim. Ni watu walioendesha kampeni ya kumchagua Kikwete ndo walimpaka matope Dk. Salim kiasi cha kuchezesha karata ya rangi ya SAS na ya kuwa kwa sababu hiyo na hiyo peke yake Dr. Salim hastahili kuwa Rais!! Sifikiri hata chembe kuwa yaliyofanywa dhidi ya Salim hayakuwa na baraka na viongozi wa CCM au Kikwete Mwenyewe!!

Leo, Rais Kikwete atakwenda kwenye taasisi ya Mwalimu Nyerere ambayo inaongozwa na Dr. Salim! (sijui ka SAS yuko nyumbani au bado yuko Darfur) kushiriki katika ufunguzi wa bahati nasibu maalum. Wakati umefika kwa Mhe. Kikwete kumuomba radhi SAS kwa yale mabaya yaliyofanywa na wapambe wake kina EN, na wenzake na kujaribu kumvuta tena kwenye utumishi wa Taifa letu. Haiwezekani tuache Dr. Salim afe akiwa na kinyongo na nchi na watu aliowatumikia tangu akiwa na miaka 21!!

Kama JK hatachukua nafasi na kulizungumzia hili, basi tusishangae ndani ya miaka michache ijayo suala la rangi litaota mzizi sana wakati wa utawala wa Kikwete kama vile suala la Udini lilivyoota mzizi wakati wa Utawala wa AHM na kama vile suala la Umimi lilivyoota mizizi wakati wa BWM. Hili hatuwezi kulifumbia macho.

Ninalizungumza kwa kina kwenye Podcast siku ya leo..

http://mwanakijiji.podomatic.com
 
Wanabodi,

Nimesoma hizi posti na nidhani msimamo wangu kama utabaki paleplae kuwa rangi, nywele nk siyo tatizo tatizo ni nia ya huyo mtu kuutaka urais wa nchi yetu. Kama ni mzawa na ana nia njema na tanzania nadhani huyo anakukuwa bora kuliko mtanzania mweusi asiyeipenda tanzania na ambaye anataka kwenda ikulu ili ajilimbikizie mali.

La mwisho ni hivi, naona baadhi ya wachangiaji wanasema kwani uingereza, marekanai au india nk. zinaweza kutawaliwa na mgeni? (wakimaanisha mzawa ambaye kidogo siyo mweusi sana, au tuseme aliyechanganya)
Mimi naweza kusema hivi Tanzania kwa upendo na kupendana kulikuwa hakuna nchi inayotukuta, kutokana na uzembe wa viongozi tunaochagua nyufa kwenye mambo ya dini zishaanza kuonekana, pia kuchanganya au mtu kutokuwa mweusii ishakuwa ishu! Kisa tu ni kwa sababu baadhi ya mabomu (viongozi) tunaochangua hawajui hili wala lile wanachoweza kukimbilia ni dini, kabila au asili ya mtu ili waweze mfanyia "character assassination" Na yale tuloyasikia Nigeria, Rwanda, USA, India nk yanatunyemelea bila sisi wenyewe kujua!
 
Choveki,
Ndugu yangu nakubaliana na wewe kwa kina fulani. Kweli wapo wazawa wenye asili ya nje ambao naweza kukubaliana na mawazo yako. lakini mshikaji swala la kuwa na rais toka sehemu yeyote ati kwa sababu tunakisia anaweza kuwa na nia nzuri na nchi yetu hii ni ndoto.
Sababu kubwa ya kutokuwepo nasheria kama hiyo nchi zote duniani ni kwa sababu ya mipaka iliyokwisha wekwa. Leo hii hatuwezi kabisa kusema tunaweza kuondoa mipaka Tanzania ati kwa sababu ya mapenzi yetu ktk usawa wa binadamu hali dunia nzima bado wanaitambua mipaka. Kumbuka tu hakuna usawa wa binadamu zaidi ya matamanio yetu na bado tunapishana priorities zetu.
Kuiongoza nchi ama kabila sio sawa kabisa na kuongoza dini kwa sababu dini haina rangi wala kabila. Nchi zina makabila na asili ya makabila hayo. Tatizo la ukabila ni pale mtu anapoutumia ukabila huo kama anavyofanya M7 na kosa ni la waganda kuwa na rais Mnyankole (Mnya-Rwanda). Tumeyaona Peru na kadhalika, South Africa na ndio chimbuko la historia ya nchi zetu kutawaliwa. Yaliyotokea nchi za jirani na Nigeria sio kwa sababu watu hao hamejali makabila ya viongozi ila ni kwamba wananchi wa nchi hizo hawakujali makabila ya viongozi wao.. Kwa hiyo hapa Ukabila ni pale mtu kama salim atakapo tumia urais wake kuwapa nafasi Wapemba na sio watu wa makabila mengine kupinga mapendeleo ya rais huyo. Huu ni mfano tu sisemi salim atawapendelea waarabu ama wapemba. Even though there is possibility! kutokana na historia ya nchi zetu maskini.
Tukiwa na rais Mkenya mwenye nia nzuri na nchi yetu, rais huyu atashindwa kutoa maamuzi pale tunapofikia matatizo na Kenya hasa ikiwa Kenya ndiye atakae loose. Kama yanavyopkuwa mashindano ya mpira...subiri World cup utaona ukweli wa asili za watu hasa nchi za magharibi. Aghalabu kumkuta muingereza akishabikia Italia wakati nchi hizo zinacheza... na ajabu kubwa ni nchi maskini hasa zile zilizotawaliwa na kupoteza tamaduni zao ndizo zisizokuwa na msimamo hata kwa nchi zao wenyewe. Kibao Marekani hudanganya wametoka wapi kwa sababu ya aibu tunayoipata toka matangazo ya world vision.
Lakini basi tukirudi ktk swala la Salim na baadhi ya wazawa ambao hawana uraia nchi nyingine isipokuwa Tanzania, hapa nakubaliana na hoja yako. Lakini kwa wale wote wenye asili ya nje na bado familia zao zina uraia nje sidhani kama ni uamuzi wa busara kuwapa kiti cha URAIS..
Naweza kukubali Mtanzania mzawa ambaye amekulia nje kwa sababu bado ana asili kubwa ya Tanzania, kama sheria za passport zilivyo nchi nchi nyingine. Mzawa mwenye asili ya nchi hiyo hushika first class citizenship na mgeni kupewa second class. Kuna usemi usemao kila passport hasa za Ulaya kuna herufi ama nambari ambayo inatofautisha kati ya mzawa mwenye asili ya pale na yule wa kuja. Na ukija fanya crime moja kubwa sana, wanaweza kukunyang'anya uraia kurudishwa kule kwenye asili yako....Japokuwa huu ni ubaguzi ambao umefichika lakini ndio ukweli uliosimama. Hatuwezi kufanya hivyo inapofikia ktk kiti cha Urais, rais ni citizen nambari moja.
Kisheria na kufuata katiba ya nchi hatuna hila isipokuwa kukubali matokeo. Na kumbuka wakati wa mchonga hatukuwa na matatizo ya Ukabila kwa sababu Nyerere alikuwa tofauti na marais wote Afrika. one in fifty... kwa hiyo fahamu kwamba kuna chance ndogo sana ya kumpata kiongozi kama Nyerere na Nkurumah ambao walikuwa color blind. Kisha tumeona kwamba Nyerere huyo huyo hakuwa na uchaguzi mzuri ktk warithi wake. Warithi wake wote wameonyesha ile true color zao. Leo hii Afrika imesimama bila kiongozi asiyekuwa na upendeleo ambao unatokana asili yake, dini yake ama familia yake. Pia tumejifunza kwamba hatuwezi kufahamu uwezo wa rais yeyote kwa maneno ya propaganda zao kwani huko Ikulu ndiko picha kamili huonekana.
Does it worth a risk?
 
Ndo maana Mwalimu alisema kuwa uraia uhukumiwe kwa kitu kimoja tu nacho ni loyalty to the country, na ni kwa sababu hiyo alipinga kwa Watanzania kuwa na uraia wa zaidi ya nchi moja.
 
Mzee Es said:
Mheshimiwa,

Wako Watanzania kibao wanaoweza kuwa marais wa bongo na wana uwezo na vitu vyao vimeonekana, watu kama Kaduma, Mramba, Asha Rose ni viongozi ambao wanaweza kuiongoza hii nchi na ikaelekea inakotakiwa na wakatuwakilisha mahali popote kama Watanzania, hatuhitaji waarabu, aliyesema "Mwarabu No way!" ni mimi Mzee Es na ninarudia kuwa bongo hatuwezi kutawaliwa na waarabu, UN alikataliwa na Reagan kwa sababu nyingi mojawapo ikiwa ni pamoja na uarabu wake,

Let me get this straight, waliompiga vita huko yaani Mtandao walikosea kitu kimoja tu, nacho kumtumia rais anayetoka kumpiga vita they did not have to that, kwa sababu record ya Salim ni clear kutoka CIA kuwa alihusika na kifo cha Karume, na kwamba alipelekwa na Babu Cuba na wenziwe kina Mahfudhi kufundishwa ukomaandoo kwa ajili moja tu nayo ni kuja baadaye kuipindia serikali ya ZNZB. Alipogombea UN, Reagan alipewa faili la Salim na akamuita ili akanushe yale yaliyokuwemo kwenye faili akashindwa, serikali yetu chini ya Mwalimu akjaribu kufuatilia wakaishia kupewa copy ya hilo faili, ambalo baadaye kuna mtu alili-leak kwa baadhi ya viongozi wa ZNZB, ndio maana kwenye uchaguzi wa mwaka 1985 juhudi zote za Mwalimu kumpitisha Salim ziligonga mwamba kwani ni wazanzibari wenziwe walioweka mguu chini na kumuonyesha Mwalimu lile faili ambalo lina mambo mengi ambayo mengine hatuwezi kusema ni aibu juu ya Salim, sasa kisiasa Salim alitakiwa kuanza na Zanzibar si ndiko anakotokea kwa nini asigombee urais wa huko kwanza alikotokea na baadaye agombee bara?

Watanzania sio wajinga mzee, ndio maana safari hii yale mambo ya kusema zamu ya rais wa ZNZB tumekataa na hayatarudiwa tena, kwani hayamo kwenye katiba ya nchi rais atatoka bara tu bro!

Rawlings hakuwasaidia kitu wa-Ghana, ambao mpaka leo wanaenda kulia kwenye kaburi la Nkurumah kila siku, halafu nashangaa jinsi unavyoweza kumsifia kiongozi aliyepindua nchi, kama angekuwa kama unavyosema basi angegombea kura kwani kama ni kupindua hata Salima akipindua hakuna atakaye mkataa, lakini kwa njia ya kura alikataliwa kule Dodoma, Rawlings hakugombea kura bro! na halafu hajawasaidia kitu huko Ghana, njaa ni ile ile tu kama ya bongo!

Kuhusu Mzee JK sio lazima wote tusubiri miaka kumi, NO! dalili zimeshaanza kuonekana, rais wako anapowakimbia wananchi huko NY, halafu huko DC wakapandikizwa wazee wawili kuuliza maswali ya compromise, halafu yakaruhusiwa maswali mawili tu! Something is wrong na hiyo serikali sasa hatuwezi kuachia midomo wazi hadi baada ya miaka kumi ndio maana tunaanza sasa kusema kuwa serikali mpya ina matatizo, serikali amabayo tayari imeshaanza kujigamba kwamba imeomba na kupewa hela nyingi itatufikisha wapi? Rais wa bongo anaposafiri na watu 50, mpaka nchi nyingine zinashituka sisi watanzania tukae tuuu kimya eti tunasubiri miaka kumi!

Salim ni mwarabu aliyetokea Zanzibar, basi akaanzie huko kwanza tuone lakini bara hatuwezi kuongozwa na mwarabu wakati wabongo kibao wapo wenye uwezo, hakuna ubaguzi hapa ni ukweli bongo ni ya wabongo na tupo ni sisi, wenye uwezo wapo lakini system imewanyima nafasi lakini pole pole ipo siku watanzania watadai kiongozi mwenye uwezo kwani hii tabia ya kuchaguana kwa ujanja haitadumu daima kwani kadri wanavyoshindwa kuongoza ndivyo wananchi wanajifunza, ndio maana safari hii suala la rais atoke Zanzibar lilizimwa mapema maana wanachi hawajasahu mambo ya Mwinyi, na take it from me baada ya huyu rais wa sasa wananchi hawatarudia tena kuchagua rais maarufu asiyekuwa na record!

Mzee ES
Siamini umemuweka Mramba kwenye list yako! Kama mawazo ya watanzania wengi yako kwa watu kama Mramba, basi ile nchi inahitaji mapinduzi ya hali ya juu.
 
Tatu,

Kati ya viongozi ninaowaheshimu bongo na nitawatetea mpaka dakika ya mwisho, Mramba ni mmoja wao, kazi aliyoifanya hazina kipindi cha Mkapa, haina mfano,

sasa hivi amepewa wizara yenye mlo, na yeye si mtandao ndio maana kuna kampeni kubwa sana ya kumdhalilisha ili hatimaye atolewe, na hiyo ndio siasa mpya ya kimtandao tuliyonayo sasa, leo uongozi ni unamjua nani, sio tena unajua nini,

lakini Mramba is a good man, na technically a good leader, isipokuwa sio politician, kama Mkapa alivyokuwa, hakuwa mwanasiasa!
 
hivi hii mada nikiwa na maana ya kichwa cha habari kinaendana na haya mnayo jadili ama sasa tumeachana na utaratibu wa kuchangia mahapa panapo faa ?
 
Mzee ES, mimi nilikuwa shabiki wa Mkapa just kutokana na habari za magazetini, lakini jinsi JK anavyoanza kufanya haya mambo naanza kujiuliza hivi Mkapa alikuwa ni Rais wa nchi gani? Nafikiri kama kuna mtu ambaye Nyerere anajutia kutupa Watanzania ni Mkapa. Angalau Mwinyi ilikuwa ni majaribio ya utawala bila Mwalimu!! Mimi nafikiri Rais afanya hatua moja zaidi. Kama kuna kiongozi yeyote aliyenunua nyumba za serikali zaidi ya moja, basi warudishe hizo nyingine serikalini!!! Wachague ni ipi wanataka kuendelea kuwa nayo, na hizo nyingine zirudishwe kwenye matumizi ya serikali au ziuzwe kwa wafanyakazi wa kati!!

Halafu atuhakikishie kuwa hizo nyumba mpya walizopewa Mawaziri haziauzwa kwao baada ya uchaguzi ujao. Hizo zibakie kuwa ni nyumba za serikali.
Hata hili kwangu naona lilikuwa changa la macho. Mwanakijiji, hii ni post yako ya mwezi Mei tarehe 27 mwaka 2006 na naamini sasa unamjua Mkapa zaidi ya ilivyokuwa kipindi hicho. Bado una matumaini kwa JK? JF ni shule ama kweli.
 
lakini Mramba is a good man, na technically a good leader, isipokuwa sio politician, kama Mkapa alivyokuwa, hakuwa mwanasiasa!
ES, hii post yako mara nyingi huwa naikumbuka. Unajua Mramba ni fisadi mzuri sana?

Unajua anamiliki Hoteli moja kubwa ya kitalii? Kwangu hizi ni tetesi na watu wa Arusha wanaweza kuja na facts. Naambiwa ana Hoteli kubwa na ya gharama sana pale iitwayo "Kibo Palace Hotel".

Sidhani kama ulikuwa unamjua vema nyakati hizo...
 
Ni upumbavu na naamini kuwa kila alokusudiwa kupata hizo nyumba ameshapata ndio akachukua hatua hiyo na hii haimpi alama hata nusu katika utendaji wake ni mbolongaji wa mwisho katika historia ya maraisi wa Tz.
Bikirembwe, nilikuwa nafufua viporo hivi. Inaweza kuwapa mwanga wale wageni ambao hawakujua kuna mambo haya tuliyajadili miaka miwili iliyopita.

Kipindi hiki wakati JK ameingia madarakani alikuwa anafanya maamuzi ambayo wengi walikuwa wanammwagia sifa kem kem. Bado anaweza kufanya kweli, "tumpe muda"! Na ikiwezekana mwaka 2010 tumwongezee 'tu-miaka tutano tu' aweze kumalizia kazi nzuri aliyopanga kutufanyia watanzania.

Mac
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom