Hatimaye Jerry Muro ashinda kesi yake

Hatimaye Jerry Muro ashinda kesi yake

Sishangai Jerry kuachiwa huru na sitaki kuamini kabisa kuwa hakuhusika na tuhuma kwa sababu hata Zombe naye aliachiwa huru japo bado ninaamini alihusika na tuhuma.
 
Dah! Pole sana Jerry..Karibu tena uraiani. Lakini naamini utakuwa umeshapata fundisho. Siyo kila mtu ni wa kuchezea ndani ya TZ hii

Haijui serikali ya chama chako huyu teh!
 
sasa tafuta haki ya kusafisha jina lako. Kaa na wanasheria wako muone kama kuna haja na uwezekano wa kufungua kesi ya madai dhidi ya jeshi la polisi na serikali yake. Kama utafanya hivyo wapigia bili kubwa tu. Na ikiwezekana iwe zaidi ya hili ya dowans. Ili wakome kabisa kufungulia rai wasiokuwa na hatia kesi za kubambikiza.

Polisi badala ya kushughulika na waalifu halisi wao wanafanya mambo ya kijinga kama hayo.

pia nakushauri ujichunge sana, kwani hao jamaa wanaweze kutumia mbinu nyingine za kishenzi kukumaliza. Si unaona yanayumsumbua Mwakyembe lakini. Lakini usigope maana uko vitani. Wanajeshi huwa hawaogopi kupigana vita ingawa wanajua kuwa kuna kufa au kupona upokuwa vitani. Wanachofanya ni kuchukua taadhari tu za kujilinda dhidi ya adui huku wakiendeleza mashambulizi dhidi ya adui.
 
Wapi Champaigne ni furaha kwa kwenda mbele,SIKU HAZIGANDI

acha wanaosukutua waendelee, lakini sisi twafurahia tu Jerry yuko huru huria

wasukutuaji endeleeni, mkihitaji miswaki ya miti au mkaa tutawaletea....

shampeni na ndafu mwaya eeeh!!!
 
Jamaa hana hatia.Tulijua tuhuma zilikuwa za kuumba ili kumkomoa baada ya kuonyesha machachali yake dhidi ya rushwa.Kama TBC1 walimtimua kazi sio issue!Kuna msemo unasema "jalala moja kamwe halimkondeshi mbwa".Jerry atapata kazi sehemu nyingine na maisha yataendelea.Pole sana Jerry na endeleza mapambano.
 
Hivi nyie vipi mnashangalia kuachiwa kwa mume wa mwenzenu?

heheheeeeee huyo mume wa mwenzetu wengine ni ndugu wa damu....
karibu hata wewe tufurahi sote...
Mungu ampe nini

Mke mwema kapata
kesi imetupiliwa mbali
wacha tufurahi na ndugu yetu Mwita25
 
bravooo j, alijuwa ndiyo maana aka amua nakufunga ndoa..
 
Sasa atulie na aidai ile zawadi yake iliyozuiliwa na MCT baada ya kushinda tuzo ya uandishi bora.Nasikia na TBC One walimsimamisha kazi bila kufuata utaratibu wa kisheria.Atuone wataalam wa sheria za kazi tukamsaidie mara moja.

Asimame tena na kufuta vumbi kisha asonge mbele na maisha.Lakini kapata funzo kuwa katika uandishi wa aina ile aliokuwa anafanya ilibidi atunze sana siri...lakini yeye alikuwa dhaifu kwa akina dada na aliwahi kuonekana bar huko Iringa akimuonyesha zile video pics alizowapiga polisi wakipokea rushwa.

Amekuwa mtu mzima sana.
 
heheheeeeee huyo mume wa mwenzetu wengine ni ndugu wa damu....
karibu hata wewe tufurahi sote...
Mungu ampe nini

Mke mwema kapata
kesi imetupiliwa mbali
wacha tufurahi na ndugu yetu Mwita25
Santeeeeee!

Nawasubiria pale pa siku zote tuje tuanze kuparty kwa furaha!
 
Dah! Pole sana Jerry..Karibu tena uraiani. Lakini naamini utakuwa umeshapata fundisho. Siyo kila mtu ni wa kuchezea ndani ya TZ hii


Watanzania wenzangu hii ndio comment ya Kada Nguli wa Chama fulani hapa Tanzanzania. can you please connect dots and see where we are?
 
acha wanaosukutua waendelee, lakini sisi twafurahia tu Jerry yuko huru huria

wasukutuaji endeleeni, mkihitaji miswaki ya miti au mkaa tutawaletea....

shampeni na ndafu mwaya eeeh!!!
Lol, waambie tunayo miswaki mpaka ile inayolimwa huko kondoa, (MDAAA) KAZI KWAO WASUKUtuaji washindwe wenyewe.
 
  • Thanks
Reactions: bht
4.jpg


[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD="class: contentheading"]Jerry Muro aachiwa huru na kesi yake imefutwa[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
Mtangaza wa Shirika la habari Tanzania TBC, Jerry Muro kesi yake imefutwa na yeye ameachiwa huru pamoja na wenzake. Hizi ni habri ambazo zimetufikia hivi punde kutoka Mahakama ya Hakimu mkazi wa Kisutu jijini Dar es Salaam. Jiunge nasi kesho ili upate habari kamili.

Gazeti la Mwananchi habari kwa ufupi
 
Lol, waambie tunayo miswaki mpaka ile inayolimwa huko kondoa, (MDAAA) KAZI KWAO WASUKUtuaji washindwe wenyewe.

hahahaa ulijuaje nilikuwa nalitafuta hilo jina la miswaki ya Kondoa....lol!!

usivae kodos kodos ukija, usije ukazishikilia mkononi buree!!!
 
Ninachokiona humu sio kigeni kwa jamii yetu ya Kitanzania. Wezi, mafisadi, walaRushwa wanatukuzwa, wanaogopwa, wanaheshimika, wanachaguliwa, wanateuliwa, wanabadili ajira na kuabudiwa sana tu!
 
Back
Top Bottom