Hatimaye Dr. Slaa amjibu Nape, aingizwa 'King'?

Hatimaye Dr. Slaa amjibu Nape, aingizwa 'King'?

Hapa namsubiri Le Mutuz atoe pumba zake! W2 wengine hamnazo kweli,mimi nina kadi ya NCCR,CCM & CDM lakini mimi ni CDM damu! Mbona Six na Kajembe wana kadi za CCK & CCJ? Nape aje hapa akanushe kuwa hana kadi ya CCK na mfu CCJ? Sisyem in action! Just keep on shouting! The killer M4C is behind you....
 
Ndiyo slaa ni active member na analipia ada zote za wamachama huko anazuga tuuu kwa ushahidi njooni mjengoni mpewe data zote.na c slaa tu lipumba,hamad,zito,mbowe wote ni wanaccm

we kama siyo German Shepherd sijui
 
A very good question. Nilikuwepo siku mzee Paulo Ndobo anajiunga tena na CCM kutoka NCCR. Alipewa kadi ya CCM na mwenyekiti Mkapa, akaeleza wazi kuwa ataendelea kuitunza kadi yake ya NCCR kama kumbukumbu ya kuwahi kuwa mwanachama huko na ni mali yake, akaendelea kusema kuwa hata kadi ya TANU bado anayo hadi leo. Hakuna asiyejua kuwa Dr Slaa amewahi kuwa mwanachama wa CCM. kuwa kwake na kadi sijui kwa nini iwe issue ya kujadiliwa humu. Nape analo jukumu la kututoa kwenye mambo muhimu. Tutakuwa wajinga tukinasa kwenye mtego wake.

you are right,
Hakuna sheria inayosema ukijiunga na chama kingine lazima urudishe kadi ya chama ulichotoka. Sheria inakataza uanachama - yaani kuwa mwanachama hai wa vyama viwili tofauti. Mwanachama hai ni lazima awe amelipia kadi yake kwa mujibu mwongozo wa chama husika.
Mimi napendekeza mleta mada au Nape angeleta huo ushahidi wa kadi hai ya CCM YA Dr Slaa nadhani tungekuwa na mjadala mzuri zaidi.
Hapa tunapoteza muda kujadili hisia tu na kila mtu kuvutia kwake
 
Hii inaonyesha mnavyoweza kutekwa akili na vitu vidogo, hasa akishakuwa nayo so what? kuna zaidi cha kujadili zaidi ya kuwa anayo hiyo kadi? mnaacha mambo ya muhimu yanapita tunaishia kudiscuss kadi na vibajaji.......dayuuum!
 
Kadi inanunuliwa na mwanachama, na usipoilipia muda kadhaa unakuwa mwanachama mfu! Swala la kuirudisha au la, ni mapenzi ya mtu, maana ile inakuwa ni mali halali ya mwanachama. Mwacheni vuvuzela nepi ahangaike na kupiga ngumi upepo, mwisho atachoka mwenyewe.

Havizyakadi ni mali ya chama.....soma vizuri nyuma ya kadi husika...............
 
Last edited by a moderator:
Hii inaonyesha mnavyoweza kutekwa akili na vitu vidogo, hasa akishakuwa nayo so what? kuna zaidi cha kujadili zaidi ya kuwa anayo hiyo kadi? mnaacha mambo ya muhimu yanapita tunaishia kudiscuss kadi na vibajaji.......dayuuum!
[MENTION]
Elizabeth Dominic[/MENTION] Kadi ndilo jambo muhimu kulikoni yote.........................ndiyo mlango wa uzalendo na kuaminika..................kama Dr. Slaa bado ni ccm sasa khali ya cdm imekaaje? Pili kwanini hafuati sheria ya kuwa chama kimoja tu?
 
Kwani ni lazima uwe nayo live? Mimi niliflash choo cha mtaloni.
 
Rutashubanyuma, naomba majibu yangu yale uwaquote Dr Slaa, ZItto , Nape na some other verified users ambao ni watu wa maamuzi, sorry sijui unafanyaje kutag mtu

Nsiande usihofu wamo humu wanajisoimea laivu
 
Last edited by a moderator:
Jambo usilolijua ni kama usiku wa giza. Hivyo ni vema kukaa pembeni ukashuhudia game linavyochezwa ulingoni ili uone mwisho wake nani mbabe...

Ishaka Hebu nielimishe Dr. Slaa kuishinikiza cdm imlipe kama mbunge huyo siyo askari wa kukodiwa.............kujitolea kukoa wapi na mapenzi ya chama yako wapi kama siyo mamluki?
 
(f) Kujiunga na Chama kingine chochote cha siasa.
(2) Mwanachama ambaye uanachama wake unakwisha kwa sababu yoyote ile hatarudishiwa kiingilio alichokitoa, ada aliyotoa wala michango yoyote aliyoitoa...

Labda FJM unielimishe kidogo..........Dr. Slaa anapodai anaienzi kadi ya ccm yawezekana akaienzi huku ni mwanachama mfu?
 
mi navyoona tu some extent dr.slaa anaweza akawa na huruma na CCM kama sio spy na hii ndiyo sababu uu naomba kila siku uchaguzi ujao dr.slaa asigombee kiti cha urais sababu gani unakumbuka uchaguzi uliopita cdm ilishinda kiti cha urais
lakini cha ajabu ni kwamba ccm wakatuibia kula lakini jambo la kushangaza ni kwamba badala ya slaa kuwaamuru watu waingie mitaani wasikubali yeye kataka kujifanya mcha mungu sana eti msimwage damu!sasa atakayemwaga damu nani?....

Mentali Kama kweli Dr. Slaa angelikuwa mcha Mungu hivi angelidai mshahara wa mbunge chama hoehae kimlipe kama siyo angelijitolea?
 
Elizabeth Dominic Kadi ndilo jambo muhimu kulikoni yote.........................ndiyo mlango wa uzalendo na kuaminika..................kama Dr. Slaa bado ni ccm sasa khali ya cdm imekaaje? Pili kwanini hafuati sheria ya kuwa chama kimoja tu?

Kama ndivyo, kadi ni ile gamba yenye maandishi kwa nyuma. Unataka kusema nini kuhusu Karume kuwa na kadi ya ASP NA CCM? Je, kwanini na yeye hafuati ya sheria husika.
Je, yeye kutangaza kadi ya mbele ya mkutano mkuu wa ccm ni hakuna aliyelalamikia kadi hiyo ina maana kwamba wewe Rutashbolwa ni mwana ccm kuliko wale wote waliokuwepo Dodoma? Au wao wote walipitiwa kuhusu sheria husika? Naomba jibu.
 
Nsiande, our media gives what we derseve! Maana tumekuwa wapumbavu, tunapenda kusoma na kujadili watu badala ya hoja.
Usijeshangaa hata Rutashubanyuma aliyeleta mada hii jamvini, naye ni mwanahabari/ mwandishi wa habari!
 
Mentali Kama kweli Dr. Slaa angelikuwa mcha Mungu hivi angelidai mshahara wa mbunge chama hoehae kimlipe kama siyo angelijitolea?

Kwa hiyo, yeye na watoto wake wakale polisi? Kama sisi wanachama na viongozi hatulalamiki, kwa nini nyinyi wanaccm mnalalamika sana? Kwani kazi ya ruzuku ni nini? Ulitaka tufanye kama ccm?
 
Labda FJM unielimishe kidogo..........Dr. Slaa anapodai anaienzi kadi ya ccm yawezekana akaienzi huku ni mwanachama mfu?

Sasa hujengi hoja unabisha. Neno mfu maana yake kufa, mfu inatokana na kufa. Kwa hiyo mwanachama mfu maana yake mwanachama aliyekufa kiitikadi na kiuanchama hai kwa mujibu wa sheria pia. Kwa hiyo, mwanachama mfu ni sawa sawa kabisa kwa 100% kuwa siyo mwanachama. Jenga hoja usipige kelele.
 
Labda FJM unielimishe kidogo..........Dr. Slaa anapodai anaienzi kadi ya ccm yawezekana akaienzi huku ni mwanachama mfu?

Hivi ukienzi kaburi, maana yake, aliyezikwa humo ndani badi yu hai? Au ukienzi picha ya marehemu inaama huyo mtu bado yu hai?

Masharti ya uachama wa CCM yamo kwenye katiba, and I dont even understand CCM watatibiwa na dawa gani ili wawe wanasoma? Na kama wanashindwa kusoma mistari michache inayohusu uanachama, kwanini tuwaamini kwenye ku-sign mikataba?
 
Ishaka Hebu nielimishe Dr. Slaa kuishinikiza cdm imlipe kama mbunge huyo siyo askari wa kukodiwa.............kujitolea kukoa wapi na mapenzi ya chama yako wapi kama siyo mamluki?

Naomba usipige kelele na usipotoshe.
Dr Slaa hakuomba kugombea urais, aliombwa. Kwa hiyo, kusema kwamba alishinikiza ni uwongo na upotoshaji. Dr Slaa alishachukua fomu ya kugombea ubunge mwaka 2010 kama unakumbuka. Sisi viongozi wa chama ndo tulimwomba huku akiwa na uhakika wa kuwa mbunge wa Karatu.
Pili, Dr Slaa analipwa pesa kidogo sana kulinganisha pesa wanazolipwa Makamba,Mkama na Kinana. Kama ubisha leta ushahidi.
Tatu, mapato ya Dr Slaa ni kidogo sana ukilinganisha na Mbunge mwenye vikao vingi vyenye marupu rupu mengi.
Kiujumla mkuu hapa unapotosha.
 
Hivi ukienzi kaburi, maana yake, aliyezikwa humo ndani badi yu hai? Au ukienzi picha ya marehemu inaama huyo mtu bado yu hai?

Masharti ya uachama wa CCM yamo kwenye katiba, and I dont even understand CCM watatibiwa na dawa gani ili wawe wanasoma? Na kama wanashindwa kusoma mistari michache inayohusu uanachama, kwanini tuwaamini kwenye ku-sign mikataba?

Kwa kuongeza,
Kama ukiwa mwanachadema huku una kadi mfu ya ccm kama Dr Slaa unakuwa na ujasiri wa kuwataja mafisadi hadharani akiwepo Rais. Basi mimi jimboni kwangu nawahitaji wanaccm watakaojiunga na Chadema ambao nitawaachia kadi za ccm halafu wafanye kazi kama Dr Slaa.
 
Back
Top Bottom