:target:Another nonesense! kwa hiyo wewe na mfyatukaji Nape mnafikiri hiyo n credit? ndo maana Dr wa ukweli kawambia kuwa anayo na anaienzi na naamini c wewe wala Nape aliyemwelewa Dr. na ndiyo maama bila aibu umejifaragua kuleta janvin uozo huu.Nape ni kijana ambaye mara nyingi kama siyo zote huwa mropokaji na hana khoja ya tija ni mtazamo ambao ni sahihi kabisa.
Nape alipodai viongozi wengi wa cdm wana kadi za ccm na huzilipia michango ya kila mwaka kimyakimya ungelitegemea cdm aidha kumpuuzilia mbali au kumpa mojawapo ya majibu yafuatayo:-
a) ccm wamekuwa mstari wa mbele kupokea kadi za wanachama wa upinzani ambao wameamua kujiunga na ccm badala ya kuzirudisha kwenye vyama husika kama kadi tajwa zinavyoweka bayana juu umiliki wa kadi husika. Kwa hiyo ccm kutarajia viongozi wa cdm kuzirudisha kadi za ccm kwa ccm ni unafiki. ccm ionyeshe njia kwa kurudisha kadi zote tajwa za vyama vya upinzani walizokabidhiwa khalafu ndiyo ije na maswali ya kuulizia kadi zao zilizoko upinzani.
b) Kama Nape anao ushahidi wa hilo angeliripoti kwa msajili wa vyama vya siasa kwa sababu ni makosa ya jinai kuwa mwanachama wa chama cha siasa zaidi ya kimoja.
c) Nape atoe ushahidi kwa tuhuma zake juu ya malipo ya michango husika kabla hajajibiwa.
Kwa kuchelea kutoa majibu tajwa na kukiri ana kadi ya ccm na kuwa anaienzi kikamilifu, Dr. Slaa kaingizwa "kingi" na Mpayukaji Nape kwenye nyanja zifuatazo:-
i) Je Dr. Slaa anaweza kuienzi kadi ya ccm kwa kuwa mwanachama mfu au kwa kuwa mwanachama hai kwa maana ya kulipia michango husika kila mwaka?
ii) Je kwa kuienzi kadi ya ccm ambayo ni mali ya ccm huku kila nafasi ikijitokeza Dr. Slaa hupokea kadi za ccm kutoka kwa wanachama wapya wa cdm ambao wanatoka ccm haoni yeye ni mnafiki? Dr. Slaa kadi yake kumbe kaibana lakini za ccm anapokea badala ya kuwaasa nao wazienzi au hata basi kubaini masilahi ya muda mrefu aliyonayo juu ya kadi husika........... badala ya kuzipokea kadi za ccm huku yeye binafsi ana masilahi mazito ya kuienzi kadi tajwa tena kimya kimya.
iii) Kwa kukiri kadi anayo na kuwa anaienzi anaonyesha jinsi ambavyo alivyo ndumila kuwili na kutia mashaka makubwa kama yeye siyo askari mamluki ndani ya cdm ambayo ccm humtumia kuidhoofisha badala ya kuimarisha. Mfano hai ni pale ambapo alidai ana ushahidi JK kaiba kura zake na hakupaswa kutangazwa Raisi lakini hadi leo kabana kimya na huo ushahidi (Kama kweli upo au kauli ya asiyekubali kushindwa) kama siyo kula sahani moja na mahasimu wake kisiasa ni nini?
iv) Kitendo cha kuwa na kadi ya chama ambacho Dr. Slaa siyo mwanachama kinakiuka masharti yote ya kadi hiyo sasa kama haheshimu masharti husika hivi sheria zetu kweli angelizithamini kama angelishinda uraisi?
v) Upeo wa Dr. Slaa nao unatia mashaka sana kama mitazamo hii haikumpitia kichwani kwake kabla hajatoa majibu husika na kutathmini athari zake.
Kweli upinzani tz ni kulitumika tumbo; kama ilivyo ccm, na ndiyo maana Dr. Slaa kabla hajakubali kugombea uraisi alihakikisha cdm inaingia mkataba naye kumlipa sawa na mbunge nafasi ambayo hatakuwa nayo kwa miaka mitano (2010-15) na hivyo kuleta upendeleo usiyo wa lazima ndani ya waajiriwa ndani ya cdm....Kumbuka "Some animals are equal but others are more equal than others"............Orwellian principle
kwa taarifa yako mtu anapohama chama kimoja kwena kingine harudishi kadi kule anakotoka bali anaikabidhi kule anakokwenda. hivyo kwa kuwa Dr Slaa ndie katibu wa chama na ndiye mtunza kumbukumbu wa chama anatunza kadi yake na pia anatunza kadi zote za ccm zilizokabidhiwa kwake zilizotoka kwa wale wote ambao walikuwa wana ccm na sasa wapo cdm. na ndo maana hata kadi za waliookuwa wana cdm na sasa wapo ccm hazikurudi cdm bali zilikabidhwa kwa uongozi wa ccm.
Sasa nikuingize shule kidogo, kadi huwa azirudishwi unakotoka bali unakokwenda ili kutunza kumbukumbu ya watu uliowavuna toka kwa mpinzani wako. KARAGABAHO!