domokaya
JF-Expert Member
- Apr 22, 2010
- 3,588
- 1,758
Kwa utumbo ulioharisha hapa na uhakika hujui maana ya demokrasia, tanzania hakuna udikiteta na demokrasia vilevile hakuna. Ila kwa akili zako nimekuona wewe unapoana hakuna udikiteta unaita ni demokrasia aibu ilioje hii? Nenda kajifue upya uje utueleze demokrasia ni nini?
Blac Kid katika jamvi la weledi hoja hujibiwa kwa hoja, hoja dhaifu huangushwa na hoja yenye nguvu Barbarosa amejenga hoja yake, ameipanga, kama wewe unaamini na kujua kuwa hoja yake ni dhaifu basi jenga hoja yenye nguvu na si kufanya haya uliyoyafanya, umetukana halafu hujasema kitu. Eleza unachokifahamu wewe kuhusu demokrasia, eleza kwa nini unadhani hakuna demokrasia na demokrasia gani ungeitaka wewe maana kuna demokrasia za aina nyingi. Pengine demokrasia anayoizungumzia Barbarosa si ile unayoitaka wewe, mi naona hicho ndio kingekuwa kipimo bora kabisa cha kupima akili za mwanajamvi mwenzako kuliko kuhamaki na kujionesha namna ulivyo na uwezo wako wa kujenga na kuhimili hoja za watu wengine