Hatari ya mafanikio - CHADEMA/UKAWA & Lowassa

Hatari ya mafanikio - CHADEMA/UKAWA & Lowassa

Nadhani ni mwandishi wa kimarekani Cristoper Dikens kama sijakosea jina, wakati Marekani ikijiandaa kuishambulia Iraq ili kumuondoa Sadam madarakani mandishi huyu aliandika makala "The perils of victory" Kwa Kiswahili unaweza kusema “hatari za ushindi”. Kwenye makala hii alitahadharisha mambo ambayo yangetokea baada ya ushindi wa kijeshi wa marekani dhidi ya Sadam. Alitabiri karibu kila kilichotokea baadaye kuanzia the cilivil war hadi kugeuka kwa Iraq kuwa a save heaven kwa magaidi.

Si lengo langu kuijadili makala ile, nimechukua kichwa cha makala ile vile kinawiana sana na yanayoelekea kutokea kwenye siasa za Tanzania kwa sasa. Kuna fununu kwamba kada wa CCM Mh Edward Lowassa anaelekea ku hama chama chake na kujiunga na chama kikuu cha upinzani (CDM) na labda akapitishwa kugombea uraisi kupitia UKAWA.

Uchambuzi wangu finyu unaniambia uwezekano wa Lowassa kushinda uraisi kupitia UKAWA ni mkubwa. Kwa nini! Wengi wanafikiria juu wa watu walioko nyuma yake lakini sidhani kama hilo ndilo lenye umuhimi wa kwanza. Kuna mambo kadhaa yanayompa Lowassa na UKAWA nafasi nzuri ya kuiangusha CCM.

CONNECTIONS ZA LOWASSA NDANI YA SYSTEM NA CHAMA Kushinda uchaguzi ni zaidi ya kuungwa mkono na watu, ni zaidi ya kupigiwa kura za kutosha. Uchaguzi ni kama vita na unapojipenyeza kwenye ngome ya adui yako na kujua anachopanga kufanya hakika una nafasi nzuri zaidi ya kushinda. Lowassa ana watu ndani ya system na CCM. Kuna watakaotoka naye iwapo atatoka (wana CCM) na kuna watakaobaki na kuendelea kumtumikia kichini chini wakiwa CCM, kuihujumu CCM toka ndani. Watu wake ndani ya system watasaidia sana kukabili juhudi wa system kuuhujumu upinzani. CCM na system iliyoko nyuma yake italazimika kupigana vita mbili kwa wakati mmoja, vita na upinzani wa wan je upande mmoja na upande wa pili itakuwa vita dhidi ya upinzani wa ndani. War on two fronts is the last thing strategist would wish for.

RASILIMALI FEDHA Ni wazi kuwa nyuma ya Lowassa kuna massive financial resources kulinganisha na kile ambacho CDM/UKAWA inaweza ku mobilize bila Lowasa. Rasilimali fedha ni muhimu sana kushinda uchaguzi, huu ni mchakato ghali sana ambapo uwezo wa kifedha una nafasi yake katika kuleta matokeo.

ORGANISATION Mnyonge mnyongeni ila haki yake mpeni, 4u movement ilikuwa the best organised campaign within CCM, ilikuwa movement iliyoazima mbinu nyingi za kibiashara kufanya siasa, kosa kubwa lilikuwa ni kutokuweka msisitizo wa kutosha kwenye siasa yenyewe, siku nikiwa na nafasi nitalieleza hili kwa kina. Sasa organisation hii ikijumlishwa naya UKAWA itakuwa ni kikosi mahiri kabisa na tutaona mambo mapya kwenye kampeni za kisiasa. Sioni namna gani CCM inaweza kutengeneza timu ya kushindana na hii hapa.

WATU Hili wa watu nimelipa kipaumbele cha mwisho, Yes Lowasa ana watu wa kutosha (watu wa kawaida) japo si wengi kama anavyotaka kutuaminisha, jambo kubwa hapa watu hawa wengi wao si undecided voter bali ni wapiga kura wa CCM, watu wa Lowasa wana double effect iwapo wataipigia kura UKAWA, kwanza watoongeza kura za UKAWA na pili watapunguza kura ambazo kwa kawaida CCM inakuwaga imeshajihakikishia.

JE LOWASA NA CHADEMA/UKAWA WANA AGENDA MOJA?
Lowasa anautaka uraisi kwa gharama yeyote na UKAWA wanataka kuchukua dola. Hapa they both have something in common ila ukienda mbele zaidi utagundua wanaachana. Siamini kama Lowasa anataka madaraki ili kuleta mabadiliko chanya kwa Tanzania na Watanzania, kama ni hivyo basi hilo ni la mwisho katika vipaumbele vyake. Namuona kama mtu anayeendeshwa zaidi na ego yake na maslahi yake binafsi yale ya marafiki zake. Upande wa pili kuna element ndani ya UKAWA/CDM strong enough elements zilizodhamiria kuleta mabadiliko chanya kwa Tanzania/watanzani. Ni wazi kuwa pande hizi mbili kila moja inamjua mwenzia fika, ndoa hii iwapo itafungwa haiongozwi na mapenzi bali maslahi fulani fulani ya pande hizi mbili, mengine yenye manufaa kwa Tanzania na mengine yasiyo na manufaa kwa Tanzania. Of course siasa ni mchezo wa mahesabu makali na average brains zinaweza zisielewe most of the policial moves, siasa haziongozwi na hisia za mapenzi au chuki, zinaongozwa na maslahi ya mudu mrefu.

NINI HATARI YA USHINDI WA UKAWA? CDM/UKAWA wanaamini wataweza kudhibiti Lowassa baada ya kumtumia kuchuka dola, hili si jambo rahisi sana kwa kaliba yake Lowasa ninayemfahamu. Uwezo wake wa kujua bei za watu na staili yake ya kufanya siasa isiyo na jambo la kuonea aibu kufanya iwe baya kiasi gani inatoa picha tofauti. Naona hatari ya Lowasa kuununua uongozi wa juu wa CDM/UKAWA na akaishia yeye kuwaendesha badala ya wao kumuendesha. Hili likitokea tutaona muendelezo wa uozo ule ule tuliouona ndani ya serekali ya CCM na watu watajiuliza ilikuwa ni kwa manufaa gani waliiondoa CCM madarakani? Mbona majizi yale yale yaliyotamalaki chini ya utawala wa CCM bado yanaendelea kubaka rasilimali zetu chini ya utawala wa UKAWA? Huo utakuwa mwisho wa kisiasa wa baadhi ya vyama ndani ya UKAWA, nadhani muathirika namba moja atakuwa CHADEMA.

Hatari hii ikiwa kweli tutasema “not all is lost”: kwanza itakuwa ngumu sana kupitisha mambo bungeni kwa msimamo wa chama, for sure no matter what happens UKAWA ikishinda hatutaona chama kimoja kikiwa na udhibiti wa bunge kama ule iliokuwa nao CCM. Hii ni habari njema sana kwa wapenda mabadiliko. Pili: Baada ya kuiondo CCM madarakani, itakuwa kazi nyepesi sana kuving’o vyama vitakavyofuatia, CCM ni chama dola, chama kilichotuletea uhuru, chama chenye mizizi iliyojikita chini sana, hao wengine watakuwa wepesi sana kuwaondoa na tutaendelea kubadilisha vyama hadi tupate watawala sahihi. Hakutakuwa na chama kimoja kinachohodhi madaraka kama ilivyo CCM sasa!

HITIMISHO Kama hitimisho, iwapo Lowassa atahamia UKAWA kuna uwezekano mkubwa wa kuong’oa CCM madarakani japo kuna hatari kubwa ya uozo wa CCM kujirudia chini ya utawala huo mpya. Hata hivyo bado naona “it is a risk worth taking! Kuiondoa CCM madarakani itakuwa hatua ya kwanza, tutakuwa tumeondoa kikwazo kikubwa kabisa cha kwanza hivyo vingine tutaendele navyo hatu kwa hatua.

Umeandika hoja chanya kwa asilimia 75 na hoja hasi kwa asilimia 25.Hii inakufanya uwe na hoja chanya asilimia 50.Sio mbaya!

Kuna vitu tunatofautiana ufikiri,ntataja viwili:
#War on two fronts is the last thing a strategists would wish for.
#Na hoja ya kwamba ajenda ya mabadiliko ni ya Ukawa na sio Lowasa.

Hoja ya kwanza inapingwa tu na hali halisi duniani kwa sasa.Every individual,every nation,every political party has war on multiple fronts.Organization,discipline and leadership ndio determinants za mafanikio.
Ndio maana CCM inapaswa kujitafakari sana kwenye nafasi ya mwenyekiti na katibu mwenezi wa chama.Nape anawagarimu sana na matamshi ya mihemko.Magufuli is not mwenyekiti material!

Hoja ya pili nayenyewe haina tu uhalisia kwenye siasa,Muungano wa kisiasa is never a marriage made in heaven.Hizi ni dili za Muda mfupi.Kuna notion unataka kuileta kama Lowasa anaweza kutaka kujenga ufalme ndani ya Ukawa!
I strongly doubt that for 2 reasons:
1.He couldn't do that in CCM all his life time,how could he do it in Ukawa within 5 or 10 years?
2.The environment for empire building in short time is not there.Ukawa is too many pieces to glue together easly and I say this frankly given his age.
 
Nadhani ni mwandishi wa kimarekani Cristoper Dikens kama sijakosea jina, wakati Marekani ikijiandaa kuishambulia Iraq ili kumuondoa Sadam madarakani mandishi huyu aliandika makala "The perils of victory" Kwa Kiswahili unaweza kusema “hatari za ushindi”. Kwenye makala hii alitahadharisha mambo ambayo yangetokea baada ya ushindi wa kijeshi wa marekani dhidi ya Sadam. Alitabiri karibu kila kilichotokea baadaye kuanzia the cilivil war hadi kugeuka kwa Iraq kuwa a save heaven kwa magaidi.

Si lengo langu kuijadili makala ile, nimechukua kichwa cha makala ile vile kinawiana sana na yanayoelekea kutokea kwenye siasa za Tanzania kwa sasa. Kuna fununu kwamba kada wa CCM Mh Edward Lowassa anaelekea ku hama chama chake na kujiunga na chama kikuu cha upinzani (CDM) na labda akapitishwa kugombea uraisi kupitia UKAWA.

Uchambuzi wangu finyu unaniambia uwezekano wa Lowassa kushinda uraisi kupitia UKAWA ni mkubwa. Kwa nini! Wengi wanafikiria juu wa watu walioko nyuma yake lakini sidhani kama hilo ndilo lenye umuhimi wa kwanza. Kuna mambo kadhaa yanayompa Lowassa na UKAWA nafasi nzuri ya kuiangusha CCM.

CONNECTIONS ZA LOWASSA NDANI YA SYSTEM NA CHAMA Kushinda uchaguzi ni zaidi ya kuungwa mkono na watu, ni zaidi ya kupigiwa kura za kutosha. Uchaguzi ni kama vita na unapojipenyeza kwenye ngome ya adui yako na kujua anachopanga kufanya hakika una nafasi nzuri zaidi ya kushinda. Lowassa ana watu ndani ya system na CCM. Kuna watakaotoka naye iwapo atatoka (wana CCM) na kuna watakaobaki na kuendelea kumtumikia kichini chini wakiwa CCM, kuihujumu CCM toka ndani. Watu wake ndani ya system watasaidia sana kukabili juhudi wa system kuuhujumu upinzani. CCM na system iliyoko nyuma yake italazimika kupigana vita mbili kwa wakati mmoja, vita na upinzani wa wan je upande mmoja na upande wa pili itakuwa vita dhidi ya upinzani wa ndani. War on two fronts is the last thing strategist would wish for.

RASILIMALI FEDHA Ni wazi kuwa nyuma ya Lowassa kuna massive financial resources kulinganisha na kile ambacho CDM/UKAWA inaweza ku mobilize bila Lowasa. Rasilimali fedha ni muhimu sana kushinda uchaguzi, huu ni mchakato ghali sana ambapo uwezo wa kifedha una nafasi yake katika kuleta matokeo.

ORGANISATION Mnyonge mnyongeni ila haki yake mpeni, 4u movement ilikuwa the best organised campaign within CCM, ilikuwa movement iliyoazima mbinu nyingi za kibiashara kufanya siasa, kosa kubwa lilikuwa ni kutokuweka msisitizo wa kutosha kwenye siasa yenyewe, siku nikiwa na nafasi nitalieleza hili kwa kina. Sasa organisation hii ikijumlishwa naya UKAWA itakuwa ni kikosi mahiri kabisa na tutaona mambo mapya kwenye kampeni za kisiasa. Sioni namna gani CCM inaweza kutengeneza timu ya kushindana na hii hapa.

WATU Hili wa watu nimelipa kipaumbele cha mwisho, Yes Lowasa ana watu wa kutosha (watu wa kawaida) japo si wengi kama anavyotaka kutuaminisha, jambo kubwa hapa watu hawa wengi wao si undecided voter bali ni wapiga kura wa CCM, watu wa Lowasa wana double effect iwapo wataipigia kura UKAWA, kwanza watoongeza kura za UKAWA na pili watapunguza kura ambazo kwa kawaida CCM inakuwaga imeshajihakikishia.

JE LOWASA NA CHADEMA/UKAWA WANA AGENDA MOJA?
Lowasa anautaka uraisi kwa gharama yeyote na UKAWA wanataka kuchukua dola. Hapa they both have something in common ila ukienda mbele zaidi utagundua wanaachana. Siamini kama Lowasa anataka madaraki ili kuleta mabadiliko chanya kwa Tanzania na Watanzania, kama ni hivyo basi hilo ni la mwisho katika vipaumbele vyake. Namuona kama mtu anayeendeshwa zaidi na ego yake na maslahi yake binafsi yale ya marafiki zake. Upande wa pili kuna element ndani ya UKAWA/CDM strong enough elements zilizodhamiria kuleta mabadiliko chanya kwa Tanzania/watanzani. Ni wazi kuwa pande hizi mbili kila moja inamjua mwenzia fika, ndoa hii iwapo itafungwa haiongozwi na mapenzi bali maslahi fulani fulani ya pande hizi mbili, mengine yenye manufaa kwa Tanzania na mengine yasiyo na manufaa kwa Tanzania. Of course siasa ni mchezo wa mahesabu makali na average brains zinaweza zisielewe most of the policial moves, siasa haziongozwi na hisia za mapenzi au chuki, zinaongozwa na maslahi ya mudu mrefu.

NINI HATARI YA USHINDI WA UKAWA? CDM/UKAWA wanaamini wataweza kudhibiti Lowassa baada ya kumtumia kuchuka dola, hili si jambo rahisi sana kwa kaliba yake Lowasa ninayemfahamu. Uwezo wake wa kujua bei za watu na staili yake ya kufanya siasa isiyo na jambo la kuonea aibu kufanya iwe baya kiasi gani inatoa picha tofauti. Naona hatari ya Lowasa kuununua uongozi wa juu wa CDM/UKAWA na akaishia yeye kuwaendesha badala ya wao kumuendesha. Hili likitokea tutaona muendelezo wa uozo ule ule tuliouona ndani ya serekali ya CCM na watu watajiuliza ilikuwa ni kwa manufaa gani waliiondoa CCM madarakani? Mbona majizi yale yale yaliyotamalaki chini ya utawala wa CCM bado yanaendelea kubaka rasilimali zetu chini ya utawala wa UKAWA? Huo utakuwa mwisho wa kisiasa wa baadhi ya vyama ndani ya UKAWA, nadhani muathirika namba moja atakuwa CHADEMA.

Hatari hii ikiwa kweli tutasema “not all is lost”: kwanza itakuwa ngumu sana kupitisha mambo bungeni kwa msimamo wa chama, for sure no matter what happens UKAWA ikishinda hatutaona chama kimoja kikiwa na udhibiti wa bunge kama ule iliokuwa nao CCM. Hii ni habari njema sana kwa wapenda mabadiliko. Pili: Baada ya kuiondo CCM madarakani, itakuwa kazi nyepesi sana kuving’o vyama vitakavyofuatia, CCM ni chama dola, chama kilichotuletea uhuru, chama chenye mizizi iliyojikita chini sana, hao wengine watakuwa wepesi sana kuwaondoa na tutaendelea kubadilisha vyama hadi tupate watawala sahihi. Hakutakuwa na chama kimoja kinachohodhi madaraka kama ilivyo CCM sasa!

HITIMISHO Kama hitimisho, iwapo Lowassa atahamia UKAWA kuna uwezekano mkubwa wa kuong’oa CCM madarakani japo kuna hatari kubwa ya uozo wa CCM kujirudia chini ya utawala huo mpya. Hata hivyo bado naona “it is a risk worth taking! Kuiondoa CCM madarakani itakuwa hatua ya kwanza, tutakuwa tumeondoa kikwazo kikubwa kabisa cha kwanza hivyo vingine tutaendele navyo hatu kwa hatua.

Imekaa vizur sna hongera.
 
Mkuu usiwe na wasiwasi. CCM ing'oke kwanza. Uozo mwingine unaobaki utashughulikiwa hatua kwa hatua. Kumbuka hata Roma haikujengwa kwa Siku moja.
 
Nadhani ni mwandishi wa kimarekani Cristoper Dikens kama sijakosea jina, wakati Marekani ikijiandaa kuishambulia Iraq ili kumuondoa Sadam madarakani mandishi huyu aliandika makala "The perils of victory" Kwa Kiswahili unaweza kusema "hatari za ushindi". Kwenye makala hii alitahadharisha mambo ambayo yangetokea baada ya ushindi wa kijeshi wa marekani dhidi ya Sadam. Alitabiri karibu kila kilichotokea baadaye kuanzia the cilivil war hadi kugeuka kwa Iraq kuwa a save heaven kwa magaidi.

Si lengo langu kuijadili makala ile, nimechukua kichwa cha makala ile vile kinawiana sana na yanayoelekea kutokea kwenye siasa za Tanzania kwa sasa. Kuna fununu kwamba kada wa CCM Mh Edward Lowassa anaelekea ku hama chama chake na kujiunga na chama kikuu cha upinzani (CDM) na labda akapitishwa kugombea uraisi kupitia UKAWA.

Uchambuzi wangu finyu unaniambia uwezekano wa Lowassa kushinda uraisi kupitia UKAWA ni mkubwa. Kwa nini! Wengi wanafikiria juu wa watu walioko nyuma yake lakini sidhani kama hilo ndilo lenye umuhimi wa kwanza. Kuna mambo kadhaa yanayompa Lowassa na UKAWA nafasi nzuri ya kuiangusha CCM.

CONNECTIONS ZA LOWASSA NDANI YA SYSTEM NA CHAMA Kushinda uchaguzi ni zaidi ya kuungwa mkono na watu, ni zaidi ya kupigiwa kura za kutosha. Uchaguzi ni kama vita na unapojipenyeza kwenye ngome ya adui yako na kujua anachopanga kufanya hakika una nafasi nzuri zaidi ya kushinda. Lowassa ana watu ndani ya system na CCM. Kuna watakaotoka naye iwapo atatoka (wana CCM) na kuna watakaobaki na kuendelea kumtumikia kichini chini wakiwa CCM, kuihujumu CCM toka ndani. Watu wake ndani ya system watasaidia sana kukabili juhudi wa system kuuhujumu upinzani. CCM na system iliyoko nyuma yake italazimika kupigana vita mbili kwa wakati mmoja, vita na upinzani wa wan je upande mmoja na upande wa pili itakuwa vita dhidi ya upinzani wa ndani. War on two fronts is the last thing strategist would wish for.

RASILIMALI FEDHA Ni wazi kuwa nyuma ya Lowassa kuna massive financial resources kulinganisha na kile ambacho CDM/UKAWA inaweza ku mobilize bila Lowasa. Rasilimali fedha ni muhimu sana kushinda uchaguzi, huu ni mchakato ghali sana ambapo uwezo wa kifedha una nafasi yake katika kuleta matokeo.

ORGANISATION Mnyonge mnyongeni ila haki yake mpeni, 4u movement ilikuwa the best organised campaign within CCM, ilikuwa movement iliyoazima mbinu nyingi za kibiashara kufanya siasa, kosa kubwa lilikuwa ni kutokuweka msisitizo wa kutosha kwenye siasa yenyewe, siku nikiwa na nafasi nitalieleza hili kwa kina. Sasa organisation hii ikijumlishwa naya UKAWA itakuwa ni kikosi mahiri kabisa na tutaona mambo mapya kwenye kampeni za kisiasa. Sioni namna gani CCM inaweza kutengeneza timu ya kushindana na hii hapa.

WATU Hili wa watu nimelipa kipaumbele cha mwisho, Yes Lowasa ana watu wa kutosha (watu wa kawaida) japo si wengi kama anavyotaka kutuaminisha, jambo kubwa hapa watu hawa wengi wao si undecided voter bali ni wapiga kura wa CCM, watu wa Lowasa wana double effect iwapo wataipigia kura UKAWA, kwanza watoongeza kura za UKAWA na pili watapunguza kura ambazo kwa kawaida CCM inakuwaga imeshajihakikishia.

JE LOWASA NA CHADEMA/UKAWA WANA AGENDA MOJA?
Lowasa anautaka uraisi kwa gharama yeyote na UKAWA wanataka kuchukua dola. Hapa they both have something in common ila ukienda mbele zaidi utagundua wanaachana. Siamini kama Lowasa anataka madaraki ili kuleta mabadiliko chanya kwa Tanzania na Watanzania, kama ni hivyo basi hilo ni la mwisho katika vipaumbele vyake. Namuona kama mtu anayeendeshwa zaidi na ego yake na maslahi yake binafsi yale ya marafiki zake. Upande wa pili kuna element ndani ya UKAWA/CDM strong enough elements zilizodhamiria kuleta mabadiliko chanya kwa Tanzania/watanzani. Ni wazi kuwa pande hizi mbili kila moja inamjua mwenzia fika, ndoa hii iwapo itafungwa haiongozwi na mapenzi bali maslahi fulani fulani ya pande hizi mbili, mengine yenye manufaa kwa Tanzania na mengine yasiyo na manufaa kwa Tanzania. Of course siasa ni mchezo wa mahesabu makali na average brains zinaweza zisielewe most of the policial moves, siasa haziongozwi na hisia za mapenzi au chuki, zinaongozwa na maslahi ya mudu mrefu.

NINI HATARI YA USHINDI WA UKAWA? CDM/UKAWA wanaamini wataweza kudhibiti Lowassa baada ya kumtumia kuchuka dola, hili si jambo rahisi sana kwa kaliba yake Lowasa ninayemfahamu. Uwezo wake wa kujua bei za watu na staili yake ya kufanya siasa isiyo na jambo la kuonea aibu kufanya iwe baya kiasi gani inatoa picha tofauti. Naona hatari ya Lowasa kuununua uongozi wa juu wa CDM/UKAWA na akaishia yeye kuwaendesha badala ya wao kumuendesha. Hili likitokea tutaona muendelezo wa uozo ule ule tuliouona ndani ya serekali ya CCM na watu watajiuliza ilikuwa ni kwa manufaa gani waliiondoa CCM madarakani? Mbona majizi yale yale yaliyotamalaki chini ya utawala wa CCM bado yanaendelea kubaka rasilimali zetu chini ya utawala wa UKAWA? Huo utakuwa mwisho wa kisiasa wa baadhi ya vyama ndani ya UKAWA, nadhani muathirika namba moja atakuwa CHADEMA.

Hatari hii ikiwa kweli tutasema "not all is lost": kwanza itakuwa ngumu sana kupitisha mambo bungeni kwa msimamo wa chama, for sure no matter what happens UKAWA ikishinda hatutaona chama kimoja kikiwa na udhibiti wa bunge kama ule iliokuwa nao CCM. Hii ni habari njema sana kwa wapenda mabadiliko. Pili: Baada ya kuiondo CCM madarakani, itakuwa kazi nyepesi sana kuving'o vyama vitakavyofuatia, CCM ni chama dola, chama kilichotuletea uhuru, chama chenye mizizi iliyojikita chini sana, hao wengine watakuwa wepesi sana kuwaondoa na tutaendelea kubadilisha vyama hadi tupate watawala sahihi. Hakutakuwa na chama kimoja kinachohodhi madaraka kama ilivyo CCM sasa!

HITIMISHO Kama hitimisho, iwapo Lowassa atahamia UKAWA kuna uwezekano mkubwa wa kuong'oa CCM madarakani japo kuna hatari kubwa ya uozo wa CCM kujirudia chini ya utawala huo mpya. Hata hivyo bado naona "it is a risk worth taking! Kuiondoa CCM madarakani itakuwa hatua ya kwanza, tutakuwa tumeondoa kikwazo kikubwa kabisa cha kwanza hivyo vingine tutaendele navyo hatu kwa hatua.
Ulichosahau kuzungumzia ni kwamba Chama KUBWA kuliko Lowassa!.. Na ule mtandao wake sasa hivi umeshapigwa kombora la kwanza ambalo walitegemea Kikwete alikuwa upande wao wangepita CC bila kupingwa!..

2. Mtandao hatari wa Lowassa ulishatangaza kulipa kisasi kwa kambi ya Kikwete na familia yake hata kabla ya kuingia madarakani kuwa wakiingia madarakani watakiona cha moto sijui kwanza watamvua JK Uenyekiti na kinga zote!. Huwezi kuutafuta urais kwa kutishia watu hasa kumtishia rais wa nchi hata kama.. Kikwete kama mwenyekiti wa CCM na rais wa nch hii ana ushawishi mkubwa sana kwa wananchi kuliko mnavyofikiria na atahakikisha Lowassa haingii IKULU... Chama kubwa!

3. Mbali na kuwa na mtando mkubwa, Kukatwa jina la Lowassa CC haikuwa bahati mbaya, bali ilishapangwa na kukubaliwa kwa sababu ndani ya CC kuna wazee waheshimiwa ambao wanamjua Lowassa kiundani zaidi. Lowassa ana maadui wengi pia ambao kwa njia zake za uungu mtu aliyaweka maisha yao katika wakati mgumu sana haswa wale CCM Asilia toka Mkapa, Mwinyi, Sumaye, Warioba, Salim na wote hawa wanayajua madudu yake mengi hivyo wanamsubiri tu wakati wa kampeni.

4. Mtandano mkubwa wa Lowassa ni watu waloahidiwa vyeo, Kila mshirika ameahidiwa uongozi wa wizara, idara ama shirika na taasisi za Umma hata kabla ya kupimwa uwezo wake kama kiongozi. Hii ni hatari kubwa zaidi kiutawala ikiwa Cartel inajipanga tayari kuchukua nchi. Haya ni Mapinduzi ya nchi kupitia watu hatari kabisa. Mtu mmoja hawezi tishia amani nchini hata kama Apson yupo nyuma yake, .huu ni mwaka wa Usalama wa Taifa kuhakikisha amani inapatikana nchini.

Lowassa hawezi kuwa rais wa nchi hii, Uongozi haupatikani kwa kupitia ukubwa wa Cartel ingelikuwa hivyo Pablo Escoba angekuwa rais wa Colombia!..
 
Lowassa hata akienda chama gani hatashinda urais, Halafu mnapozungumzia ukawa ya lowassa je mmejumuisha vyama vingine kama CUF na wengine? Naona hapa kuna makubaliano ya chadema na lowassa sio lowassa na ukawa, kwa hiyo kuna uwezekano wa lowassa kwenda chadema na akagombea kwa chadema sio ukawa, kwa sababu vyama vingine havijaonyesha kukubaliana na mpango huo,
Hapo ndio ccm watatumia ile ile ya kugawa kura wao wapite kama mwewe,

Mr hero katika ubora wake
 
Nitajie huyo aliyetoka mfumo wa kama CCM halafu akaenda The Hague! Hivi hata unajua The Hague ni nini na kwanini hata ilianzishwa? Unafikiri kila nchi inapelekwa the Hague basi ingekuwa hivyo kungejaa huko Tha Hague!
Mbona Kagame anapiga risasi live wapinzani kila siku na hayuko The Hague? Na anakula bata na wazungu kila siku tena ni hivi majuzi wazungu wamemteua kuwa Kiongozi mwenye Utawala Bora Duniani
Mwambie JK naye awapige risasi wapinzani wake kama Kagame kisha uone kitakachotokea. Wapinzani wa Kagame wengi sio wa mfumo wa kidemokrasia bali ni uasi ambao mapambano yake yanakwenda kwa mtindo huohuo wa risasi.
Kwani Gabgo yuko wapi baada ya kuleta za kuleta baada ya uchaguzi? Uhalifu wa kivita ni huo wa kusababisha upotevu wa maisha ya wengine pasipo sababu ya msingi bali matumizi mabaya ya madaraka.
 
Nadhani ni mwandishi wa kimarekani Cristoper Dikens kama sijakosea jina, wakati Marekani ikijiandaa kuishambulia Iraq ili kumuondoa Sadam madarakani mandishi huyu aliandika makala "The perils of victory" Kwa Kiswahili unaweza kusema “hatari za ushindi”. Kwenye makala hii alitahadharisha mambo ambayo yangetokea baada ya ushindi wa kijeshi wa marekani dhidi ya Sadam. Alitabiri karibu kila kilichotokea baadaye kuanzia the cilivil war hadi kugeuka kwa Iraq kuwa a save heaven kwa magaidi.

Si lengo langu kuijadili makala ile, nimechukua kichwa cha makala ile vile kinawiana sana na yanayoelekea kutokea kwenye siasa za Tanzania kwa sasa. Kuna fununu kwamba kada wa CCM Mh Edward Lowassa anaelekea ku hama chama chake na kujiunga na chama kikuu cha upinzani (CDM) na labda akapitishwa kugombea uraisi kupitia UKAWA.

Uchambuzi wangu finyu unaniambia uwezekano wa Lowassa kushinda uraisi kupitia UKAWA ni mkubwa. Kwa nini! Wengi wanafikiria juu wa watu walioko nyuma yake lakini sidhani kama hilo ndilo lenye umuhimi wa kwanza. Kuna mambo kadhaa yanayompa Lowassa na UKAWA nafasi nzuri ya kuiangusha CCM.

CONNECTIONS ZA LOWASSA NDANI YA SYSTEM NA CHAMA Kushinda uchaguzi ni zaidi ya kuungwa mkono na watu, ni zaidi ya kupigiwa kura za kutosha. Uchaguzi ni kama vita na unapojipenyeza kwenye ngome ya adui yako na kujua anachopanga kufanya hakika una nafasi nzuri zaidi ya kushinda. Lowassa ana watu ndani ya system na CCM. Kuna watakaotoka naye iwapo atatoka (wana CCM) na kuna watakaobaki na kuendelea kumtumikia kichini chini wakiwa CCM, kuihujumu CCM toka ndani. Watu wake ndani ya system watasaidia sana kukabili juhudi wa system kuuhujumu upinzani. CCM na system iliyoko nyuma yake italazimika kupigana vita mbili kwa wakati mmoja, vita na upinzani wa wan je upande mmoja na upande wa pili itakuwa vita dhidi ya upinzani wa ndani. War on two fronts is the last thing strategist would wish for.

RASILIMALI FEDHA Ni wazi kuwa nyuma ya Lowassa kuna massive financial resources kulinganisha na kile ambacho CDM/UKAWA inaweza ku mobilize bila Lowasa. Rasilimali fedha ni muhimu sana kushinda uchaguzi, huu ni mchakato ghali sana ambapo uwezo wa kifedha una nafasi yake katika kuleta matokeo.

ORGANISATION Mnyonge mnyongeni ila haki yake mpeni, 4u movement ilikuwa the best organised campaign within CCM, ilikuwa movement iliyoazima mbinu nyingi za kibiashara kufanya siasa, kosa kubwa lilikuwa ni kutokuweka msisitizo wa kutosha kwenye siasa yenyewe, siku nikiwa na nafasi nitalieleza hili kwa kina. Sasa organisation hii ikijumlishwa naya UKAWA itakuwa ni kikosi mahiri kabisa na tutaona mambo mapya kwenye kampeni za kisiasa. Sioni namna gani CCM inaweza kutengeneza timu ya kushindana na hii hapa.

WATU Hili wa watu nimelipa kipaumbele cha mwisho, Yes Lowasa ana watu wa kutosha (watu wa kawaida) japo si wengi kama anavyotaka kutuaminisha, jambo kubwa hapa watu hawa wengi wao si undecided voter bali ni wapiga kura wa CCM, watu wa Lowasa wana double effect iwapo wataipigia kura UKAWA, kwanza watoongeza kura za UKAWA na pili watapunguza kura ambazo kwa kawaida CCM inakuwaga imeshajihakikishia.

JE LOWASA NA CHADEMA/UKAWA WANA AGENDA MOJA?
Lowasa anautaka uraisi kwa gharama yeyote na UKAWA wanataka kuchukua dola. Hapa they both have something in common ila ukienda mbele zaidi utagundua wanaachana. Siamini kama Lowasa anataka madaraki ili kuleta mabadiliko chanya kwa Tanzania na Watanzania, kama ni hivyo basi hilo ni la mwisho katika vipaumbele vyake. Namuona kama mtu anayeendeshwa zaidi na ego yake na maslahi yake binafsi yale ya marafiki zake. Upande wa pili kuna element ndani ya UKAWA/CDM strong enough elements zilizodhamiria kuleta mabadiliko chanya kwa Tanzania/watanzani. Ni wazi kuwa pande hizi mbili kila moja inamjua mwenzia fika, ndoa hii iwapo itafungwa haiongozwi na mapenzi bali maslahi fulani fulani ya pande hizi mbili, mengine yenye manufaa kwa Tanzania na mengine yasiyo na manufaa kwa Tanzania. Of course siasa ni mchezo wa mahesabu makali na average brains zinaweza zisielewe most of the policial moves, siasa haziongozwi na hisia za mapenzi au chuki, zinaongozwa na maslahi ya mudu mrefu.

NINI HATARI YA USHINDI WA UKAWA? CDM/UKAWA wanaamini wataweza kudhibiti Lowassa baada ya kumtumia kuchuka dola, hili si jambo rahisi sana kwa kaliba yake Lowasa ninayemfahamu. Uwezo wake wa kujua bei za watu na staili yake ya kufanya siasa isiyo na jambo la kuonea aibu kufanya iwe baya kiasi gani inatoa picha tofauti. Naona hatari ya Lowasa kuununua uongozi wa juu wa CDM/UKAWA na akaishia yeye kuwaendesha badala ya wao kumuendesha. Hili likitokea tutaona muendelezo wa uozo ule ule tuliouona ndani ya serekali ya CCM na watu watajiuliza ilikuwa ni kwa manufaa gani waliiondoa CCM madarakani? Mbona majizi yale yale yaliyotamalaki chini ya utawala wa CCM bado yanaendelea kubaka rasilimali zetu chini ya utawala wa UKAWA? Huo utakuwa mwisho wa kisiasa wa baadhi ya vyama ndani ya UKAWA, nadhani muathirika namba moja atakuwa CHADEMA.

Hatari hii ikiwa kweli tutasema “not all is lost”: kwanza itakuwa ngumu sana kupitisha mambo bungeni kwa msimamo wa chama, for sure no matter what happens UKAWA ikishinda hatutaona chama kimoja kikiwa na udhibiti wa bunge kama ule iliokuwa nao CCM. Hii ni habari njema sana kwa wapenda mabadiliko. Pili: Baada ya kuiondo CCM madarakani, itakuwa kazi nyepesi sana kuving’o vyama vitakavyofuatia, CCM ni chama dola, chama kilichotuletea uhuru, chama chenye mizizi iliyojikita chini sana, hao wengine watakuwa wepesi sana kuwaondoa na tutaendelea kubadilisha vyama hadi tupate watawala sahihi. Hakutakuwa na chama kimoja kinachohodhi madaraka kama ilivyo CCM sasa!

HITIMISHO Kama hitimisho, iwapo Lowassa atahamia UKAWA kuna uwezekano mkubwa wa kuong’oa CCM madarakani japo kuna hatari kubwa ya uozo wa CCM kujirudia chini ya utawala huo mpya. Hata hivyo bado naona “it is a risk worth taking! Kuiondoa CCM madarakani itakuwa hatua ya kwanza, tutakuwa tumeondoa kikwazo kikubwa kabisa cha kwanza hivyo vingine tutaendele navyo hatu kwa hatua.

Low.....war....Sir
 
Kama waliweza kumkata akiwa CCM humo humo akiwa nje ya CCM atakuwa mlaini kama kate uliochovywa kwenye chai
 
Usiishushe CCM kwa kiasi hicho! CCM ni Chama Dola usisahau hilo, kama Bw.Lowasa akihamia CHADEMA ujue sasa Bw.Lowasa siyo tu adui wa CCM bali ni adui wa Serikali ya JMT na mfumo wake wote kuanzia TRA, Polisi, Magereza, JWTZ n.k chini ya Raisi wa JMT ambaye ndiye Kiongozi wa CCM, usisahau pia uhusiano mzuri wa TanZania na nchi kubwa Duniani kama Uchina, Marekani, Ulaya n.k hawa wote mpaka sasa hivi wanaipenda na kuikubali TanZania kama ilivyo kumbuka Upinzani wamejaribu sana kuisemea Serikali ya TanZania kwa wazungu lkn walipuuziwa kwa maana TanZania ni kipenzi cha Wazungu pmj na Wachina!

Nafasi pekee ya Bw.Lowasa na CHADEMA wake ni labda waasi waingie porini kwa kutumia fedha zao walipe wagaidi na kuanza kufanya nchi isitawalike lkn wakifanya hivyo kama wana huo uwezo kumbuka WatanZania watawageuka na kuwaona wanaleta machafuko pmj na UN na wengineo!

Kumbuka mpaka sasa hivi ukisikia CCM na Serikali wako kimya usifikiri wamelala wanaangalia kila kitu na wanajipanga kumbuka wana uwezo tu wa kufungia chombo chochote kile cha habari pmj na JF na hakuna kitu tutafanya! Hivyo kwa kifupi kama Bw.Lowasa kweli anataka kwenda Upinzani basi naweza kusema kama wazungu wasemavyo yuko out of touch with reality!

Comment yako utasema vyama hivi vya siasa vinafanya kazi kinyume na taratibu
 
Dzerzhinsky

Hata Libya, Misri na Iraq nao walikuwa wanawaza kama wewe lakini kwa sasa hawawezi kuwaza kutamani kuwaza,kama wewe.
Achana na mifano ya nchi za kiarabu, zungumzia nchi za kariba yetu Kama Kenya, Zambia n.k hafu tuone Kama point yako itakua Na umuhimu!
 
Last edited by a moderator:
I Salute You My Brother,you Have Brains.The Best Of Analyses
 
Yaani unatumia malengo yetu kiondoa CCM madarakani kwa kumpigia Lowassa kampeni kujiunga CHADEMA na UKAWA hali yakuwa Lowassa ni fisadi........ Lowassa ni fisadi na ataenelea kuwa fisadi. Ye asubili tuchukuwe dora mwaka huu tumfunge na kumfilisi mali. Nae analifahamu hili ndio maana anahangaika kujinga CHADEMA ili kukwepa kifungo. Ashindwe na alege.... atuachie CHADEMA na UKAWA yetu!
 
Usiishushe CCM kwa kiasi hicho! CCM ni Chama Dola usisahau hilo, kama Bw.Lowasa akihamia CHADEMA ujue sasa Bw.Lowasa siyo tu adui wa CCM bali ni adui wa Serikali ya JMT na mfumo wake wote kuanzia TRA, Polisi, Magereza, JWTZ n.k chini ya Raisi wa JMT ambaye ndiye Kiongozi wa CCM, usisahau pia uhusiano mzuri wa TanZania na nchi kubwa Duniani kama Uchina, Marekani, Ulaya n.k hawa wote mpaka sasa hivi wanaipenda na kuikubali TanZania kama ilivyo kumbuka Upinzani wamejaribu sana kuisemea Serikali ya TanZania kwa wazungu lkn walipuuziwa kwa maana TanZania ni kipenzi cha Wazungu pmj na Wachina!

Nafasi pekee ya Bw.Lowasa na CHADEMA wake ni labda waasi waingie porini kwa kutumia fedha zao walipe wagaidi na kuanza kufanya nchi isitawalike lkn wakifanya hivyo kama wana huo uwezo kumbuka WatanZania watawageuka na kuwaona wanaleta machafuko pmj na UN na wengineo!

Kumbuka mpaka sasa hivi ukisikia CCM na Serikali wako kimya usifikiri wamelala wanaangalia kila kitu na wanajipanga kumbuka wana uwezo tu wa kufungia chombo chochote kile cha habari pmj na JF na hakuna kitu tutafanya! Hivyo kwa kifupi kama Bw.Lowasa kweli anataka kwenda Upinzani basi naweza kusema kama wazungu wasemavyo yuko out of touch with reality!

Tumeona vyama dola vikubwa duniani vilivyoangushwa kwa sanduku la kura. Kama ccm ilikuwa na mwanzo pia ina mwisho wake. Na mwisho wake kwa asilimia kubwa mwaka huu.
 
Juhudi ni kubwa ili kuendelea kuficha mafisadi wa nchi. Chadema wajitambue, haingii akilini ganda la ccm kuwa mtaji wa chadema
 
Sumu haionjwi

Hii ni hatari kubwa!
Watu wanaonadiwa na mamluki wa kibiashara inaelekea watainunua UKAWA wakati wowote ule na ni kwa nia moja tu, kukamata dili zote za dola ili wanufaike kiuchumi.

Lakini wananchi makini wanaendekea kugutuka.
Tunajua kuwa hata wapinzani ni watanzania na huko kuna watu makini kitaifa.
Simpigii debe Dr Skaa lakini haingii akilini Dr Slaa kumtangaza Lowassa kuwa fisadi, halafu kula matapishi yake bila maelezo na kumkaribisha fisadi huyo huyo kukipigia debe chama chao.

Maendeleo ya Tanzania ni kuwa na upinzani makini utakao sahihisha kama sio kupiku chama tawala.

Kwa ujinga huu wa kukumbatia ufisadi ulio temwa na chama tawala, UKAWA unawakaribisha kina Rosta na Karamagi and co. iliwagawane rasilmali za nchi hii.

...... mpaka hivi sasa ndani ya UKAWA ni mtafaruku wa kukaribia kusambaratika kwani hawajui wanaenda Ikulu kufanya nini na kwa madhumuni gani kwa mwananchi wa kawaida.

Sumu haionjwi wanaukawa mutakufa bure!!!
 
Back
Top Bottom