Usiishushe CCM kwa kiasi hicho! CCM ni Chama Dola usisahau hilo, kama Bw.Lowasa akihamia CHADEMA ujue sasa Bw.Lowasa siyo tu adui wa CCM bali ni adui wa Serikali ya JMT na mfumo wake wote kuanzia TRA, Polisi, Magereza, JWTZ n.k chini ya Raisi wa JMT ambaye ndiye Kiongozi wa CCM, usisahau pia uhusiano mzuri wa TanZania na nchi kubwa Duniani kama Uchina, Marekani, Ulaya n.k hawa wote mpaka sasa hivi wanaipenda na kuikubali TanZania kama ilivyo kumbuka Upinzani wamejaribu sana kuisemea Serikali ya TanZania kwa wazungu lkn walipuuziwa kwa maana TanZania ni kipenzi cha Wazungu pmj na Wachina!
Nafasi pekee ya Bw.Lowasa na CHADEMA wake ni labda waasi waingie porini kwa kutumia fedha zao walipe wagaidi na kuanza kufanya nchi isitawalike lkn wakifanya hivyo kama wana huo uwezo kumbuka WatanZania watawageuka na kuwaona wanaleta machafuko pmj na UN na wengineo!
Kumbuka mpaka sasa hivi ukisikia CCM na Serikali wako kimya usifikiri wamelala wanaangalia kila kitu na wanajipanga kumbuka wana uwezo tu wa kufungia chombo chochote kile cha habari pmj na JF na hakuna kitu tutafanya! Hivyo kwa kifupi kama Bw.Lowasa kweli anataka kwenda Upinzani basi naweza kusema kama wazungu wasemavyo yuko out of touch with reality!