Hata kama una haki....

Hata kama una haki....

Naona kanda imeguswa ni kujisafisha tu hatukubali kuwa wakabila tutajitoa ufahamu kwa namna yoyote iwayo!
 


Hata kama tuna haki ya kuwasema wale wote tuliowapa mamlaka...
Hata kama tuna haki ya kuwakosoa wale wote tuliowapa mamlaka...
Hata kama tuna haki ya kuwakemea wale wote tuliowapa mamlaka...

Wewe Tundu Lissu wewe...kuwa tu na haki ya kufanya jambo fulani haimaanishi ndo ujitoe kabisa fahamu na kuanza kuropoka ropoka kama mwendawazimu.

Kuwa tu na haki ya kusema, kukosoa, na kukemea haimaanishi ndiyo usitumie hekima na busara katika kufanya hivyo.

Ni lazima uwe mwangalifu. Ni muhimu kuchagua maneno yako vizuri hususan kama wewe ni mmoja wa viongozi wenye ushawishi kwenye jamii.

Kusema rais Magufuli anaendesha nchi kwa upendeleo wa kikabila na kikanda ni uongo. Ni uzushi. Na ulikosea.

Hata kama una haki ya kusema hayo uliyoyasema, huna haki ya kuzusha mambo ili tu ujipatie pointi za kisiasa.

Leo hii likitokea sokomoko kati ya wananchi wa kanda ya ziwa na wa kwingine kisa hayo maneno yako, utalizuia? Si ajabu utajificha kama ulivyojificha mahakamani kule Dodoma ukiogopa kupandishwa kwenye Difenda😀.

Kuwa na haki si sababu ya kuacha kuwa makini. Jirekebishe.

Pangua hoja kwa hoja,

Ni sababu ipi inayomsababisha Naibu waziri wa nishati na madini kuendelea kuwepo kwenye ofisi husika ili hali amekuwa ktk ofisi hiyo kwa miaka zaidi ya 20 akihudumu kama mwanasheria wa wizara na report ya Osoro imesema wazi watendaji wote waliokuwepo kipindi mikataba inapitishwa wanapaswa kuchukuliwa hatua ikiwemo kuwaondosha ktk wizara husika?

Mradi ya Chato Internatinational Aiport bajeti yake imepitishwa na bunge lipi zaidi za mpwa Dotto kusaini mapesa yaelekee huko tena bila kuzingatia mfumo wa kutangaza tenda??

Gorofa la TRA huko chato tender yake ilitangazwa lini na wapi zaidi ya kampuni ya binamu kupewa deal kinyemela??

Watanzania wangapi wamefukuzwa kazi na kunyimwa stahiki zao kwa tuhuma za vyeti feki wakati huo-huo Bashite mtuhumiwa wa cheti feki anabebwa mgongoni na Magufuli?

Ni mtanzania gani mwenye jeuri zaidi ya Bashite anayeweza kuvamia media house akiwa na mitutu ya bunduki pamoja na walinzi wa rais alafu rais husika anasimama mbele ya watanzania na kumpongeza muhusika kwa uvamizi huo??

USUKUMA pekee ndiyo sababu ya vituko hivi vinavyofungiwa macho na mpendwa wenu Pombe.
 
Hivi ninyi mna


Hata kama tuna haki ya kuwasema wale wote tuliowapa mamlaka...
Hata kama tuna haki ya kuwakosoa wale wote tuliowapa mamlaka...
Hata kama tuna haki ya kuwakemea wale wote tuliowapa mamlaka...

Wewe Tundu Lissu wewe...kuwa tu na haki ya kufanya jambo fulani haimaanishi ndo ujitoe kabisa fahamu na kuanza kuropoka ropoka kama mwendawazimu.

Kuwa tu na haki ya kusema, kukosoa, na kukemea haimaanishi ndiyo usitumie hekima na busara katika kufanya hivyo.

Ni lazima uwe mwangalifu. Ni muhimu kuchagua maneno yako vizuri hususan kama wewe ni mmoja wa viongozi wenye ushawishi kwenye jamii.

Kusema rais Magufuli anaendesha nchi kwa upendeleo wa kikabila na kikanda ni uongo. Ni uzushi. Na ulikosea.

Hata kama una haki ya kusema hayo uliyoyasema, huna haki ya kuzusha mambo ili tu ujipatie pointi za kisiasa.

Leo hii likitokea sokomoko kati ya wananchi wa kanda ya ziwa na wa kwingine kisa hayo maneno yako, utalizuia? Si ajabu utajificha kama ulivyojificha mahakamani kule Dodoma ukiogopa kupandishwa kwenye Difenda😀.

Kuwa na haki si sababu ya kuacha kuwa makini. Jirekebishe.



Hivi ninyi mnaomtuhumu Lissu mnawaza vizuri? kwanini mnashindwa kumshauri mungu wenu anayekandamiza demokrasia na kuwatolea watanzania lugha zisizo na staha.
 
Ben si ajabu kapotezwa na Mbowe na CHADEMA yake....

Hata kuanzisha harambee kwenye GoFundMe mchangishe pesa za kutumika kumtafuta hamjafanya.

Aibu.
Mimi siku zote nalia na Red Brigade, kikundi rasmi cha Chadema kwa mujibu wa katiba wa chama hicho kwa ajili ya kulinda maliza chama na viongozi waandamizi wa chama hicho. Ben alikuwa kiongozi mwandamizi , nina imani alikuwa na ulinzi pia. Sikuwahi kusikia kauli kutoka Redbrigade.
 
Mnaoshadadia huo utumbo wa Lissu Serikali kususiwa msifikiri ikisusiwa Magufuli atakosa lolote, narudia vijana angalieni siyo kila jambo ni kushangilia tu kisa limesemwa na unaempenda sana, kwa wale mnaotembea duniani humo mkifanikiwa kufika Harare mtaona maisha ya pale na mjiulize baada ya maisha yale Mugabe kakosa nini na familia yake, maneno kama ya Lissu ni ya kupingwa na kila mwenye akili timamu, ukiwaza chama chako peke yake utashindwa kutumia bongo kufikiria otherwise endeleeni kushadadia ujinga. Tanzania ikisusiwa kiuchumi inamaana pamba, kahawa, madini, katani, korosho na mazao mengine yanafungiwa kuingia ktk soko la dunia sasa jiulize Magu analima kweli hayo mazao? Unafikiri kama huyo mnaesema asusiwe halimi wala hachimbi dhahabu atakaeathirika siyo baba, mama, shangazi au mjombaako...Think twice unaweza kushadadia lkn mwisho ukaĺia wakati Magu anakula pensheni yake, Magu tumsemeni lkn kwa staha huku Utaifa ukiwekwa mbele kama tai

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Daudi we acha tu kila mahali Ni kanda maalum! Chief Chenge, Makonda, Ngeleja wanapeta tu hatukubali sisi wasukuma safari hii lazima mtujue sisi ni Ngoshas family na tutahakikisha hakuna vyama vingi 2020 itakuwa Ni kama enzi za Ng'anamalundi chiefdom! Mmetupa wenyewe dola so what!!! What do you expect!
 
Anasahau hii Ibara ya 29 (5) ya katiba ya JMT ya 1977 ;
.... (5) In order that all persons may benefit from the rights and freedoms guaranteed by this Constitution, every person has the duty to so conduct himself and his affairs in the manner that does not infringe upon the rights and freedoms of others or the public interest.
Halafu mtu ....(jina kapuni) miaka hiyo anasema"...inchi fulani...isusiwe kisiasa, kidiplomasia, kiuchumi..." ! Hii kauli ni threat to the public interest.
 
Wabeba maboksi walioko kule US wanapofanya jitihada kubwa kumtetea dikteta, sijui kama wanaguswa na adha hii waipatayo watumishi wa umma walioko hapa nyumbani.
 
Nilikuwa namuamini sana Namesake wangu lakini kajivua taulo!
 
Anasahau hii Ibara ya 29 (5) ya katiba ya JMT ya 1977 ;

29.-(1) Every person in the United Republic has the right to enjoy fundamental human rights and to enjoy the benefits accruing from the fulfillment by every person of this duty to society, as stipulated under Article 12 to 28 of this Part of this Chapter of the Constitution. Art.6
(2) Every person in the United Republic has the right to equal protection under the laws of the United Republic.

(3) A citizen of the United Republic shall not have a right, status or special position on the basis of his lineage, tradition or descent.

(4) It is hereby prohibited for any law to confer any right, status, or special position upon any citizen of the United Republic on the basis of lineage, tradition or descent.

(5) In order that all persons may benefit from the rights and freedoms guaranteed by this Constitution, every person has the duty to so conduct himself and his affairs in the manner that does not infringe upon the rights and freedoms of others or the public interest.
Fafanua
 
Busara maana yake nini?
unaitambuaje hiyo busara?
Inapimwaje hiyo busara?
Nani na nani nchi hii wanayo hiyo busara?
 
Ngoja nikuwekee toleo la kiswahili hapa;

Masharti ya Jumla Haki ya wajibu muhimu Sheria ya 1984 Na.15 ib.6 29.-(1) Kila mtu katika Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kufaidi haki za msingi za binadamu, na matokeo ya kila mtu kutekeleza wajibu wake kwa jamii, kama zilzivyofafanuliwa katika ibara ya 12 hadi ya 28 za sehemu hii ya Sura hii ya Katiba.
(2) Kila mtu katika Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kupata hifadhi sawa chini ya sheria za Jamhuri ya Muungano.

(3) Raia yoyote wa Jamhuri ya Muungano hatakuwa na haki, hadhi au cheo maalum kwa misingi ya nasaba, jadi au urithi wake.

(4) Ni marufuku kwa sheria yoyote kutoa haki, hadhi au cheo maalum kwa raia yeyote wa Jamhuri ya Muungano kwa misingi ya nasaba, jadi au urithi.

(5) Ili watu wote waweze kufaidi haki na uhuru vilivyotajwa na Katiba hii kila mtu ana wajibu wa kutenda na kuendesha shughuli zake kwa namna ambayo haitaingilia haki na uhuru wa watu wengine au maslahi ya umma.

Bottom lime is; No right is absolute.
 
Halafu mtu ....(jina kapuni) miaka hiyo anasema"...inchi fulani...isusiwe kisiasa, kidiplomasia, kiuchumi..." ! Hii kauli ni threat to the public interest.
Lisu anavunja katiba anayoigiza kuitetea; halafu bila hata kujiuliza wafuasi wake wanashangilia.
 


Hata kama tuna haki ya kuwasema wale wote tuliowapa mamlaka...
Hata kama tuna haki ya kuwakosoa wale wote tuliowapa mamlaka...
Hata kama tuna haki ya kuwakemea wale wote tuliowapa mamlaka...

Wewe Tundu Lissu wewe...kuwa tu na haki ya kufanya jambo fulani haimaanishi ndo ujitoe kabisa fahamu na kuanza kuropoka ropoka kama mwendawazimu.

Kuwa tu na haki ya kusema, kukosoa, na kukemea haimaanishi ndiyo usitumie hekima na busara katika kufanya hivyo.

Ni lazima uwe mwangalifu. Ni muhimu kuchagua maneno yako vizuri hususan kama wewe ni mmoja wa viongozi wenye ushawishi kwenye jamii.

Kusema rais Magufuli anaendesha nchi kwa upendeleo wa kikabila na kikanda ni uongo. Ni uzushi. Na ulikosea.

Hata kama una haki ya kusema hayo uliyoyasema, huna haki ya kuzusha mambo ili tu ujipatie pointi za kisiasa.

Leo hii likitokea sokomoko kati ya wananchi wa kanda ya ziwa na wa kwingine kisa hayo maneno yako, utalizuia? Si ajabu utajificha kama ulivyojificha mahakamani kule Dodoma ukiogopa kupandishwa kwenye Difenda😀.

Kuwa na haki si sababu ya kuacha kuwa makini. Jirekebishe.

Ujinga ni kumkanya mtoto wakati wewe baba una tabia hiyo hiyo.Huu ndio tunaita upuuzi wa kiwango cha lami
 
Back
Top Bottom