Hakika.
Hasira ni jambo moja, ila kufuata hasira inavokutuma ni jambo jingine.
Ni sawa na mtu mlevi anayeamini kuwa kuna baadhi ya matendo anayoyafanya yanapelekewa na pombe anazotumia. Ila mimi nimejenga imani tofauti.
Ukija kujichunguza utagundua kuwa pamoja na hasira zako lakini wewe ni mtu unayejali sana. (Concern, compassion) Ila kauli unazozitoa ukikasirika hupunguza kujiamini kwako na pia huondoa nafasi yako na uaminifu wako na huvunja malengo yako ghafla. Kumbe tatizo sio hasira. Tatizo lako ni kauli. Unaweza kukasirika na ukazichunguza kauli zako.
Mie mwanzoni nilikuwa najizuia kuongea nikikasirika, ilikuwa inasaidia ila mwanzo nilikuwa naharibu nilicholishika au najiumiza mikono kwa kupiga ukuta. Ilifika wakati nikaweza kumudu hasira ndani kwa ndani bila mabadiliko usoni wala bila viashiria vya kauli za maudhi.
Inawezekana