Hard working woman

Hard working woman

dada kama umeyagusa maisha ya dada mmoja na so called mume wake, leo umenifumbua macho nilikuwa sioni nahisi naona. ni kweli wanafanya malavidavi but majukumu yote ni yako wewe(mama).
but huyo dada ameshindwa amemwambia tafute kipato aje wasaidiane sio kumtegemea yeye tu alikuwa anasaidia hadi ndugu zake huko kijijini kwao.

Wananume wasasa ni wavivu wanapenda kuletewa sijui wakoje, na wapo wanawake wengi wanalea familia wanaficha kuogopa aibu, wakati umefika wanawake tuamke .
mwambie awe anapika msosi ale na wanae waoshe vyombo na masufuria waanike . warudishe kabatini,akirudi wajidai hawajala siku mbili tatu ataaanza hata kupiga debe.kama mtu anapewa chakula anashiba kwanini ajitese
 
Wanawake wa zamani wanachapa kazi sana,,

Nimekua maisha ya mama ana kazi nzuri tu kiasi chake lakini sijawahi kuona akilipa ada au kufanya manunuzi yeyote makubwa... Ikifika muda wa kwenda shule anawakumbusha andaeni orodha ya mahitaji mumpe mzee haraka maana ana mambo mengi... Tena unakuta anachokoza wakati tupo kwenye chakula cha jioni mzee anabaki anaguna tu,,

Kuna siku dada yangu alimuuliza mama hela zako zinafanya nini akamjibu ndo hizo hizo zinazolipa ada, kujenga na mambo yote ila mzee ndo anazi control so huwa tunapeana wenyewe kisiri siri lakini mzee ndo anapaswa ku distribute kwenu mi nabaki na hela ya chakula na mahitaji madogo madogo ya familia...

Ila sisi kizazi cha dot com kila mtu mjanja,,, so cost sharing haiepukiki tena kwa kukabana kabana..

I real like Arabs lifestyle Mke anabaki nyumbani au anashinda dukani tu huku kapendeza,, mume ndo anachakarika kila kitu kiende sawa na wanaishi kwenye ndoa miaka mingi bila kukwarudhana,,,

Most of my friends wa kiarabu wamekuwa katika familia zisizo na mgogoro hata kidogo yaani zile za full bata,, na mama zao wavivu wanajua kupika tu na kupaka hina lakini waume zao wanachapa kazi wanahakikisha familia inaishi maisha mazuri, mke anendesha flashy cars, mahitaji kwenye malls, etc yaani mke ni full matunzo,

But wanaume wa kibongo kumtunza mwanamke tunaona kama tunampendelea na wake zetu wa kibongo wamekaa kisanii sanii ndo maana wanaachiwa majukumu maana ukimsaidia hachelewi pesa zake kuonga kina mario

mm huwa nashanga sana spirit ya wababa wa kibongo. yaani mie hadi nimeheka kwa aina hii ya maisha yao. wajua nini??
nimekumbuka siku moja tumekwenda kuuza kahawa ambazo kuchuma tulichuma sisi watoto na mama. tukamenya kuosha na kuanika. magunia siku yanapelekwa KNCU baba alivaa na ovaroli kana kwamba yeye ndiye aliyezichuma.

magunia yakashuka KNCU mzee akatoka karatasi yake akapimiwa kahawa zake kisha akapewa hela akaziia kwenye soksi na kurudi nyumban.

binafsi nilijiuliza mbona baba hata tu kukata matawi kwenye kahawa aliacha mama akaweka mtu wa kukata?? kwann kwenye kuuza tu ndo baba anaenda?? na kibaya zaid shamba lake lilikua la mfano sasa wakija wale watu wa coffee waki mark miche yake msmamizi ni mama ila siku ya kupeleka tu kncu ndo huonekana dah!!

lakian anyways tulikuwa tukijua baba yetu ni mtu anayejipenda na hapendi shida kabisaaa hivyo ni kawaida yake na ni mpaka leo ndivyo alivyo.
 
Ndivyo ilivyo always maisha ni vice versa.
usijali nawe pia ni mmoja wao jiangalie tu.

mimi nimejaribu kuuliza wengi sana ninakuta kama vile wote mambo ni yale yale nikajiuliza hivi wanaume hawa wametulisha nini?? yaani kama ni kuhonga ama kutuhadaaa basi hawa wameturubuni manake zaid ya care na love tumeridhika hatutak kitu kingine kwao. mpaka wamelemaa kabisaaa.

halafu sasa ile familia ambayo mama ni too demanding unakuta baba ni mtafutaji balaa ili aweze kutimiza majukumu yote kwa mama na yake
 
Basi una moyo kama wangu

Siwezi mwambia mtu alipe ada, kwani yeye hajui? Anajidai bize na nini? KAma hawezi kumbuka ada ya watoto?
akisahau ni kulipa tu, afu unaskia ungeniambia. Nabaki na swali, huo ubize wee unautoa wapi wa kusahau ada?

aisee mimi simsumbui mtu juu ya majukumu yake ambayo anatakiwa ayafanye hata siku moja. kama huoni kuna la kufanya utakuta nimefanya na hapo itakuwa basi.
 
basi mama yako ana moyo wa tofauti. binafsi mama yangu tuikuwa tukirudishwa anaumia sana na alikuwa halali hadi apate ada na twende shule.

baba alikuwepo lkn binafsi sijaona alichokitoa ukilinganisha na mama na walikuwa wanapenda had leo so to me nilijua kabisaaa mama ndo mwenzeshaji wa maisha mengine ya ndani hata kama baba ndiye msimamizi.

tena siku watu tuna graduate baba anapewa sifa zote kasomesha watoto ila ukweli mama ndo anajua na sisi. binafsi sionagi manitiki ya kumwambaia mtu naomba hela ya ada ya watoto kwan hawaoni?? kwann nimwambie?? kwanza naanzaje kumwambia?? kwann asisieme ada hi hapa??

Mimi mama yangu namuunga mkono asilimia 100! Angekua mnyonge angefubaaa sanaa. Kwanini atoe yeye helea? Hela za baba zilikuwa zinaenda wapi????????? Kwanini ashindwe kutunza familia wakati ana sources of income?

Maza aliona upuuuzi, wote mnaenda kazini afu kwenye majukumu mwenzio kila siku hana! Kufanyana watoto huko! Yeye akimaliza quota yake ya expenses Baaaaaaass! Hata luku ikiisha mnangoje mdingi arudi. Kama kasafiri anaweka buku 5, ikiisha 5 tena, hadi anahakikisha akirudi anakuta Luku hamna!

Ukienda shule ananipa pocket money nyingi karibia sawa na ada, tena anasisitiza ikiisha tu agiza, sitaki unyasisike, watoto wenyewe 2 tu, usitumie kwa mawazo wakati mzazi wako niko hai. Hapo ada sijapewa naambiwa na dingi nitaleta mwenyewe. Nikimchokoza maza ada bado! Hilo halinihusu kabisaaa, ongea na baba yako muelewane mtajua wenyewe.

The Argument zake naziunga mkono!
1.Wote wanaenda kazini hela za baba zilikuwa zinaenda wapi??????
2.Kama akisema atoe kumsaidia, ndo inageuka tabia, kwa mahesabu yake hela ya mdingi ingetosha kabisaaa na kubaki kutufanya tuishi kama ulaya sema ndo sio mtoaji.
3.Kama anahonga huko, ahonge tu ila viporo vyake vya majukumu ya kifamilia atakuja tu kuvicover kwa muda wake.

Wanaume wa siku hizi bila kukomaaa nao, pesa nyumbani haionekani kabisaaaaa! Yeye zile activities za luxry anazojua mdingi hatotoa hela anakupa tu! Ila kila mtu afanye majukumu yake ya msingi!!!!!! Baaaaaaaaass!
 
rafiki yangu gfsonwin asante kwa mada hii
kabla sijamwaga sumu naomba kuuliza kwanza, wakati mimi nafanya hayo yote ni kwamba huyo husband hana uwezo wa kusaidia hayo? i.e. ana kipato kidogo kuliko mimi? au naye ana kipato cha kueleweka ila anategea kwa hiyo mimi naamua niachane naye na badala yake nijiue tu ili familia iishi maisha mazuri?
 
Last edited by a moderator:
lara 1 mie simsumbui mtu hta kidogo kama anajua wajibu wake .............why shld i do that?? tena nafanya with happiness kwamba sina donge nafsini sasa yeye akili imkae sawa kwamba huyu mama anapata wapi hadi za kufanya haya yote.
 
Last edited by a moderator:
Ni kweli haya yanatokea??

Sitamani hata kuliona lidume la namna hiyo.....

Yaani lenyewe linafanya kazi moja tu ya kumzeesha mtoto wa watu??

Hata sijui nisemeje...inakera sana!!

Babu DC!!
 
rafiki yangu gfsonwin asante kwa mada hii
kabla sijamwaga sumu naomba kuuliza kwanza, wakati mimi nafanya hayo yote ni kwamba huyo husband hana uwezo wa kusaidia hayo? i.e. ana kipato kidogo kuliko mimi? au naye ana kipato cha kueleweka ila anategea kwa hiyo mimi naamua niachane naye na badala yake nijiue tu ili familia iishi maisha mazuri?
sio kwamba hana uwezo ama sio kwamba kipato hake ni kidogo hapana ila tu haoni FP. yaani unakuta baba haoni hata kitasa cha mlango kimeharibika na sio kwamba hana hela yeye anajua kukuta vitu vizuri tu vimefanyika humo ndani siku zote ila aliyevifanya nani ni mama. na hapo utamsikia akikusifia kweli kweli.
 
Mimi mama yangu namuunga mkono asilimia 100! Angekua mnyonge angefubaaa sanaa. Kwanini atoe yeye helea? Hela za baba zilikuwa zinaenda wapi????????? Kwanini ashindwe kutunza familia wakati ana sources of income?

Maza aliona upuuuzi, wote mnaenda kazini afu kwenye majukumu mwenzio kila siku hana! Kufanyana watoto huko! Yeye akimaliza quota yake ya expenses Baaaaaaass! Hata luku ikiisha mnangoje mdingi arudi. Kama kasafiri anaweka buku 5, ikiisha 5 tena, hadi anahakikisha akirudi anakuta Luku hamna!

Ukienda shule ananipa pocket money nyingi karibia sawa na ada, tena anasisitiza ikiisha tu agiza, sitaki unyasisike, watoto wenyewe 2 tu, usitumie kwa mawazo wakati mzazi wako niko hai. Hapo ada sijapewa naambiwa na dingi nitaleta mwenyewe. Nikimchokoza maza ada bado! Hilo halinihusu kabisaaa, ongea na baba yako muelewane mtajua wenyewe.

The Argument zake naziunga mkono!
1.Wote wanaenda kazini hela za baba zilikuwa zinaenda wapi??????
2.Kama akisema atoe kumsaidia, ndo inageuka tabia, kwa mahesabu yake hela ya mdingi ingetosha kabisaaa na kubaki kutufanya tuishi kama ulaya sema ndo sio mtoaji.
3.Kama anahonga huko, ahonge tu ila viporo vyake vya majukumu ya kifamilia atakuja tu kuvicover kwa muda wake.

Wanaume wa siku hizi bila kukomaaa nao, pesa nyumbani haionekani kabisaaaaa! Yeye zile activities za luxry anazojua mdingi hatotoa hela anakupa tu! Ila kila mtu afanye majukumu yake ya msingi!!!!!! Baaaaaaaaass!
lara 1 ni mamako huyu huyu aliyekuwa anafuga kuku na kufanya overtime ili msome au?
well ni kutaka tu kusema kuwa familia nyingi na hatukuanza sisi leo
vitu vinarun kwa nguvu ya mama!
hili nilikua nikiliona nafikir sidhani kama naweza kubadilika sasa!
 
Last edited by a moderator:
Ni kweli haya yanatokea??

Sitamani hata kuliona lidume la namna hiyo.....

Yaani lenyewe linafanya kazi moja tu ya kumzeesha mtoto wa watu??

Hata sijui nisemeje...inakera sana!!

Babu DC!!
babu wewe hujawah kuona haya??
ni ukweli usiopingika kwamba familia nyingi zina run kwa nguvu ya mama.
tena tokea tuakua hadi leo bado mama amekuwa ni mwezeshaji wa kila jambo katika familia kwa mikono yake mwenyewe.
 
sio kwamba hana uwezo ama sio kwamba kipato hake ni kidogo hapana ila tu haoni FP. yaani unakuta baba haoni hata kitasa cha mlango kimeharibika na sio kwamba hana hela yeye anajua kukuta vitu vizuri tu vimefanyika humo ndani siku zote ila aliyevifanya nani ni mama. na hapo utamsikia akikusifia kweli kweli.
samahani rafiki yangu, labda mimi kuna vitu sivielewi.
huyo ni mume wangu kabisa tunaishi wote home.....
watoto tumezaa wote......
maendeleo ya nyumba/watoto/ndugu ni kwa faida yetu wote.....
ana kipato kizuri tu....
kama yeye haoni, si ni wajibu wangu mimi kumkumbusha hapa tunatakiwa tufanye hivi na vile?
nakubaliana nawe kabisa kuwa sisi wamama labda kwa vile tunashinda zaidi nyumbani tunaona mengi kuliko wao, lakini mimi sioni tatizo kushirikishana kwamba tufanye hivi.....
kama yeye hana muda basi alete tu hizo hela mimi nitatafuta mafundi/ nitaenda shule kulipa ada, n.k.....
ninachojiuliza kama mimi inabidi nifanye kazi zaidi ili mambo ya home yaende, yeye hela zake atakuwa anafanyia nini?
 
lara 1 ni mamako huyu huyu aliyekuwa anafuga kuku na kufanya overtime ili msome au?
well ni kutaka tu kusema kuwa familia nyingi na hatukuanza sisi leo
vitu vinarun kwa nguvu ya mama!
hili nilikua nikiliona nafikir sidhani kama naweza kubadilika sasa!

mwali mzima wewe?? jana ulifika salama na ile njia?? je ni rahisi kama ndivyo siku nazuka mabwe fasta mwali.

acha tu hapa watu wabishe ila ukweli tumeona jinsi ambavyo familia mama ndo mwenzeshaji wa kila kitu.
 
rafiki yangu gfsonwin asante kwa mada hii
kabla sijamwaga sumu naomba kuuliza kwanza, wakati mimi nafanya hayo yote ni kwamba huyo husband hana uwezo wa kusaidia hayo? I.e. Ana kipato kidogo kuliko mimi? Au naye ana kipato cha kueleweka ila anategea kwa hiyo mimi naamua niachane naye na badala yake nijiue tu ili familia iishi maisha mazuri?
wanatoa dozi nene eti!
 
samahani rafiki yangu, labda mimi kuna vitu sivielewi.
huyo ni mume wangu kabisa tunaishi wote home.....
watoto tumezaa wote......
maendeleo ya nyumba/watoto/ndugu ni kwa faida yetu wote.....
ana kipato kizuri tu....
kama yeye haoni, si ni wajibu wangu mimi kumkumbusha hapa tunatakiwa tufanye hivi na vile?
nakubaliana nawe kabisa kuwa sisi wamama labda kwa vile tunashinda zaidi nyumbani tunaona mengi kuliko wao, lakini mimi sioni tatizo kushirikishana kwamba tufanye hivi.....
kama yeye hana muda basi alete tu hizo hela mimi nitatafuta mafundi/ nitaenda shule kulipa ada, n.k.....
ninachojiuliza kama mimi inabidi nifanye kazi zaidi ili mambo ya home yaende, yeye hela zake atakuwa anafanyia nini?

rafiki yangu FP, kwanini kila mara uwe ndo mtu unayeazisha jambo wewe?? binafsi mie kwangu iko hivi nitasema kazi iliyoko mbele yetu ila silazimiki kukwambia toa hela ili kufanikisha manake ni wazi wajua kwamba unatakiwa kutoa na usipotoa ala sikuulizi manake ya nini?? kwan wewe ni mtoto??
 
mwali mzima wewe?? jana ulifika salama na ile njia?? je ni rahisi kama ndivyo siku nazuka mabwe fasta mwali.

acha tu hapa watu wabishe ila ukweli tumeona jinsi ambavyo familia mama ndo mwenzeshaji wa kila kitu.
yani nilifika salama mwali wangu!
mabwe fasta!
 
Back
Top Bottom