nia yenu mnataka mzidi kandamiza wanyonge tu hakuna lolote, ahadi si zile zile kila baada ya miaka mi5, sana sana nchi inadidimia, tembo wamepungua, meno ya tembo yamepamba moto, madawa ya kulevya ndo usiseme, wanajulikana lakini hawasemwi, wanateketeza cosmetics lakini madawa yakikakamatwa sijawahi sikia wakiyateketeza, na wanaokamatwa wala sura zao huzioni, sasa tunapelekwa wapi jamani, fikiri kwanza,
sasa hivi ccm ilitakiwa itoe sera zake na waombe msamaha kwa wananchi kwa yaliyotokea, tuyaache ya zamani tuunde serikali mpya yenye hiki na hiki, hapo wananchi watawaelewa, lakini nyie kutukanana tu, uchaguzi ukiisha mtaweka wapi sura zenu, lowassa imekuwa ni sera na ilani ya uchaguzi ccm, lililopo ccm iwaombe wananchi msamaha kwani imewakosea, ukidai haki unang'olewa kucha na meno, sasa hao hao wananchi wamechoka na huu uonevu, mtu anakamatwa kabisa na kosa anakwambia umeona flani alishawahi fungwa kwa hiyo mie sitafungwa na kweli hafungwi,