Hapa ndipo yanapofeli makanisa ya kiroho

Hapa ndipo yanapofeli makanisa ya kiroho

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,508
Reaction score
830,009
Dhima ya kanisa kama taasisi yenye kutoa tumaini kwa waliokata tamaa, wahitaji wa ujenzi wa kiroho ili kuweza kuwa na imani thabiti juu ya kile wanachohubiriwa na kukiamini
Kanisa ni sehemu ya jamii na ni jamii yenye wanadamu... Viumbe wa mwili wenye nyama... Mwili huu wenye nyama ni muunganiko wake na roho... Hivyo basi kanisa kama taasisi ya kiimani haipaswi kushughulika na roho tu bali na mwili pia... Huwezi ukashughulika na kimoja na kuacha kingine na bado ukadhani unatenda kwa ukamilifu.... Utakuwa umekengeuka...!

. Kanisa lina dhima ya kutoa chakula cha kiroho lakini pia na chakula cha kimwili
. Kanisa lina dhima ya kutoa uponyani wa kiroho lakini na wa kimwili pia
. Kanisa lina dhima ya kutoa elimu ya kiroho lakini na ya kidunia pia
. Kanisa lina dhima ya kusaidia matatizo yote ya kiroho lakini na ya kimwili pia

Hili litawezekanaje?
Huyu unayetarajia kumlisha chakula cha kiroho hakikisha kabla hajapata hicho cha kiroho amepata cha kimwili... Hivyo mjengee mazingira na uwezo ili aweze kujihudumia kimwili...
Huyu unayetarajia kumpa uponyaji wa kiroho... Msaidie kwanza apate uponyaji wa kimwili kwa kuwekeza kwenye Huduma za afya na vifaa tiba, hospital, na vituo vya afya
Huyu unayetarajia kumpa elimu ya kiroho.... Msaidie aelimike kiakili kwanza kwa kuwekeza kwenye elimu, shule vyuo na taasisi za kielimu.. Kwa njia hii ataweza kujihudumia kimwili.....
Huyu unayetarajia kumsaidia kiroho msaidie kwa kuwekeza kwenye vituo vya yatima wajane na wasiojiweza.....

Je makanisa haya ya watu binafsi... Yanayojulikana kama ya kiroho yanafanya yote haya ama yameweke tu kiroho kwa kufanya miujiza yenye harufu ya utapeli, wizi na mambo ya kishirikina? Kishapo matoleo ya waumini masikini kutumika kutimiza matakwa ya mwili na tamaa za kidunia zilizopiliza?
They are failing big time... Huruma ni kwa hao waamini na waumini wao
 
Na cha ajabu waumini wao walio wengi ni wale wa maisha ya chini kabisa!!!kutwa nzima nimkushinda makanisani tu hata shughuri za kujipatia kipato huwa cjui wanazifanya saa ngapi??na hasa wanawake jamani hadi wengine ndoa zao zinavunjika kwani yeye ni kanisani tu!!kuna kanisa moja eti mafuta,maji ya ubavuni kwa yesu na sticker ni 75,000!! Na mtu ana nunua!!kuna mwingine nimemuona jana kwenye tv alikuwa anazindua huduma yake daa hayo mavazi kama FIELD MARSHAL ,wa jeshi la anga la Australia!!
 
SAA hivi makanisa mengi yanafanya investment yakutosha ndo maana yanafocus kwenye kurudisha gharama za uwekezaji na kutengeneza faida.
 
Kunawakati nilichemka sana, nilihitaji mwaka mzima wa kupanga maisha yangu upya. Nilikuwa na muda mwingi for nothing.

Kanisani walihitaji secretary, nilijitolea. Kushinda kanisani niligundua vitu vingi sana.

Kuna waliokuja wanatoka hospitali lakini nyumbani hawana chakula hivyo hawawezi kuanza dawa, kuna walioshindwa kulipa pango wanafukuzwa kwenye nyumba.

Kuna wanaotoka jela hawajui jinsi ya kuanza tena maisha uraiani. Basi ilimradi kuanzia saa mbili asubuhi ni simu na hodi mlangoni
 
Last edited:
Nikuulize kidogo mkuu Mshana ukisema makanisa unakuwa na maana ipi?

Hawa kwa mfano Mzee wa Upako, Mwamposa, na wanaofanana nao nao wanaingia kwenye makanisa?

Maana unaweza kuwalaumu kumbe wao hawapo kwenye category hiyo
 
Well Mshara umetoa elimu nzuri sana kwa hawa viongozi wa makanisa. Jambo moja huwa natafakari msingi wa haya makanisa ni nini? Mi naona kuna shida ya kiroho ambazo zimetawala kuna unclean spirit zinatakontrol haya makanisa .Unakuta mwanzilishi wa kanisa alikuwa anahudumu kanisa flani wakatofautiana (hapa tusitake kujua msingi wa tofauti zao)na kiongozi mwingine roho ya uasi(rebellion) inamuingia anaondoka anaanzisha kanisa lake. Kumbuka hata akiondoka atatafuta watu wake wa kuondoka nao sasa asimame madhabahuni sasa majigambo yakutosha too much controlling anaona waumni kama ni mali yake , ataka kunyenyekewa mpk kuna wakati unajiuliza hawa ni kwamba wameamua kuwa mateka wa mtu .

Ndugu zangu wakristo wenzangu tusome biblia tutafute maarifa, na roho wa Mungu hatakuacha upotee ukimuweka Mungu mbele
 
Na cha ajabu waumini wao walio wengi ni wale wa maisha ya chini kabisa!!!kutwa nzima nimkushinda makanisani tu hata shughuri za kujipatia kipato huwa cjui wanazifanya saa ngapi??na hasa wanawake jamani hadi wengine ndoa zao zinavunjika kwani yeye ni kanisani tu!!kuna kanisa moja eti mafuta,maji ya ubavuni kwa yesu na sticker ni 75,000!! Na mtu ana nunua!!kuna mwingine nimemuona jana kwenye tv alikuwa anazindua huduma yake daa hayo mavazi kama FIELD MARSHAL ,wa jeshi la anga la Australia!!
Yani ni kweli kabisa. Wanawake tangu kuumbwa kwa dunia tunatumiwa tu.
 
Thumbs up kiongozi. Viongozi wa makanisa ya kilokole/kiroho wapitie hapa kupata abc's za muhimu kwao.
 
Na cha ajabu waumini wao walio wengi ni wale wa maisha ya chini kabisa!!!kutwa nzima nimkushinda makanisani tu hata shughuri za kujipatia kipato huwa cjui wanazifanya saa ngapi??na hasa wanawake jamani hadi wengine ndoa zao zinavunjika kwani yeye ni kanisani tu!!kuna kanisa moja eti mafuta,maji ya ubavuni kwa yesu na sticker ni 75,000!! Na mtu ana nunua!!kuna mwingine nimemuona jana kwenye tv alikuwa anazindua huduma yake daa hayo mavazi kama FIELD MARSHAL ,wa jeshi la anga la Australia!!
hii ni kitu kibaya sana na inaumiza kuchukua pesa kutoka maskini bora umwibie tajiri aisee
 
Well Mshara umetoa elimu nzuri sana kwa hawa viongozi wa makanisa. Jambo moja huwa natafakari msingi wa haya makanisa ni nini? Mi naona kuna shida ya kiroho ambazo zimetawala kuna unclean spirit zinatakontrol haya makanisa .Unakuta mwanzilishi wa kanisa alikuwa anahudumu kanisa flani wakatofautiana (hapa tusitake kujua msingi wa tofauti zao)na kiongozi mwingine roho ya uasi(rebellion) inamuingia anaondoka anaanzisha kanisa lake. Kumbuka hata akiondoka atatafuta watu wake wa kuondoka nao sasa asimame madhabahuni sasa majigambo yakutosha too much controlling anaona waumni kama ni mali yake , ataka kunyenyekewa mpk kuna wakati unajiuliza hawa ni kwamba wameamua kuwa mateka wa mtu .

Ndugu zangu wakristo wenzangu tusome biblia tutafute maarifa, na roho wa Mungu hatakuacha upotee ukimuweka Mungu mbele
hakika mkuu ukosoma bible hakuna atakaye kudanganya
 
Acheni kuwasema watumishi mtapata laana,kwasababu hao wanaokwenda huko hawaitwi wanakwenda wakiwa na akiri zao timamu na nyie wote mnajua wajinga ndiyo waliwao unakosaje kupambanua wapiga dili na kanisa la Mungu ?
 
Mshana jr spiritual protocol ya kupokea ni kutoa, the more you give the more you receive especially when you give to the less privilage people Luka 6:38
Hii sheria naonaga wamebadilisha wameona wao hawana obligation na wamesahau baraka huambatana na laana. Badala yake wanaeneza chuki kwa T B Joshua badala ya kujifunza na kufanyia kazi.
Angalia pamoja na idadi kubwa ya makanisa bado maasi yameongezeka mana tuna muita Mungu mdomoni na sio kutoka moyoni.


. Kanisa lina dhima ya kutoa chakula cha kiroho lakini pia na chakula cha kimwili
. Kanisa lina dhima ya kutoa uponyani wa kiroho lakini na wa kimwili pia
. Kanisa lina dhima ya kutoa elimu ya kiroho lakini na ya kidunia pia
. Kanisa lina dhima ya kusaidia matatizo yote ya kiroho lakini na ya kimwili pia
 
Back
Top Bottom