Wasema serikali imejitakia yenyewe
Kapuya alipoulizwa akadai `nipo majuu`
Hamad Rashid, kiongozi wa upinzani bungeni,Dk. Wilbroad Slaa, Mbunge wa Karatu (katikati)na Waziri wa kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana Prof. Juma Kapuya.
Wakati serikali ikihaha kujaribu kuzuia mgomo ulioitishwa na Shirikisho la Wafanyakazi nchini (TUCTA), baadhi ya wanasiasa wa vyama vya upinzani wameibuka na kuisuta kuwa imejitakia yenyewe na kuishauri kuwa njia pekee ya kujinasua ni kutekeleza madai wafanyakazi.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na gazeti hili jana kuhusiana na tishio hilo la mgomo, wanasiasa hao wamesema wanaunga mkono mgomo huo, kwa kile walichodai kuwa wafanyakazi wanatekeleza haki yao ya kikatiba baada ya kuona kuwa kwa muda mrefu sasa serikali imekuwa ikipuuza malalamiko yao.
Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni (CUF), Hamad Rashid, alisema serikali imejitakia yenyewe kuingia katika mgogoro na wafanyakazi, kutokana na hatua yake kutosikiliza na kutekeleza madai yao ambayo wamekuwa wakiyatoa mara kwa mara.
Alisema serikali imeshindwa kufuata taratibu na sheria za utumishi katika kushughulikia masuala ya wafanyakazi na matokeo yake wafanyakazi wameona njia pekee ya kudai haki yao ni kupitia migomo.
"Tatizo ni serikali haifuati taratibu na sheria za utumishi, haya mambo ya yakusubiri mpaka mambo ya haribike ndiyo kulazimisha vikao vya maridhiano ni utaratibu mbaya, taratibu na sheria za utumishi zipo kila siku kinachotakiwa ni serikali kuzifuata na si kusubiri vikao" alisema.
Alisema ugoigoi wa serikali katika kushughulikia masuala mbalimbali unawajengea tabia wanachi kuwa matatizo yao hayawezi kushughulikiwa mpaka kwa migomo, akitolea mfano mgomo wa walimu na wafanyakazi wa kampuni ya reli nchini TRL.
"Serikali imewafanya wananchi waone kuwa matatizo yao hayawezi kushughulikiwa mpaka kwa migomo, ona walimu walianza kulipwa madai yao baada ya migomo, halikadhalika wafanyakazi wa TRL ni hadi pale walipoanza migomo. Swali la kujiuliza ni kwanini wanagoma?.... ni kwa sababu madai yao hayasikilizwi na hii ni mbaya sana", alisema kiongozi huyo wa upinzani bungeni.
Hamad Rashid alitoa ushauri kwa serikali kuwa ifanye haraka kukaa meza moja na wafanyakazi ili kujadiliana nao na kisha kutekeleza malalamiko yao kwani endapo mgomo utafanyika kutaleta athari kubwa kwa taifa na wananchi.
Alisema endapo serikali itaendelea kupiga danadana malalamiko ya wafanyakazi, ipo hatari ya kundi la wafanyakazi kuondoa kabisa imani na taasisi zinazoshughulikia masuala yao ikiwemo serikali yenyewe.
Aliongeza kusema kuwa endapo mgomo huo utafanyika, pia utakuwa na athari kubwa kwa uchumi wa nchi kwani shughuli nyingi za maendeleo na huduma zitasimama.
"Mgomo huo pia utawatisha wawekezaji wa nje kuwekeza nchini, kwani wengi wao hupendelea kuwekeza kwenye nchi ambazo hazina migomo" alisema.
Alisema anaunga mkono mgomo huo endapo umefuata taratibu zote zinazotakiwa.
Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilbroad Slaa, alisema anaunga mkono moja kwa moja mgomo huo, kwani ni haki ya msingi ya wafanyakazi pale wanapohisi kutotendewa haki.
Aliilaumu serikali kuwa haipo makini katika kushughulikia masuala ya wafanyakazi na kwamba mgomo ndiyo njia pekee ya wafanyakazi kufikisha kilio chao kwa wahusika. Dk. Slaa, alisema wafanyakazi kwa muda mrefu wamekuwa wakitoa malalamiko yao bila ya kushughulikiwa na kuongeza kuwa hata yeye mwenyewe amekuwa akilipigia kelele suala hilo mara kwa mara lakini serikali imekuwa haisikilizi.
"Nimepiga kelele siku nyingi, bungeni nimezungumza sana na hata kutahadharisha kuwa suala hili litatela matatizo lakini hakuna anayejali, kwa hiyo njia pekee ya kidemokrasia sasa ni mgomo", alisema Dk. Slaa, ambaye pia ni Mbunge wa Karatu na Naibu Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni. Alisema katika bajeti ya mfano iliyopendekezwa na kambi ya upinzani bungeni, walipendekeza kuwa kutokana na kupanda kwa hali ya maisha kima cha chini cha mshahara kiwe Sh 315,000 kwa mwezi lakini serikali ikapuuza.
"Nilionya kuwa tofauti kubwa ya mishahara itajenga matabaka hakuna aliyejali, sasa kwa wakati wa sasa hata hiyo 315, 000 tuliyopendekeza haitoshi tena, maisha yamepanda sana.
Hili ni fundisho kuwa serikali kuwa ikipata notisi za migomo inatakiwa kuchukua hatua za haraka badala ya kutoa visingizo kuwa hadi hali ya uchumi itakapokuwa nzuri ", aliongeza kusema.
TUCTA imeitisha mgomo wa wafanyakazi nchini nzima kuanzia Mei Mosi mwaka huu, wakishinikiza serikali itekeleze madai yao mbalimbali ikiwemo nyongeza ya mishahara na kupunguziwa kodi kwenye mishahara.
Kufuatia tishio hilo, juzi Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Profesa Juma Kapuya, aliitisha mkutano na waandishi wa habari na kuwaomba wafanyakazi wasitishe mgomo huo na badala yake warejee kwenye meza ya majadiliano.
Hata hivyo, pamoja na ombi hilo la waziri, TUCTA imeendelea na msimamo wake wa kuendelea na mgomo huo, kwa kile inachoeleza kuwa tayari yameshafanyika mazungumzo mengi lakini serikali imeshindwa kutekeleza.
Profesa Kapuya alipotafutwa kwa njia ya simu na gazeti hili jana ili aweze kueleza msimamo wa serikali baada ya TUCTA kukataa ombi lake, alisema yupo nje ya nchi.
"Nipo nje ya nchi siwezi kuongea simu yangu haina dola ya kutosha", alisema Profesa Kapuya.
Alipoelezwa kuwa mwandishi wa habari hii ndiye aliyepiga simu hivyo asiwe na wasiwasi wa kuishiwa na muda wa maongezi, alisisitiza msimamo wake na kukataa kuendelea kuzungumza.
"Huku hata ukipiga wewe na mimi nakatwa nisamehe sana sitaweza kuzungumza", alisema waziri huyo.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI
MAoni yangu: serikali itafute ufumbuzi na sio vitisho kwa wafanya kazi kwani ufanisi utapungua. Waziri ni Muongo angalia red highlighted, iweje ukipokea simu ukatwe fedha, nijulisheni jamani.
Hamad Rashid, kiongozi wa upinzani bungeni,Dk. Wilbroad Slaa, Mbunge wa Karatu (katikati)na Waziri wa kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana Prof. Juma Kapuya.
Wakati serikali ikihaha kujaribu kuzuia mgomo ulioitishwa na Shirikisho la Wafanyakazi nchini (TUCTA), baadhi ya wanasiasa wa vyama vya upinzani wameibuka na kuisuta kuwa imejitakia yenyewe na kuishauri kuwa njia pekee ya kujinasua ni kutekeleza madai wafanyakazi.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na gazeti hili jana kuhusiana na tishio hilo la mgomo, wanasiasa hao wamesema wanaunga mkono mgomo huo, kwa kile walichodai kuwa wafanyakazi wanatekeleza haki yao ya kikatiba baada ya kuona kuwa kwa muda mrefu sasa serikali imekuwa ikipuuza malalamiko yao.
Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni (CUF), Hamad Rashid, alisema serikali imejitakia yenyewe kuingia katika mgogoro na wafanyakazi, kutokana na hatua yake kutosikiliza na kutekeleza madai yao ambayo wamekuwa wakiyatoa mara kwa mara.
Alisema serikali imeshindwa kufuata taratibu na sheria za utumishi katika kushughulikia masuala ya wafanyakazi na matokeo yake wafanyakazi wameona njia pekee ya kudai haki yao ni kupitia migomo.
"Tatizo ni serikali haifuati taratibu na sheria za utumishi, haya mambo ya yakusubiri mpaka mambo ya haribike ndiyo kulazimisha vikao vya maridhiano ni utaratibu mbaya, taratibu na sheria za utumishi zipo kila siku kinachotakiwa ni serikali kuzifuata na si kusubiri vikao" alisema.
Alisema ugoigoi wa serikali katika kushughulikia masuala mbalimbali unawajengea tabia wanachi kuwa matatizo yao hayawezi kushughulikiwa mpaka kwa migomo, akitolea mfano mgomo wa walimu na wafanyakazi wa kampuni ya reli nchini TRL.
"Serikali imewafanya wananchi waone kuwa matatizo yao hayawezi kushughulikiwa mpaka kwa migomo, ona walimu walianza kulipwa madai yao baada ya migomo, halikadhalika wafanyakazi wa TRL ni hadi pale walipoanza migomo. Swali la kujiuliza ni kwanini wanagoma?.... ni kwa sababu madai yao hayasikilizwi na hii ni mbaya sana", alisema kiongozi huyo wa upinzani bungeni.
Hamad Rashid alitoa ushauri kwa serikali kuwa ifanye haraka kukaa meza moja na wafanyakazi ili kujadiliana nao na kisha kutekeleza malalamiko yao kwani endapo mgomo utafanyika kutaleta athari kubwa kwa taifa na wananchi.
Alisema endapo serikali itaendelea kupiga danadana malalamiko ya wafanyakazi, ipo hatari ya kundi la wafanyakazi kuondoa kabisa imani na taasisi zinazoshughulikia masuala yao ikiwemo serikali yenyewe.
Aliongeza kusema kuwa endapo mgomo huo utafanyika, pia utakuwa na athari kubwa kwa uchumi wa nchi kwani shughuli nyingi za maendeleo na huduma zitasimama.
"Mgomo huo pia utawatisha wawekezaji wa nje kuwekeza nchini, kwani wengi wao hupendelea kuwekeza kwenye nchi ambazo hazina migomo" alisema.
Alisema anaunga mkono mgomo huo endapo umefuata taratibu zote zinazotakiwa.
Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilbroad Slaa, alisema anaunga mkono moja kwa moja mgomo huo, kwani ni haki ya msingi ya wafanyakazi pale wanapohisi kutotendewa haki.
Aliilaumu serikali kuwa haipo makini katika kushughulikia masuala ya wafanyakazi na kwamba mgomo ndiyo njia pekee ya wafanyakazi kufikisha kilio chao kwa wahusika. Dk. Slaa, alisema wafanyakazi kwa muda mrefu wamekuwa wakitoa malalamiko yao bila ya kushughulikiwa na kuongeza kuwa hata yeye mwenyewe amekuwa akilipigia kelele suala hilo mara kwa mara lakini serikali imekuwa haisikilizi.
"Nimepiga kelele siku nyingi, bungeni nimezungumza sana na hata kutahadharisha kuwa suala hili litatela matatizo lakini hakuna anayejali, kwa hiyo njia pekee ya kidemokrasia sasa ni mgomo", alisema Dk. Slaa, ambaye pia ni Mbunge wa Karatu na Naibu Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni. Alisema katika bajeti ya mfano iliyopendekezwa na kambi ya upinzani bungeni, walipendekeza kuwa kutokana na kupanda kwa hali ya maisha kima cha chini cha mshahara kiwe Sh 315,000 kwa mwezi lakini serikali ikapuuza.
"Nilionya kuwa tofauti kubwa ya mishahara itajenga matabaka hakuna aliyejali, sasa kwa wakati wa sasa hata hiyo 315, 000 tuliyopendekeza haitoshi tena, maisha yamepanda sana.
Hili ni fundisho kuwa serikali kuwa ikipata notisi za migomo inatakiwa kuchukua hatua za haraka badala ya kutoa visingizo kuwa hadi hali ya uchumi itakapokuwa nzuri ", aliongeza kusema.
TUCTA imeitisha mgomo wa wafanyakazi nchini nzima kuanzia Mei Mosi mwaka huu, wakishinikiza serikali itekeleze madai yao mbalimbali ikiwemo nyongeza ya mishahara na kupunguziwa kodi kwenye mishahara.
Kufuatia tishio hilo, juzi Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Profesa Juma Kapuya, aliitisha mkutano na waandishi wa habari na kuwaomba wafanyakazi wasitishe mgomo huo na badala yake warejee kwenye meza ya majadiliano.
Hata hivyo, pamoja na ombi hilo la waziri, TUCTA imeendelea na msimamo wake wa kuendelea na mgomo huo, kwa kile inachoeleza kuwa tayari yameshafanyika mazungumzo mengi lakini serikali imeshindwa kutekeleza.
Profesa Kapuya alipotafutwa kwa njia ya simu na gazeti hili jana ili aweze kueleza msimamo wa serikali baada ya TUCTA kukataa ombi lake, alisema yupo nje ya nchi.
"Nipo nje ya nchi siwezi kuongea simu yangu haina dola ya kutosha", alisema Profesa Kapuya.
Alipoelezwa kuwa mwandishi wa habari hii ndiye aliyepiga simu hivyo asiwe na wasiwasi wa kuishiwa na muda wa maongezi, alisisitiza msimamo wake na kukataa kuendelea kuzungumza.
"Huku hata ukipiga wewe na mimi nakatwa nisamehe sana sitaweza kuzungumza", alisema waziri huyo.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI
MAoni yangu: serikali itafute ufumbuzi na sio vitisho kwa wafanya kazi kwani ufanisi utapungua. Waziri ni Muongo angalia red highlighted, iweje ukipokea simu ukatwe fedha, nijulisheni jamani.