Mkuu kuna ka system tunako waafrica. Mfano vyuoni mwalimu akifelisha anaonekana ni mtabe kweli kweli!!! Lakini ukienda kwa wenzetu mwalimu akishika mwanafunzi basi huyo mwalim atahuzunika sana!!
Haya tuje kwa rais wetu... Kwake yeye kuwa na roho mbaya na kutoa vitisho kwa watu ndio anaona anaongoza...
Sasa ukienda kwa wenzetu mambo ni tofauti....
Huyo ni Obama rais mstaafu wa marekani!!
Ivi kuna rais anatukanwa kama rais wa marekani?? Achilia mbali obama, trump mwenyewe kila saa anatukanwa!! Je angekua kama sizonje marekani ingekalika??
Kwa kifupi hatuwezi kuwa na mtazamo mmoja japo wote tuna common goal! Kukosolewa ni lazima japo rais wetu hataki!! Rais unatakiwa ujiamini na sio kujishtukia ukiona lissu anaongea!!
Huku kwetu wanaamini maneno makali na vitisho ndio uongozi...kwa kifupi hawajui maana ya uongozi!!
Tanzania ya viwanda haitakuja kwa kamatakamata ya wapinzani, rais unapoteza muda tu!! Bila uongozi bora tutakua tanzania ya vi wonder na sio tanzania ya viwanda!!