Halima Mdee kamtukana Rais kwa tusi gani?

Halima Mdee kamtukana Rais kwa tusi gani?

Sijui kama uzi utaunganishwa.

Ebu Watanzania tuwe watu wa analysis. Watu wengi wamekuwa wakiunga mkono kukamatwa kwa Halima Mdee na kusema kuwa Mdee alimtukana Mtukufu Rais wa Tanzania. Pia wengine wanasema kamkashifu Rais.

Baada ya mjadala mrefu, ebu tuelezane sasa, Rais katukanwa kwa tusi lipi?
Sidhani kama alimtukana Rais ila kwa mujibu wa maelezo ya mkuu wa wilaya ya kinondoni Halima katika hotuba yake alisema ni vema Rais Magufuli akafungwa break..! so anawasaidia polisi kujua ni aina gani ya break ambayo anategemea kuitumia kumfunga rais.
hivyo sidhani kama anatarajiwa kutoka hivi karibuni..
ni mpaka pale polisi watakaporidhika kuwa hiyo aina ya break aliyoisema ndio aliyo ikusudia..
kuna watu wanasumbua Kibiti ni vizuri tukafahamu pia huenda wana mahusiano.
 
kamtukana Rais kimantiki..hana adabu lazima aendelee kushughulikiwa. namnukuu

"eti ipo siku atatuambia tutembee hatujavaa nguo za juu na ni lazima tutii"
kimantiki ni tusi kubwa kwa Rais wa Jamhuri..

wacha anyooshwe tu hamna namna..
Kwanini aseme hivyo kwa namna alivyo mtukufu wetu rais anaweza kusema hayo
 
kamtukana Rais kimantiki..hana adabu lazima aendelee kushughulikiwa. namnukuu

"eti ipo siku atatuambia tutembee hatujavaa nguo za juu na ni lazima tutii"
kimantiki ni tusi kubwa kwa Rais wa Jamhuri..

wacha anyooshwe tu hamna namna..
Sasa kwa mpinzani kutoa huo mfano katika mjadala ni tusi.? Na hapo utamshitaki kwa tusi lipi?
 
kamtukana Rais kimantiki..hana adabu lazima aendelee kushughulikiwa. namnukuu

"eti ipo siku atatuambia tutembee hatujavaa nguo za juu na ni lazima tutii"
kimantiki ni tusi kubwa kwa Rais wa Jamhuri..

wacha anyooshwe tu hamna namna..
Hakuna tusi mkuu, labda kama kiswahili hakipandi....
 
Uzuri kuna kitu kimoja watu wanajisahau sana,aliyemuweka ndani kwa kujipendekeza hicho cheo amepewa kama mtu unvyopewa gazeti usome,dakika yeyote mwenye nalo anaweza kulichukua na ukabakia mikono mitupu
 
kamtukana Rais kimantiki..hana adabu lazima aendelee kushughulikiwa. namnukuu

"eti ipo siku atatuambia tutembee hatujavaa nguo za juu na ni lazima tutii"
kimantiki ni tusi kubwa kwa Rais wa Jamhuri..

wacha anyooshwe tu hamna namna..

Kamtukana wapi? Unaweza kuonyesha hilo tusi? Kama Rais anasema hakuna binti atakaerudi shule baada ya kupata mimba unadhani ni kila mtu atakubaliana nae? Sio kila anachosema Rais lazima kifatwe,vingine ni vya kuacha tu. Kama alisema fyatueni yeye atasomesha,hivi hii ni kauli ya kutolewa na Rais kweli?
Kweli akisema mtembee uchi na nyie mtatembea.
 
Sijui kama uzi utaunganishwa.

Ebu Watanzania tuwe watu wa analysis. Watu wengi wamekuwa wakiunga mkono kukamatwa kwa Halima Mdee na kusema kuwa Mdee alimtukana Mtukufu Rais wa Tanzania. Pia wengine wanasema kamkashifu Rais.

Baada ya mjadala mrefu, ebu tuelezane sasa, Rais katukanwa kwa tusi lipi?

Katukunwa kwa tusi la "lugha isiyokuwa ya staha" "lugha ya maudhi" na kwa kuwa action na reaction always ziko sawa! Mtu huvuna anachopanda!
 
Wenyewe wanadai kwamba alisema Rais "anaropoka" na ipo siku ataamuru raia watembee vifua wazi au peku. Pili, ati kusema "kuna haja ya kuwapa semina elekezi" wagombea wa Urais au "kuwafanyia interview". Hili nalo ni kosa kwa "sheria" zao maana inaimply malaika wetu anaonekana ni unfit and incompetent kwa kazi tuliyompa
 
Kuhoji huku jf kuwa huyo mama alitukana tusi gani haimsaidii chochote. Cha msingi nenda central ukamshauri ale chakula maana jumanne anaweza akafunguliwa kesi ya suicide attempt.
 
Tanzania inawatu wa ovyo hawajawai kutokea Nchi yoyote wasomi wamekua watumwa wa wanasiasa hili mradi wapate shibe wakitokea wakina Mdee ambao wanatukumbusha kwamba Rais sio MUNGU wanatokea wapumbavu wanamweka ndani hii Nchi ni ya ovyo kumtambua mwenyewe PhD na Darasa wote wanafanana akiri bora hata mda mwingine darasa la saba kuliko mwenye PhD mfano kama Lipumba
 
Katukunwa kwa tusi la "lugha isiyokuwa ya staha" "lugha ya maudhi" na kwa kuwa action na reaction always ziko sawa! Mtu huvuna anachopanda!
Mbona ni wengi tu kwa vyeo vyao wana "lugha ya kuudhi" na "isiyokuwa na staha"? Tofauti ni nani kashika kwenye mpini.
 
Umeshajiuliza kwanini amechukuliwa hatua na mkuu wa wilaya na sio chombo cha sheria? Mkuu the 48 hrs of those who only know 3Rs are un questionable!!!
 
Raisi Magufuli anatakiwa ateue mtu atakae muongoza katika mambo ya siasa, hili eneo hafanyi vizuri, anatakiwa awe ni mtu wa kujiamini na kutetea agenda zake bila ukali na ajifunze kudebate na watu wa upinzani bila woga /ukali, kusoma sayansi sio sababu ya kushindwa kuvumilia hoja za upande wa pili, mambo mengine ni kujifunza na kufuatilia. Suala la kukosolewa haliepukiki na akikosolewa ndo njia ya kumjenga awe kiongozi mzuri sio kukumbilia polisi, kwa hili anatuabisha sana. Mimi bado sikubaliani na watu wanaosema Halima amemtusi mheshimiwa Rais, Halima kaongea vizuri tu tena ametoa Rai kwa wananchi kuwa Rais lazima afuate sharia za nchi na matamko yake sio sharia ,kosa lake liko wapi? hebu tueni serious kama Taifa tusiwe na Taifa la bendera kufuata upepo, mawazo tofauti ndo yatajenga nchi hii.
 
Back
Top Bottom