mimi ni mkazi wa kawe kura yangu na ya mke wangu amepata....anadeserve kwa kweli.....
ila kibarua kikubwa ni kummwaga mzee wa NCCR...naona amezindua matawi jimboni kawe na sio sehemu zingine kumbe alikuwa ana malengo binafsi sio ya kichama zaidi.....
ACHENI MAMBO YA SIASA NA DEBE,ningependa kujua ameolewa?
Na je kama ameolewa anaishi vipi na mumewe?Je anafamilia?
Baada ya hapo tujadili sasa uwezo wake kiuongozi
Huyu dada kushinda pale ni ndoto, najua wengi mtakasirika nikisema hivi ila ukweli ndio huo. Walipotaka kugawana kura na Mbatia hapo ndipo kosa limefanyika. Atachukua kidogo, Mbatia kidogo, na yule mrembo wa chama tawala atapata zaidi. Tukutane Oktoba nitawathibitishieni hili. Ila namkubali.
Mbatia ni kibaraka tu. Anafikiri kuwa mwanaume ndio kushinda!
Peleka, ujinga wako huko wanabidii na siyo hapa.... Hivi ni kwa nini unapenda kutisha watu sana? au kwa kuwa umepewa mlungula wa kupiga kampeni kwenye ka-google group kako? eeeh hivi umejiuzulu kuendesha kale ka group?Kuna mmoja ameshashtakiwa kwa kuleta upupu wa north mara na ushahidi unatumika michango ya watu mbalimbali waliyochangia watu hao
Namuita iron lady!!! huyu mheshimiwa anayemaliza muda wake kama mbuge wa kuteuliwa, sasa anagombea kupitia chadema kwenye jimbo ambalo yule anayemalizia kaamua kulikimbia (kwa kumwogopa halima???) na kugombea kupitia nafasi ya NGOs.
kihistoria ametoka kwenye familia ya ccm lakini akaamua kutoka kivyake; akiweka 'historia' kisogoni (kwanini asiitwe bold/iron lady?)
akiwa mjengoni amefanikiwa kutoa mchango wa mawazo kwa ujasiri wa hali ya juu kiasi cha kufikia kukwaruzana na kigogo wa ccm ambaye aliamua kumpeleka 'nusu-mahakama' (kwa 6) lakini kwa ujasiri wake mhe. mdee (as she then was), ilibidi mzee wa bumbuli alazimike ku 'drop charges'
my take:
huyu mdada anafaa kupewa nafasi ya ubunge katika jimbo la uchaguzi la kawe; she is bold and yet beautiful!!!
(huo mtazamo wangu tu usijali sana!!!)
.Mkuu umenena wazi na kweli kabisa. Wapinzani hapa ndipo wanapoudhi wapiga kura. Kwanza kila mpinzani ni lazima atizame maeneo ambayo comperative advantage kwa chama chake ipo. Kwa mantiki hii kama chama pinzani kina political comperative advantage jimbo fulani basi wakiachie ili kipambane na mmbadala wake ambao kwa sasa ni CCM. Kwa kawe ninaona Halima anafaa kuliko Mbatia hivyo Mbatia angemwacha Halima apambane na huyo msanii wa CCM na lazima angedondoka tu. Hata hivyo, bado mapema na Mbatia anaweza shauriwa ajitoe kwa sasa na kutangaza wafuasi wake wampe Halima. Kiukweli kama watabaki vijana hawa jua kabisa jimbo litachukuliwa na CCM. Upinzani ukitaka kufanikiwa ni lazima wakubali kufanya maamuzi magumu. Hii pia hata kwa wagombea urais sikuona mantiki ya kutoamua kumwachia yule ambaye tayari watu wana Imani naye na badala yake mnaweka wagombea ambao hata hawajawahi kusikika katika redio mbao na wengine ni wale wale ambao walishajaribu awamu zilizopita na kushindwa vibaya.
Huyu na Makamba nani amekaa Ki Bongo flava.:becky:Mzuri! hana sura ya uongozi Ameka ki bongo Flava zaidi kama SUGU ! namshauri ASUBIRI KWANZA MUDA WAKE UTAFIKA
Kuweka post kila kona si hoja. Hoja ni kugawana kura na Mbatia. Hivi huyu Mbatia akili zake bado zinafanya kazi sawa kweli, hasomi alama za nyakati bwana ntoke vipi? Hii sio 1995 bana.