Hali ya Mtwara mchana huu

Hali ya Mtwara mchana huu

Chadema wanahusika na kila kitu hapo wanawaokota sana na kutafuta umaarufu wa kisiasa

Tangu Mwaka huu uanze haya ndiyo maoni ya kiwango cha chini kabisa kuwahi kutokea kwenye jukwaa hili !
 
CCM watakata umeme ili mshindwe kusikiliza hotuba ya wizara...

Kama ulikuwepo baba, huku kwetu Tabora maeneo ya Cheyo A umeme wameshakata lakini hata hivyo nimesikia bado naleo wanaendelea kujadili bajeti ya Dr. Mwakyembe na siyo hayo mambo ya hao akina chamaki nchanga.
 
mbona leo ni kuna muendelezo wa mjadala wa bajeti ya uchukuzi ya dr.mwakyembe..nani kawaambia leobajeti ya wizara ya nishati na madini...ukweli hili jambo la gas kuna watu wako nyuma ndio wanahamamsisisha wananchi vyema serikali ikawa makini na hawa watu wachache wanao chochea vurugu baada ya mshakamano na kuwaeleza wananchi ukweli.....

ndugu kibe ..kweli kupenda kuligeuza chongo kuwa kengeza...

hapo nilipo-bold in red...hao watu unaowasema wako nyuma yake kwa ges ya mtwara ni pamoja na sisi watanzania tuliotoka maeneo ya Tarime, nzega, geita, kahama na mererani arusha ambako serikali imechimba madini yetu na kutuacha masikini na huku tukifa kwa maji yenye sumu toka mto tigite...vaa viatu vya watu wa maeneo hayo kisha hamia kuwa mwananchi wa mtwara lazma upingane na serikali na kusema "HAITOKIIIIII...BORA TUFE SOTE ILA HAITOKIIIIIII.

Hako nilipobold in blue...unaongelea serikali gani iwe makini?..kama wapi ilivyokuwa makini..taja sehemu moja tuu unayoijuwa wewe serikali yako tiifu ilishawahi kuwa makini..1)-tarime?? 2)- kahama? 3) geita? 4)- nzega? 5)- mererani? taja nyingine hata kama haipo katika hayo niliyokuwekea kuwa hapa serikali ilikuwa makini kuona wananchi wananufaika na rasilimali zao.

ukisema serikali iwe makini wao wanakuelewa kupiga mabomu na kuuwa watu kama walivyofanya kule geita miaka ya 90 ya mkapa na kuwatoa wazawa na kuwafukia mashimoni wachimbaji wadogowadogo ili "mabwana zao wazungu" wachukuwe utajiri wetu.

KIBE AND THE LIKES OF YOUR CHARACTER...naunga mkono kwa chochote kilichofanywa, kinachofanywa na kitakachofanywa siku zijazo na wananchi wa mtwara na lindi katika kuhakikisha kabla gesi yao haijatoka wanaona na kwa vitendo maendeleo kwenye eneo lao kwanza na taifa letu kwa ujumla wake...CHARITY BEGINS AT HOME....
 
Nielimisheni wana JF. Hivi gesi inayopatikana maili 250 kutoka pwani ya Mtwara inazuiliwa vipi isitoke na wana-Mtwara? Hatua zipi zitachukuliwa na wana-Mtwara ili kuhakikisha meli hazichimbi gesi huko huko baharini na ?

Napata tabu kujua uwezo wa wana-mtwara kufikia huko gesi inakochimbwa na kuizuia. Naomba nielimishwe tafadhali. Maana nasikia kuna meli kila siku ya mungu zinafanya uvuvi haramu kwenye bahari pasipo serikali kujua. Sasa sipati picha wana-Mtwara wakipanda mitumbwi kwenda ku patrol umbali wa kilometer 250.
 
Wana jf, updates kutoka Mtwara zinasema wananchi wameitikia wito wa kutofanya kazi yeyote na kwamba ofisi za serikali tu ndio zinatoa huduma huku kila mwananchi akiwa nyumbani kwake.

.....Inaonekana wako serious serikali isipuuze madai yao... inasemekana walifanya shooping mapema ya mahitaji yao ya kila siku kama chakula na mboga kusubiri bajeti...............

 
Chinga wamekomaa ukigeuka nshale ukiinama nshale hatoki ntu.
 
Wana jf, updates
kutoka Mtwara zinasema wananchi wameitikia wito wa kutofanya kazi yeyote
na kwamba ofisi za serikali tu ndio zinatoa huduma huku kila mwananchi
akiwa nyumbani kwake.

Yaani hata wanafunzi wamegomeshwa kwenda shule?
 
Wana jf, updates kutoka Mtwara zinasema wananchi wameitikia wito wa kutofanya kazi yeyote na kwamba ofisi za serikali tu ndio zinatoa huduma huku kila mwananchi akiwa nyumbani kwake.

Ni habari yenye kuleta matumaini sana. Ila kama nimesikia ya kuwa bajeti ya Wizara ya Nishati sasa itasomwa Jumatatu 22.5 badala ya leo. Huenda ni njama za serikali ya jk kuwawezesha wabunge wa ccm wafanye kikao chao wikiendi hii bila kuwa na wingu la Mtwara na pia kuwafanya watu wa Mtwara siku ya Jumatatu wasiwe na habari ili wasisikilize hiyo bajeti...

Watahangaika sana, lakini ukweli na kwamba wananchi wameshaamka na hakuna kurudi nyuma...
 
mbona leo ni kuna muendelezo wa mjadala wa bajeti ya uchukuzi ya dr.mwakyembe..nani kawaambia leobajeti ya wizara ya nishati na madini...ukweli hili jambo la gas kuna watu wako nyuma ndio wanahamamsisisha wananchi vyema serikali ikawa makini na hawa watu wachache wanao chochea vurugu baada ya mshakamano na kuwaeleza wananchi ukweli.....


Kaka ukweli ni kwamba imearishwa lakini ilikuwa iwasilishwe leo badala itawasilishwa baada ya Rais kukutana na wabunge wa CCM kesho na kesho kutwa.Hivyo itawasilishwa tarehe 20.05.2013 lakini ilikuwa iwasilishwe leo tambua na wao wana ratiba ya vikao vya bunge.Pia wanasema ilikuwa leo Waziri mkuu aulizwe katika kipindi cha maswali ya papo kwa papo..nalo limepigwa chini
 
mbona leo ni kuna muendelezo wa mjadala wa bajeti ya uchukuzi ya dr.mwakyembe..nani kawaambia leobajeti ya wizara ya nishati na madini...ukweli hili jambo la gas kuna watu wako nyuma ndio wanahamamsisisha wananchi vyema serikali ikawa makini na hawa watu wachache wanao chochea vurugu baada ya mshakamano na kuwaeleza wananchi ukweli.....

kila jambo mnasema hayahaya uhalisia hamuuoni?wataje sasa wahusika
 
Back
Top Bottom