Hali ya Mtwara mchana huu

Hali ya Mtwara mchana huu

Taarifa hizo ni za kweli,sizinga ataleta picha mda si mrefu sana

Nyingine hizi hapa

1.jpg


Soko Kuu, Kituo Kikuu cha Mabasi na madula yalikuwa wamefungwa tokea asubuhi

2.jpg


Polisi wakiwa kwenye doria

3.jpg


Hapa ni stendi ya mabasi Mtwara. Sijawahi kuona hii stendi ikiwa tupu hivi. cc Sizinga
 
Last edited by a moderator:
hakuna lolote hapo,hilo bomba la gesi litajengwa tu kwenda Dar es salaam,sisi Mitanzania tunamsimamo wa vitu tusivyokuwa na ufahamu navyo ikiambatana na kutokuwa na msimamo endelevu,uwoga na kutokushirikiana ndiyo ugonjwa wetu mkubwa,akivunjwa mguu mmoja mijitu yote inakimbia kujificha chini ya uvungu wa kitanda na kwenye dali na wengine wanakimbilia kujificha porini wakihofia kukamatwa huku tukiwaacha akina mama na watoto wakiathiriwa na migomo ya kipumbavu isiyokuwa well programmed,tangu nipate akili ya kiutu uzima sijawahi kuskia mgomo au msimamo wowote toka mahali popote Tanzania ukileta matunda sehemu husika,jambo la msingi linalotakiwa kufanyika hapo ni kuwa tayari kumwaga damu kwa namna yoyote ndipo serikali itakuwa sikivu kwa wanachokitaka wananchi
 
Wana JF, updates kutoka Mtwara zinasema wananchi wameitikia wito wa kutofanya kazi yeyote na kwamba ofisi za serikali tu ndio zinatoa huduma huku kila mwananchi akiwa nyumbani kwake.


GOOOOD MOVE AND GOOD STANDING, ...BRAVO MTWARANs!

STRONG AS NO OTHER ....like Niger Delta ni Nigeria! ...'Wananchi kwanza, na uwekezaji uje baadaye'. kila siku serikali inapoleta miradi FEKI ya walaji wachache na viongozi wake walafi, inabadili tu lugha na kuipaka Miradi mafuta ili wananchi wapokee tu kama vipofu...! Mara oooh Richmond ni muhimu sana kuokoa tatizo la dharura la Umeme...!, miaka ikaenda, wananchi wakaliwa! Tena Dowans ikazaliwa-po...wakaendelea kuwanywa wananchi, mara..oooh Dowans itakuwa kubwa zaidi, mitambo imara zaidi na itasaidia kuondoa tatizo la siku zote...!...wananchi wakaliwa!....ikaja TRL...oooh wawekezaji wataleta treni mpya, zitafanya kazi kuzunguka mikoa yote yenye reli, na watajenga reli mpya na mabehewa mapya....TRL wakaja, hawana hata ofisi, jamaa Wahindi hoi, wamebeba mabegi tu, viongozi wakashiba..hadi serikali ikalazimishwa kuwasaidia Wahindi hao wezi kuwalipia wafanyakazi wake mishahara, safari za treni raia wanalala stesheni, hakuna kitu, hadi wiki...wananchi wakaingizwa 'cha kike'...! Yaani...haina idadi miradi feki isiyohesabika...wananchi wanaliwa tu!...Na sasa Serikali hii, inakuja gesi imegundulika, chakula na mirija ya wenye matumbo...imechongwa mipango NA MIRADI hewa..., kazi ya 'SHEMEJI MCHEKAJE'...WANANCHI WAKAGOMA!...hadi Pinda anatumwa Mtwara, analia machozi...eti ni kwa manufaa ya wote...Kumbe yanakuja mapya, Dangote anaweka mitambo ya kuzalisha cement...eti ajira kwa wananchi...yeye hajui thamani ya mtaji wake?? na kumbe inazidi kufumuka...kumbe Dangote kaingia ubia na CCM...! ndio wandeshe mradi wa kiwanda cha Cement...ili kujihifadhi na fedha kuvuka 2015 wawe madarakani, kwa gharama yoyote! Je CCM ndio maana ya Pinda kusema 'wananchi wote?' useless! Ni matumbo ya wachache tu hawa ili wabaki madarakani! kwa nguvu yoyote wakamilishe wizi na ujangili wao kwa kutumia miradi yao ya kuangamiza umma, raia maskini waendelee kuzagaa...na wananchi waendelee kukaa kimya...! HAPANA, SIKU zinakuja...Sio Niger Delta, bali ni Tanzania, na tena Mikoa yote inazinduka...hakuna tena nafasi...kuuibia umma, hali hii itakwisha...YES MTWARA...na LINDI...ndio sasa mwamko wa umma kwa manufaa ya sasa navizazi vijavyo!

Kwa Uchungu...Nawasilisha... Naunga mkono hoja! Mtwara hoyee...na kwingineko, Ngorongoro! Geita...Kahama...na sehemu zote zenye Uranium...NENO MOJA NI HILI..'WANANCHI KWANZA' Ulafi wa viongozi no more!
 
EMT

Hizo Snaps za ukweli sana...

Hiyo inaitwa PASSIVE RESISTANCE...
 
Last edited by a moderator:
ni kwa mtwara mjini huku wilayani shughuli zinaendelea kama kawaida.
Ni kawaida ya vijijini, sikuzote huwa wanakuwa wa mwisho kufunguka. Hata mtaji mkubwa wa CCM kubaki madarakani umekuwa ni vijijini.
 
Historia ya nchi inataja mashujaa kwa majina kama vile Mkwawa,Isike,Songea nk nk.
Historia ya vizazi vijavyo haitaongeza majina tu bali itaweka mikoa shujaa, list ya mikoa shujaa itaongozwa na Mtwara! Ndio, lile jiwe lililo dharauliwa limekuwa jiwe kuu la pembeni. Mikoa mingine hatuna sababu ya kutokuwemo kwenye hiyo list tukufu ya wajukuu na vitukuu vyetu.
Let we join them!
Bravo Mtwara people, hiyo ndio pipoz power in its nature. No politics. Pipooz power is sacred.
 
Yote haya tunajuwa ni turufu ya chama gani wanachojali wao ni kuungwa mkono na wananchi tuu na syo kuangalia maslahi ya nchi
 
Mkuu hizi harakati zinabidi zipelekwe kule Tarime....Watu wa mara wanasoma namba hapa


Sio mara tuh,hata arusha wanasubiri kwa harakati hizi...!!

Usifanye mchezo na passive resistance,siku ya leo yote watu wamepiga kimyaaa..!!

Policcm wanalanda landa na gari zao wanafuja mafuta watu wametulia wanawashangaa tuh wanavojitoa ufaham...

Na harakati zitaendelea...
 
Hata punda ukimpeleka mtoni kunywa maji kama hataki hata umfanyeje ng'o hanywi!tusidhani kila wananchi wanapopata uelewa kuhusu rasilimali zao na jinsi zinavyotumika msifikiri nyuma yao kuna ushawishi hasi hapana tujitafakari na tuone na kwa jinsi gani tumewatendea wananchi ipasavyo?
 
mafahari wawili wapiganapo zinazoumia ni nyasi siku zote.hivi wale wananchi wenzangu ambao tunategemea tukazunguke mitaani il tuweze kupata mkate wetu wa kila siku tunandewa haki kwa njia hii?,hivi ni kweli hiyo ndio njia ya kutatua tatizo?mbona ni kama tunatesana sisi wanyonge kwa wanyonge,eeeeh zakwako changanya na za kuambiwa.
 
Hakika wanamtwara wanayo haki kushikamana, ukiangalia barabara zao, hali ya mji ulivyo inatia hamasa kuwa wanamtwara wanajiandaa kuweka historia katika nchi hii. Naungana na watanzania wenzangu walioko maeneo hayo ili kukomesha hii tabia ya serikali ya kupuuza.
 
Back
Top Bottom