Hali ya mgonjwa wetu si shwari

Hali ya mgonjwa wetu si shwari

Pamoja na maonyo ya watu wazima ya kwamba mgonjwa wetu yu mahututi hata mkimpa dawa ni sawa na kujisumbua maana ile pumzi ya uhai imeshakata.

Lakin kwa kuwa bado tulikua na imani na mgonjwa wetu na bado tulimhitaji ikatubidi tuwe na kichwa ngumu na kutosikiliza maneno ya watu wazima.

Tukampa dawa ili angalau asogeze siku za kuishi japo hata miaka 5 lakini naona kama tulimzidishia dozi maana aliinuka kwa sipidi sana na muda mwingne wanandugu tukapata matumaini ya kwamba sasa mgonjwa wetu kapona.

Lakini hata mwaka aujaisha toka tumpe dawa naona ameanza kulegalega kila uchwao sasa sijui kama tutafika nae hiyo miaka mitano au ndio atatufia njiani sijui ila ni maombi tu ndio yanahitajika kwa sasa wananzengo.
Hodi humu ndani?
 
hahhahaaaa!!jamani nyie sio watu wema,kama mnafikia hatua ya kumwombea mgonjw kifo hiyo ni hatareee.Tatizo ni kwamba mgonjwa yuko mahututi lakini akishtuka akakushtukia wewe unayemtakia kifo hapo ndo utakuwa mwisho wako wa kumjaribu.
 
Pamoja na maonyo ya watu wazima ya kwamba mgonjwa wetu yu mahututi hata mkimpa dawa ni sawa na kujisumbua maana ile pumzi ya uhai imeshakata.

Lakin kwa kuwa bado tulikua na imani na mgonjwa wetu na bado tulimhitaji ikatubidi tuwe na kichwa ngumu na kutosikiliza maneno ya watu wazima.

Tukampa dawa ili angalau asogeze siku za kuishi japo hata miaka 5 lakini naona kama tulimzidishia dozi maana aliinuka kwa sipidi sana na muda mwingne wanandugu tukapata matumaini ya kwamba sasa mgonjwa wetu kapona.

Lakini hata mwaka aujaisha toka tumpe dawa naona ameanza kulegalega kila uchwao sasa sijui kama tutafika nae hiyo miaka mitano au ndio atatufia njiani sijui ila ni maombi tu ndio yanahitajika kwa sasa wananzengo.
Umetumia lenzi mbonyeo ww
 
kwa jinsi anavyokurupuka kitandani kila anaposhika afikii atakua na malaria
 
Huyo mgonjwa alikuwa afe kabisa, alikata kauli Nov. 2015, ugonjwa wa mamvi ulimshika, akakata kauli, alikaa wiki bila kuongea, ghafla akazinduka, sindano ya Pombe kali aina ya Magufuli alichomwa... si akasimama... anadunda..!! na Alipozinduka, aliimba sana, Sisi mbele kwa mbeleee, mtaisoma namba eeehh... sisi mbele kwa mbeleeee...!!

Mgonjwa sasa hv hafi tena, anatembea na HAPA KAZI TU...!!

Na juzi kati, sauti ilisikika ktk kikao huko Dodoma cha huyo mgonjwa, kwambaaaa... kama Nov. 2015 hajafa, hatakufa tenaaaaa....!!! ataishi mileleee...!! Hapa Kazi tu..!!

🙄😛😀😀😀

 
kuugua ni jambo la kawaida, na kuugua sio kufa. wangapi wazima, tena wauguzaji, hufa na kuwaacha wagonjwa? magonjwa mengi ya siku hizi huletwa na mtindo wa maisha kama ulaji mbaya, kutofanya mazoezi nk. lakini pia kuna maradhi ya kurithi, ambayo naamini ndio yanayomsumbua mgonjwa. historia ya ukoo wake inaonesha umekuwa na magonjwa sugu kizazi hadi kizazi. lakini tusikate tamaa. japo wasima dawa nyingi katumia, tiba mbadala mmejaribu? kuna taarifa kuwa mgonjwa wako anachagua sana dawa na hata wanaotaka kumwona na walau kumpa ushauri wakifika wodini hataki kuwaona, anafumba macho, je ni kweli? mshauri awe na amani ya nafsi, nayo ni tiba pia.
 
mgonjwa mbishi hatari,anawapangia jinsi ya kumchoma sindano hadi madaktari,sijui kama atapona.
 
Na huyu mtu mzima aliyetushauri vibaya kwamba mgonjwa yu mahututi hivyo tusijisumbue naona nae pumzi imeshakata kabisa, maana hata hatupi ushirikiano, au katususia.

Nadhani tulikuwa sawa kutosikiliza maneno ya mtu mzima huyu kwani tungemsikiliza leo hii tungekuwa tulishampoteza mgonjwa wetu. Kama aliinuka kwa spidi sana wanandugu tuendelee kuwa na matumaini ya kuwa anaweza ku survive, siunajua tena ugonjwa huwa unaingia kwa nguvu ila unatoka polepole.
 
Familia ya Huyu mgonjwa nilikuwa siipendi hata kidogo kwa sababu nyingi tuu, wezi, wabaguaji, madikteta, ni nyingi sana tabia chafu wanazo kuliko nzuri, na watu wengi wanajua hivyo.
Sasa walikuwa watu kutaka kuiondoa hii familia na mgonjwa wao ili balaa lisiendelee kuwakandamiza watu, lakini baadhi ya watu wakawa wanawatetea saaana juu ya ubaya wao wote huo walikokuwa nao, maana baadhi walikuwa wakifaidika na familia ya mgonjwa .
Wakafanya JUHUDI kubwa sana ili mgonjwa apone CHINJA UWA ,
Ikaishia mgonjwa akapona, alipopona wakafurahia sana wana familia na wale wasaidizi kumuokoa mgonjwa, mmmhhh mgonjwa akasahau kuwa alisaidiwa ikawa kila Yule ambae anaona yupo KINYUME NYUME ANAMGEUZA KIMBELEMBELE, walijuta wengi kumsaidia na walilaani maana mgonjwa kawa na jeuri sana ila wakati mwengine ubinaadamu unamjia anawahurumia.
Sasa basi la muhimu tumuache mgonjwa aendelee na dawa huenda ni side effect za dawa ndio zinamzingua. Kwa sababu tulipo tunapomuombea mgonjwa mauti, huenda tukawa sisi. TUMUOMBEE KHERI MUNGU AM-BADILISHE NA AWE MFANO MZURI SANA KWA WAGONJWA WENGINE WANAOUGUA
 
Huyo mgonjwa alikuwa afe kabisa, alikata kauli Nov. 2015, ugonjwa wa mamvi ulimshika, akakata kauli, alikaa wiki bila kuongea, ghafla akazinduka, sindano ya Pombe kali aina ya Magufuli alichomwa... si akasimama... anadunda..!! na Alipozinduka, aliimba sana, Sisi mbele kwa mbeleee, mtaisoma namba eeehh... sisi mbele kwa mbeleeee...!!

Mgonjwa sasa hv hafi tena, anatembea na HAPA KAZI TU...!!

Na juzi kati, sauti ilisikika ktk kikao huko Dodoma cha huyo mgonjwa, kwambaaaa... kama Nov. 2015 hajafa, hatakufa tenaaaaa....!!! ataishi mileleee...!! Hapa Kazi tu..!!

🙄😛😀😀😀

Naona umekunywa uji na kumeza dawa ya mgonjwa ona sasa unaweweseka.Naona dawa imekulevya naona umepata kisulisuli.Wakati mwingine tafakari,kisha chukua hatuaaa
 
ole wao wauguzaji waliokunywa uji wa mgonjwa, wajiandae kutapishwa mgonjwa ana hila sana huyu.
Allah mpe siha njema mgonjwa.
 
Uholanzi walipitisha sheria kama mgonjwa asipopata nafuu kwa mda mrefu,anaweza chomwa sindano ya kutangulia akhera!
Hii sheria imekaaje?mgonjwa wetu pamoja na maombi haponi!
 
Mgonjwa juzi kakurupuka anasema fyatuen matofar aaaah,watoto anadai atawasomeshea,hawa watoto watakula nini,mgonjwa huyu hatari sana,leo nesi kakurupuka anasema mgonjwa alifanya utani.
 
Back
Top Bottom