Uzalendo TZ umekwenda na Mwl. Hivi inakuwaje mtu mwenye akili timamu anakichukia chama kingine cha upinzani hata kukiombea kifo? Haiingii akilini kwamba tunaweza kufikia hapo.
Badala ya kukashifu CDM au |CCM tungekuwa tunazipima zile sera zao na kuzikosoa ili ziwe nzuri zaidi lakini wengi wanaropoka tu.
Weye mleta thread hii, ungepata faida gani kama wanachama woote wa CDM wangehamia CCM leo? Unatamani tuendelee kuongozwa na huo upofu wa CCM mpaka lini?? Miaka zaidi ya 50 ya uhuru, maendeleo ni shule za sekondari za kata zenye ufaulu wa div. 5?? Tutawapeleka wapi? Tungekuwa hata na viwanda vya kutengenezea pumba za kuku basi, hivyo vyote mmeuza mkagawana pesa. Oh! My,my.
Jamani msiombee CDM ife, iombeeni ikomae, huenda hata ikawaamsha nyie Maccm. Nakuarifu, huyo ripota wako alieko humo ndani ya ofisi pale Ufipa, alikulamba hizo buku 7 za bure. Mmezoea kulambwa, alianza ZZK sasa huyu mliye mpenyeza humo kama yupo kweli, ni tapeli la kimafia. Linawalamba bure tu.
Ati ugomvi umeanzia Baraza kivuli la mawaziri. Shame on yu. Hakuna viongozi wanaoelewana kama Dr. Slaa na Mh. Mbowe. Subirini 2015. Mvua ya mawe itakapoanza kunyesha. Kila kona ya nchi itafikiwa na hawa viongozi wawili. Bado tuna nyenzo kibao listi ni ndefu, Aanze Prof. msomi wa kweli Safari aanzie Mtwara kuelekea Bukoba, aje Marando kutoka Musoma kwenda Mbeya, Aje Mh. Mbowe toka Kilimanjaro kwenda Kigoma, Dr. Aanzie Dodoma kuizungusha Tz. Nakuambia hicho kipondo, CCM mtaona nyota tu.
Hoja za ukabila na ukanda na udini zimeshachuja. Mtaipenda CDM kwa nguvu tu.