Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,632
- 697,796
Ngoma unayocheza ni ya kitoto mno.. Haina ubavu wa kukesha.... Huna uwezo wa kucheza mnanda au mchiriku siku hizi wanaita singeli.. Hizo ndio ngoma za kihuni sasa.. Kama huna pumzi unaumbuka...!
Salamu kidogo ulizotumiwa ni onyo la kishkaji sana, hizi sio nyakati za jiwe hizi ni nyakati za watoto wa mjini hawakutoi damu wala manundu wanakunjia tu yai kwenye mpasuko kisha wanakupiga picha...
Hakuna anatakayekudhuru hata ukucha ila utabadilishiwa tu santuri za mjini tena kwa mitindo tofauti tofauti.. Wewe ni chawa tena yule kiroboto.. Wanakujua vema.. Ndio maana wameamua kukucheza shere japo kiduchu.. Hizo ni salam tuu ..kama unagutuka gutuka sasa!.. Ukiendeleza ushamba wako hakuna rangi utaacha kuona.. Utasagiwa mpaka kunguni
Hili dubwana linaloitwa SIRIKALI lione hivi hivi...! Unamsikia tena Gwajiboi? Hajaguswa hata ukucha Lakini umeona alivyopoa kuliko marehemu mochwari? Vp na mzee wa PhD famba ya kupigwa? Cheza michezo yako yote lakini ukifika kwenye kibao kilichoandikwa SIRIKALI.. Brother nakushauri ufyate kama mbwakoko ugenini..!
Brother sikio litabaki kuwa sikio.. Kamwe halitakaa lizidi kichwa... Kuna viungo bandia vya kila aina lakini sio sikio lililozidi kichwa! Labda liwe la mdoli...! Ukinyonga na ukigeugeu wako vinasadifu ufinyu wa fikra ulionao.. Dr. Bashiru aliyeamua kukaa kimya sio mjinga..AMEJITAMBUA...!!!
Ulipewa salio la msg ukataka na kifurushi cha internet..! Ulikaribishwa upenuni, ukajiingiza sebuleni sasa unataka kuingia chumbani..Thubutuu.. Hizi adabu umefunzwa wapi? Na nani?
Kama walozi wenyewe tunaigwaya serikali wewe ni nani mpaka ujitie kifutu? Brother angalia na makinika usije ukawa na tabia za kenge! Maana kenge hasikii mpaka damu zimtoke masikioni...!
Usije ukajaribu kuinua kichwa tena.. Rungu zito zaidi litatua juu yake kwa style zilezile za watoto wa mjini...
Salamu kidogo ulizotumiwa ni onyo la kishkaji sana, hizi sio nyakati za jiwe hizi ni nyakati za watoto wa mjini hawakutoi damu wala manundu wanakunjia tu yai kwenye mpasuko kisha wanakupiga picha...
Hakuna anatakayekudhuru hata ukucha ila utabadilishiwa tu santuri za mjini tena kwa mitindo tofauti tofauti.. Wewe ni chawa tena yule kiroboto.. Wanakujua vema.. Ndio maana wameamua kukucheza shere japo kiduchu.. Hizo ni salam tuu ..kama unagutuka gutuka sasa!.. Ukiendeleza ushamba wako hakuna rangi utaacha kuona.. Utasagiwa mpaka kunguni
Hili dubwana linaloitwa SIRIKALI lione hivi hivi...! Unamsikia tena Gwajiboi? Hajaguswa hata ukucha Lakini umeona alivyopoa kuliko marehemu mochwari? Vp na mzee wa PhD famba ya kupigwa? Cheza michezo yako yote lakini ukifika kwenye kibao kilichoandikwa SIRIKALI.. Brother nakushauri ufyate kama mbwakoko ugenini..!
Brother sikio litabaki kuwa sikio.. Kamwe halitakaa lizidi kichwa... Kuna viungo bandia vya kila aina lakini sio sikio lililozidi kichwa! Labda liwe la mdoli...! Ukinyonga na ukigeugeu wako vinasadifu ufinyu wa fikra ulionao.. Dr. Bashiru aliyeamua kukaa kimya sio mjinga..AMEJITAMBUA...!!!
Ulipewa salio la msg ukataka na kifurushi cha internet..! Ulikaribishwa upenuni, ukajiingiza sebuleni sasa unataka kuingia chumbani..Thubutuu.. Hizi adabu umefunzwa wapi? Na nani?
Kama walozi wenyewe tunaigwaya serikali wewe ni nani mpaka ujitie kifutu? Brother angalia na makinika usije ukawa na tabia za kenge! Maana kenge hasikii mpaka damu zimtoke masikioni...!
Usije ukajaribu kuinua kichwa tena.. Rungu zito zaidi litatua juu yake kwa style zilezile za watoto wa mjini...