Hakuna Rais atakayetatua tatizo sugu la ajira ila sisi wenyewe kama China

TUMI EPAFRA

Member
Jul 12, 2020
59
56
Hakuna Rais atakaye tatua tatizo sugu la ajira ila sisi wenyewe kama watu wa China walivyo jielimisha, hata kama CCM ikiondoka madarakani. Kwa sababu tatizo la ajira linatokana na ukosefu wa uzalishaji mali barani Afrika, ukosefu wa wataalamu wa viwanda ingawaje tuna wasomi wengi.

Rais wa kupambana na hili lazima aanzie kwenye mfumo wa elimu, kuhamasisha wanafunzi kusoma technology, la sivyo Rais yoyote atakaye ingia bila hii sera atazidisha umasikini kwa kutegemea mikopo ya nje, na kula chote kidogo tulichonacho mwenyewe na watu wake.

Wapinzani wote ni maneno matupu na wanategemea Ulaya kuiongoza nchi hii kiuchumi na kisiasa, jambo ambalo ni kinyume kabisa kwa nchi yeyote ya Afrika kufanya hivyo sasa, ni kuturudisha kwenye utumwa wa remote control.

Tatizo la Afrika sote tunakimbilia elimu zinazotuelimisha kuajiriwa sio kuajiri, kujiajiri au kuunda bidhaa zozote, mpaka leo tunaaigiza kila kitu toka Ulaya, kuanzia madawa mpaka chupi za kuvaa, sasa wanawake wanaagiza hata nywele za Ulaya

Angalau Magufuli anadumisha sera ya viwanda, lakini viwanda hivi inabidi viajiri wataalamu toka nje kuvisimamia na kuvirekebisha, na spare parts zake zinaagizwa toka Ulaya, Marekani au Asia.

Siku nchi yetu itakapozalisha kila kitu bila kutegemea nchi za nje, kuanzia madawa mpaka mavazi, peni na mashine za viwanda, simu na magari hata radio na fridges, tutapounda barabara zetu wenyewe, mungu akijalia tutakapo tengeneza hata computers, ndipo umasikini na ukosefu wa ajira utakapoisha.
 
Hakuna Rais atakaye tatua tatizo sugu la ajira ila sisi wenyewe kama watu wa China walivyo jielimisha, hata kama CCM ikiondoka madarakani. Kwa sababu tatizo la ajira linatokana na ukosefu wa uzalishaji mali barani Afrika, ukosefu wa wataalamu wa viwanda ingawaje tuna wasomi wengi.
Hata China sio kuwa wametatua tatizo la ajira kwa jinsi unavyoeleza. Bado walizitegemea sana nchi kama Marekani.

Angalia simu zako, laptop, radio, friji, na hata nguo, ambazo zina lebel ya kampuni ya nchi za magharibi kama USA, au Ulaya. Utaona kwamba zimetengenezwa China. Kwa hiyo TV za Phillips zinatengenezwa China, pamoja na nguo za H&M, kampuni ya Sweden, zinatengenezwa China.

Hivyo China waliona umuhimu wa kuvutia wawekezaji ili wahamishie viwanda kwao na kusambaza bidhaa kwenda nchi mbalimbali toka China.

Sasa sisi uongozi wetu hilo haulioni. Tumezidi kuwatukana wawekezaji hawa kuwa mabeberu nk, bila kujua kwamba kujenga uhusiano mzuri kunaweza kufanywa waamue kuweka viwanda vyao hapa. Hiyo sio lugha itampa confidence Mercedes Benz au BMW kuweka plant yake Dar es Salaam.

Ona kwamba nchi kama Kenya sasa ina kiwanda cha magari ya VW ya Germany. Kwa hiyo ukanda wote wa Afrika Mashariki kwenda Afrika ya Kaskazini ukitaka gari ya VW itatoka Kenya, sio Germany au Afrika Kusini. Jiulize kwa nini VW walienda Kenya na sio Tanzania?

Kwa hiyo wapinzani wanachotaka ni kuweka mazingira mazuri, kuwa na uhusiano mzuri na mataifa ili hilo lifanyike. WEwe unachopendekeza ni Tanzania kuanzisha simu zake, magari yake nk ndio tuendelee. Hizo ni ndoto. Ni lini Tanzania itaanzisha TV zake ambazo zitashindana ubora na Samsung? Au gari zetu zikashindana ubora na Benz?

Ndio maana wakati Magufuli anakazana kuziita nchi za Magharibi mabeberu. Lissu anasema nia yangu ni kutengeneza uhusiano mzuri na hizi nchi. Uhusiano mzuri ndio utafanya BMW wajenge plant Tanzania badala ya Kenya. Ona kwamba China pamoja na sera zao za Kimomunist walifanikiwa kuweka mazingira mazuri. Sisi tunajiona wajuaji tukiwafukuza mabalozi wao toka Tanzania. Ujinga mtupu.
 
Wachina wanatengeneza hizo bidhaa zote wenyewe, ila sie tukifungua viwanda vya simu itabidi tuajiri wazungu na wachina kutengeneza bidhaa hata kufanya matengenezo ya viwanda. Hivyo inabaki pale pale, lazima tujielimishe teknoojia la sivyo tutarudisha utumwa na viwanda hivyo, tutauza nchi wala hatutafaidika na viwanda hivyo bila sisi wenyewe kuwa wafanyakazi wake.
 
Wachina wanatengeneza hizo bidhaa zote wenyewe, ila sie tukifungua viwanda vya simu itabidi tuajiri wazungu na wachina kutengeneza bidhaa hata kufanya matengenezo ya viwanda. Hivyo inabaki pale pale, lazima tujielimishe teknoojia la sivyo tutarudisha utumwa na viwanda hivyo, tutauza nchi wala hatutafaidika na viwanda hivyo bila sisi wenyewe kuwa wafanyakazi wake.
Kwani unafikiri nchi za Magaharibi wakiweka plant ya BMW hapa watakuja na wafanya kazi wao? KUna sheria na utaratibu unaotumika China na ndio utatumika hapa, kwamba nafasi za juu fulani wanapewa wao na nyingine zote ni Watanzania. Kwa hiyo unakuta kwa mfano, 15% ya wafanyakazi ni kutoka Germany, na 85% ni wazawa. Sasa wee usichotaka hapo ni nini hadi useme tutengeneze BMW zetu wenyewe kwa kutumia wazawa? Usifikiri kila mahari uzalendo ni suluhisho
 
..serikali inaweza kuajiri.

..serikali inaweza kuweka mazingira yatakayowezesha wawekezaji wakubwa kuajiri.

..serikali pia inaweza kuweka mazingira wezeshi kwa wananchi kujiajiri wenyewe, na kuajiri wenzao.

..Na anayeongoza serikali ni RAISI.
 
Ajira ni "tatizo " kila mahali, piga kitabu ukiwa na wazo la kujiajiri, ukibahatika kuajiriwa shukuru. Ila kusiwe na upendeleo katika ajira.
 
Hata China sio kuwa wametatua tatizo la ajira kwa jinsi unavyoeleza. Bado walizitegemea sana nchi kama Marekani.

Angalia simu zako, laptop, radio, friji, na hata nguo, ambazo zina lebel ya kampuni ya nchi za magharibi kama USA, au Ulaya. Utaona kwamba zimetengenezwa China. Kwa hiyo TV za Phillips zinatengenezwa China, pamoja na nguo za H&M, kampuni ya Sweden, zinatengenezwa China.

Hivyo China waliona umuhimu wa kuvutia wawekezaji ili wahamishie viwanda kwao na kusambaza bidhaa kwenda nchi mbalimbali toka China.

Sasa sisi uongozi wetu hilo haulioni. Tumezidi kuwatukana wawekezaji hawa kuwa mabeberu nk, bila kujua kwamba kujenga uhusiano mzuri kunaweza kufanywa waamue kuweka viwanda vyao hapa. Hiyo sio lugha itampa confidence Mercedes Benz au BMW kuweka plant yake Dar es Salaam.

Ona kwamba nchi kama Kenya sasa ina kiwanda cha magari ya VW ya Germany. Kwa hiyo ukanda wote wa Afrika Mashariki kwenda Afrika ya Kaskazini ukitaka gari ya VW itatoka Kenya, sio Germany au Afrika Kusini. Jiulize kwa nini VW walienda Kenya na sio Tanzania?

Kwa hiyo wapinzani wanachotaka ni kuweka mazingira mazuri, kuwa na uhusiano mzuri na mataifa ili hilo lifanyike. WEwe unachopendekeza ni Tanzania kuanzisha simu zake, magari yake nk ndio tuendelee. Hizo ni ndoto. Ni lini Tanzania itaanzisha TV zake ambazo zitashindana ubora na Samsung? Au gari zetu zikashindana ubora na Benz?

Ndio maana wakati Magufuli anakazana kuziita nchi za Magharibi mabeberu. Lissu anasema nia yangu ni kutengeneza uhusiano mzuri na hizi nchi. Uhusiano mzuri ndio utafanya BMW wajenge plant Tanzania badala ya Kenya. Ona kwamba China pamoja na sera zao za Kimomunist walifanikiwa kuweka mazingira mazuri. Sisi tunajiona wajuaji tukiwafukuza mabalozi wao toka Tanzania. Ujinga mtupu.
Well said. Tatizo watu wengi hawajui kuwa China, Korea, Japan, Hong Kong, Malaysia zimeendelea kwa ajili ya Uwekezaji wa Mabeberu. Bila uwekezaji, technolojia na sokp la Mabeberu .... itakuwa sawa na mbio za sakafuni.

Badala ya kuwaza kuibiwa kila mara inabidi tuangalie opportunity cost pia ..... it's a game of give and take!
 
Kwani unafikiri nchi za Magaharibi wakiweka plant ya BMW hapa watakuja na wafanya kazi wao? KUna sheria na utaratibu unaotumika China na ndio utatumika hapa, kwamba nafasi za juu fulani wanapewa wao na nyingine zote ni Watanzania. Kwa hiyo unakuta kwa mfano, 15% ya wafanyakazi ni kutoka Germany, na 85% ni wazawa. Sasa wee usichotaka hapo ni nini hadi useme tutengeneze BMW zetu wenyewe kwa kutumia wazawa? Usifikiri kila mahari uzalendo ni suluhisho
Unajua tulikuwa na kiwanda cha Scania na malori mengine? Viwanda vilikufaje? Sababu hatukuwa na wataalamu wa kuvihudumia na kuviendesha. Unafikiri wakileta kiwanda cha magari ghafla watanzania watajua jinsi ya kuunda magari hayo bila elimu?
 
Unajua tulikuwa na kiwanda cha Scania na malori mengine? Viwanda vilikufaje? Sababu hatukuwa na wataalamu wa kuvihudumia na kuviendesha. Unafikiri wakileta kiwanda cha magari ghafla watanzania watajua jinsi ya kuunda magari hayo bila elimu?
Si kweli. Kiwanda cha Scania hakikuhitaji utalaamu wowote, maana ilikuwa ni assembly plant. KIlichotokea ni kwamba kilikuwa na soko kubwa wakati hakuna uhuru wa kuagiza mabasi/malori toka nje ya mitumba na mabasi. Baada ya serikali kufungulia malori ya mitumba nani tena alitaka kununua Scania mpya?

Kiwanda cha Scania kiliendelea kutumika kwa ajili ya mabasi ya Scania ambapo bodi zilitengenezwa hapa hapa nchini na kina Quality Garage , Yusufu Ali nk. Unakumbukka Kwacha, Scandnavia etc enzi hizo ilikuwa ni Scania tupu. Baadae wakaja wachina na basi zao cheap za Yutong sijui.

Ndivyo pia KIA kwa ajili ya daladala Chai Maharage zilivyokufa. Mitumba ya daladala iliziua baada ya kuanza kuingia awamu ya Mwinyi ambapo uliipata kwa bei rahisi kuliko KIA mpya. Kumbuka wakati huo hata dumping tax ilikuwa hakuna.

Kwa hiyo Scania (TAMCO) haikufa kwa ajili ya kukosa watalaamu, bali mazingira ya biashara nchini. Hata sasa Scania wana mpango wa kutengeneza mabasi cheap ili washindane na Yutong za China kwenye soko la Tanzania, kwa kuwa wanasema waliuza sana enzi hizo hasa kwenye basi. Kuna nchi kama South Africa ambao wana assembly za magari huruhusiwi hata kuingiza gari jipya toka nje au unalimwa kodi kichizi, na used ndio kabisa hawataki kusikia mtu anaingiza. Unatakiwa kununua yanayotengenezwa nchini.
 
Hakuna Rais atakaye tatua tatizo sugu la ajira ila sisi wenyewe kama watu wa China walivyo jielimisha, hata kama CCM ikiondoka madarakani. Kwa sababu tatizo la ajira linatokana na ukosefu wa uzalishaji mali barani Afrika, ukosefu wa wataalamu wa viwanda ingawaje tuna wasomi wengi.

Rais wa kupambana na hili lazima aanzie kwenye mfumo wa elimu, kuhamasisha wanafunzi kusoma technology, la sivyo Rais yoyote atakaye ingia bila hii sera atazidisha umasikini kwa kutegemea mikopo ya nje, na kula chote kidogo tulichonacho mwenyewe na watu wake.

Wapinzani wote ni maneno matupu na wanategemea Ulaya kuiongoza nchi hii kiuchumi na kisiasa, jambo ambalo ni kinyume kabisa kwa nchi yeyote ya Afrika kufanya hivyo sasa, ni kuturudisha kwenye utumwa wa remote control.

Tatizo la Afrika sote tunakimbilia elimu zinazotuelimisha kuajiriwa sio kuajiri, kujiajiri au kuunda bidhaa zozote, mpaka leo tunaaigiza kila kitu toka Ulaya, kuanzia madawa mpaka chupi za kuvaa, sasa wanawake wanaagiza hata nywele za Ulaya

Angalau Magufuli anadumisha sera ya viwanda, lakini viwanda hivi inabidi viajiri wataalamu toka nje kuvisimamia na kuvirekebisha, na spare parts zake zinaagizwa toka Ulaya, Marekani au Asia.

Siku nchi yetu itakapozalisha kila kitu bila kutegemea nchi za nje, kuanzia madawa mpaka mavazi, peni na mashine za viwanda, simu na magari hata radio na fridges, tutapounda barabara zetu wenyewe, mungu akijalia tutakapo tengeneza hata computers, ndipo umasikini na ukosefu wa ajira utakapoisha.
Comments reserved
 
Hakuna Rais atakaye tatua tatizo sugu la ajira ila sisi wenyewe kama watu wa China walivyo jielimisha, hata kama CCM ikiondoka madarakani. Kwa sababu tatizo la ajira linatokana na ukosefu wa uzalishaji mali barani Afrika, ukosefu wa wataalamu wa viwanda ingawaje tuna wasomi wengi.

Rais wa kupambana na hili lazima aanzie kwenye mfumo wa elimu, kuhamasisha wanafunzi kusoma technology, la sivyo Rais yoyote atakaye ingia bila hii sera atazidisha umasikini kwa kutegemea mikopo ya nje, na kula chote kidogo tulichonacho mwenyewe na watu wake.

Wapinzani wote ni maneno matupu na wanategemea Ulaya kuiongoza nchi hii kiuchumi na kisiasa, jambo ambalo ni kinyume kabisa kwa nchi yeyote ya Afrika kufanya hivyo sasa, ni kuturudisha kwenye utumwa wa remote control.

Tatizo la Afrika sote tunakimbilia elimu zinazotuelimisha kuajiriwa sio kuajiri, kujiajiri au kuunda bidhaa zozote, mpaka leo tunaaigiza kila kitu toka Ulaya, kuanzia madawa mpaka chupi za kuvaa, sasa wanawake wanaagiza hata nywele za Ulaya

Angalau Magufuli anadumisha sera ya viwanda, lakini viwanda hivi inabidi viajiri wataalamu toka nje kuvisimamia na kuvirekebisha, na spare parts zake zinaagizwa toka Ulaya, Marekani au Asia.

Siku nchi yetu itakapozalisha kila kitu bila kutegemea nchi za nje, kuanzia madawa mpaka mavazi, peni na mashine za viwanda, simu na magari hata radio na fridges, tutapounda barabara zetu wenyewe, mungu akijalia tutakapo tengeneza hata computers, ndipo umasikini na ukosefu wa ajira utakapoisha.
mbona jk aliweza kuajiri walimu wote na madaktari. Jpm ndo tatizo hivyo apumzishwe ikiwezekana kwa amani
 
Inasikitisha mno,

Lisu anatokea Ubelgiji kuja kugombea Urais,

Wapinzani Bado wanataka kutufanya tuwe tegemezi.
 
Tat
Inasikitisha mno,

Lisu anatokea Ubelgiji kuja kugombea Urais,

Wapinzani Bado wanataka kutufanya tuwe tegemezi.
Tatizo ni kwamba watu wengi mnatoa comment bila kuwa na elimu ya kutosha ya siasa za duniani

- Samora alitokea Tanzania kuwa Raisi wa Msumbiji
- Museveni alitokea Tanzania kuwa Raisi wa Uganda
- Nujoma alitokea Tanzania kuwa Raisi wa Namibia
- Gandhi alitokea South Afrika kuwa waziri mkuu wa India
- Laurent Kabila alitokea Tanzania kuwa Raisi wa DRC
- Ellen Johnson alitokea USA kuwa raisi wa LIberia, nk

Sasa tatizo lako nini hasa?
 
Si kweli. Kiwanda cha Scania hakikuhitaji utalaamu wowote, maana ilikuwa ni assembly plant. KIlichotokea ni kwamba kilikuwa na soko kubwa wakati hakuna uhuru wa kuagiza mabasi/malori toka nje ya mitumba na mabasi. Baada ya serikali kufungulia malori ya mitumba nani tena alitaka kununua Scania mpya?

Kiwanda cha Scania kiliendelea kutumika kwa ajili ya mabasi ya Scania ambapo bodi zilitengenezwa hapa hapa nchini na kina Quality Garage , Yusufu Ali nk. Unakumbukka Kwacha, Scandnavia etc enzi hizo ilikuwa ni Scania tupu. Baadae wakaja wachina na basi zao cheap za Yutong sijui.

Ndivyo pia KIA kwa ajili ya daladala Chai Maharage zilivyokufa. Mitumba ya daladala iliziua baada ya kuanza kuingia awamu ya Mwinyi ambapo uliipata kwa bei rahisi kuliko KIA mpya. Kumbuka wakati huo hata dumping tax ilikuwa hakuna.

Kwa hiyo Scania (TAMCO) haikufa kwa ajili ya kukosa watalaamu, bali mazingira ya biashara nchini. Hata sasa Scania wana mpango wa kutengeneza mabasi cheap ili washindane na Yutong za China kwenye soko la Tanzania, kwa kuwa wanasema waliuza sana enzi hizo hasa kwenye basi. Kuna nchi kama South Africa ambao wana assembly za magari huruhusiwi hata kuingiza gari jipya toka nje au unalimwa kodi kichizi, na used ndio kabisa hawataki kusikia mtu anaingiza. Unatakiwa kununua yanayotengenezwa nchini.
Hiyo ni moja ya sababu ndogo ya kuua kiwanda cha Scania, sababu kubwa utake usitake nenda kafanye uchunguzi kwa nini waziri wa viwanda Mahinda aliuwawa kwa risasi, utagundua tulikwama spare parts na wataalamu wa kurekebisha mashine, sio kwa Scania tu, ila kwa viwanda vingi hasa vya ngo vilivyoitwa something text. Mahinda aligundua mashine zilizonunuliwa ni za zamani na mbovu, spare parts zake hazitengenezwi tena. Kwa ujumla tulitegemea wazungu kurekebisha na kuendesha viwanda vyetu.

"Tumechoka taifa hili, unalima pamba unakwenda unasafirisha malighafi..halafu wakishatengeneza nguo, wanazivaa wanakuletea mitumba wakati pamba yako, mnalitaka hilo vijana?..sisi tunataka tukilima pamba yetu, tuna-process, zile nguo tunawapelekea ikiwezekana tunazivaa kwanza"..JPM
 
Sisi tunajiona wajuaji tukiwafukuza mabalozi wao toka Tanzania. Ujinga mtupu.
Mkuu mengine yote uliyosema nakuunga mkono 100% sema haya niliyo kunukuu nina tofautiana nawe.
China nayo huwa inafunga kabisa balozi za hao jamaa kama ikilazimu.
Uchochezi au kuingilia mambo yetu ya ndani hakuvumiliki kwa sababu yeyote ile ikiwemo umaskini wetu.
 
Mkuu mengine yote uliyosema nakuunga mkono 100% sema haya niliyo kunukuu nina tofautiana nawe.
China nayo huwa inafunga kabisa balozi za hao jamaa kama ikilazimu.
Uchochezi au kuingilia mambo yetu ya ndani hakuvumiliki kwa sababu yeyote ile ikiwemo umaskini wetu.
Mkuu utakuwa unaongelea China kufunga ofisi ndogo ya ubalazi hivi karibuni. Hiyo ilikwa reciprocity Marekani ndio walianza. Anyway, sisi hatujafunga hata siku moja toka Nyerere alipowatimua West Germany na Israel. NIlichoongelea ni kukorofishana na mabalozi kwa kuwa wametukosea na mara nyingine kudai wabadilishwe
 
Hiyo ni moja ya sababu ndogo ya kuua kiwanda cha Scania, sababu kubwa utake usitake nenda kafanye uchunguzi kwa nini waziri wa viwanda Mahinda aliuwawa kwa risasi, utagundua tulikwama spare parts na wataalamu wa kurekebisha mashine, sio kwa Scania tu, ila kwa viwanda vingi hasa vya ngo vilivyoitwa something text. Mahinda aligundua mashine zilizonunuliwa ni za zamani na mbovu, spare parts zake hazitengenezwi tena. Kwa ujumla tulitegemea wazungu kurekebisha na kuendesha viwanda vyetu.

"Tumechoka taifa hili, unalima pamba unakwenda unasafirisha malighafi..halafu wakishatengeneza nguo, wanazivaa wanakuletea mitumba wakati pamba yako, mnalitaka hilo vijana?..sisi tunataka tukilima pamba yetu, tuna-process, zile nguo tunawapelekea ikiwezekana tunazivaa kwanza"..JPM
I say, wewe una conspiracy theory za ajabu sana! Tatizo la kuchukua hadithi za vijiweni mitaani na kuzileta JF!
 
Back
Top Bottom