KIGENE
JF-Expert Member
- Jan 22, 2011
- 1,552
- 813
Kwetu kamwe sikubali,si kwetu ni kwa wenzetu,
Sio yale ya awali,tukiwa na utu wetu,
Kwa sasa hawatujali.tunaswagwa kwa mtutu,
Kwetu palikuwa kwetu,kwa sasa ni kwa wenzetu.
Hawatujali wenzetu.kwetu wameshapauza,
Hawatabakiza kitu,vyote wataangamiza,
Tubaki kama Wahutu,wakuja wala wasaza,
Kwetu palikuwa kwetu,kwa sasa ni kwa wenzetu.
Si ardhi si wanyama,urithi wetu asili,
Madini yetu wachuma,kwa kejeli na kibuli,
Ni wezi waso huruma,kwa zetu rasilimali,
Kwetu palikuwa kwetu, kwa sasa ni kwa wenzetu.
Baba keshauza nyumba,pamoja na wapangaji,
Kigamboni inayumba,wameuziwa walaji,
Wao wanao wajomba,pasi mbili na mtaji,
Kwetu palikuwa kwetu,kwa sasa ni kwa wenzetu.
Kwetu Mola pabariki,wanao twaangamia,
Kwa sasa hapakaliki,ni pazuri palikua,
Wageuze hambiliki,wabadili zao nia,
Kwetu palikuwa kwetu kwa sasa ni kwa wenzetu.
Sio yale ya awali,tukiwa na utu wetu,
Kwa sasa hawatujali.tunaswagwa kwa mtutu,
Kwetu palikuwa kwetu,kwa sasa ni kwa wenzetu.
Hawatujali wenzetu.kwetu wameshapauza,
Hawatabakiza kitu,vyote wataangamiza,
Tubaki kama Wahutu,wakuja wala wasaza,
Kwetu palikuwa kwetu,kwa sasa ni kwa wenzetu.
Si ardhi si wanyama,urithi wetu asili,
Madini yetu wachuma,kwa kejeli na kibuli,
Ni wezi waso huruma,kwa zetu rasilimali,
Kwetu palikuwa kwetu, kwa sasa ni kwa wenzetu.
Baba keshauza nyumba,pamoja na wapangaji,
Kigamboni inayumba,wameuziwa walaji,
Wao wanao wajomba,pasi mbili na mtaji,
Kwetu palikuwa kwetu,kwa sasa ni kwa wenzetu.
Kwetu Mola pabariki,wanao twaangamia,
Kwa sasa hapakaliki,ni pazuri palikua,
Wageuze hambiliki,wabadili zao nia,
Kwetu palikuwa kwetu kwa sasa ni kwa wenzetu.