Mwafrika wa Kike
JF-Expert Member
- Jul 5, 2007
- 5,185
- 56
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
VIONGOZI WA USHIRIKIANO WA VYAMA VYA UPINZANI KUZUNGUMZA NA WANANCHI KUHUSU UFISADI
• ‘Kuanika' jinsi mabilioni mengine ‘yalivyochotwa' benki kuu
• Kutaja viongozi wa serikali walivyohusika na ‘kampuni hewa' ilivyotumika
• Kugawa mkataba wa Richmond kwa umma
Viongozi wa Ushirikiano wa Vyama Vya Upinzani vya CHADEMA, CUF, NCCR Mageuzi na TLP siku ya jumapili tarehe 28 Oktoba, 2007 watazungumza na wananchi katika mkutano wa ndani kutoa taarifa kwa umma kuhusu ufisadi.
Mazungumzo hayo ya ndani ambayo wananchi mbalimbali wanaalikwa kushiriki yatafanyika katika Ukumbi wa Urafiki uliopo Manispaa ya Kinondoni Jimbo la Ubungo Mkoani Dar e salaam kuanzia saa 4 mpaka saa 5 na nusu asubuhi.
Katika mazungumzo hayo viongozi wa Vyama vya Upinzani wataanika jinsi mabilioni mengine zaidi yalivyochotwa katika benki kuu ya Tanzania na kutaja viongozi wa serikali walivyohusika na ‘kampuni hewa' ilivyotumika.
Itakumbukwa kwamba tarehe 15 Septemba, 2007 katika mkutano wa hadhara uwanja wa Mwembeyanga uongozi wa ushirikiano wa vyama vya upinzani ulitaja orodha ya mafisadi nchini yenye kueleza ufisadi, wizi na/au ubadhirifu au matumizi mabaya ya rasilimali za taifa.
Pamoja na viongozi wengine pia, Dr Wilbroad Slaa, Mbunge wa Karatu(CHADEMA) atazungumza katika mkutano huo. Dr Slaa ndiye aliyeibua hoja ya kutaka kuundwa kwa kamati teule ya kuchunguza tuhuma za ufisadi katika benki kuu na kupelekea kutangazwa kwa orodha ya mafisadi. Dr Slaa amerejea hivi karibuni kutoka Marekani ziarani nchini Marekani na Mkutano wa Bunge la Kusini mwa Afrika SADC nchini Malawi.
" Katika mkutano huu hatutataja orodha nyingine ya mafisadi. Tutajenga katika orodha ya awali ya mafisadi. Katika mkutano huu kitakachotajwa ni ufisadi mwingine uliopelekea mabilioni mengine kuchotwa katika benki kuu. Pia katika Mkutano huo tutagawa mkataba wenye utata wa Richmond kama tulivyofanya kwa mkataba wa Madini wa Buzwagi ili umma"
Imetolewa na 26/10/2007:
John Mnyika
Mjumbe wa Kamati ya Maandalizi na
Mkurugenzi wa Vijana Taifa(CHADEMA)
0754694553
__________________
Kizazi Kipya, Maisha Mapya
New Generation, New Life
Mabadiliko ya Kweli, Uhuru wa Kweli
Real Change, Real Freedom
John Mnyika
haombwi mtu msamaha, na safari hii nawahakikishia msikose mkutano huo, kwani siyo majina tu, bali hadi ushahidi wa kisayansi (forensics) utawekwa hadharani kuonesha ni jinsi gani CCM imetumia vibaya nafasi yake katika nchi.
Kazi iliyofanyika kukusanya ushahidi huo (kama mnakumbuka mkutano wa awali uliahirishwa) ilikuwa ngumu kwa kila aliyehusika, lakini kwa mara nyingi Watanzania wameonesha ushirikiano kupita kiasi.
Mlio mstari wa mbele, ongozeni mapambano na sisi tuko nyuma yenu kama tunaoshiriki katika mchakato wa ugavi... !!
Kwa mwana Mapinduzi mwenzenu.. katika mapammbano ya Kifikra!
M. M.
leo ijumaa ! mtu wa pwani, brazameni, mswahili, na wengine wa Mchambawima mko wapi ??
nilikuwa nimepanga mkubwa mmoja hivi lakini hili la Msiba limewapa udhuru. Tutaona itakuwaje.
Na swali lako la kwanza jibu ni ndiyo.. hili litakaloibuliwa na wanaharakati walio mstari wa mbele ni kubwa zaidi kwani lina specifics na siyo general statement..
Kwa kifupi, ile mada ya "jinsi ya kuibia serikali ya Muungano" itaoneshwa ni kwanini iliandikwa na ni jinsi gani watu walikuwa sahihi. Itaoneshwa mifano ya wizi ulivyofanywa...
Kikwete nimeahidi kukupa zawadi kama ukisalenda kwa wapinzani na kuvunja baraza lako la mawaziri, kuwaomba msamaha watanzania, na kuomba upewe second chance ili ufanye the right thing!
Nakubaliana na wewe Mwafrika. kuna haja ya Kikwete kuangalia ni wakina nani wanaweza kumsupport au kumwangusha, ambao ni wapiga kura tulio wengi. Asipende kujisafisha kwa mawaziri wake wachahe akasahau sehemu kubwa ya watanzania, sio ajabu hata hao mawaziri wake kuna ambao hawakupiga kura siku ile wakiwa wapo busy kuhonga wapiga kura.
Kikwete anatakiwa asome alama za nyakati na azitekeleze kwa haraka sana, Nashindwa kuelewe ile speed aliyoanza nayo imeishia wapi.. Hivi wana JF mnakumbuka alivyoanza kwa speed ya JET? sijui imeishia wapi maskini wa Mungu.
Kikwete Rais wetu amkaaa!!!
Huo mkutano wa Jpili kwangu naona utata kidogo.
The issues at hand are noble, but the timing is bad.
Watu (taifa) watakuwa bado na sentiments za msiba wa Salome Mbatia, na itawapa wakati mgumu sana kumeza yanayosemwa na akina Dr. Slaa. Hiyo itapoteza impact ya yatakayosemwa na kufanya issue nzima iwe mute.
Remember, you can not unring the bell.
My suggestion: Waahirishe hadi kipindi ikaribiane na Mkutano Mkuu wa CCM. Kwa kufanya hivyo, wata-overshadow maamuzi ya Mkutano Mkuu bila kuonekana kuwa hawana moyo kwa wafiwa na wahanga wa ajali ya Salome Mbatia.
Kiungani,
huu mkutano wa jumapili ni upi? labda nimekosa hiyo news kidogo
Viongozi wa Ushirikiano wa Vyama Vya Upinzani vya CHADEMA, CUF, NCCR Mageuzi na TLP siku ya jumapili tarehe 28 Oktoba, 2007 watazungumza na wananchi katika mkutano wa ndani kutoa taarifa kwa umma kuhusu ufisadi.
Mazungumzo hayo ya ndani ambayo wananchi mbalimbali wanaalikwa kushiriki yatafanyika katika Ukumbi wa Urafiki uliopo Manispaa ya Kinondoni Jimbo la Ubungo Mkoani Dar e salaam kuanzia saa 4 mpaka saa 5 na nusu asubuhi.
Angalia post ya kwanza kwenye hii thread.
haombwi mtu msamaha, na safari hii nawahakikishia msikose mkutano huo, kwani siyo majina tu, bali hadi ushahidi wa kisayansi (forensics) utawekwa hadharani kuonesha ni jinsi gani CCM imetumia vibaya nafasi yake katika nchi.
Kazi iliyofanyika kukusanya ushahidi huo (kama mnakumbuka mkutano wa awali uliahirishwa) ilikuwa ngumu kwa kila aliyehusika, lakini kwa mara nyingi Watanzania wameonesha ushirikiano kupita kiasi.
Mlio mstari wa mbele, ongozeni mapambano na sisi tuko nyuma yenu kama tunaoshiriki katika mchakato wa ugavi... !!
Kwa mwana Mapinduzi mwenzenu.. katika mapammbano ya Kifikra!
M. M.