Hakuna kuomba msamaha kwa Kikwete

Mwafrika wa Kike

JF-Expert Member
Jul 5, 2007
5,185
56
Nilijua tu kuwa hawa Rai wanaongopa. Hii ni taarifa ya Mnyika kwa vyombo habari:

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

VIONGOZI WA USHIRIKIANO WA VYAMA VYA UPINZANI KUZUNGUMZA NA WANANCHI KUHUSU UFISADI
• ‘Kuanika' jinsi mabilioni mengine ‘yalivyochotwa' benki kuu
• Kutaja viongozi wa serikali walivyohusika na ‘kampuni hewa' ilivyotumika
• Kugawa mkataba wa Richmond kwa umma

Viongozi wa Ushirikiano wa Vyama Vya Upinzani vya CHADEMA, CUF, NCCR Mageuzi na TLP siku ya jumapili tarehe 28 Oktoba, 2007 watazungumza na wananchi katika mkutano wa ndani kutoa taarifa kwa umma kuhusu ufisadi.

Mazungumzo hayo ya ndani ambayo wananchi mbalimbali wanaalikwa kushiriki yatafanyika katika Ukumbi wa Urafiki uliopo Manispaa ya Kinondoni Jimbo la Ubungo Mkoani Dar e salaam kuanzia saa 4 mpaka saa 5 na nusu asubuhi.

Katika mazungumzo hayo viongozi wa Vyama vya Upinzani wataanika jinsi mabilioni mengine zaidi yalivyochotwa katika benki kuu ya Tanzania na kutaja viongozi wa serikali walivyohusika na ‘kampuni hewa' ilivyotumika.

Itakumbukwa kwamba tarehe 15 Septemba, 2007 katika mkutano wa hadhara uwanja wa Mwembeyanga uongozi wa ushirikiano wa vyama vya upinzani ulitaja orodha ya mafisadi nchini yenye kueleza ufisadi, wizi na/au ubadhirifu au matumizi mabaya ya rasilimali za taifa.

Pamoja na viongozi wengine pia, Dr Wilbroad Slaa, Mbunge wa Karatu(CHADEMA) atazungumza katika mkutano huo. Dr Slaa ndiye aliyeibua hoja ya kutaka kuundwa kwa kamati teule ya kuchunguza tuhuma za ufisadi katika benki kuu na kupelekea kutangazwa kwa orodha ya mafisadi. Dr Slaa amerejea hivi karibuni kutoka Marekani ziarani nchini Marekani na Mkutano wa Bunge la Kusini mwa Afrika SADC nchini Malawi.

" Katika mkutano huu hatutataja orodha nyingine ya mafisadi. Tutajenga katika orodha ya awali ya mafisadi. Katika mkutano huu kitakachotajwa ni ufisadi mwingine uliopelekea mabilioni mengine kuchotwa katika benki kuu. Pia katika Mkutano huo tutagawa mkataba wenye utata wa Richmond kama tulivyofanya kwa mkataba wa Madini wa Buzwagi ili umma"

Imetolewa na 26/10/2007:


John Mnyika
Mjumbe wa Kamati ya Maandalizi na
Mkurugenzi wa Vijana Taifa(CHADEMA)
0754694553
__________________
Kizazi Kipya, Maisha Mapya
New Generation, New Life

Mabadiliko ya Kweli, Uhuru wa Kweli
Real Change, Real Freedom

John Mnyika

Kama Kikwete alizani anapata breki, basi ajiandae for mambo zaidi yake yawekwe wazi hapa. Kuna uwezekano zaidi wa kupata mikataba mingine ya madini iliyosainiwa wakati wa Kikwete na kama kawaida ya JF, hiyo mikataba itawekwa hapa mchana kweupe!

Hizi propaganda za Rostam zitampoteza Kikwete!

Kikwete nimeahidi kukupa zawadi kama ukisalenda kwa wapinzani na kuvunja baraza lako la mawaziri, kuwaomba msamaha watanzania, na kuomba upewe second chance ili ufanye the right thing!
 
KAMA KWELI SLAA NA WENZAKE WANATAKA KUOMBA MSAMAHA KWA JK, MAANA YAKE NI KWAMBA YAFUATAYO NI UONGO:
" Kabla ya kuwa Rais, Mheshimiwa Kikwete alikuwa Waziri wa Mambo Nje na Uhusiano wa Kimataifa kuanzia 1995 hadi 2005, Waziri wa Fedha 1994 hadi 1995 na Waziri wa Maji, Nishati na Madini kuanzia mwaka 1990 hadi 1994.
Kama Waziri wa Maji, Nishati na Madini, Mheshimiwa Kikwete alishiriki moja kwa moja katika kusaini mikataba mibovu ya madini na makampuni ya madini ya kimataifa ambayo kwayo taifa limeendelea kupoteza utajiri mkubwa na kuinyima Serikali uwezo wa kifedha wa kuhudumia wananchi. Kwa mfano, mnamo tarehe 10 Aprili 1990, Major Jakaya Mrisho Kikwete aliingia mkataba wa madini ya kampuni ya SAMAX Limited ambapo kampuni hiyo ilipewa leseni ya kuchimba dhahabu katika eneo la Lusu, Wilayani Nzega Mkoa wa Tabora. Matokeo ya mkataba huo, maelfu wa wachimbaji wadogo wadogo wa dhahabu waliokuwa eneo hilo waliondolewa kwa nguvu na vikosi vya FFU na bila ya kulipwa fidia yoyote. Hadi leo wananchi hao hawajalipwa fidia yoyote licha ya miaka zaidi ya kumi ya kufuatilia haki zao. Baada ya kutwaa utajiri wa dhahabu wa eneo hilo, SAMAX Limited iliuza eneo hilo kwa kampuni ya Ashanti Goldfields ya Ghana kwa dola za Marekani milioni 253. Ashanti Goldfields nao wakauza eneo kwa kampuni ya Resolute Limited ya Australia kwa kiasi kisichojulikana cha fedha za kigeni. Resolute Limited ndio waliojenga na wanamiliki Mgodi wa Dhahabu wa Golden Pride ulioko eneo la Lusu, Nzega hadi sasa na ambao ulifunguliwa mwezi Novemba 1998.
Mnamo tarehe 5 Agosti 1994 Luteni Kanali Jakaya Mrisho Kikwete aliingia tena mkataba na kampuni ya madini Kahama Mining Corporation Ltd., kampuni tanzu ya kampuni ya Sutton Resources ya Canada. Ijapokuwa mkataba huu unaonyesha wazi kwamba ulikuwa unahusu eneo la Butobela Wilaya ya Geita Mkoani Mwanza, mwezi Agosti mwaka 1996 Kahama Mining Corporation wakisaidiwa na vikosi vya FFU walivamia eneo la Bulyanhulu, Wilaya ya Kahama Mkoani Shinyanga na kuwaondosha kwa nguvu watu takriban laki nne waliokuwa wakiishi na kuchimba dhahabu katika eneo hilo. Baada ya kutwaa eneo hilo kwa nguvu za kijeshi, Sutton Resources iliiuza Kahama Mining Corporation na Bulyanhulu kwa Kampuni ya Dhahabu ya Barrick Gold Corporation ya Toronto, Canada kwa dola za Marekani milioni 280. Leo hii Bulyanhulu ni moja ya migodi tajiri kwa dhahabu katika Bara la Afrika.
DK SLAA TUAMBIE KAMA YALIOPO JUU SIO KWELI NA MIMIMNITAKOSA IMANI KWA MENGINE YOTE ULIYOSEMA.
macinkus
 
haombwi mtu msamaha, na safari hii nawahakikishia msikose mkutano huo, kwani siyo majina tu, bali hadi ushahidi wa kisayansi (forensics) utawekwa hadharani kuonesha ni jinsi gani CCM imetumia vibaya nafasi yake katika nchi.

Kazi iliyofanyika kukusanya ushahidi huo (kama mnakumbuka mkutano wa awali uliahirishwa) ilikuwa ngumu kwa kila aliyehusika, lakini kwa mara nyingi Watanzania wameonesha ushirikiano kupita kiasi.

Mlio mstari wa mbele, ongozeni mapambano na sisi tuko nyuma yenu kama tunaoshiriki katika mchakato wa ugavi... !!

Kwa mwana Mapinduzi mwenzenu.. katika mapammbano ya Kifikra!

M. M.
 
haombwi mtu msamaha, na safari hii nawahakikishia msikose mkutano huo, kwani siyo majina tu, bali hadi ushahidi wa kisayansi (forensics) utawekwa hadharani kuonesha ni jinsi gani CCM imetumia vibaya nafasi yake katika nchi.

Kazi iliyofanyika kukusanya ushahidi huo (kama mnakumbuka mkutano wa awali uliahirishwa) ilikuwa ngumu kwa kila aliyehusika, lakini kwa mara nyingi Watanzania wameonesha ushirikiano kupita kiasi.

Mlio mstari wa mbele, ongozeni mapambano na sisi tuko nyuma yenu kama tunaoshiriki katika mchakato wa ugavi... !!

Kwa mwana Mapinduzi mwenzenu.. katika mapammbano ya Kifikra!

M. M.

Mhh Mwanakijiji,

ina maana kuna mambo zaidi yanakuja kuhusu ufisadi Tanzania kuliko haya tuliyopata so far!

BTW, mkubwa gani serikalini atatembelea kijiji this weekend?\
Ngabu alipendekeza umwalike Lowasa, vipi umefanikiwa?
 
kama ufisadi wa namna ile tunaambiwa BADO......sijui tutaambiwa yepi tena!

tusubiri tuambiwe wananchi tumeuzwa sisi kama watu tu ndo lililobakia, maana rasilimali na ardhi tayari vishamalizika.
 
nilikuwa nimepanga mkubwa mmoja hivi lakini hili la Msiba limewapa udhuru. Tutaona itakuwaje.

Na swali lako la kwanza jibu ni ndiyo.. hili litakaloibuliwa na wanaharakati walio mstari wa mbele ni kubwa zaidi kwani lina specifics na siyo general statement..

Kwa kifupi, ile mada ya "jinsi ya kuibia serikali ya Muungano" itaoneshwa ni kwanini iliandikwa na ni jinsi gani watu walikuwa sahihi. Itaoneshwa mifano ya wizi ulivyofanywa...
 
nilikuwa nimepanga mkubwa mmoja hivi lakini hili la Msiba limewapa udhuru. Tutaona itakuwaje.

Na swali lako la kwanza jibu ni ndiyo.. hili litakaloibuliwa na wanaharakati walio mstari wa mbele ni kubwa zaidi kwani lina specifics na siyo general statement..

Kwa kifupi, ile mada ya "jinsi ya kuibia serikali ya Muungano" itaoneshwa ni kwanini iliandikwa na ni jinsi gani watu walikuwa sahihi. Itaoneshwa mifano ya wizi ulivyofanywa...

Unaweza kumwalika Butiku!
 
hamna neno bana ! salat IJUMAAT ! waombee baadhi ya wanaJF pia wawe na mwelekeo mzuri na wapende nchi yao !
 
Kikwete nimeahidi kukupa zawadi kama ukisalenda kwa wapinzani na kuvunja baraza lako la mawaziri, kuwaomba msamaha watanzania, na kuomba upewe second chance ili ufanye the right thing!

Nakubaliana na wewe Mwafrika. kuna haja ya Kikwete kuangalia ni wakina nani wanaweza kumsupport au kumwangusha, ambao ni wapiga kura tulio wengi. Asipende kujisafisha kwa mawaziri wake wachahe akasahau sehemu kubwa ya watanzania, sio ajabu hata hao mawaziri wake kuna ambao hawakupiga kura siku ile wakiwa wapo busy kuhonga wapiga kura.

Kikwete anatakiwa asome alama za nyakati na azitekeleze kwa haraka sana, Nashindwa kuelewe ile speed aliyoanza nayo imeishia wapi.. Hivi wana JF mnakumbuka alivyoanza kwa speed ya JET? sijui imeishia wapi maskini wa Mungu.

Kikwete Rais wetu amkaaa!!!
 
Inabidi sasa kikwete akubali mwaliko wa Ben (mwanaJF) na kwenda India maana kama kuna mengine yamevuja basi kazi anayo!
 
Huo mkutano wa Jpili kwangu naona utata kidogo.

The issues at hand are noble, but the timing is bad.

Watu (taifa) watakuwa bado na sentiments za msiba wa Salome Mbatia, na itawapa wakati mgumu sana kumeza yanayosemwa na akina Dr. Slaa. Hiyo itapoteza impact ya yatakayosemwa na kufanya issue nzima iwe mute.

Remember, you can not unring the bell.

My suggestion: Waahirishe hadi kipindi ikaribiane na Mkutano Mkuu wa CCM. Kwa kufanya hivyo, wata-overshadow maamuzi ya Mkutano Mkuu bila kuonekana kuwa hawana moyo kwa wafiwa na wahanga wa ajali ya Salome Mbatia.
 
Nakubaliana na wewe Mwafrika. kuna haja ya Kikwete kuangalia ni wakina nani wanaweza kumsupport au kumwangusha, ambao ni wapiga kura tulio wengi. Asipende kujisafisha kwa mawaziri wake wachahe akasahau sehemu kubwa ya watanzania, sio ajabu hata hao mawaziri wake kuna ambao hawakupiga kura siku ile wakiwa wapo busy kuhonga wapiga kura.

Kikwete anatakiwa asome alama za nyakati na azitekeleze kwa haraka sana, Nashindwa kuelewe ile speed aliyoanza nayo imeishia wapi.. Hivi wana JF mnakumbuka alivyoanza kwa speed ya JET? sijui imeishia wapi maskini wa Mungu.

Kikwete Rais wetu amkaaa!!!

Asante Msesewe,

Mwenzako JK akiwa ndani ya nchi anasema kuwa hizi ni tuhuma tu na akienda nje ya nchi anadai kuwa kuna uchunguzi unaendelea. Inaonekana the guy amefuata ushauri aliopewa wa kupuuzia tu haya mambo kwa hofu kuwa magazeti ya Rostam na makada wa chama all over the country watayazima.

I double dare Kikwete kuchukua action.
So far sidhani kama atafanya chochote!
 
Huo mkutano wa Jpili kwangu naona utata kidogo.

The issues at hand are noble, but the timing is bad.

Watu (taifa) watakuwa bado na sentiments za msiba wa Salome Mbatia, na itawapa wakati mgumu sana kumeza yanayosemwa na akina Dr. Slaa. Hiyo itapoteza impact ya yatakayosemwa na kufanya issue nzima iwe mute.

Remember, you can not unring the bell.

My suggestion: Waahirishe hadi kipindi ikaribiane na Mkutano Mkuu wa CCM. Kwa kufanya hivyo, wata-overshadow maamuzi ya Mkutano Mkuu bila kuonekana kuwa hawana moyo kwa wafiwa na wahanga wa ajali ya Salome Mbatia.

Kiungani,

huu mkutano wa jumapili ni upi? labda nimekosa hiyo news kidogo
 
Kiungani,

huu mkutano wa jumapili ni upi? labda nimekosa hiyo news kidogo

Angalia post ya kwanza kwenye hii thread.

Viongozi wa Ushirikiano wa Vyama Vya Upinzani vya CHADEMA, CUF, NCCR Mageuzi na TLP siku ya jumapili tarehe 28 Oktoba, 2007 watazungumza na wananchi katika mkutano wa ndani kutoa taarifa kwa umma kuhusu ufisadi.

Mazungumzo hayo ya ndani ambayo wananchi mbalimbali wanaalikwa kushiriki yatafanyika katika Ukumbi wa Urafiki uliopo Manispaa ya Kinondoni Jimbo la Ubungo Mkoani Dar e salaam kuanzia saa 4 mpaka saa 5 na nusu asubuhi.
 
haombwi mtu msamaha, na safari hii nawahakikishia msikose mkutano huo, kwani siyo majina tu, bali hadi ushahidi wa kisayansi (forensics) utawekwa hadharani kuonesha ni jinsi gani CCM imetumia vibaya nafasi yake katika nchi.

Kazi iliyofanyika kukusanya ushahidi huo (kama mnakumbuka mkutano wa awali uliahirishwa) ilikuwa ngumu kwa kila aliyehusika, lakini kwa mara nyingi Watanzania wameonesha ushirikiano kupita kiasi.

Mlio mstari wa mbele, ongozeni mapambano na sisi tuko nyuma yenu kama tunaoshiriki katika mchakato wa ugavi... !!

Kwa mwana Mapinduzi mwenzenu.. katika mapammbano ya Kifikra!

M. M.

Mzee Mwanakijiji

Hapo patamu kweli kweli

Mwaka huu naona unaweza kuwa mwaka wa kihistoria Tanzania.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom