Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,908
- 6,494
Nahodha wa Morocco, Achraf Hakimi, atafikishwa mahakamani kujibu shtaka la ubakaji, waendesha mashtaka wa Ufaransa wamethibitisha.
Mwanamke mmoja alimshutumu beki huyo wa klabu ya Paris Saint-Germain kwa kumbaka nyumbani kwake katika eneo la Paris mwaka 2023, akiwa na umri wa miaka 24. Hakimi amekanusha tuhuma hizo tangu mwanzo.
Mahakama ya rufaa ya Ufaransa imekataa rufaa yake dhidi ya uamuzi wa kufikishwa mahakamani, hivyo kesi hiyo sasa itaendelea kusikilizwa katika mahakama ya jinai. Hata hivyo, tarehe ya kuanza kwa kesi bado haijatangazwa.
Hakimi amesema anasubiri kwa hamu kusikilizwa kwa kesi hiyo ili aweze kutoa upande wake wa simulizi hadharani, huku mawakili wake wakisisitiza kuwa hana hatia.
#Michezo #Hainakuchoka #EastAfricaTV
Mwanamke mmoja alimshutumu beki huyo wa klabu ya Paris Saint-Germain kwa kumbaka nyumbani kwake katika eneo la Paris mwaka 2023, akiwa na umri wa miaka 24. Hakimi amekanusha tuhuma hizo tangu mwanzo.
Mahakama ya rufaa ya Ufaransa imekataa rufaa yake dhidi ya uamuzi wa kufikishwa mahakamani, hivyo kesi hiyo sasa itaendelea kusikilizwa katika mahakama ya jinai. Hata hivyo, tarehe ya kuanza kwa kesi bado haijatangazwa.
Hakimi amesema anasubiri kwa hamu kusikilizwa kwa kesi hiyo ili aweze kutoa upande wake wa simulizi hadharani, huku mawakili wake wakisisitiza kuwa hana hatia.
#Michezo #Hainakuchoka #EastAfricaTV